Ili Elimu yetu iwe bora, wanasiasa wana mchango gani?

Ili Elimu yetu iwe bora, wanasiasa wana mchango gani?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
images - 2024-07-20T113033.710.jpeg

Baada ya kuona matamanio ya baadhi ya watanzania juu ya kuwa na kizazi cha Gen Z kama cha Kenya, nimejikuta najiuliza ni kwa nini tuwatamani vijana wa kenya wakati na sisi tuna vijana wetu wasomi kama wao!?

Lakini pia huwa humu kunakuwa na mijadala ya jinsi vijana wa China walivyoiendeleza nchi yao kupitia Elimu ya Teknolojia waliyo nayo.

Hapa kwetu, watunga na wapanga sera wetu ambao ni wanasiasa, wana mchango gani kwenye kuifanya Elimu yetu iwe bora ili ichochee ukuaji wa uchumi wetu na maendeleo ya kijamii kwa ujumla!?

Je, unaona kwa kiasi gani wanasiasa wetu wanajishughulisha na kujali ubora wa Elimu yetu?
 
Elimu ikiwa bora watapoteza vyao vingi, ujinga mwingi mtaji mkubwa.
 
Elimu inaendana na Maarifa ya kile ulichosomea au karirishwa

Elimu ya bongo kwa kiasi kikubwa haitoi Maarifa Zaidi ya kukariri theories

Safari bado ni ndefu Sana 🐼
Ndiyo nauliza, jee tunaona kuna mwanasiasa anahusisha Elimu na maendeleo yetu?

Yaani mbali ya Abdacadabra za kisiasa, kuna wanasiasa wanamakinika kuifanya elimu yetu iwe Bora zaidi kuliko ilivyo sasa!?
 
Kiukwel wanasiasa wana mchango mkubwa sana katika kuinua elimu yetu kwani wao ndio viongoz wetu
Lakini tatizo hawaeki mkazo sana katika kuinua elimu ili kuendeleza mtaji wa wajinga wengi ambao watawasaidia kuimarisha uchumi wa vizazi vyao na sio maendeleo ya taifa kwa ujumla
 
Wanasiasa hawana mchango wa aina yoyote katika hili taifa.
Ndiyo wanaorudisha nyuma maendeleo kwa kujidai wanakula kwa urefu wa kamba.
 
Ndiyo nauliza, jee tunaona kuna mwanasiasa anahusisha Elimu na maendeleo yetu?

Yaani mbali ya Abdacadabra za kisiasa, kuna wanasiasa wanamakinika kuifanya elimu yetu iwe Bora zaidi kuliko ilivyo sasa!?
Wanasiasa wa bongo hawawezi kuhusisha Elimu yao na Maendeleo kwa sababu Elimu yao haina " Maarifa"

Angalia kwa mfano PhD za hawa Mawaziri wetu wamezipataje?

Ni afadhali Babu Tale kwa sababu Maarifa yake Yako dhahiri kwenye Ukuaji wa Industry ya Muziki na Comedy journalism 😄😄

Sabato Njema
 
Wanatakiwa kuacha kusaini mikataba, na kupokea msaada wenye masharti yenye lengo la kuzorotesha utoaji wa elimu kulingana na mazingira ya kitanzania. Wanafunzi leo hii wanalelewa kama yai. Wasikaripiwe, wasichapwe, wasipewe adhabu. Eti waonywe tu kwa ustaraabu! Kisa mikataba ya kimataifa. Khaa! Kazi kwelikweli
 
Wanatakiwa kuacha kusaini mikataba, na kupokea msaada wenye masharti yenye lengo la kuzorotesha utoaji wa elimu kulingana na mazingira ya kitanzania. Wanafunzi leo hii wanalelewa kama yai. Wasikaripiwe, wasichapwe, wasipewe adhabu. Eti waonywe tu kwa ustaraabu! Kisa mikataba ya kimataifa. Khaa! Kazi kwelikweli
Unadhani viboko vikiwepo vinaboreshaje elimu yetu??

Sipingani na hoja yako ila nataka ufafanuzi kidogo ili nijue mahusiano yaliyopo kati ya wanafunzi kuchapwa na ubora wa Elimu itolewayo.
 
Fatma karume once said " Elimu ya kenya ina educate lakini ya Tanzania ina indoctrinate"
Kama yuko sahihi wakili msomi hapo.

Critical thinking huipati kwa watanzania rational thinking and decision making inatupwa kwenye unyayo hasa yanapokuja mambo muhimu ya maisha sababu ya uchawa juu ya chama fulani.
 
Dhana ya mtihani na usomi ndiyo johnthebaptist anaisema...

Mpaka Sasa nahisi wengi wetu hatujui tatizo liliopo kwenye elimu yetu.

Kwa mfano mtu aliyeishia darasa la pili lakini ni fundi uashi mzuri, jee utakataa akujengee nyumba yako?

Kina Socrates na Plato, walikuwa na Digrii ngapi? Hivi waliogundua tarakimu walipata division ngapi darasani!?

Ni vizuri tukaiangalia hoja ya johnthebaptist kuhusu vyeti bila elimu.

Tunakuwaje na wasomi wasio na elimu?
 
Back
Top Bottom