Ili kuinua ubora wa elimu kila mmoja anapaswa kuwajibika na kucha mchezo wa lawama

Ili kuinua ubora wa elimu kila mmoja anapaswa kuwajibika na kucha mchezo wa lawama

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
ILI KUINUA ELIMU NCHINI TUNAHITAJI KUWAJIBIKA
Ili kuweza kuinua ubora wa elimu tunapaswa kutambua kinaganaga maeneo yote ya uwajibikaji, kutambua wakati maeneo hayo yanapokuwa na tatizo, mahali panapokuwa na tatizo na hatua zinazopaswa kuchukuliwa. Hii ndiyo maana ya uwajibikaji. Kukosekana kwa uwajibikaji ndicho chanzo cha mrundikano wa changamoto.

Ikumbukwe kila mmoja wetu anao wajibu katika kuinua kiwango cha ubora wa elimu. Hii inaanza na wananchi wenyewe wakisaidiwa na asasi za kiraia pamoja taasisi za utafiti ambazo huonesha masuala yaliyoachwa katika kuinua ubora na usawa kwenye elimu.

Uwajibikaji hapa ni mchakato unaolenga kuwasaidia watendaji kutekeleza majukumu yao na kufikia lengo. Uwajibikaji haumlengi mtendji mmoja tu ila wote wanaohusika. Suala la elimu bora ni jukumu la wote na siyo suala la kutafuta wa kumlaumu kwa sababu kila mmoja anawajibika.

Mifumo ya uwajibishaji inaweza ikawa na madhara mkubwa kama ikiandaliwa vibaya. Tafiti zinaonesha kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuwa kigezo cha kuwajibisha kwa kuangalia matokeo ni kigezo bora.

Ukweli unaosikitisha katika elimu ni kwamba "ni rahisi sana kumlaumu mwingine kuliko kutatu changamoto". Suala la elimu bora ni jukumu la wote "collective responsibility".Watu hufanya vizuri kama wakiwajibishwa kutokana na mamuzi kuliko matokeo ambayo yanaweza kuwa juu ya uwezo wao. Mazingira wezeshi huwawezesha watendaji kutekeleza majukumu yao. Hakuna mkabala wa uwajibikaji unaweza kufanikiwa kama hakuna mazingira wezeshi. Mazingira wezeshi yanatawaliwa na:
1. Taarifa sahihi
2. Zana za kuwezesha kukamilisha shughuli
3. Uwezo wa watendaji kutekeleza wajibu wao.
4. Motisha au hamasa ya kutekeleza wajibu.

Watendaji wote hutegemeana Ili kufikia malengo ya pamoja ya elimu. Kufikia malengo ya elimu kunahitaji ushirikiano na mawasiliano. Imani ya wanajamii na michango yao hupata nafasi ikiwa watendaji wataweka mlengo yanayotekelezeka kulingana na raslimali zilizopo. Jakubowsk (2017) Katika utafiti wake alionesh mkanganyiko wanaoupata wananchi wa Mexico na Poland kutokana na kukosekana kwa ubora kwenye maeneo ya uwajibikaji jambo lilowafanya viongozi kulaumu wananchi.

Licha ya Serikali ya Mexico kuazimia kufanya ugatuaji na ukasimishaji wa madaraka ngazi za chini Ili kuipunguzia Serikali kuu mzigo mwaka 1999 bado azimio hili halijatimizwa katika ukamilifu wake (Jakubowsk, 2017).
 
1.Wazazi
2.Walimu
3.Wanafunzi
4. Wanajamii
5 .Asasi za kiraia
..................................
Education is collective responsibility
 
1.Wazazi
2.Walimu
3.Wanafunzi
4. Wanajamii
5 .Asasi za kiraia
..................................
Education is collective responsibility
Well mkuu ila BILA POLITICAL WILL hapo hakuna kitakachofanyika,baada ya politicians wetu kutokufanya uamuzi na kuamua kuiweka kwenye vumbi yale mapendekezo ya Tume ya Mh.J.Makwetta(rip)kuhusu hatima ya mfumo wa kielimu kwa nchi yetu haya tunayoyaona sasa politicians wetu, kwa makusudi kabisa waliyataka,sababu kubwa ni status ago iendelee maana wao watoto wao wapo nje ya nchi, wakirudi waendelee kuwatawala hii generation duni kutokea lingusenguse na kwingineko,mfumo uliopendekezwa na tume ile ilikua ni pamoja muda wa miaka ya masomo upunguzwe, yaani mtoto akifika grade 12 aweze kwenda varsity au technical colleges
 
Well mkuu ila BILA POLITICAL WILL hapo hakuna kitakachofanyika,baada ya politicians wetu kutokufanya uamuzi na kuamua kuiweka kwenye vumbi yale mapendekezo ya Tume ya Mh.J.Makwetta(rip)kuhusu hatima ya mfumo wa kielimu kwa nchi yetu haya tunayoyaona sasa politicians wetu, kwa makusudi kabisa waliyataka,sababu kubwa ni status ago iendelee maana wao watoto wao wapo nje ya nchi, wakirudi waendelee kuwatawala hii generation duni kutokea lingusenguse na kwingineko,mfumo uliopendekezwa na tume ile ilikua ni pamoja muda wa miaka ya masomo upunguzwe, yaani mtoto akifika grade 12 aweze kwenda varsity au technical colleges
Well said Brother political will ni changamoto sana na ikiwepo inakuja na vested interests
 
Well said Brother political will ni changamoto sana na ikiwepo inakuja na vested interests
Tatizo tunalokabiliwa hapa nchini hatuna taasisi imara za kutuletea utawala bora,matokeo yake kila kitu kinategemea politicians wanaamua vipi, tungekua na judiciary iliyohuru, wewe mkuu ungeweza kuipeleka mahakamani serikali ili tuwe na elimu bora maana hili ni hitaji letu kikatiba na serikali inawajibika nalo, ila hatuna judiciary huru, all judges wanategemea kupata hizi nafasi kupitia politicians sio taaluma zao
 
Kufikia kwenye viwango vya ubora sawa na lengo namba nne(4) katika SDG 2030 Kwa hali hii tutaumia sana
 
Tatizo jingine kubwa tunalokabiliwa nalo ni our majority ya middle class uwezo wa kufikiri maisha hawana,wengi wako kwenye ngono na viajira uchwara, hii ni mada nzuri ila haina wachangiaji ila ingekua ya ngono ingekua tofauti ,hatuwezi laumu ila ndio system imetaka hivyo ili uzuzu huu uendelee
 
Hali ni mbaya juu ya vigezo vya kupima uwajibikaji katika suala la elimu nchini kuliko tunavyofikiri, hatuna standards zetu kabisa. Tuliiga BRN, tumeiga Ep4R najiuliza tunaegemea wapi na tunaelekea wapi?
 
Watanzania wamelala kwanza, siku wakiamka hayo yote yatawezekana hata elimu bora, uongozi bora, huduma bora ya afya, miundombinu mizuri na mengine.

Lakini sasa ivi bado vijana wako kwenye bodaboda, michezo ya kubahatisha halafu Simba na Yanga.
Mambo ya kijinga tu mengi hata uskize radio na luninga ujinga tu nchi ina matatizo lukuki kipindi cha mpira sijui michezo kinajadiliwa siju nzima.
Kama uko abroad tune radio za Tz utaeza fikiri nchi hiyo ni ya dunia ya kwanza. Muda wote wao michezo, michezo, michezo, udaku hata radio ya taifa.

Maana yake nini mambo haya? Matatizo haya kama elimu bora bado Watanzania hawajaona au kama wameona hawajali mana hakuna hata sauti za kutaka mabadiliko au hata kuonesha hivi vitu ni vya hovyo.

Hata habari za kiuchunguzi huwezi kupata yani hata gazeti moja la habari za kiuchunguzi hakuna?
 
Watanzania wamelala kwanza, siku wakiamka hayo yote yatawezekana hata elimu bora, uongozi bora, huduma bora ya afya, miundombinu mizuri na mengine.

Lakini sasa ivi bado vijana wako kwenye bodaboda, michezo ya kubahatisha halafu Simba na Yanga.
Mambo ya kijinga tu mengi hata uskize radio na luninga ujinga tu nchi ina matatizo lukuki kipindi cha mpira sijui michezo kinajadiliwa siju nzima.
Kama uko abroad tune radio za Tz utaeza fikiri nchi hiyo ni ya dunia ya kwanza. Muda wote wao michezo, michezo, michezo, udaku hata radio ya taifa.

Maana yake nini mambo haya? Matatizo haya kama elimu bora bado Watanzania hawajaona au kama wameona hawajali mana hakuna hata sauti za kutaka mabadiliko au hata kuonesha hivi vitu ni vya hovyo.

Hata habari za kiuchunguzi huwezi kupata yani hata gazeti moja la habari za kiuchunguzi hakuna?
Hali ya ujinga nchini ni kweli inapaswa kutazamwa zaidi ya kufahamu kusoma na kuandika.
 
Hali ya ujinga nchini ni kweli inapaswa kutazamwa zaidi ya kufahamu kusoma na kuandika.
Na ujinga ndiyo mtaji wa watawala.
Rahisi sana kuwatawala wajinga kama walivyo Watanzania.

Elimu ya hovyo inazalisha wajinga ambao inakua kazi rahisi kwa watawala dhalimu kuwatawala hawa.

Nini kifanyike sasa?
Watawaliwa wanatakiwa kuamka usingizini.

Watawezaje kuamka?
Mada kama hizi zinatakiwa zipewe airtime ili kuwaamsha watanzania, taasisi zisizo za kiserikali kuandaa majukwaa yasiyo ya kisiasa kuwafumbua hawa waliolala kama ilivyokua Haki elimu.
Vyombo vya habari kuandaa vipindi vinavyotoa elimu ili kuwaamsha wadanganyika.
 
Embu tujifunze kitu kwenye mfumo wa elimu wa nchi ya Ufini(Finland)
Kwa mujibu wa Ashok Frederick(2020) katika andiko liitwalo " Mfumo wa elimu wa Ufini"aliweza kuonesha yafuatayo:
Ufini ni taifa lenye takribni Watu 5,518,371 linalofuata falsafa ya kijamaa ya kilutheri (Lutheran communist). Kabla ya mwaka 1990 nchi hii ilikuwa ikitegemea kilimo kuinua uchumi wake lakini Sasa ni kituo cha teknolojia Duniani.
Elimu ya Dini ni suala la mzazi. Katika nchi hii Serikali ndiyo inyogharamia suala la ada za wanafunzi (no tuition fee). Mtaala wa elimu unasimamiwa na utatu wa (Serikali, wizara husika na vyuo vibavyotoa mafunzo ya elimu).

Suala la mabadiliko ya kiongozi katika nchi ya Ufini hayasababishi kubadilika kwa sera ya elimu. Ndani ya miaka takribani 14 Ufini imekuwa namba moja Kwa elimu bora Duniani.
Darasa moja katika nchi hii linakuwa na walimu watatu. Walimu wawili wao hujikita katika kufundisha huku mwalimu mmoja akijikita katika kuwasaidia wale wasioelewa Kwa haraka. Walimu wote wana elimu ya uzamili (Masters) na Mwalimu wa ngazi ya shahada haruhusiwi kufundisha hata katika shule ya msingi.
Walimu huchaguliwa kutoka kwenye wanafunzi kumi wanaofanya vizuri zaidi vyuoni na mchujo huendelea hata wanapokuwa kazini. Kilimo cha ubora wa elimu siyo kipato, teknolojia au jeshi ila tabia bora za watu wake.
Nadhani tunaweza tukona tunchokifanya kinatupekeka wapi kwa kuangalia mfano huu.
 
Watanzania wamelala kwanza, siku wakiamka hayo yote yatawezekana hata elimu bora, uongozi bora, huduma bora ya afya, miundombinu mizuri na mengine.

Lakini sasa ivi bado vijana wako kwenye bodaboda, michezo ya kubahatisha halafu Simba na Yanga.
Mambo ya kijinga tu mengi hata uskize radio na luninga ujinga tu nchi ina matatizo lukuki kipindi cha mpira sijui michezo kinajadiliwa siju nzima.
Kama uko abroad tune radio za Tz utaeza fikiri nchi hiyo ni ya dunia ya kwanza. Muda wote wao michezo, michezo, michezo, udaku hata radio ya taifa.

Maana yake nini mambo haya? Matatizo haya kama elimu bora bado Watanzania hawajaona au kama wameona hawajali mana hakuna hata sauti za kutaka mabadiliko au hata kuonesha hivi vitu ni vya hovyo.

Hata habari za kiuchunguzi huwezi kupata yani hata gazeti moja la habari za kiuchunguzi hakuna?
Kweli kabisa, watu bado wapo usingizini. Unajiuliza wakati mwingine kuwa kwanini namba ya wanaodaiwa kuwa wasomi inaongezeka kila uchao, lakini matatizo ndo kwanza yanazidi.

Shida ni Elimu, bado elimu inayotolewa haijalenga kuwakomboa watu ili waweze kukabiliana na changamoto na kutawala mazingira yao.

Lazima tuamshane Kama hivi ,la sivyo! Kuna bomu litalipuka siku zijazo.
 
Tukae tujiulize hivi wale wataalamu wa kilimo wanao graduate pale Sokoine university wapo wapi?na nini mchango wao kwenye kuleta mabadiliko ya kilimo kwa nchi yetu?,mfumo wetu wa kielimu je unatupa wataalamu ambao nchi inayowahitaji kwa sector hii ya kilimo?,Zambia 🇿🇲 kilimo chake kimebadilika mno kwa miaka Michaele iliyopita ikiwa ni pamoja na kunufaika na wakulima waliofukuzwa Zimbabwe, mahindi (chakula kikuu)wanajitegemea na ukitoka southern province hadi Northern province ni mahindi tu, ukifika Mazabuka ndio kiini cha uzalishaji wa sukari, na almost local demands wanajitosheleza,kilombero yetu bado ni politics tupu, we need to be smart sasa watanzania wenzangu
 
Back
Top Bottom