NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Naaam!! kila ligi msimu inapoanza na kuisha lazima kuwe na malalamiko ya kuonewa haswa kwa hizi timu za kariakoo (Simba na Yanga) ni muda sasa wa Tff na Bodi ya ligi kushughulika na hizi lawama au lawama na makelele yanayojitokeza kila msimu unapoisha
Tff na Bodi ya ligi ishughulike na haya yafuatayo ilikutokomeza ama kupunguza lawama kutoka kwa wapenzi wa mpira katika ligi yetu ya NBCPL
(1) uchunguzi wa hali ya juu kwa timu zinazotoa rushwa kwa marefa, hiki kimekua ni kilio cha kila msimu unapoisha, mpira ni mchezo wa wazi wala hauchezwi ndani mashabiki huwa wanaona na wanajua kabisa hili ni kosa ama siyo kosa na refa anastahili kutoa kadi au kupuliza filimbi.
kuna baadhi ya timu zinalalamikiwa sana kuwa zinahonga marefa ili wapate ushindi na pointi tatu muhimu katika mchezo na kweli ukiangalia refa anavyochezea unaona kabisa kuna namna imetumika timu kupata point tatu muhimu, Tff na Bodi ya ligi inapaswa kubuni mbinu za kuwakamata marefa wanaokula rushwa na kutoa adhabu kali sana kwa wahsika
(2) tuzo zitolewe kwa wakati , hii inafanya ligi ichangamke sana tena mno lakini kilichofanyika msimu uliopita ni madudu matupu na aibu kwa Tff na bodi ya ligi yaani msimu kuisha na tuzo kutolewa msimu mwingine unaoanza kwa kweli imefanya ligi yetu kukosa mvuto kabisa, Tff wanapaswa kutoa ligi kwa wakati.
(3)Viwanja vikaguliwe kwa wakati na siyo mpaka Simba na Yanga wacheze ndiyo vionekane ni vibovu, ligi inafatiliwa sana hii ni aibu kubwa viwanja havikaguliwi haswa viwanja vya mikoani mpaka Simba na Yanga wakicheza na mashabiki kuanza kulalamika ndipo Tff na Bodi ya ligi hujitokeza na kufungia uwanja, kwa mantiki hiyo watendandaji hawafanyi kazi mpaka washituliwe na kelele za mashabiki .
Tff iliangalie sana hili suala la uakaguzi wa viwanja kwanni viwanja bora huleta hamasa katika ukuaji wa ligi
(4) Marefa walipwe stahiki zao na waboreshewe posho , marefa hawana pa kulalamika kutoka kwenye vyanzo vyangu vya ndani marefa hawapewi posho zao kwa wakati na muda mwingine wanadhurumika kabisa , sasa kwa hali kama hii lazima refa auze mechi lakini akipewa stahiki zake kwa wakati hii itapunguza lawama za refa kuuza mechi, Tff na bodi ya ligi waangalie hili suala.
(5) Zitolewe semina na elimu ya kutosha kwa marefa , hili ni jambo la ,muhimu sana kuna makosa madogo madogo hufanywa na marefa ya kushindwa kutafsiri sheria za mpira na kufanya timu pinzani kujipatia pointi tatu muhimu lakini kama Tff na bodi ya ligi itaandaa mkakati maalumu wa kuchukua marefa wanaohudhuria training na semina za kila muda wanapohitajika itafanya ligi yetu ikue.
(6) iboreshwe sheria inayohusu imani za kishirikina kama ipo na kama haipo itungwe lakini iwe na uthibitisho kwa timu itakayotuhumiwa, kuruka ukuta, kutoa taulo kuchimba katikati ya uwanja n.k Tff na Bodi ya ligi imekua ikipiga faini kwa timu zitakazoonesha viashiria vya imani za kishirikina, ombi langu kama hii sheria ipo basi iboreshwe maana limekua ni suala la kujirudirudia.
Endapo haya niliyoyaorodhesha yatapuuzwa basi tusitegemee kuona ligi yetu ikikua bali itaendelea kudumaa kwani kwa mujibu wa utafiti sasa tunashika nafasi ya sita kwa ligi bora africa, kwa mantiki hiyo tumepolomoka kutoka nafsi ya tano mpaka nafasi ya sita.
Tff na Bodi ya ligi ishughulike na haya yafuatayo ilikutokomeza ama kupunguza lawama kutoka kwa wapenzi wa mpira katika ligi yetu ya NBCPL
(1) uchunguzi wa hali ya juu kwa timu zinazotoa rushwa kwa marefa, hiki kimekua ni kilio cha kila msimu unapoisha, mpira ni mchezo wa wazi wala hauchezwi ndani mashabiki huwa wanaona na wanajua kabisa hili ni kosa ama siyo kosa na refa anastahili kutoa kadi au kupuliza filimbi.
kuna baadhi ya timu zinalalamikiwa sana kuwa zinahonga marefa ili wapate ushindi na pointi tatu muhimu katika mchezo na kweli ukiangalia refa anavyochezea unaona kabisa kuna namna imetumika timu kupata point tatu muhimu, Tff na Bodi ya ligi inapaswa kubuni mbinu za kuwakamata marefa wanaokula rushwa na kutoa adhabu kali sana kwa wahsika
(2) tuzo zitolewe kwa wakati , hii inafanya ligi ichangamke sana tena mno lakini kilichofanyika msimu uliopita ni madudu matupu na aibu kwa Tff na bodi ya ligi yaani msimu kuisha na tuzo kutolewa msimu mwingine unaoanza kwa kweli imefanya ligi yetu kukosa mvuto kabisa, Tff wanapaswa kutoa ligi kwa wakati.
(3)Viwanja vikaguliwe kwa wakati na siyo mpaka Simba na Yanga wacheze ndiyo vionekane ni vibovu, ligi inafatiliwa sana hii ni aibu kubwa viwanja havikaguliwi haswa viwanja vya mikoani mpaka Simba na Yanga wakicheza na mashabiki kuanza kulalamika ndipo Tff na Bodi ya ligi hujitokeza na kufungia uwanja, kwa mantiki hiyo watendandaji hawafanyi kazi mpaka washituliwe na kelele za mashabiki .
Tff iliangalie sana hili suala la uakaguzi wa viwanja kwanni viwanja bora huleta hamasa katika ukuaji wa ligi
(4) Marefa walipwe stahiki zao na waboreshewe posho , marefa hawana pa kulalamika kutoka kwenye vyanzo vyangu vya ndani marefa hawapewi posho zao kwa wakati na muda mwingine wanadhurumika kabisa , sasa kwa hali kama hii lazima refa auze mechi lakini akipewa stahiki zake kwa wakati hii itapunguza lawama za refa kuuza mechi, Tff na bodi ya ligi waangalie hili suala.
(5) Zitolewe semina na elimu ya kutosha kwa marefa , hili ni jambo la ,muhimu sana kuna makosa madogo madogo hufanywa na marefa ya kushindwa kutafsiri sheria za mpira na kufanya timu pinzani kujipatia pointi tatu muhimu lakini kama Tff na bodi ya ligi itaandaa mkakati maalumu wa kuchukua marefa wanaohudhuria training na semina za kila muda wanapohitajika itafanya ligi yetu ikue.
(6) iboreshwe sheria inayohusu imani za kishirikina kama ipo na kama haipo itungwe lakini iwe na uthibitisho kwa timu itakayotuhumiwa, kuruka ukuta, kutoa taulo kuchimba katikati ya uwanja n.k Tff na Bodi ya ligi imekua ikipiga faini kwa timu zitakazoonesha viashiria vya imani za kishirikina, ombi langu kama hii sheria ipo basi iboreshwe maana limekua ni suala la kujirudirudia.
Endapo haya niliyoyaorodhesha yatapuuzwa basi tusitegemee kuona ligi yetu ikikua bali itaendelea kudumaa kwani kwa mujibu wa utafiti sasa tunashika nafasi ya sita kwa ligi bora africa, kwa mantiki hiyo tumepolomoka kutoka nafsi ya tano mpaka nafasi ya sita.