Ili ligi yetu iwe bora na ya kuvutia TFF na Bodi ya ligi inapaswa kushughulika na haya yafuatayo

Ili ligi yetu iwe bora na ya kuvutia TFF na Bodi ya ligi inapaswa kushughulika na haya yafuatayo

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Naaam!! kila ligi msimu inapoanza na kuisha lazima kuwe na malalamiko ya kuonewa haswa kwa hizi timu za kariakoo (Simba na Yanga) ni muda sasa wa Tff na Bodi ya ligi kushughulika na hizi lawama au lawama na makelele yanayojitokeza kila msimu unapoisha

Tff na Bodi ya ligi ishughulike na haya yafuatayo ilikutokomeza ama kupunguza lawama kutoka kwa wapenzi wa mpira katika ligi yetu ya NBCPL

(1) uchunguzi wa hali ya juu kwa timu zinazotoa rushwa kwa marefa, hiki kimekua ni kilio cha kila msimu unapoisha, mpira ni mchezo wa wazi wala hauchezwi ndani mashabiki huwa wanaona na wanajua kabisa hili ni kosa ama siyo kosa na refa anastahili kutoa kadi au kupuliza filimbi.

kuna baadhi ya timu zinalalamikiwa sana kuwa zinahonga marefa ili wapate ushindi na pointi tatu muhimu katika mchezo na kweli ukiangalia refa anavyochezea unaona kabisa kuna namna imetumika timu kupata point tatu muhimu, Tff na Bodi ya ligi inapaswa kubuni mbinu za kuwakamata marefa wanaokula rushwa na kutoa adhabu kali sana kwa wahsika

(2) tuzo zitolewe kwa wakati , hii inafanya ligi ichangamke sana tena mno lakini kilichofanyika msimu uliopita ni madudu matupu na aibu kwa Tff na bodi ya ligi yaani msimu kuisha na tuzo kutolewa msimu mwingine unaoanza kwa kweli imefanya ligi yetu kukosa mvuto kabisa, Tff wanapaswa kutoa ligi kwa wakati.

(3)Viwanja vikaguliwe kwa wakati na siyo mpaka Simba na Yanga wacheze ndiyo vionekane ni vibovu, ligi inafatiliwa sana hii ni aibu kubwa viwanja havikaguliwi haswa viwanja vya mikoani mpaka Simba na Yanga wakicheza na mashabiki kuanza kulalamika ndipo Tff na Bodi ya ligi hujitokeza na kufungia uwanja, kwa mantiki hiyo watendandaji hawafanyi kazi mpaka washituliwe na kelele za mashabiki .
Tff iliangalie sana hili suala la uakaguzi wa viwanja kwanni viwanja bora huleta hamasa katika ukuaji wa ligi

(4) Marefa walipwe stahiki zao na waboreshewe posho , marefa hawana pa kulalamika kutoka kwenye vyanzo vyangu vya ndani marefa hawapewi posho zao kwa wakati na muda mwingine wanadhurumika kabisa , sasa kwa hali kama hii lazima refa auze mechi lakini akipewa stahiki zake kwa wakati hii itapunguza lawama za refa kuuza mechi, Tff na bodi ya ligi waangalie hili suala.

(5) Zitolewe semina na elimu ya kutosha kwa marefa , hili ni jambo la ,muhimu sana kuna makosa madogo madogo hufanywa na marefa ya kushindwa kutafsiri sheria za mpira na kufanya timu pinzani kujipatia pointi tatu muhimu lakini kama Tff na bodi ya ligi itaandaa mkakati maalumu wa kuchukua marefa wanaohudhuria training na semina za kila muda wanapohitajika itafanya ligi yetu ikue.

(6) iboreshwe sheria inayohusu imani za kishirikina kama ipo na kama haipo itungwe lakini iwe na uthibitisho kwa timu itakayotuhumiwa, kuruka ukuta, kutoa taulo kuchimba katikati ya uwanja n.k Tff na Bodi ya ligi imekua ikipiga faini kwa timu zitakazoonesha viashiria vya imani za kishirikina, ombi langu kama hii sheria ipo basi iboreshwe maana limekua ni suala la kujirudirudia.

Endapo haya niliyoyaorodhesha yatapuuzwa basi tusitegemee kuona ligi yetu ikikua bali itaendelea kudumaa kwani kwa mujibu wa utafiti sasa tunashika nafasi ya sita kwa ligi bora africa, kwa mantiki hiyo tumepolomoka kutoka nafsi ya tano mpaka nafasi ya sita.
 
7. Mdhamini mmoja kudhamini vilabu zaidi ya 5 ni indication ya match fixing.
Mawazo mafupi sana haya yanyotoka upande wa Simba luza. Wakati SportPesa (ya Tarimba) ilipokuwa inadhamini timu zote (including Simba) ndipo wakati Simba iling'ara saba, je ilikuwa ni matokeo match fixing? Azam TV ianadhamini timu zote za ligi ikiwemo Simba, je hiyo nayo ni match fixing?
 
Mawazo mafupi sana haya yanyotoka upande wa Simba luza. Wakati SportPesa (ya Tarimba) ilipokuwa inadhamini timu zote (including Simba) ndipo wakati Simba iling'ara saba, je ilikuwa ni matokeo match fixing? Azam TV ianadhamini timu zote za ligi ikiwemo Simba, je hiyo nayo ni match fixing?
Udhamini wa Sportpesa ni sawa na CRD na NMB.

GSM ni muwekezaji directly wa Yanga na ndio maana ana hisa 49%
 
Naaam!! kila ligi msimu inapoanza na kuisha lazima kuwe na malalamiko ya kuonewa haswa kwa hizi timu za kariakoo (Simba na Yanga) ni muda sasa wa Tff na Bodi ya ligi kushughulika na hizi lawama au lawama na makelele yanayojitokeza kila msimu unapoish...
Kungekuwa hakuna Yanga na Simba Timu za Wanasiasa hayo yangewezekana.
 
Udhamini wa Sportpesa ni sawa na CRD na NMB.

GSM ni muwekezaji directly wa Yanga na ndio maana ana hisa 49%
GSM siyo mwekezaji, ni kampuni ya biashara na wala siyo mwekezaji wa hisa hizo 49% unazosema, labda ulikuwa na maana ya MO anayemiliki 49% za Simba na unadhani kuwa Yanga pia inaendeshwa kiswahiliswahili kama SImba waligawa 49% bila kuwa na tathmini yoyote. Share za Yanga bado hazijatolewa kwa vile bado timu infanyiwa tathmini.

Sikiliza hapa


View: https://www.youtube.com/watch?v=MHDE4PAwUSA
 
7. Mdhamini mmoja kudhamini vilabu zaidi ya 5 ni indication ya match fixing.
Kwa bongo bado muitikio wa wadhamini ni mdogo tutaathiri zaidi timu ndogo ambazo hazina brand kubwa ya kjwavuta wadhamini kama simba na yanga. Tusijilinganishe na ulaya
 
Iyo namba sita ili itekelezwe vizuri itabidi aongezeke refa mwenye utaalam wa kuagua na kugangua ili kutoa maamuzi sahihi
 
Naaam!! kila ligi msimu inapoanza na kuisha lazima kuwe na malalamiko ya kuonewa haswa kwa hizi timu za kariakoo (Simba na Yanga) ni muda sasa wa Tff na Bodi ya ligi kushughulika na hizi lawama au lawama na makelele yanayojitokeza kila msimu unapoisha

Tff na Bodi ya ligi ishughulike na haya yafuatayo ilikutokomeza ama kupunguza lawama kutoka kwa wapenzi wa mpira katika ligi yetu ya NBCPL

(1) uchunguzi wa hali ya juu kwa timu zinazotoa rushwa kwa marefa, hiki kimekua ni kilio cha kila msimu unapoisha, mpira ni mchezo wa wazi wala hauchezwi ndani mashabiki huwa wanaona na wanajua kabisa hili ni kosa ama siyo kosa na refa anastahili kutoa kadi au kupuliza filimbi.

kuna baadhi ya timu zinalalamikiwa sana kuwa zinahonga marefa ili wapate ushindi na pointi tatu muhimu katika mchezo na kweli ukiangalia refa anavyochezea unaona kabisa kuna namna imetumika timu kupata point tatu muhimu, Tff na Bodi ya ligi inapaswa kubuni mbinu za kuwakamata marefa wanaokula rushwa na kutoa adhabu kali sana kwa wahsika

(2) tuzo zitolewe kwa wakati , hii inafanya ligi ichangamke sana tena mno lakini kilichofanyika msimu uliopita ni madudu matupu na aibu kwa Tff na bodi ya ligi yaani msimu kuisha na tuzo kutolewa msimu mwingine unaoanza kwa kweli imefanya ligi yetu kukosa mvuto kabisa, Tff wanapaswa kutoa ligi kwa wakati.

(3)Viwanja vikaguliwe kwa wakati na siyo mpaka Simba na Yanga wacheze ndiyo vionekane ni vibovu, ligi inafatiliwa sana hii ni aibu kubwa viwanja havikaguliwi haswa viwanja vya mikoani mpaka Simba na Yanga wakicheza na mashabiki kuanza kulalamika ndipo Tff na Bodi ya ligi hujitokeza na kufungia uwanja, kwa mantiki hiyo watendandaji hawafanyi kazi mpaka washituliwe na kelele za mashabiki .
Tff iliangalie sana hili suala la uakaguzi wa viwanja kwanni viwanja bora huleta hamasa katika ukuaji wa ligi

(4) Marefa walipwe stahiki zao na waboreshewe posho , marefa hawana pa kulalamika kutoka kwenye vyanzo vyangu vya ndani marefa hawapewi posho zao kwa wakati na muda mwingine wanadhurumika kabisa , sasa kwa hali kama hii lazima refa auze mechi lakini akipewa stahiki zake kwa wakati hii itapunguza lawama za refa kuuza mechi, Tff na bodi ya ligi waangalie hili suala.

(5) Zitolewe semina na elimu ya kutosha kwa marefa , hili ni jambo la ,muhimu sana kuna makosa madogo madogo hufanywa na marefa ya kushindwa kutafsiri sheria za mpira na kufanya timu pinzani kujipatia pointi tatu muhimu lakini kama Tff na bodi ya ligi itaandaa mkakati maalumu wa kuchukua marefa wanaohudhuria training na semina za kila muda wanapohitajika itafanya ligi yetu ikue.

(6) iboreshwe sheria inayohusu imani za kishirikina kama ipo na kama haipo itungwe lakini iwe na uthibitisho kwa timu itakayotuhumiwa, kuruka ukuta, kutoa taulo kuchimba katikati ya uwanja n.k Tff na Bodi ya ligi imekua ikipiga faini kwa timu zitakazoonesha viashiria vya imani za kishirikina, ombi langu kama hii sheria ipo basi iboreshwe maana limekua ni suala la kujirudirudia.

Endapo haya niliyoyaorodhesha yatapuuzwa basi tusitegemee kuona ligi yetu ikikua bali itaendelea kudumaa kwani kwa mujibu wa utafiti sasa tunashika nafasi ya sita kwa ligi bora africa, kwa mantiki hiyo tumepolomoka kutoka nafsi ya tano mpaka nafasi ya sita.
Zawadi zitolewe kwa wakati
 
Back
Top Bottom