DOKEZO Ili uruhusiwe kufanya biashara jimbo la Ukonga ni lazima uwe na Cheti cha COVID-19 pamoja na cheti cha afya

DOKEZO Ili uruhusiwe kufanya biashara jimbo la Ukonga ni lazima uwe na Cheti cha COVID-19 pamoja na cheti cha afya

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Nimeshuhudia patashika ya migambo na wafanyabiashara kata ya Buyuni wakiwakamata wafanyabiashara mbalimbali na kuwapeleka ofisi ya mtendaji kata Buyuni iliyopo Chanika kwa kosa la kufanya biashara bila cheti cha afya na cha COVID-19.

Pamoja na mambo mengine msako huu umekuwa mkali kiasi kwamba watu wamefunga ofisi na kurudi majumbani, wametakiwa kulipa faini ya Tsh 500,000/= na wengine laki tatu mpaka 50000 kulingana na biashara ya mhusika.

Watu wa saloon na migahawa, maduka na mafundi viatu wamesombwa na kupelekwa ofisi ya kata. Mpaka naandika hapa bado kuna wafanyabiashara wanashikiliwa hapo Buyuni kata.

Tunaomba ofisi ya mbunge au mtendaji na mamlaka husika zitoe ufafanuzi juu ya ujinga huu unaofanywa kwa maelekezo ya bwana afya na mtendaji wa kata. Tafuteni vyanzo vya mapato acheni kusumbua mama zetu kwa mambo ya kijinga.
 
Fuata maelekezo ya serikali. Kapime afya, pata cheti, ufanye biashara.
 
Ni vigumu sana kuitafautisha CCM na ushetani......yaani wao furaha yao ni kuona wananchi wanapata tabu tu.....na sio vinginevyo....yaani jambo lolote linaloonekana kuwaletea unafuu wananchi wao hawalipendi......Sasa tofauti yao na mashetani nini.....????
 
Fuata maelekezo ya serikali. Kapime afya, pata cheti, ufanye biashara.
Huyo mgambo anayekamata wenzake yeye wala hana hicho cheti!! Hii nchi ya ajabu sana, kila mtu anamega kipande na kujiwekea sheria zake!! cheti cha covid wapi na wapi? Kesho atakamata wafanyabiashara wasiovaa barakoa!!
 
Maelekezo wanayopewa Kuna Siku wataturahi.
 
Back
Top Bottom