Ilikuwa kosa kubwa sana Joseph Kabila kumuibia Tshisekedi ushindi wa urais Congo dhidi ya mshindi halali, Fayulu

Ilikuwa kosa kubwa sana Joseph Kabila kumuibia Tshisekedi ushindi wa urais Congo dhidi ya mshindi halali, Fayulu

Uchaguzi wa Congo DRC wa mwaka 2018 ulikuwa ni fursa ya dhahabu ya Congo kurekebisha mambo mengi sana na kuipa nchi hiyo muelekeo sahihi wa kitaifa kwa mara ya kwanza ila uroho wa madaraka wa Kabila kulinda maslahi yake na kutoheshimu matakwa ya raia ukaikosesha Congo fursa hiyo.

Katika uchaguzi wa DRC wa mwaka 2018 ni wazi kwamba Martin Fayulu alishinda uchaguzi huo kwa kura nyingi sana lakini Kabila akaingilia Tume ya Taifa ya uchaguzi(CENI) kumsimika Tshisekedi aliyemuahidi atakuwa kibaraka wake.

Martin Fayulu alikuwa ni mgombea aliyeweza kuunganisha makundi mengi tofauti ya Congo, alikuwa na ushawashi mkubwa, huenda angeweza kuipa Congo ahueni kwa mara ya kwanza tofauti na Tshisekedi aliyeingizwa kwa msaada wa Kabila kupora uchaguzi.
Issue ya congo si rahisi km watu wengi wanavyoiongelea, congo inahitaji kiongozi haswaa mwenye uwezo na nguvu ya kurekebisha mambo tena ajitoe mhanga kwelikweli kwa haya matatizo ya congo ni ya mda mrefu na ni yakutengeneza. Waliyoyatengeneza wanawalisisha watu wao kwa kuwa wanapata faida. Congo pia iwekeze kwa nchi rafiki ktk mkutadha wa diplomasia ya uchumi ili kusaidiwa na madui zake hawa huku izidi kujijenga kijeshi.
 
Sitashangaa siku moja kusikia Kongo kuna Vita kati ya waongea Lingala na waongea Kiswahili.

Kwamba waongea Lingala wanasema waongea Kiswahili sio Wakongo bali ni wavamizi.
 
Uchaguzi wa Congo DRC wa mwaka 2018 ulikuwa ni fursa ya dhahabu ya Congo kurekebisha mambo mengi sana na kuipa nchi hiyo muelekeo sahihi wa kitaifa kwa mara ya kwanza ila uroho wa madaraka wa Kabila kulinda maslahi yake na kutoheshimu matakwa ya raia ukaikosesha Congo fursa hiyo.

Katika uchaguzi wa DRC wa mwaka 2018 ni wazi kwamba Martin Fayulu alishinda uchaguzi huo kwa kura nyingi sana lakini Kabila akaingilia Tume ya Taifa ya uchaguzi(CENI) kumsimika Tshisekedi aliyemuahidi atakuwa kibaraka wake.

Martin Fayulu alikuwa ni mgombea aliyeweza kuunganisha makundi mengi tofauti ya Congo, alikuwa na ushawashi mkubwa, huenda angeweza kuipa Congo ahueni kwa mara ya kwanza tofauti na Tshisekedi aliyeingizwa kwa msaada wa Kabila kupora uchaguzi.
Mifumo ya chaguzi ya Uganda, Rwanda, Burundi na Tanzania haitofautiani sana. Tume za uchaguzi zinao uwezo wa kubambikia wananchi kiongozi wasiyemtaka. Hapo Rwanda ni mgumu kuamini kuwa kagame anashinda kwa % 99.
Huku wapinzani wakiuliwa na kupotezwa.
 
Mtaongea Yote Ila Shida za Wakongomani zinaletwa na west wakubwa wa dunia wananjaa na madini (resources) Njia inayotumika (Divide & Rule). Unafikiri Rwanda anapata wapi kiburi yote hiyo kufadhili M-23? Anaback up kubwa ya mabepari PK anakuambia Usiponikaribisha NitajikaribishaMwenyewe.
 
Kama Kagame pia anavyoshinda kwa 99.99% na kuua wapinzani wake, tabia hizo Magufuli alijifunza kwa KAGAME.
Hiyo 99.99% inawezekana kwasababu Kagame kaleta Amani ambayo haijawahi kuonekana Rwanda mimi nimeshawahi kuishi Rwanda ya Habyarimana ilikuwa hakuna Amani kama hii ya sasa.

Wanyarwanda wanajua nini maana ukosefu wa Amani ndio maana wanampenda Kiongozi wao.
 
Nataka nite Neno hapa maaana uchaguzi ule nilikuwepo kule na nilikua sehemu ya waangalizi wakujitolea mjini Likasi

Ila naona UZI unapotea njia
 
Hiyo 99.99% inawezekana kwasababu Kagame kaleta Amani ambayo haijawahi kuonekana Rwanda mimi nimeshawahi kuishi Rwanda ya Habyarimana ilikuwa hakuna Amani kama hii ya sasa.

Wanyarwanda wanajua nini maana ukosefu wa Amani ndio maana wanampenda Kiongozi wao.
Hahahaha,Ina maaana hkn mwingine atakaye simamia Aman , Rwanda zaidi ya Kagame?
 
Katumbi ndio anafaa kuwa raisi wa Kongo DRC.
Nyinyi mashabiki wa Rwanda mnajulikana kwa kutaka Katumbi aongoze nchi, na akiwa Rais bado mtampinga mtaunga mkono mpinzani. Mobutu mlimpinga, mkaja na Laurent Kabila baadae mkampinga, Kabila Jr hamkumtaka, kaja Felix hamumtaki. Hata wakija hao Katumbi au Fayulu mnaofagilia sasahivi bado mtasema hamuwataki.

Sasa ikitokea raia wa nje anapendekeza nani awe Rais pale Rwanda, Kagame hufura. Kwanini msipendekeze nani aongoze Rwanda?
 
Uchaguzi wa Congo DRC wa mwaka 2018 ulikuwa ni fursa ya dhahabu ya Congo kurekebisha mambo mengi sana na kuipa nchi hiyo muelekeo sahihi wa kitaifa kwa mara ya kwanza ila uroho wa madaraka wa Kabila kulinda maslahi yake na kutoheshimu matakwa ya raia ukaikosesha Congo fursa hiyo.

Katika uchaguzi wa DRC wa mwaka 2018 ni wazi kwamba Martin Fayulu alishinda uchaguzi huo kwa kura nyingi sana lakini Kabila akaingilia Tume ya Taifa ya uchaguzi(CENI) kumsimika Tshisekedi aliyemuahidi atakuwa kibaraka wake.

Martin Fayulu alikuwa ni mgombea aliyeweza kuunganisha makundi mengi tofauti ya Congo, alikuwa na ushawashi mkubwa, huenda angeweza kuipa Congo ahueni kwa mara ya kwanza tofauti na Tshisekedi aliyeingizwa kwa msaada wa Kabila kupora uchaguzi.
Laana ya utajiri wa Congo
 
Back
Top Bottom