Ilikuwa ni muhimu kwa baadhi ya nchi kutawaliwa na wazungu

Ilikuwa ni muhimu kwa baadhi ya nchi kutawaliwa na wazungu

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Siwatetei Wakoloni, lakini, nafikiri kulikuwa na umuhimu wa wao kutawala baadhi ya nchi kwa kipindi hicho, hasa za Kiafrika, kama walivyofanya. Walinufaika na rasilimali za Afrika, lakini Waafrika nao hawakubaki kama walivyokuwa. Wamechangia mabadiliko chanya.

1. Walisadia kutokomeza baadhi ya mila potofu
Kwa mfano, baadhi ya makabila yalikuwa yakiamini kuwa kuzaa watoto mapacha au Zeru Zeru ni mkosi na hivyo walikuwa wakitupwa. Sheria walizozianzisha, pamoja na Elimu iliyopatikana kupitia taasisi za Kielimu na Kidini, zilisadia sana kupunguza na hata kutokomeza hizo mila mbaya

2. Elimu waliyoitoa iliwazaa "great thinkers!"
Nawataja baadhi yao: Julius K. Nyerere, Kwame Nkurumah, Robert Mugabe, Jomo Kenyatta, Nelson Mandela, Benjamin W. Mkapa, n.k. Huwa najiuliza, ikiwa Elimu ya Kikoloni ilikuwa ni dhaifu kuliko Elimu iliyotolewa baada ya Ukoloni kama tulivyokuwa tukifundishwa "mashuleni", iliwezaje kuwatengeneza Waafrika waliokuja kuwa viongozi mashuhuri duniani?

Mimi ninafikiri, pamoja na athari mbaya za Ukoloni, kuna faida pia ambazo wanafunzi huwa hawaambiwi. Wanakazaniwa tu kulishwa nusu taarifa kuwa umasikini wa Afrika ulichangiwa na Wazungu.

Viongozi, huo ni mtazamo wangu, lakini nipo tayari kuelimishwa!

Naomba kuwasilisha
 
Mtu mweusi kazi anayoweza kuifanya kwa moyo na kujitoa sana ni kupiga dili, kula michongo na kujikusanyia mali
 
Kwenye Mila potofu sawa ila kwenye ELIMU tulipigwa changa la macho.

Mtu una degree ya mipango ila huna mpango wowote....sio mpango wa kazi, biashara, utumwa, wizi, kuoa au kuolewa, sio mango wa kuokoka au kusilim , sio mpango wa kuritadi.

Yaan elimu yetu majanga
 
Mtu mweusi kazi anayoweza kuifanya kwa moyo na kujitoa sana ni kupiga dili, kula michongo na kujikusanyia mali
Hotuba ya P. W. Botha 1985 ilikuwa imesheheni matusi makubwa sana dhidi ya mtu mweusi lakini kwa "mbaali", kuna "kaukweli" ndani yake.

Alisema: "Pretoria imetengenezwa na watu weupe kwa ajili ya watu weupe..."
"... Hadi Sasa imeonekana kwa vitendo kuwa Weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama hawataanza kuuana"
"Hawana lolote jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake wengi na kupenda sana ngono. Hebu Sasa tukubali kuwa mtu mweusi ni alama ya umasikini, udumavu wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani ..."

" ... watu Weusi wanapenda sana pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo... Hawana upeo wa kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbaali..."

"... Kwa kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi kipindi cha mwaka mmoja"

Ni hotuba inayokasirisha, lakini kwa kiasi fulani, inaakisi uhalisia wa tabia ya Waafrika wengi.
 
Kwenye Mila potofu sawa ila kwenye ELIMU tulipigwa changa la macho.

Mtu una degree ya mipango ila huna mpango wowote....sio mpango wa kazi, biashara, utumwa, wizi, kuoa au kuolewa, sio mango wa kuokoka au kusilim , sio mpango wa kuritadi.

Yaan elimu yetu majanga
Shule ya Msingi tuliimbishwa:
"Tumeizika Elimu, Elimu ya Kizamani,
Elimu Ile Haramu, Maana ya Kikoloni,
Elimu Yetu ya Sasa, Yawafaa Wananchi,
Elimu Yetu ya Sasa, Yawafaa Wananchi"

Lakini baada ya kuhitimu masomo na kukumbana na msoto wa kutafuta ajira bila mafanikio na huku nina vyeti vizuri, niliukumbuka huo wimbo tuliouimba kwa bashasha, na nikahisi nao ulikuwa ni "matango pori"
 
Mzungu arudi tu. Tuna watawala vilaza zaidi ya akina Mngungo na wenzake.
 
Mzungu arudi tu. Tuna watawala vilaza zaidi ya akina Mngungo na wenzake.
Hapana! Hapana mkuu!!!
Wasirudi, ila tutafute kuwa na mapinduzi ya kifikra yatakayotufanya "viongozi" wenye tija duniani.
Waafrika wanahitaji mapinduzi ya kifikra.
 
Wazungu wasingekuwa wabaguzi na kutugawa kimatabaka Nadhani Nationalist wasingechukua maamuzi ya kulipigania bara la Afrika..ila walitugawa kimafungu sana,,waliamini mtu mweusi si lolote si chochote,,Hebu Fikiria suala la discrimination jinsi lilivyotupumbaza wa AFRICAN

Mkuu umezungumzia Hiyo Elimu ya mkoloni lakini hiyo Elimu ilikua na Effect kibao,,na hata lengo la hiyo Elimu halikulenga kutukwamua kifikra ila walikua na maslahi yao binafsi

Right kama tungemuacha Mzungu ktk hizi nchi zetu za Africa nadhani mimi nawewe huenda tusingekuwepo hapa mjini,,,pengine tungekua mashambani huko tuna henya....
 
Hotuba ya P. W. Botha 1985 ilikuwa imesheheni matusi makubwa sana dhidi ya mtu mweusi lakini kwa "mbaali", kuna "kaukweli" ndani yake.

Alisema: "Pretoria imetengenezwa na watu weupe kwa ajili ya watu weupe..."
"... Hadi Sasa imeonekana kwa vitendo kuwa Weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama hawataanza kuuana"
"Hawana lolote jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake wengi na kupenda sana ngono. Hebu Sasa tukubali kuwa mtu mweusi ni alama ya umasikini, udumavu wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani ..."

" ... watu Weusi wanapenda sana pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo... Hawana upeo wa kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbaali..."

"... Kwa kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi kipindi cha mwaka mmoja"

Ni hotuba inayokasirisha, lakini kwa kiasi fulani, inaakisi uhalisia wa tabia ya Waafrika wengi.
Ni ubishi tu lakini alikuwa sawa. Mpe Tanzania Makaburu ndani ya miaka ishirini itakuwa kama Ulaya.

Mtanzania atakuletea visingizio vitupu. Umeme, maji, barabara, masoko, hospitali tozo na teuzi za ajabu, hatuwezi kujipanga.
 
Siwatetei Wakoloni, lakini, nafikiri kulikuwa na umuhimu wa wao kutawala baadhi ya nchi kwa kipindi hicho, hasa za Kiafrika, kama walivyofanya. Walinufaika na rasilimali za Afrika, lakini Waafrika nao hawakubaki kama walivyokuwa. Wamechangia mabadiliko chanya.

1. Walisadia kutokomeza baadhi ya mila potofu
Kwa mfano, baadhi ya makabila yalikuwa yakiamini kuwa kuzaa watoto mapacha au Zeru Zeru ni mkosi na hivyo walikuwa wakitupwa. Sheria walizozianzisha, pamoja na Elimu iliyopatikana kupitia taasisi za Kielimu na Kidini, zilisadia sana kupunguza na hata kutokomeza hizo mila mbaya

2. Elimu waliyoitoa iliwazaa "great thinkers!"
Nawataja baadhi yao: Julius K. Nyerere, Kwame Nkurumah, Robert Mugabe, Jomo Kenyatta, Nelson Mandela, Benjamin W. Mkapa, n.k. Huwa najiuliza, ikiwa Elimu ya Kikoloni ilikuwa ni dhaifu kuliko Elimu iliyotolewa baada ya Ukoloni kama tulivyokuwa tukifundishwa "mashuleni", iliwezaje kuwatengeneza Waafrika waliokuja kuwa viongozi mashuhuri duniani?

Mimi ninafikiri, pamoja na athari mbaya za Ukoloni, kuna faida pia ambazo wanafunzi huwa hawaambiwi. Wanakazaniwa tu kulishwa nusu taarifa kuwa umasikini wa Afrika ulichangiwa na Wazungu.

Viongozi, huo ni mtazamo wangu, lakini nipo tayari kuelimishwa!

Naomba kuwasilisha
Wazungu wanapaswa kuja kuendelea walipoachia.
 
In the near future kutakuwa na WASHINGTON DC CONFERENCE,,, kugawana AFRIKA kwa mara nyingine tena, halafu safari hii WAFRIKA ndo watachagua WAKOLONI wao wenyewe...
 
Ni
Hapana! Hapana mkuu!!!
Wasirudi, ila tutafute kuwa na mapinduzi ya kifikra yatakayotufanya "viongozi" wenye tija duniani.
Waafrika wanahitaji mapinduzi ya kifikra.
Ni kweli, lakini itahitajika gharama kubwa sana ya muda na hata maisha ya watu. Maana mfumo tulionao umesha jiambukiza kwenye DNA zetu.
 
Ni ubishi tu lakini alikuwa sawa. Mpe Tanzania Makaburu ndani ya miaka ishirini itakuwa kama Ulaya.

Mtanzania atakuletea visingizio vitupu. Umeme, maji, barabara, masoko, hospitali tozo na teuzi za ajabu, hatuwezi kujipanga.
Mkuu Charles177, mbona miaka 20 ni mingi sana?

Kwa rasilimali tulizo nazo, na kiwango cha Sayansi na Teknikojia iliyofikiwa duniani, miaka 10 tu ya "useriousness" yanatosha kuibadili Tanzania kabisa.

Ilimchukua miaka mingapi Mcanada, Dr. Williamson kuujenga mji wa Mwadui? Inasemekana kampuni ya Almasi ya Mwadui ilianzishwa mwaka 1940, lakini kufikia 1947, kupitia uwekezaji alioufanya, alikuwa ameshafanikuwa kupafanya Mwadui miongoni mwa miji ya kisasa Afrika.
 
Back
Top Bottom