Ilkuwaje baada ya kubadilisha mazingira ya utafutaji na ukajutia kutoka sehemu ulipokuwepo? Toa ujuzi wako hapa tupate nguvu

navigator msomi

Senior Member
Joined
May 8, 2018
Posts
188
Reaction score
224
Wakuu ni takribani wiki kadhaa nilkuja na uzi wa kuhamia mwanza, niseme tu ukweli tangu nimefika hapa jijini sijawahi kupaelewa katika harakati zangu.

Mbaya zaidi sehemu nilipokuepo mwanzo nishaondoa rasilimali zote nikahamishia huku.

Kila kitu naona hakiendi, mtaji niliokuja nao naona unazidi kukata na nisjue kipi chakufanya mpaka saizii.

Najua hii sio new experience kwa wengi wetu, jaribu kushare uliwezaje ku copy mazingira kwa uharaka na kuacha kuwaza sana sehemu ulipotoka na kuona kama ulifanya maamuzi yasio sahihi kuhama.!

Pia Soma: Mwanza mshikaji wenu nimetia mguu, nipeni ramani

Pia Soma: Ni ipi sehemu nzuri ya kuanzia maisha kati ya Kibaha mjini na Mwanza kwa mtaji wa milioni 10
 
Changamka uko uliko usitizame nyuma
Kama unekaa sehem moja miaka na ujafanikiwa hama
 
Nilikatwa bogi juu kwa juu nikapelekwa det moja rusumo huko balaa tu
 
Usiache kazi kabla ya kusaini mkataba wa kazi mpya,mm nliacha kazi kwenye Ile media house Kwa mbwembwe na kejeli kuwa waendelee kupokea 150k zao,mm naenda kula 500k,nikachana mkataba nikatimua mkoani.
kufika tu ofisini jumatatu asbuhi nikiwa namatumaini lukuki wakaja TCRA wakasema wametumwa Hela na Magu kwa hiyo chimbo lifungwe mpaka deni la million 800 lilipwe.
Basi bwana nikakaaa miaka miwili Hadi magu kafa ndio nimekuja Anza kazi na mshahara wa kichumba Kinoma kisa makato na mashono...najuuuta.
 
KUWA MVUMILIVU . MIMI NILIVOTOKA USA 2006 NILIJIKUTA NAANZA UPYA KWENYE NCHI YA CCM MPAKA NIMECHOKA
 
Hapo hadi huo mtaji uishe kabisa maana hiyo ilikuwa ni pesa ya kuendeleza kule ulipotoka sasa wewe ukakimbia nayo kwenda mwanza,

Ikimalizika hiyo pesa,hapo ndio utakuwa umeingia mwanza rasmi na tayari katika upambanaji mechi itakuwa 0-0 ukitoboa hapo sasa ndio utakuwa kidume

Kuja na mtaji mkononi ni sawa na kuja kwenye mechi na goli la ugenini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…