Imani juu ya kurogana ndiyo imefanya wabantu kuwa jamii maskini zaidi duniani

Imani juu ya kurogana ndiyo imefanya wabantu kuwa jamii maskini zaidi duniani

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Kuna mama mmoja aliandikwa kwenye gazeti, aliunguliwa na nyumba huko SA. Akaanza kulalamika. "Sina ugomvi na mtu, nashangaa kurogwa namna hii." Yaani anaamini moto umeletwa ma wachawi. Mbantu akiumwa anaamini kuwa amerogwa anaenda kuagua, wakati mwenzie mmasai anaenda porini kutafuta miti shamba.

Mwingine anasema, "Lambalamba lazima aje, wachawi wamezidi kututesa. Mtu unalima hadi vinakomaa hauumwi, ukivuna tu unaanza kuumwa. Ukishatumia mavuno yote kujitibu ndiyo unapona."

Imani za kishirikina kwa wabantu hadi kwa waliopita shule zimejaa, "daktari asipoona ugonjwa kwa sababu uwezo wake mdogo utasikia anasema jaribu mambo ya kienyeji."


Mbantu biashara ikienda vibaya anaamini karogwa, mmoja juzi kati namwambia business imeenda hovyo, anasema, "Au mambo ya uchawi!"

Wakati mzungu anahangaika na teknolojia ya kuchimba dhahabu, mbantu anahangaika na waganga wa kienyeji. Mahindi shambani yasipokomaa, badala ya kuangalia quality ya udongo nk, anaamini karogwa.

Unakuta barabara ni mbaya na sehwmu hiyo ni mbaya, ajali Ikitokea mara kwa mara, mbantu anaamini kuna uchawi!

Imani hii kuwa matatizo yanaletwa na wachawi ipo kwa wabantu tu. Pengine ndiyo maana wabantu ndiyo watu maskini zaidi duniani. Wabantu suluhisho ya matatizo yao ni kuagua na mbinu zingine za kichawi. Utamaduni unaamua kwa kiasi kikubwa mafanikio ya jamii fulani, inawezekana adui mkubwa wa maendeleo ya wabantu ni hii imani yao juu ya uchawi. Imani hii inaendesha maisha yetu, hatuumizi kichwa kutatua matatizo bali tunaenda kuagua.
 
Tuache na utamaduni wetu...Kuna maana gani kuwa na mamisitu yote haya halaf tusirogane..miti ya nini sasa? Mtu akikudhulumu na mahakamani hakuna haki unataka nikashtaki wapi? Mtu akinichukulia mke na amenizidi uwezo wa kipesa unataka nipambane nae aje? Tuache na mambo yetu
 
Uchawi sio kuroga tu hata roho mbaya,kuumia wengine wakifanikiwa au kufurahia majanga ya wengine ndio uchawi wa Watanzania kuliko hata hao wabeba tunguri.
Na uchawi huo inasababishwa na umaskini, na maskini wengi ndio wachawi.
N. B uchawi upo na utaendelea tu kuwepo Hadi mwisho wa dunia.
 
Kuna mama mmoja aliandikwa kwenye gazeti, aliunguliwa na nyumba huko SA. Akaanza kulalamika. "Sina ugomvi na mtu, nashangaa kurogwa namna hii." Yaani anaamini moto umeletwa ma wachawi. Mbantu akiumwa anaamini kuwa amerogwa anaenda kuagua, wakati mwenzie mmasai anaenda porini kutafuta miti shamba.

Mwingine anasema, "Lambalamba lazima aje, wachawi wamezidi kututesa. Mtu unalima hadi vinakomaa hauumwi, ukivuna tu unaanza kuumwa. Ukishatumia mavuno yote kujitibu ndiyo unapona."

Imani za kishirikina kwa wabantu hadi kwa waliopita shule zimejaa, "daktari asipoona ugonjwa kwa sababu uwezo wake mdogo utasikia anasema jaribu mambo ya kienyeji."


Mbantu biashara ikienda vibaya anaamini karogwa, mmoja juzi kati namwambia business imeenda hovyo, anasema, "Au mambo ya uchawi!"

Wakati mzungu anahangaika na teknolojia ya kuchimba dhahabu, mbantu anahangaika na waganga wa kienyeji. Mahindi shambani yasipokomaa, badala ya kuangalia quality ya udongo nk, anaamini karogwa.

Unakuta barabara ni mbaya na sehwmu hiyo ni mbaya, ajali Ikitokea mara kwa mara, mbantu anaamini kuna uchawi!

Imani hii kuwa matatizo yanaletwa na wachawi ipo kwa wabantu tu. Pengine ndiyo maana wabantu ndiyo watu maskini zaidi duniani. Wabantu suluhisho ya matatizo yao ni kuagua na mbinu zingine za kichawi. Utamaduni unaamua kwa kiasi kikubwa mafanikio ya jamii fulani, inawezekana adui mkubwa wa maendeleo ya wabantu ni hii imani yao juu ya uchawi. Imani hii inaendesha maisha yetu, hatuumizi kichwa kutatua matatizo bali tunaenda kuagua.
Kuwa makini mkuu umegusa kijiji
 
Tuache na utamaduni wetu...Kuna maana gani kuwa na mamisitu yote haya halaf tusirogane..miti ya nini sasa? Mtu akikudhulumu na mahakamani hakuna haki unataka nikashtaki wapi? Mtu akinichukulia mke na amenizidi uwezo wa kipesa unataka nipambane nae aje? Tuache na mambo yetu
Kwamba unaroga nyumba yake inaungua au gari yake inapata ajali?
 
Uchawi sio kuroga tu hata roho mbaya,kuumia wengine wakifanikiwa au kufurahia majanga ya wengine ndio uchawi wa Watanzania kuliko hata hao wabeba tunguri.
Na uchawi huo inasababishwa na umaskini, na maskini wengi ndio wachawi.
N. B uchawi upo na utaendelea tu kuwepo Hadi mwisho wa dunia.
Kwamba mtu anarogwa anaanza kuumwa? Ni wabantu tu ndiyo tunaamini hii kitu. Jamaa mmoja tulipanga wote, akaniambia, "Kuwa makini, maza house siyo mtu poa. Usishangae kuona pesa zinapotea bila kujua!!"

Kwahiyo mtu anaacha kupanga bajeti au kutafuta pesa inapopotelea anaridhika kuwa mazahouse ananipiga kichawi. Hili limeturudisha sana nyuma.
 
Back
Top Bottom