Imani potofu huchangia sana umaskini

Imani potofu huchangia sana umaskini

Kuna mtoto wa jirani mtaa wa pili kamezoea kila nikipita kakiniona lazima kanipungie, japo hajawai kuniona ana kwa ana basi tu hivyo.

Kakiona gari kanaikimbilia na kuipungia. Sasa leo nimepita kwa mguu nilivokaona nikakaita, nikamuuliza jina na ufaham wa hapa na pale. Lakini kakaniomba hela kakadai kana njaa hawajala, mama yao kaenda kwenye kibaruani (ni mtoto km miaka minne ivi).

Basi nikamuita mkubwa wake ambae ana umri km miaka 8,9 ivi nikaenda nako dukani nikamuemelea mchele, sukari, mafuta, chumvi, na mahitaji muhimu ya kula. Nikampandisha kwenye boda ninaemfahamu na kunifahamu akampereka nyumbani.

Nashangaa boda huyo ananipigia simu eti kamkuta mamake mtoto karudi yuko nyumbani, amekataa kupokea huo mzigo eti siku izi watu wanachukua nyota za watu kupitia misaada izo, kanamwambia boda arudi navyo.

Kwaio ananihisi huo msaada wangu una lengo lake.
Kwa mazingira ya hiyo familia na hivyo huyo mtoto alivyonambia ana njaa ndo ikanishawishi nimsaidie na ni kweli alionekana ana njaa,na niliplan kumfanyia mengine zaidi. Na si kwamba mamake hanifahamu, ananifahamu.

Kwanini maskini ukimpa kitu cha bure anahisi ni mtego na ukimwambie akilipie anaona ni gharama au unataka umuibie!?

Nimelishangaa sana hili.
Umekosea kufanya mambo makubwa na watoto.

Umekosea kuingilia mambo ya nyumba ya watu. Hapo huyo mama kamanangekuwa na mumewe au bwana wake ungeweza kupewa kesi ya kuingukia unyumba wa watu.
 
Kuna mtoto wa jirani mtaa wa pili kamezoea kila nikipita kakiniona lazima kanipungie, japo hajawai kuniona ana kwa ana basi tu hivyo.

Kakiona gari kanaikimbilia na kuipungia. Sasa leo nimepita kwa mguu nilivokaona nikakaita, nikamuuliza jina na ufaham wa hapa na pale. Lakini kakaniomba hela kakadai kana njaa hawajala, mama yao kaenda kwenye kibaruani (ni mtoto km miaka minne ivi).

Basi nikamuita mkubwa wake ambae ana umri km miaka 8,9 ivi nikaenda nako dukani nikamuemelea mchele, sukari, mafuta, chumvi, na mahitaji muhimu ya kula. Nikampandisha kwenye boda ninaemfahamu na kunifahamu akampereka nyumbani.

Nashangaa boda huyo ananipigia simu eti kamkuta mamake mtoto karudi yuko nyumbani, amekataa kupokea huo mzigo eti siku izi watu wanachukua nyota za watu kupitia misaada izo, kanamwambia boda arudi navyo.

Kwaio ananihisi huo msaada wangu una lengo lake.
Kwa mazingira ya hiyo familia na hivyo huyo mtoto alivyonambia ana njaa ndo ikanishawishi nimsaidie na ni kweli alionekana ana njaa,na niliplan kumfanyia mengine zaidi. Na si kwamba mamake hanifahamu, ananifahamu.

Kwanini maskini ukimpa kitu cha bure anahisi ni mtego na ukimwambie akilipie anaona ni gharama au unataka umuibie!?

Nimelishangaa sana hili.
Mi naona wewe pia una imani za kishirijina. Kwa nini usimpatie fedha akanunue hitajio lake?

Huyo mama anajitambua sana. Umasukini wake haumfanyi apokee kila kitu bila kuhoji dhamira. Kuwa na shida usipoteza uhuru wako.

Huyo mama anajitambua sana. Kama ulikuwa na nia njema ungewasiliana na yeye kwanza


Lakini pia kwanni umlazimishe mtu akuamini kwa lazima?
Kwa dunia ya sasa nani atamwanini mwenzake.

Katoto kila siku kanakupungia mkono, leo umeamua kutembea kwa mguu ili usishtukiwe na jamii na ukaanza kukahoji bila ridhaa ya mzazi wake na kuamua kutatua changamoto zake bila kuwasiliana na mzazi wake , huoni kuwa unjitengenezea mazingira ya kuja kukalawiti hako katoto?

Hayo uliyofanya, chukulia yanafanywa kwako na kwa watoto wako
 
Hakuna Mtu Mwenye akili timamu atachukulia poa Msaada uletwe Kupitia mwanae.Yaani hiyo ni aibu kubwa Sana.Yaani ukiona mwanao anakuja na kitu na amepewa unatamani akitupe.Tukiwa wadogo tukiambatana na mama zetu Kwa Majirani,hata kama tuna njaa,kwa Majirani kuna msosi,mama alikuwa anapiga jicho 1 la kukwambia ukome.Utakula nyumbani.Marehem mama yangu nikiwa sekondari aliwahi niambia,Mwanangu kama Karo na Matumizi ya Shule hutapewa hapa ndani usiende Kwa Mjomba wala Kwa shangazi,vumilia Hadi utumiwe Kwa posta.Baadaye niligundaua hekima iliokuwa ndani Yake.Shule inapoisha hata ambaye hakukusaidia anaanza Kupiga mayowe tumekusomesha.Marehem Mkapa akiwa Rais hakuwa anapenda Mawaziri wawe wakitangatanga Kwa donors Kuomba msaada.Nenda straight Kwa Mkuu wa Kaya saidia.
Mkuu ratizo la vijana show off na mbwembwe vinawaharibu. Wanakosa akili ya kujiongeza.

Ukitaka kumsaidia mtu hata kama ni maskini kwanza linda dhamani ya utu wake ili usimkwaze kwa msaada wako.

Usifanya kama bingo move unamsaidia mtu chupi unaenda na makamera
 
Back
Top Bottom