Imekaaje hii, hotelini mzungu kampa paka samaki mkubwa

Imekaaje hii, hotelini mzungu kampa paka samaki mkubwa

Wazungu upande wa njaa njaa walishamalizaga tangu 1800s
 
Ila mzungu angepeleka pwani samaki wote wawili isingekua nongwa, husda ni kwa vile samaki mmoja kafanyiwa maarifa paka...ujumbe kazi sana.

Wenzetu paka ni sehem ya familia.
 
Dah maisha kweli magumu, mmeanza kuweka roho mbaya hadi kwa wanyama?
 
Wazungu wana mambo ya ajabu sana, wacha nikupe mkasa nilioshuhudia leo

Mida ya lunch leo kuna rafiki yangu kazini katutoa lunch rafiki zake twende hotelini kupiga msosi.

wakati tunapiga msosi maeneo ya wazi nyuma ya hoteli, tukawa tunamshangaa mzungu flani yupo na paka wa pale hotelini wanacheza, mzungu alikuwa anampapasa manyoya huyo paka, tulishangaa maana paka yule alikuwa wahapo hotelini hata sijui kama anasafishwaga

Sasa kumbe mda huo nadhani alikuwa kaweka order ya samaki wa kukaanga\

tukamona waiter anamplelekea samaki mbili kubwa kiasi, tukataniana mzungu ana njaa kali.

LA HAULA!!! Samaki moja aliwekwa chini kwenye kimfunikocha ndoo paka akaanza kufaidi samaki kimasihara.

Haikutosha hivyo lakini paka anapoendelea kupata hio lishe adim, mzungu alikuwa bado anamkuna kuna kichwani guju paka akiendelea kumfanyia samaki umafia

Kwa hali hii hawa wenzetu unaweza kumtoa out na kugharamia msosi wa gharama ukaishia kumuhudumia paka

Nadhani ni muda sasa sgeria ziweke wazi kuna binadamu kupata mlo mmoja tu ni kazi, yafaa angenunulia hata watu wenye shida huyo samaki kuliko kumpa paka
Haha yaonekana chakula ulichokuwa umepewa wewe offer hakifikii garama ya huyo samaki😂😂
Ni kawaida tu especially pale unapokuwa na mapenzi na wanyama. Kama sisi home wakati tupo wadogo sometimes tulikuwa tunakula ugali maharagwe lakini paka akaenda kununuliwa samaki wake na kuchanganywa na ugali akala. Mpaka kulala tunalala nae kitanda kimoja, katengewa sehemu yake ya kujisaidi (karai tumejaza mchanga) na hajisaidii sehemu nyingine.
Mapenzi juu ya wanyama ninayo mpaka sasa hivi
 
Ni kawaida tu maana hata mimi kila baada ya siku 2 au 3 namnunuliaga Paka wetu mishikaki ya buku ila waswahili huwa wanashangaa sana...
 
Wazungu wanawajali sana wanyama tofauti na sisi negroes.Hospitali tu za wanyama za wenzetu ni nzuri kuliko hata anazojinasibu kujenga dikteta wetu
 
Paka ana umuhimu sana usiku anaona vitu ambavyo wewe huoni na anakulinda bila wewe kujua!
 
Tatizo watu wamezoea mbwa koko
Wenzenu wanawapeleka hadi veterinary clinic na kuwatimizia mahitaji mengine yote ya msingi
 
Aiseee!

Yaani we umepewa ofa halafu unamwonea wivu paka ambaye naye kapewa ofa, itakuwa nawe ulitamani kupapaswa manyoya!!

Jiepushe na ofa bwa’mdogo.
_
giphy.gif
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]haki nimecheka sana asante mkuu kwa kunifanya nitanue mapafu!!
Aiseee!

Yaani we umepewa ofa halafu unamwonea wivu paka ambaye naye kapewa ofa, itakuwa nawe ulitamani kupapaswa manyoya!!

Jiepushe na ofa bwa’mdogo.
 
Mkuu kule U.S hasa hasa kule Minnesota, Wisconsin na Michagan,paka na mbwa ni watoto,ni sehemu ya familia
Kweli kuna mkaka mmoja alioaga huko. Alitusimumia kujuta kuoa mzungu, alisema akienda kutembea ukweni hawana time nae, yaani jinsi wanavyo hudumia paka wao ni tofauti wanavyo mjali yeye.muda mwingi wako busy na.paka😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom