Imenibidi...

Mrs Mtaba

Senior Member
Joined
Jan 21, 2009
Posts
104
Reaction score
6
Wanajamii za leo jamani,

Niko kwenye ndoa ya almost two years, hatuna bado mtoto na my mr. Ktk hiki kipindi chote hadi sasa ndoa kwa kweli imekuwa na ups and downs kama kawaida. Ila cha ajabu nilichokuwa na hisia nacho toka nilipoanza kuishi na mwenzangu majibu nimeyapata...ana mega nje ya ndoa tena aliye kuwa girlfriend wake wa zamani, kutokana na taarifa niliyopewa na wake za marafiki zake wakaribu. Nampenda sana my mr. ila sijui ni nini hasa kilichompelekea kuanza tena uhusioano na huyo mama maana anamzidi kama 10 years hivi. Nikitu kimeniuma sana roho kunipelekea, ss kutokumjali tena, na kuamua kuwa na boyfriend wa kuniliwaza. Je, nimefanya kosa katika hili. All the evidence i had na akaomba msamaha nimsamehe. Nilimsamehe lakini na mimi nimehakikisha nimetafuta wangu wa nje ili tu balance.
 

umefanya kosa kubwa sana!
ni sawa na kumwambia mtu NIMEKUSAMEHE LAKINI SITASAHAU.anyways,inauma sana lakini kuna kitu tunaweza kukijadili kwa kina zaidi kikatupa uelekeo mzuri wa hii mada.ni kuhusu ndoa yako kutokuwa na mtoto..........WHO IS TO BLAME?
 
Shemeji bonge la mchemsho. Huwezi kubalance kwa kufanya ulivyoamua. Kama hataki kuachana na huyo mke mwenzio,fanya hivi,mwombee kwa Mungu kama una imani,au chomoka fasta,Tunaishi mara moja.

Huyo Boyfriend wako amekwambia hana girlfriend mwingine? Cheating cheating cheating mpaka siku ya kiama.

Maisha ya ndoa ni matamu kama huna wasiwasi na mwenzio,kinyume chake ni utumwa tu.
 

hukutatua tatizo bali umeongeza tatizo. ufafanuzi baadae
 

Sasa wewe kesi ushaiamua na kutoa hukumu hapa unatafuta nini?

Yaani umekosa moral authority yote hata ya kulalamika, maana wewe na yeye hamna tofauti wote mmekosa kosa hilo hilo.

Cha kufanya ni kupima ngoma na kuamua kama mnataka kukaa pamoja mu address issues zenu au kama unataka kuanza mbele wakati ndio huu hata mtoto wa kutoa kisingizio cha "we are doing it for the children" huna.
 
MRS MTABA,
naomba nikutahadharishe pia usije ukawa unaapply directly solutions zinazotolewa na wanawake humu jamvini!watch out.most of them sio wanawake.hata kama ni wanawake wamepinda sana
 
Safi sana Mrs. Mtaba. Wala usijisikie kama una makosa yoyote. What's good for the goose should be good enough for the gander. More girl power to you. Zaidi ya hapa niPM...
 
Inasikitisha sana, sasa mkikutana jioni kila mmoja katoka kumega/kumegwa nje mnakaa mezani mnaongea au ?
 
Naona washashi washaanza kujipalilia.

Mnapotaka kula kila kitu angalieni msile "uyoga mwitu sumu"
 
Inasikitisha sana, sasa mkikutana jioni kila mmoja katoka kumega/kumegwa nje mnakaa mezani mnaongea au ?
Tena najisikia raha sana kwa kweli. Maana nilikaa chini siku moja nikajiuliza, hivi nitabadilisha mpaka lini, maana wakati wa usichana wangu nimeachana na ma boyfriend kama wanne kwa kosa hilo hilo. Ss hata nikienda kwa mwingine mambo siyatakuwa hayo hayo. Sijipi presha tena, na moyo wangu umetulia sana kwa sasa.
 
Ni mume wa mtu naye, na wife wake alimdakaga anamegwa nje. Kwa hiyo naye alikuwa kwenye process za kutafuta wa kumega ndo akanipata mimi.
 

Mimi nimeuliza kama huwa mnaongea,sijasema presha au kutulia,narudia huwa mnachati kama vile hakuna noma?
 
Ni mume wa mtu naye, na wife wake alimdakaga anamegwa nje. Kwa hiyo naye alikuwa kwenye process za kutafuta wa kumega ndo akanipata mimi.

The risk of HIV infection is exponentially proportional to the number of partners involved in this chain.
 
Ni mume wa mtu naye, na wife wake alimdakaga anamegwa nje. Kwa hiyo naye alikuwa kwenye process za kutafuta wa kumega ndo akanipata mimi.

Imenikumbusha jamaa yangu alikuwa anakwenda msituni kukata kuni,mara gogo likaanguka mbele yake,basi jamaa akabeba na kurudi home kilaini kabisa.

Kamwaga ugali na wewe umemwaga mboga,shemeji nimekupata na kwa jinsi ulivyo wazi bila shaka umeamua kikweli kweli.
 
Oh!
1.Ulishapata kazi maana Kuna kipindi nadhani ulitaka ushauri kuhusu kuongeza kipato ...na ukawa umepata mtu wa kukusaidia ila tatizo likawa umemwambie nini mr au nimekosea?

2. Just listen to your heart Mrs Mtaba... ukiona hicho unachofanya chafaa, sisi hatuna cha kukushauri zaidi.

3.Maadam tayari ulishajitafutia solution ya tatizo lako bila kutushirikisha, sasa hivi its too late...if anything nadhani umekuja kutaka validation tu ya action uliyochukua na humu utapata maoni genuine na ya kinafiki.

Hata kwenye fani ya ushauri, mshauri anachokifanya ni kukupa options mbalimbali na wewe unachagua ile inayokufaa.JF kuna washauri wengi, na maoni kama unavyoona yametolewa mengi.Uamuzi wa njia ya kuchukua mamaa ni wako.
 
Mimi nimeuliza kama huwa mnaongea,sijasema presha au kutulia,narudia huwa mnachati kama vile hakuna noma?
Tunaongea tena sana, na akanza ku apply viufundi vyake baada ya kuona sijamind sana na mambo yake. In short he shows responsibility more than before. Ila imani sina naye tena namkodolea mimacho kama kobe tuu.
 
One more reason not to get married in the first place and avoid all this drama.
 

nilidhani ulikuwa unataka ushauri lakini kumbe tayari unaufurahia uamuzi uliouchukua. ulijiuliza utabadilisha mpaka lini, lakini je umejiuliza huo mchezo unakupeleka wapi?

quiet
 
Tunaongea tena sana, na akanza ku apply viufundi vyake baada ya kuona sijamind sana na mambo yake. In short he shows responsibility more than before. Ila imani sina naye tena namkodolea mimacho kama kobe tuu.

Kwa vile keshakiuka imani yako kwake itakuwa vigumu sana kumwamini tena. Hivyo mimi naunga kwa mkono na mguu uamuzi uliouchukua na utakaouchukua hapo siku za usoni...wink wink
 
Sio pendekezo langu, nimisukumo ya hapa na pale. Life is short everyone needs to enjoy it.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…