IMF: Kasi ya Ukuaji wa Uchumi wa Uganda Kufikia 11% Kuanzia Mwaka 2025 Baada ya Pesa za Mafuta Kuanza Kumiminika

IMF: Kasi ya Ukuaji wa Uchumi wa Uganda Kufikia 11% Kuanzia Mwaka 2025 Baada ya Pesa za Mafuta Kuanza Kumiminika

Uongo
Wakati magufuli anaingia uchumi ulikua kwa 6% , na uliendelea hiyo 6% mpaka ule mwaka wa Corona 2020 ndio ukadrop sababu ya Corona

Lakini pia nakupa angalizo kuwa na growht rate kubwa sio issue, Ethiopia wamekua na growth kubwa kwa miaka zaidi ya 10 but bado wanapumulia mashine
Wanapumulia mashine kivipi!?.. growth rate ya USA ikiwa 0.5% hiyo inakua ongezeko kubwa kuliko 3%+ ya tz,lakini kudai growth rate kuwa kubwa au laa haina maana,ni ujinga
 
Shirika la Fedha za Kimataifa IMF imesema Uchumi wa Uganda utaanza kupata Ukuaji mkubwa kuanzia mwaka 2025 ambapo Kasi ya Ukuaji wa Uchumi itaongezeka kutoka asilimia 6.2% mwaka 2024 na kufikia asilimia 10.8% kuanzia mwaka 2025.

Ukuaji huo utachangiwa na kuanza Kumiminika Kwa pesa za mauzo ya Mafuta mwishoni mwa mwaka 2025.

Kasi hii kubwa ya Uchumi wa Uganda itakuza Ukubwa wa Uchumi wa Nchi hiyo kutoka GDP ya $ 49bln (2024) Hadi GDP ya $ 120bln (2035) ambapo Wachambuzi wa Uchumi wanasema Uchumi huo utalingana Kwa Ukubwa na Tanzania.👇👇

View: https://x.com/Reuters/status/1834128627794931796?t=rBXwRZpnNB7hhcOWwp-hJQ&s=19


My Take
Kuna haja ya Tanzania kwenda kujifunza Kwa Ethiopia iliwezaje kukuza Uchumi wake Kwa double digit Kwa miaka 10 na kuzipita Kenya,Angola na Sudani kuwa Baba wa Uchumi Afrika Mashariki huku hawana Mafuta Wala gesi.
View attachment 3097657

Vinginevyo Tanzania tutapitwa na Uganda Kwa Ukubwa wa Uchumi (GDP size) baada ya mwaka 2035.

Nchi zote ambazo zilipata maendeleo makubwa ni zile ambazo Uchumi wake uliwahi kujua Kwa double digit yaani kuanzia 10% Kwa miaka 10 mfululizo Duniani kote ndipo zilipunguza umaskini Kwa nusu vinginevyo Hali itazidi kuwa tete.

Hii growth rates ya 4-7% ambayo tumekuwa nayo Kwa miaka zaidi ya 15 haijawahi na Wala haitakuja saidia kuondoa umaskini 👇👇

View: https://x.com/TanzaniaInvest/status/1833424456926044371?t=OuBdrDykvfYDPafDjZrbMg&s=19

Pia soma World Bank: Rwanda, Uganda na DRC zitaongoza kwa Kasi ya Ukuaji wa Uchumi Afrika Mashariki. Tanzania kushika nafasi ya 3.

Pia soma zaidi hapa WB: Uchumi wa Tanzania (GDP) Umeongezeka na kufikia $ 80 Bilioni mwaka 2023.


Tuendelee na hizi siasa na kujiibia wenyewe. Tuendelee na urasimu na kujidanganya mambo yote yamekaa sawa.
Anayelala usimuamshe. Ukimuamsha utalala wewe
 
Wanapumulia mashine kivipi!?.. growth rate ya USA ikiwa 0.5% hiyo inakua ongezeko kubwa kuliko 3%+ ya tz,lakini kudai growth rate kuwa kubwa au laa haina maana,ni ujinga
Growth rate utapotea tu. Achana na USA, nimekutolea mfano malawi ana growth rate kubwa kuliko nchi nyingi hapa Africa, je hali ya Malawi ni nzuri kuliko Namibia, kuliko Angola??
 
Growth rate utapotea tu. Achana na USA, nimekutolea mfano malawi ana growth rate kubwa kuliko nchi nyingi hapa Africa, je hali ya Malawi ni nzuri kuliko Namibia, kuliko Angola??
Growth rate ya malawi kuwa 12p ya marekani kuwa 0.5p haimaanishi malawi iko vizuri kuliko marekani na wala haimaanishi malawi haipigi hatua
 
Ambacho hujaelewa ni nn? Magu wakati anaingia ukuaji ulikua ni 6% na sio 7 kama ulivyosema

Pia nimekuambia hata ukuaji ukiwa 10% bado sio reflection ya Hali kuwa nzuri, nimekutolea mfano Ethiopia waliokua na ukuaji mkubwa
Hali nzuri unamaanisha nini?..kwako growth rate ya 20% na 0% ni sawa?..una shida gani wewe!?
 
Hali nzuri unamaanisha nini?..kwako growth rate ya 20% na 0% ni sawa?..una shida gani wewe!?
Hali nzuri huelewi ni nini? Kupungua kwa umaskini

Alafu hakuna niliposema growth rate ya 20 kwa 0. Tumia akili

Pia hizi mambo hakuna wa kumuongopea huku mtandaoni, wala usitumie sana nguvu
 
Growth rate utapotea tu. Achana na USA, nimekutolea mfano malawi ana growth rate kubwa kuliko nchi nyingi hapa Africa, je hali ya Malawi ni nzuri kuliko Namibia, kuliko Angola??
Kwanza umetoa wapi takwimu zinazoonesha Malawi kuwa na growth rates ya 12%? Unapenda sana kubumi mambo Yako wewe.

Mwisho nilikupa sababu za nadharia ya growth rates baina ya developed vs developing ila umekaza fuvu 👇👇
Screenshot_20240916-234425.jpg
Screenshot_20240916-234105.jpg
Screenshot_20240916-233613.jpg
 
Hizi growth rate uliwa hufahamu exactly Ni nn hutaelewa. Kwenye hizo data zako unaona hata hiyo 2012 ilidrop na kuwa 4, unahisi kwa nn ilidrop kuwa 4 wakati wa jK ambapo alianzia na 7??

Jibu utalopata hapo ndio utaelewa why hiyo 2021 ilifika pia 4.

Lakini hizi growth rate zitakumislead, sio kipimo lizuri cha nchi kufanya vizuri ndio maana unaona nchi maskini kabisa kama Malawi ana growth rate nzuri kuliko nchi nyingi sana Africa na duniani
Kipimo kizuri NJ kipi?
 
Kwa akili ya kawaida miradi yote iliyoanzishwa sehemu mbalimbali nchi kwa nguvu kubwa na bjeti kubwa inawezekana vipi hata mmoja usikamilike kwa miaka yote hii mitatu???

Kuhusu kulinganisha awamu, mbona tulijadili jana na ukasema kilimo kwa sasa kinachangia trillion 38 kwenye GDP. Nilikuwekea kwa awamu zingine zilipokua juu ya hiyo.
Wewe ni mgeni na miradi kuchukua mda mrefu? Hapo kati mvua zimekuwa nyingi mno? Utajenga miradi ya Umwagiliaji katikati ya Mafuriko ya El Nino?

Mwisho onyesha data unazodai Kilimo Kilimo kilichangia zaidi ya 38T ,weka hapa nione.
 
Wewe ni mgeni na miradi kuchukua mda mrefu? Hapo kati mvua zimekuwa nyingi mno? Utajenga miradi ya Umwagiliaji katikati ya Mafuriko ya El Nino?

Mwisho onyesha data unazodai Kilimo Kilimo kilichangia zaidi ya 38T ,weka hapa nione.
Acha uongo ,ipo miradi ya umwagiliaji iliyokamilkka na watu wananufaika nayo kwa sasa. Hizo mvua haziewezi kufanya miradi yote usikamilike kwa miaka mitatu

Kuhusu kilimo kuchangia kwenye GDP Hilo tulijadili,leo tunarudia Tena? Kwa Sasa umesema kilimo kinachangia 26% ya GDP. Basi angalia kwa miaka hiyo kilimo kilikua kinachangia percent ngapi kwenye GDP
 

Attachments

  • Screenshot_20240916-224224_1.jpg
    Screenshot_20240916-224224_1.jpg
    165.9 KB · Views: 1
Back
Top Bottom