Sera ya kijamaa uliona wapi ikafanikiwa ndo maana ujamaa uliporomoka, lakini huyo unayemsema alikuwa anavaa suti lakini ww humtendei haki mkuu Wa awamu ya nne! Kaweza kuunganisha barabara nchi nzima, kakujengea hospital ya moyo badala ya kupekeka wagojwa india ss hv ni hapahapa, kakujengea daraja la kigamboni badala ya kupiga mbizi tunasafiri kwa raha zetu ,wananchi wakiendelea na ujenzi nyumba za makazi kila kona ya nchi, katuletea umeme wa gesi na ss hv mgao umeme hakuna japo kuna matatizo madogo madogo ya kiutendaji wa shirika let, kaleta kampuni kubwa ya simenti ya dangote, katujengea hospital kubwa ilonganzila, ameweza kuongeza mishahara kwa watumishi wa uma kila mwaka na kumudu kuwalipa wafanyakazi hewa wote nchini na aliweza kuajiri watumishi kila mwaka! Na cha kupongezwa zaidi kama nilivyosema mwanzo keki ya taifa tuliigawana wote na kila mtu alikuwa na hela mfukoni na jioni unapata bia zako mbili unaenda kulala safii, na mwisho katuletea jembe letu magu ila tu azitoe hizo hela benki kuu tunazihitaji mtaani maana kwa sasa mambo hayaendi ushahidi ss hv hakuna anayejenga jengo jipya hivyo maendeleo yamesimama kote nchini, hizo pesa rais wetu azitoe benk kuu abaki na hela yake ya matumizi vinginevyo tutaisoma namba nchi nzima haijalishi ww uko wapi!