Pre GE2025 Inahitaji akili kubwa kiasi gani kuelewa kwamba kwa kuwa Zanzibar wana serikali na Rais wao, Rais wa Tanzania, kimsingi, ni Rais wa bara?

Pre GE2025 Inahitaji akili kubwa kiasi gani kuelewa kwamba kwa kuwa Zanzibar wana serikali na Rais wao, Rais wa Tanzania, kimsingi, ni Rais wa bara?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nchi hii uhitaji akili, unahitaji majeshi yawe upande wako, unafanya chochote utakacho.

Akili nchi hii za nini, utazitumia wapi, ccm wamezagaa kila kona maofisini?

Muda wa kutumia akili ukifika hutauliza swali kama hili.
 
Jibu ni moja tu katika point zako zote hapo juu, ambalolitakuja kama swali. Je wewe ulijua Magufuli angekufa na Samia kuwa raisi wa Tanzania badala yake?
Hahaaaa! Mkuu unauliza au unahoji mambo ambayo yako wazi. Sikujua kwamba Magufuli angekufa siku ile kwani hiyo ni siri anayoijua Mungu tu, kwa wale wanaoamini Mungu. Ama la Samia kuwa rais nilijua kwani katiba inaelekeza hivyo. Nisingeelewa iwapo Samia, baada ya kifo cha Magufuli, asingekuwa rais kwani huko kungekuwa ni kuvunja katiba.

Kumbuka: Tunapozungumzia Tanzania tunazungumza sheria na siyo porojo za vibarazani kama hivi unavyofanya wewe.
 
Hahaaaa! Mkuu unauliza au unahoji mambo ambayo yako wazi. Sikujua kwamba Magufuli angekufa siku ile kwani hiyo ni siri anayoijua Mungu tu, kwa wale wanaoamini Mungu. Ama la Samia kuwa rais nilijua kwani katiba inaelekeza hivyo. Nisingeelewa iwapo Samia, baada ya kifo cha Magufuli, asingekuwa rais kwani huko kungekuwa ni kuvunja katiba.

Kumbuka: Tunapozungumzia Tanzania tunazungumza sheria na siyo porojo za vibarazani kama hivi unavyofanya wewe.
Nimekusikia Mkuu, na nadhani labda hujanielewa. Nasikitika maana nimeanza kwa kueleza mazingira yaliyotuleta hapa, nikisema tunafanya kazi kwa mazoea na wishful thinking, na bila kukubali reality. Kwa mfano wewe umeandika wosia, will? Kwa nini hujaandika kama hujaandika?

Kwa hiyo ndio maana nikasema tuko kwenye jambo ambalo hatukutarajia wala kutegemea. Na jambo la msingi hapa ni kwamba Raisi Samia sio raisi kwa sababu tulimuona kuwa ana sifa za kuwa raisi wa Tanzania. Tuwe wakweli, katika hali ya kawaida, katika kuteua mgombea uraisi wa Tanzania, CCM wasingemteua Samia hata siku moja, na kama wangempima kama ndie anafaa au la kuwa raisi, wangeona hapana, sio yeye.

Samia amekuwa raisi kwa bahati tu, kufa kufaana, sio kwa kuwa tangu mwanzo alionekana kuwa na sifa ya kuwa raisi wa Tanzania. Na hata kama angeonekana anafaa, kutoka kwake Zanzibar kungekuwa kikwazo, hasa ukijua suala la kupokezana uraisi kati ya bara na visiwani siku hizi halipo tena kwenye Katiba. Linaweza kuwa halijaandikwa kuwa raisi wa Tanzania atatoka bara, lakini uwezekano wa kwamba CCM wangeteua mgombea wa uraisi toka visiwani ni mdogo mno, almost non-existent. Hebu fikiria, hata CCM wangetaka mgombea mwanamke, katika orodha yao ya wanawake vigogo wa CCM, bara na visiwani, Samia angekuwa na chance gani katika hiyo list kuwa raisi wa Tanzania?

Sasa Samia alifaa kuwa mgombea mwenza wa Magufuli, na sio raisi wa Tanzania. Sifa za mgombea mwenza, nikuibie siri, sio kwamba ni yule aliye na uwezo wa kuwa raisi ikiwa raisi atakufa, kwa sababu hakuna anaefikiria raisi atakufa wakati wa kuteua mgombea mwenza. In fact, mgombea uraisi kuna wakati atapendekeza mgombea mwenza ambae hataonekana kuwa na uwezo zaidi yake ili isije ikatokea makamu wa raisi anam-overshadow raisi. Kwa hiyo inawezekana Samia aliteuliwa pale kwa sababu alionekana hatakuwa tatizo kwa Magufuli, atakaa kimya na kando, akisubiri kuambiwa nini cha kufanya. Na ndivyo ilivyokuwa akiwa Makamu wa Raisi, Magufuli did not even bother to consult her kwenye maamuzi yake, kwa sababu alijua hakuwekwa pale kwa ajili ya kuwa smart leader wa kuwa consulted na raisi katika kufanya maamuzi. Alikuwepo kuwepo tu, for when it was convenient for her to show her beautiful face to the public. Kama Magufuli angekuwa anam-consult Samia, huenda Tundu Lissu asingepigwa risasi, Ben Saanane asingepotea, nk. Huo ndio ukweli.

Sasa yote haya ndio yamefanya niandike hii thread. Ni ukweli ambao inaonekana hupendi kuusikia.
 
Hiyo ni suluhu ya muda mrefu, lakini kwa sasa tunahitaji suluhu ya haraka, na nina uhakika Samia akijitoa uchaguzi wa 2025 itasaidia sana

..una hoja nzuri, lakini sijui kwanini hutaki kutaka jina TANGANYIKA.
 
..una hoja nzuri, lakini sijui kwanini hutaki kutaka jina TANGANYIKA.
Ni hivi Mkuu, mie nadhani hoja ya Tanganyika inatokana na mambo ya muungano yanavyoendeshwa, na kikubwa ni Tanzania bara "Tanganyika" kuona kwamba muungano huu unatumiwa kuinufaisha Zanzibar ambao inaonyesha kila dalili hawautaki. Watanzania bara hawataki kuwabembeleza Wanzanzibar, na wengi wanasema hatuchukii muungano, bali tunataka usawazishwe. Aidha kuwe na serikali moja, au ziwepo tatu. Sasa hili la serikali moja Zanzibar hawataki. Na serikali mbili bila ya Tangantika huku Tanzania bara hawataki.

Sasa swali ni kwamba, ni nani anaepinga serikali tatu? Huko nyuma ilikuwa Nyerere, na sasa je? Na hao wanaopinga serikali tatu, leo hii wanapinga wazo hilo kwa nini?
 
Tatizo Tanzania na mara nyingi Afrika kwa ujumla, tumezoea kufanya mambo kwa mazoea au kwa matarajio kwamba kama leo tumekula basi hata kesho tutakula tu. Ndio maana wengi wetu mambo ya kuandika wosia hatutaki. Hatutaki kufikiri mambo mbele kiasi hicho, au kudhani tukifa leo au kesho kutakuwa ni tatizo kwa familia zetu tutakazoacha. Na mara nyingine hatudhani kama tunaweza kufa leo au kesho!

Ndio maana hili la raisi wa Tanzania katika mazingira ya Zanzibar kuwa na serikali na raisi wake, hatukulifikiria mbali, labda tukiona kwamba tulikuwa na raisi Mkapa, kisha Kikwete na baadae Magufuli, na mambo yalikuwa sawa tu. Tuliamini kwamba siku zote raisi wa Tanzania atatoka bara, japo makamu wake alitoka visiwani. Hatukuona kwamba raisi wa Tanzania anaweza kutoka visiwani ikiwa raisi aliechaguliwa toka bara atakufa akiwa madarakani na makamu wake toka visiwani akawa raisi wa Tanzania,au raisi wa bara.

Sasa, hili sasa la kuwa na raisi wa Tanzania toka visiwani lazima tukiri linatuletea matatizo mengi sana. Na chimbuko la matatizo haya ni ukweli kwamba kimsingi, raisi wa Tanzania ni raisi wa bara, na anapaswa kuwa mtu kutoka bara. Huu ndio ukweli. Na sababu mojawapo ni kwamba kwa muundo wa muungano tulio nao sasa, raisi wa Tanzania hana sauti tena na mabo ya Zanzibar.

Tukisema raisi ni wa Jamhuri yaa Muungano ya Tanzania hivyo anaweza kutoka bara au visiwani, huko ni kujidanganya. Jiulize, ni mambo mangapi ya muungano raisi Samia anaweza kuyatolea tamko ambalo itabidi raisi wa serikali ya Zanzibar atii na kutekeleza? Hakuna hata moja! Ona kwamba hata mkataba wa Tanzania na DP World haukuhisisha Zanzibar, kwa sababu raisi Samia hana mamlaka na bandari za Zanzibar japo zinasemekana kuwa chini ya muungano.

Sasa basi, kama kweli tunataka tuwe na raisi wa Jamhuri ambaye ana sauti bara na visiwani kuna mawili - aidha kusiwe na raisi wa Zanzibar, au kuwe na raisi wa Tanganyika. Na hii ndio inachochea baadhi ya watu kudai serikali ya Tanganyika.

Kama ambavyo watu hatutaki kuandika wosia, Tanzania hatukuwahi kufikiria nini kitatokea ikiwa raisi wa Tanzania toka bara atakufa, na tukiwa na makamu wa raisi toka Zanzibar anaepaswa kuchukua nafasi yake. Kama tungefikiria mbali ju ya hili, na tukijua kwamba raisi wa Tanzania ni raisi wa bara na anapaswa kutoka bara, basi tungepaswa kusema ikiwa raisi wa Tanzania atakufa akiwa madarakani, kama uchaguzi mkuu uko mbali zaidi ya miaka miwili, makamu wa raisi atakaimu nafasi ya raisi wa Tanzania katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja, ambapo ndani ya muda huo uchaguzi mdogo wa raisi utafanyika, pasipo kuwa na uchaguzi wa wabunge. Raisi mpya atakapochaguliwa, kaimu raisi ataendelea na nafasi yake ya makamu wa raisi, ikiwa raisi aliechaguliwa atatoka tena chama tawala; la sivyo kutakuwa na raisi mpya na makamu wa raisi mpya kama uchaguzi mdogo wa raisi utatoa raisi toka chama cha upinzani.

Sasa tukijua hili, na kuelekea uchaguzi wa 2025, ingependeza ikiwa Raisi Samia asigombee tena kiti cha uraisi wa Tanzania, bali CCM walete mgombea mpya kutoka bara na mgombea mwenza mpya kutoka visiwani. Najua wengi watasema ooh, Katiba haisemi hivi. Ndio, lakini CCM wakifanya hivi hawatakuwa wamevunja katiba, bali watakuwa wameinusuru Tanzania katika mitafaruku na issues nyingi zinazoendelea kutokana na uraisi wa Samia, akiwa raisi wa bara kutoka visiwani. Na kama raisi Samia ana uchungu na mapenzi na nchi hii, ni suala la yeye kusema jamani eeh, nimeamua sintagombea uraisi 2025 ili CCM ifanye mchakato mpya kupata wagombea wapya. Baadae hili linapaswa kuwekwa kwenye katiba.

Hakuna mtu asieona kwamba uraisi wa Samia analeta mitafaruku mingi mno. Kwanza watu wengi wa bara hawamwamini kwamba anafanya kazi kwa maslahi ya Tanzania bara na si Zanzibar. Pili watu wanaona anapendelea sana Zanzibar katika miradi na uteuzi. Tatu watu wanaona ameanza kutumia njia za Magufuli. Nne watu wanaona anashindwa kudhibiti viongozi mafisadi wa bara kwa sababu anataka support yao. Tano watu wanaona anaingiza sana watu wa Zanzibar kwenye nafasi za kazi za bara. Sita watu wanaona anatumiwa vibaya na ndugu zake toka nchi za kiarabu. Saba watu wanaona anajitajirisha sana binafsi na ndugu zake ndio maana hawezi kuwakemea viongozi mafisadi kwa sababu wanafanya anachofanya yeye, nk, nk.

Watu wengi wa bara wameanza kuona kuwa support anayopata Samia toka kwa watu wa bara ni kutoka kwa wale tu wanaofaidika na nafasi yake kama raisi wa Tanzania, watu ambao inasemekana wako tayari hata kuteka na kuua Watanzania wenzao ikiwa wataonekana kupinga utawala wa raisi Samia. Sasa hali kama hii si sawa kwa nchi yetu, na inazidi kuharibika. Na ni wazi CCM inajua hili ndio maana wanatumia nguvu kubwa na fedha nyingi sana kumfanyia Samia kampeni, kabla hata ya uchaguzi mkuu.

Raisi Samia, kwa heshima na taadhima, nakuomba ujitoe kwenye kugombea uraisi 2025 ili tujipange upya. Uwepo wako katika nafasi ya uraisi una mambo mengi mazuri yanayoonekana, lakini mabaya makubwa mengi yasiyoonekana!
Kwa kweli Tanganyika kuongozwa na Mzanzibari hii haijakaa vizuri hata kidogo.
 
Muungano wa ovyo kuwahi kutokea duniani!
Na tutaendelea tu kusema hivi huku muungano ukiendelea kuwapo? Ni watu wa namna gani sisi hatuna uwezo wa kupata kile tunachotaka katika nchi yetu wenyewe? Tukisema hatutaki kikokotoo hiki tunalazimishwa bila kujali; tukisema mnatuonea na kodi za miamala tunalazimishwa; tukisema hatutaki bandari zetu ziuzwe tunalazimishwa; tukisema hatutaki nchi yetu iuzwe kwa waarabu tunalazimishwa; tukisema tunataka katiba tunalazimishwa kukubali hii; tukisema tunataka muungano tofauti tunalazimishwa; tukisema tujadili watu kutekwa tunalazimishwa hoja isijadiliwe.

Sisi ni nani sasa, raia katika nchi hii kweli?
 
Kwa mwendo tulio nao sasa nafikiri Samia ndiye Mzanzibari wa mwisho kuwa Rais wa Tanganyika.
 
Mim
ni wachache sana wenye uelewa mdogo wa aina hiyo ndio pekee wanaelewa hivyo unavyoelewa wewe gentleman na maoni yao yanaheshimiwa hata katika uchache wao..

Hata hivyo waTanzani wengi zaid wangependelea vifungu fulani vichache vya katiba vibadlilishwe ili kipenzi chao, Rais Dr Samia Suluhu Hassan aweze kupata nafasi zaidi aongoze nchi walau mpka 2035 na itapendeza zaid 🐒
i naamini Gentleman kama yupo mtu wa kuipatia hii Nchi Katiba mpya bora basi mtu huyo ni Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan !

Tumpe Muda !!
Mark my words 🙏🙌👍
 
Nchi hii uhitaji akili, unahitaji majeshi yawe upande wako, unafanya chochote utakacho.

Akili nchi hii za nini, utazitumia wapi, ccm wamezagaa kila kona maofisini?

Muda wa kutumia akili ukifika hutauliza swali kama hili.
Duh 🙄 !
 
watanganyika ni wabinafsi sana, yani wao kuwatawala wazanzibari wanahisi ni haki yao, ila wao kuongozwa na mzanzibari wamevurugwa sana.
 
Hiyo ni suluhu ya muda mrefu, lakini kwa sasa tunahitaji suluhu ya haraka, na nina uhakika Samia akijitoa uchaguzi wa 2025 itasaidia sana
Mkuu 'Synthesizer', sikutaka kutoa maoni kwenye mada yako hii, lakini nashindwa kujua hii dhana yako hasa unaitoa wapi kiasi cha kuing'ang'ania hivi!
Hivi kweli unaandika ukiamini kuwa Samia anaweza akaamua tu hivi hivi kujitoa kwa hivi vimaneno ulivyo weka kwenye mada?
Hata huko ndani ya CCM wanajuwa; hakuna mwenye uthubutu wa kuanza kusema maneno ya Samia asigombee.

Ninge kuelewa kama unge ielekeza mada yako hii kwa waTanganyika, wakatae kuongozwa na raia wa nchi nyingine yenye madaraka kamili.
WaTanganyika wakiyaelewa vizuri unayo zungumzia kwenye mada yako, wanao uwezo kamili wa kumkataa Samia na hata hiyo CCM yake ikilazimisha agombee.
 
Mkuu 'Synthesizer', sikutaka kutoa maoni kwenye mada yako hii, lakini nashindwa kujua hii dhana yako hasa unaitoa wapi kiasi cha kuing'ang'ania hivi!
Hivi kweli unaandika ukiamini kuwa Samia anaweza akaamua tu hivi hivi kujitoa kwa hivi vimaneno ulivyo weka kwenye mada?
Hata huko ndani ya CCM wanajuwa; hakuna mwenye uthubutu wa kuanza kusema maneno ya Samia asigombee.

Ninge kuelewa kama unge ielekeza mada yako hii kwa waTanganyika, wakatae kuongozwa na raia wa nchi nyingine yenye madaraka kamili.
WaTanganyika wakiyaelewa vizuri unayo zungumzia kwenye mada yako, wanao uwezo kamili wa kumkataa Samia na hata hiyo CCM yake ikilazimisha agombee.
Mkuu Kalamu nakuelewa sana. Samia kama mwanadamu huenda anapenda kuwa raisi. Madaraka ni matamu sana kwa wengi, na hata zaidi kwa wengine hadi wanafikia kuua wanaoonekana kuwa tishio la uraisi wao. Lakini pia kuna watu wazalendo wa kweli wanakuwa wanapenda kuwa maraisi kwa ajili ya upendo kwa nchi zao. Sasa sijui hili kama limo katika moyo wa Samia, kwamba niko tayari kufanya jambo kama hili kwa ajili ya kile ninachoona ni kwa manufaa ya Tanzania.

Ndio maana nikasema, "Na kama raisi Samia ana uchungu na mapenzi na nchi hii, ni suala la yeye kusema jamani eeh, nimeamua sintagombea uraisi 2025 ili CCM ifanye mchakato mpya kupata wagombea wapya. Baadae hili linapaswa kuwekwa kwenye katiba"

Asisubiri CCM wamuamulie, au watu fulani ndani ya CCM wamkatae, kwa sababu hilo litaleta mgawanyiko hata zaidi. Aamue yeye mwenyewe kwa utashi wake, kwa manufaa ya Tanzania, akiamini kuwa kama CCM bado itatoa raisi, sio kwamba yeye peke yake ndio mwenye uwezo wa kuwa raisi. Wapo wengine ambao wanaweza kuwa bora kuliko yeye. Akikubali hili atakuwa ni mnyenyekevu na mzalendo wa kweli.
 
Back
Top Bottom