Inakuwaje kamanda mkuu wa kijeshi Urusi anakuwa chini ya Wagner Group, kikundi kidogo cha kukodi?

Ungejua hao wagner group ni wakina nani wala usingeuliza hilo swali lako la kipumbavu. Baba hao watu ni hatari kuliko hatari yenyewe, hilo group linaongozwa na makomandoo wastaafu hodari sana na wanajeshi wastaafu waliokuwa mahili sana. Sasa jeshi gani linaweza likapuuza ushauri kutoka kwa watu kama wao
 
Kazi iendelee,supa pawa anaendelea kuwa supa powaaa,
Hiyo ni ishara kwamba wagner group ndo master mind wa jeshi la urusi baada ya majenerali zaidi ya 20 kulamba vumbi. Haiwezekani kumuamini mtu wa kukodi kiasi hicho.
Kumbuka kama umemkodi maana yake anatafuta pesa.
Uwe na uhakika mbaya wako akimpa pesa zaidi yako kusalitiwa ni nje nje.
 
Kama ni makini kiasi hicho kwanini walistaafu?
Angalia mkuu,swali unaweza kuliita la kipuuzi kumbe limezidi uwezo wako wa kufikiri.
 
Kustaafu na umakini mbona havihusiani

Sent using Jamii Forums mobile app
Basi shida ni uelewa.
Aliyestaafu unaweza kumpeleka apate mafunzo ya technolojia ya kisasa?
kama walistaafu kabla ya technolojia ya ndege zisizo na rubani wana uwezogani wa kuzikabili?
Ningekuwa mimi kwa kutumia akili ya kawaida.
Wastaafu ningewaita jeshi la akiba,
Na ukikuta jeshi la akiba ndilo linashika usukani,basi ujue maji yapo shingoni.
Na kama ndivyo basi putin ateue mmoja wao awe mkuu wa majeshi.
 
Siyo kuwa kwenye mapambano yanaangaliwa mafanikio, muundo na nani afanye nini yatajadiliwa kwenye historia mbele huko kwa kuulizana kwanini alifanikiwa au kwanini alishindwa ndipo kwenye maelezo utaingizia haya uliyoyaona, kwa sasa acha wasonge mbele
 
Kwani hujuj puti kaiuza Urussi kwa risiti!
 
Siyo kuwa kwenye mapambano yanaangaliwa mafanikio, muundo na nani afanye nini yatajadiliwa kwenye historia mbele huko kwa kuulizana kwanini alifanikiwa au kwanini alishindwa ndipo kwenye maelezo utaingizia haya uliyoyaona, kwa sasa acha wasonge mbele
Ukikuta mwenye mafunzo kachemka,umeanza kutumia wenye uzoefu,usisubiri mtu kukwambia umefika mwisho wa kufikiri
ie putini amefikia mwisho wa kufikiri
 
Putin amesha haribu anajuwa lazima atanyongwa kama mwenzake wa Iraq na Libya he know siku zake zinasoma kama mshale na hana ujanja kukwepa kifo. Amesha haribu anajuwa roho za wa Ukraine zina mlilia na anajuwa nayeye anaenda kufa same like wale wazee na watoto amewauwa.
Anajuwa vita alio iyanzisha nilazima atalipa trillion of dollar as compassesion kwa Ukraine anajuwa pesa hiyo itatoka kwenye mafuta na gas anayochimba mbaya kuliko yote mpaka vitukuu watalipa hasara anaileta. Putin is dead person who live and time will tell
 
VAGNER GROUP ipo chini ya GRU & MoD ya Russia. Miundombini , vifaa na huduma zote wanatumia vya wizara ya ulinzi na kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya Russia na washirika wake.. ..#LIBYA #SYRIA #VENEZUELA #MALI na kwingineko.
 
 
Daniel 11:45: "naye atapiga mahema yake ya kifalme kati ya bahari kuu na mlima mtakatifu wa lile pambo, naye atasonga kuufikia mwisho wake,NA HAKUNA ATAKAYEMSAIDIA."

Muda utatupa majibu, tukiwa hai tutajionea.
 
Wenzetu sio kama huku mtu huko anaweza akastaaf akiwa bado mdogo ila kaamua tu baada ya mission kuisha

Kigezo chako chakustaaf hakina mashiko leta kigezo kipya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amka kumekucha

Wakamnyonge kwanza BUSH OBAMA KLINTO BLAIR na NETANYAHU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…