Inaonesha Wasaidizi wa Rais hawako makini kivile!

Inaonesha Wasaidizi wa Rais hawako makini kivile!

NewPage

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2021
Posts
1,321
Reaction score
2,106
Kuhusu kukosea kosea kwa maneno kunazidi kuongezeka kwa Mheshimiwa Rais wetu. Wkt akihojiwa na BBC aliongea kuwa wenzake Mbowe walishafungwa na ilikuwa inasubiriwa Mbowe tu arudi kutoka ughaibuni naye afungwe!

Ninavyojua mimi kwa mtu asiyeelewa (yaan layman) hata kupelekwa mahakamani ni sawa na kufungwa. Kwa maana hiyo usahihi kwa wakati huo wasiadizi wa Rais walipaswa kuwa wameshaeleza kwa ufasaha kuwa Mbowe alikuwa anasubiriwa akirudi afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zake na sio kufungwa kama alivyoeleweka Rais wakati huo.

Leo pia kwa kujua kuwa suala la Mbowe lingejitokeza mkutanoni Rais alipaswa kuwekwa vema kuwa iwapo angegusia issue ya msamaha angeweka "caveat" kuwa iwapo mahakama itamwona Mbowe ana hatia basi masuala ya msamaha wa Rais yataangaliwa huko mbeleni. Au angeelekeza tu kwa DPP kuwa iwapo inaonekana kesi ya Mbowe haina maslahi kwa umoja wa Taifa letu basi aangalie namna ya kuachana nayo

Ukitafakari kwa kina maana anayokuwa amekusudia kuiongea Mh. Rais inatofautiana sana na maneno ambayo humtoka na hivyo badala yake kuzaa minong'onon mingi ambayo kwa kiasi inasumbua sana.

Ukweli wasaidizi wa Mh.Rais kwa upande wa Sheria na hotuba probably hawajajipanga vizuri na kumsababishia kutoeleweka vizuri na WaTanzania na dunia inayofuatilia siasa zetu.

Ushauri - Rais aangalie namna ya kubadili wasaidizi wake upande wa Hotuba na hata Sheria. Hawa watazidi kumharibia sana kadri siku zinavyosonga mbele!

Ni hayo tu.

Mod. ninaomba usiunganishe au kufuta uzi huu kwani umebeba ujumbe wa kipekee!
 
Mama nahisi ana ishu personal na Mbowe, kila akitajiwa kuhusu Mbowe huwa anapaniki sana na anajikuta anaropoka mambo yasiyo ya msingi.

Nadhani ni zaidi ya tunayoyajua kuhusu mama na uhusika wake kwa hii kesi ya Mbowe.

Kuhusu msamaha mwenyewe kwanza nimemshangaa yeye kusema anaweza kusamehe, sasa Mbowe bado hajahukumiwa yeye mam anawezaje kusamehe kama sio yeye ndio ameishikilia hii kesi??

Rais anaweza kusamehe mtu endapo atakutwa na hatia mahakamani, lakini mtu ambaye bado ni mtuhumiwa nadhani mtu mwenye mamlaka ya kuondoa kesi ni DPP, naelewa anapisema "anaweza kumsamehe" alimaanisha anaweza kumpa maelekezo DPP asiendelee na kesi waifunge Mahakamani which means Mbowe atakuwa Freeman kama jina lake Ila mama hakupaswa kutumia lugha za namna hiyo Kama kweli yeye Hana personal interest na hiyo kesi.

There is more into it tutakuja kujua ukweli tu.
 
Kuhusu kukosea kosea kwa maneno kunazidi kuongezeka kwa Mheshimiwa Rais wetu. Wkt akihojiwa na BBC aliongea kuwa wenzake Mbowe walishafungwa na ilikuwa inasubiriwa Mbowe tu arudi kutoka ughaibuni naye afungwe!

Ninavyojua mimi kwa mtu asiyeelewa (yaan layman) hata kupelekwa mahakamani ni sawa na kufungwa. Kwa maana hiyo usahihi kwa wakati huo wasiadizi wa Rais walipaswa kuwa wameshaeleza kwa ufasaha kuwa Mbowe alikuwa anasubiriwa akirudi afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zake na sio kufungwa kama alivyoeleweka Rais wakati huo.

Leo pia kwa kujua kuwa suala la Mbowe lingejitokeza mkutanoni Rais alipaswa kuwekwa vema kuwa iwapo angegusia issue ya msamaha angeweka "caveat" kuwa iwapo mahakama itamwona Mbowe ana hatia basi masuala ya msamaha wa Rais yataangaliwa huko mbeleni. Au angeelekeza tu kwa DPP kuwa iwapo inaonekana kesi ya Mbowe haina maslahi kwa umoja wa Taifa letu basi aangalie namna ya kuachana nayo

Ukitafakari kwa kina maana anayokuwa amekusudia kuiongea Mh. Rais inatofautiana sana na maneno ambayo humtoka na hivyo badala yake kuzaa minong'onon mingi ambayo kwa kiasi inasumbua sana.

Ukweli wasaidizi wa Mh.Rais kwa upande wa Sheria na hotuba probably hawajajipanga vizuri na kumsababishia kutoeleweka vizuri na WaTanzania na dunia inayofuatilia siasa zetu.

Ushauri - Rais aangalie namna ya kubadili wasaidizi wake upande wa Hotuba na hata Sheria. Hawa watazidi kumharibia sana kadri siku zinavyosonga mbele!

Ni hayo tu.

Mod. ninaomba usiunganishe au kufuta uzi huu kwani umebeba ujumbe wa kipekee!

Upstair mkuu ndo tatzo
 
sio kwa nia mbaya ila ni mzanzibar, uzanzibar wake una athiri uongeaji pia mfano juzi anasema polisi wanaweka ma bichwa yao kwenye gari
hivo basi haitotokea siku azungumze kama tunavotegemea
Kubali tu kuwa ni mweupe pia. Alisema pia kabla ya Uhuru hakukua na shule za private. Hii nayo utasema ni sababu ya lafudhi ya kizanzibar?
 
Hudhani kwa ni Mara ya kwanza kukosea? Umesahau juzintu kwenye ile hotuba yake kwa taifa alisema kabla ya Uhuru tulikua hatuna shule za binafsi.
Mfumo wa vyama vingi ulianza 1995
Ila hata Kama wanaoandika hotuba wanakosea, Ina maana yeye haoni hayo makosa?
Du!
 
Kubali tu kuwa ni mweupe pia. Alisema pia kabla ya Uhuru hakukua na shule za private. Hii nayo utasema ni sababu ya lafudhi ya kizanzibar?
sijawahi kumsikia akisema hivo,ila kama kweli alisema hivi huwezi kumrekebisha kwenye haya maana ni jambo ambalo alipaswa kulijua huko shuleni kwamba zilikuwepo hizo shule
 
Nasikia anaemwandikia hotuba ni yule kibiongo sijui Magoti sasa yule ana akili gani?
 
Nasikia anaemwandikia hotuba ni yule kibiongo sijui Magoti sasa yule ana akili gani?
Mkuu,labda utuambia jamaa ana shida gani mpaka umuone hivo maana sisi tunamuonaga kwenye picha tu
 
Back
Top Bottom