Tetesi: Inasemekana wagner group waamua kuisupport ukrane

Tetesi: Inasemekana wagner group waamua kuisupport ukrane

Haitakuwa mara ya kwanza China kushiriki vita za namna hii pale tu washirika wake muhimu na maslahi yake muhimu yatakapo kuwa hatarini.

China ili mtandika na kumrudisha marekani nyuma katika vita vya Korea bila China Korea kaskazini ilikuwa ina anguka rasmi.

Mpaka leo Korea kaskazini ipo kwa sababu ya China.
Taiwan ile pale, mwambie China aende akaone balaa.
 
Wana jamvi... Kwa moto wanaopelekewa jeshi la russia kuna uwezekano mkubwa vijana wa Yevgeny Prigozhin wameamua kupigana bega kwa bega kulipiza kisasi cha kuuliwa boss wao, maana mpaka muda huu tunavyoongea russia bado ana hangaika kuisogelea kursk na ameshindwa kutokana na kipigo anachokutana nacho....rais Russia ambaye ndiye amir jeshi mkuu haamini kinachotokea. Jeshi la russia jana limesema jeshi la Ukraine limevinja madaraja yote wanayokutana nayo wakisonga mbele....

1.Je huu ndio wakati wa WAGNER kumalizia safar yao walio anzisha wakiwa na boss wao Yevgeny Prigozhin kuelekea MOSCOW?

2.Je huu ndio mwisho wa PUTIN?

3.Malalamiko ya Russia kuwa Ukraine anatumia silaha za western yana mashiko ikiwa yeye pia anatumia silaha kutoka IRAN, KOREA?

4.kwa malalamiko haya russia inakili kuwa silaha za korea, iran hazijasaidia chochote dhidi ya Ukraine?

5.Russia amekili adharani kuwa Ukraine anatumia silaha za western kuishambulia Russia.... Kwa mantiki hiyo silaha za western ni bora kuliko yeye?
Binafsi mi naona NATO hawajapeleka silaha tu bali wanajeshi wa kutosha wa NATO wanapigana upande wa Ukrain.

Wanajeshi wa Ukrain peke yao wasingeweza kumtikisa Urusi hata kama wangepewa silaha kwa sababu wanajeshi wengi wa Ukrain wamekufa na raia wengine waliishakimbia nchi na pia wanajeshi waliopo hai wapo wanapambana kule upande wa Donbasa.

Hapa Urusi asipokuwa makini kuingia meza ya mazungumzo habari yake itaisha maana kaishalemazwa na vita takribani miaka 2 na sasa anashambuliwa kwa usaidizi wa NATO
 
Taiwan ile pale, mwambie China aende akaone balaa.
Umri wako unaweza akisi ulicho andika.

Kiwango cha upeo ulicho nacho wewe kuhusu masuala ya China na ya kimataifa na walichonacho viongozi wa China ni tofauti.

Si ajabu kuona una andika hiki ulicho andika.
 
Hatma ya Vita hiyo ni aidha majeshi ya kutoka nchi za Magharibi kuingia uwanjani moja kwa moja na kuwasaidia Wanajeshi wa Ukraine au kuhamishia uwanja wa vita kutoka nchini Ukraine na kupeleka nchini Urusi. Hii ifanyike kwa kuwahamasisha na kuwasaidia Wananchi wa Urusi ambao wako against dhidi ya Utawala wa Bw. Putin. To motivate, to support, to equip, to train Separatist of the Russian territory in order to sabotage the Russian Military capabilities and finally incapacitating it in launching an offensive attacks against Ukrainian territory.
Putin hapa kapatikana.

Hakuna Mwananchi wa Russia atamuunga mkono kwa yanayoendelea.
 
Putin alifanya kosa kubwa sana kuivamia Ukraine,japo hakuwa na jinsi kwa dalili za uchokozi za. NATO na US lakini angejizuiya mambo yasingekuwa magumu kiasi hiki.
Ameharibu uchumi wanchi,ameruhusu maadui kumsoma jinsi anavyo pigana,namengine mengi sasa wanaamua kumchokoza waone atafanyanini.

So far meshachelewa NATO tayari wapo kazini kumuondoa.
 
Labda Korea ya Kaskazini, lakini kwa China sidhani kama anaweza akajiunga na Urusi.
Kumbuka: China Ina maslahi makubwa zaidi nchini Marekani na kwa washirika wake kuzidi maslahi yake yaliyopo nchini Urusi au Korea ya Kaskazini.
Aidha, vita ni biashara.
Russia haitaji support toka kwa China. Russia hainunui ndege vita inatumia zake, China inanunua ndege kwa Russia. Russia hainunui air defence system toka popote inatengeneza zake, China inanunua air defence za Russia. Kwa ufupi kwenye military tech China ni tegemezi kwa Russia na hivyo mpango wake wa kuivamia Taiwan lazima ajue wapi atapata backup. Na kwenye siasa za kimataifa mkono mtupu haulambwi. China bega kwa bega na Russia.

Kuhusu Ukraine hiyo ni kazi ndogo sana. Ukraine inajua moja ya mbinu ya Russia ni kusafisha kila kitu inapofanya operation zake za kijeshi na Russia haiwezi kuuharibu mji wake kwahiyo wataachwa wajae kwanza kisha Russia itaziba njia zote za kuingia na kutoka na winter inakaribia nchini Russia.
 
Usisahau Kuna china,Korea ya kaskazini,Iran,Syria,Algeria, Yemen, Vietnam na marafiki wengine wa Urusi wataibuka mara baada ya Hali kua kama unavyosema.
Hakuna rafiki kwa mtu anaekaribia kushindwa vita. Sahau.
 
Dah aisee ila Urusi ni kiboko aisee!
Mie sikuwahi kujua kama Urusi Ina nguvu namna hii.
Yaani mnawaza Kila aina ya kuunganisha nguvu ili kuishinda Urusi moja.
Si tulikubaliana kua USA ndio super power?
Leo Tena USA na NATO hawajatosha wanataka kuungana na Wagner.?
Hii inaonesha ni jinsi Gani Urusi Ina nguvu kubwa.
Nimegundua kuwa kelele nyingi za Putin ilikuwa ni kurishia Nyau kumbe ni mweupe ka Azam flour ,pamoja na msaada wa Iran norh Korea Bado anakula kipigo Zelensk noma
 
Hivi nyie mnaijua Russia kweli? Hao Wagner Kama wanataka maslahi yao yote yafyekwe na kundi kupotea.
 
Hakuna rafiki kwa mtu anaekaribia kushindwa vita. Sahau.
Ukraine ndio inashindwa vita. Kujaribu kushikilia miji ya Russia ndio kete yake ya mwisho hiyo maana wachambuzi wa vita wanasema endapo mpango huo wa Ukraine utafeli basi kuna uwezekano wa Ukraine ika-surrender sababu kwanza Russia itayachukua maeneo yote yaliyopakana na Kursk na belgorod na kutengeneza buffer zone ili kuizuia Ukraine kurudia kujipenyeza tena.

Wakati huo huo Russia inaendelea kujitwalia maeneo zaidi ya Ukraine na mapambano yanaendelea.

Kursk ina ukubwa wa 29800km². Ukraine wanajeshi wa kulikalia eneo hilo wakati huo huo aendelee kupigana nchini mwake. Russia imeshapeleka wanajeshi Kursk na operation inaendelea taratibu hadi kazi ikamilike.
 
Ukraine ndio inashindwa vita. Kujaribu kushikilia miji ya Russia ndio kete yake ya mwisho hiyo maana wachambuzi wa vita wanasema endapo mpango huo wa Ukraine utafeli basi kuna uwezekano wa Ukraine ika-surrender sababu kwanza Russia itayachukua maeneo yote yaliyopakana na Kursk na belgorod na kutengeneza buffer zone ili kuizuia Ukraine kurudia kujipenyeza tena.

Wakati huo huo Russia inaendelea kujitwalia maeneo zaidi ya Ukraine na mapambano yanaendelea.

Kursk ina ukubwa wa 29800km². Ukraine wanajeshi wa kulikalia eneo hilo wakati huo huo aendelee kupigana nchini mwake. Russia imeshapeleka wanajeshi Kursk na operation inaendelea taratibu hadi kazi ikamilike.
Acha kujipa moyo. Russia mwaka just aliingia hadi kyyiv na wakapigwa
 
Russia haitaji support toka kwa China. Russia hainunui ndege vita inatumia zake, China inanunua ndege kwa Russia. Russia hainunui air defence system toka popote inatengeneza zake, China inanunua air defence za Russia. Kwa ufupi kwenye military tech China ni tegemezi kwa Russia na hivyo mpango wake wa kuivamia Taiwan lazima ajue wapi atapata backup. Na kwenye siasa za kimataifa mkono mtupu haulambwi. China bega kwa bega na Russia.

Kuhusu Ukraine hiyo ni kazi ndogo sana. Ukraine inajua moja ya mbinu ya Russia ni kusafisha kila kitu inapofanya operation zake za kijeshi na Russia haiwezi kuuharibu mji wake kwahiyo wataachwa wajae kwanza kisha Russia itaziba njia zote za kuingia na kutoka na winter inakaribia nchini Russia.
Siku karibu ya 10 adui kaingia chumbani kwako anajaribu miondonbinu, anauza walinzi wako hujamtoa tu unasubiri nini?
 
Hivi China huwa mnawachukulia nao hawajitambui kama hizo nchi za hao makubadhi wanaopenda vita kuliko hata ugali? Yaani China unamweka kundi moja na Syria, Yemen na North Korea ambao 24/7 wanawaza ugomvi na hawana cha kupoteza

Yaani mnafikiri wanaweza kukurupuka tu na kuanza kuvuruga kirahisi tu uchumi wao walioutolea jasho zito eti wanampambania Russia? Watu wale wanajitambua, wamepiga hesabu pale Taiwan wakaona hasara itakuwa kubwa kuliko faida wakakausha, ila waswahili tunaofananisha vita na minyukano ya simba na yanga tunadhani kila nchi ipo tayari kukurupuka na kwenda kupigana tu bila kuzingatia consequences za uamuzi huo!
Huko ngorongoro nasikia nayenyewe ngoma inachemkia chini kwa chini
 
Siku karibu ya 10 adui kaingia chumbani kwako anajaribu miondonbinu, anauza walinzi wako hujamtoa tu unasubiri nini?
Vita ni mbinu kila hatua inakuwa calculated. Kinachofanya counter offensive za Ukraine zifeli ni kwa sababu Ukraine inatafuta matokeo ya mapema ili kuwaaminisha west kuwa wanapiga kweli ndio maana taarifa nyingi za field wanazificha. Ukraine inasema Russia imeishambilia Kiev kwa ballist 2 na drone 30 na wamefanikiwa kuziangusha drone zote ila hawasemi kuhusu missiles, au drone 28 kati ya 30 zimeangushwa ila hawasemi drone mbili zimefanya nini. Kwahiyo habari za Ukraine sio za kuziamini sana.
 
Back
Top Bottom