Huu ni utani na wananchi ambao hawana ajira. Jiji la Arusha mlifikiria hili mkiwa wazima wa afya ama mlikuwa mmekunywa rubisi?? Enyi serikali hebu wajalini wananchi wenu kwa usawa. Watu hawana ajira, inatokea ajira ya muda badala muwape ajira wasiokuwa na ajira mnawapa wenye ajira??? Wacha tukae bila ajira Wala pesa. Tutashinda huku mitandaoni kuwasema hadi mlewe. Wabinafsi wakubwa nyie. Keki ya Taifa hamtaki kutugea na sisi wananchi.
WANANCHI WENZANGU, NAFASI ZA KAZI HIZO HAPO...LAKINI NI KWA WATUMISHI TU.
Mkurugenzi wa halmashauri (DED) wa jiji la Arusha John Lipesi Kayombo akikaribishwa ofisini, sasa anatumia kofia ya pili ya cheo chake cha muda kama Msimamizi wa uchaguzi halmashauri ya Jiji Arusha.
Habari za hivi punde
Picha maktaba Posted on: August 21st, 2024 Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Mhandisi Juma Hamsini (kushoto) amemkabidhi ofisi Mkurugenzi mpya wa Jiji la Arusha Bwana John Lipesi Kayombo mapema leo. Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na viongozi.
Makabidhiano ya ofisi kwa wakurugenzi (DED) hao yametokana na mabadiliko ya uteuzi yaliyofanywa mnamo Agosti 14, 2024 na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Sami Suluhu Hassan, kwa Mhandisi Juma Hamsini kuhamishiwa Jiji la Tanga na bwana John Kayombo kupangiwa Halmashauri ya Jiji la Arusha akitokea Jiji la Dodoma.
Kabla ya kwenda kuwa DED jiji la Dodoma, John Lipesi Kayombo aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufanya uteuzi tarehe 07 Julai, 2016.
Utendaji na uchapakazi wa DED John Lipesi Kayombo:
(March 2018)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akitoa ufafanuzi wa muongozo wa ukusanyaji wa mapato kwa Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa
Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo
MD Kayombo akisisitiza jambo
Maafisa Watendaji wa Kata 14, Watendaji wa Mitaa 91 pamoja na Wahasibu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo wameonywa kutopokea Rushwa wala hongo ya aina yoyote kutoka kwa wamiliki wa biashara mbalimbali katika Manispaa hiyo kwani kufanya hivyo watadhoofisha ukusanyaji wa mapato ya serikali kama ilivyokusudiwa.
Kauli ya onyo imetolewa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakati akitoa ufafanuzi wa muongozo wa ukusanyaji wa mapato na kutoa maelekezo ya majukumu ya kazi kwa Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa kwenye kikao cha kazi kilichofanyika leo Jumamosi Machi 18, 2017 katika ukumbi wa Ofisi za Manispaa hiyo ilipo Mtaa wa Kibamba CCM.
March 4 , 2017
kikao cha kazi na Wenyeviti wa Manispaa hiyo ya Ubungo mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo (Aliyesimama) Boniface Jacob akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kazi na Wenyeviti wa Manispaa hiyo, Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo na kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ubungo Ramadhan Kwangaya
Wenyeviti wakisikiliza kwa makini maelekezo mbalimbali wakati wa kikao cha kazi kilichoendeshwa na Mwenyekiti wa kikao hicho Mhe Boniface Jacob ambaye ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo (Picha zote na Nassir Bakari