INASIKITISHA: Makaburi Kinondoni yanavunjwa makusudi ili ipatikane nafasi ya kuzikia

Hata Ilala na Mbagala makaburi yalivunjwa kupisha upanuzi wa barabara
MAKABURI ya Mbagala hayakuvunjwa, yalichimbuliwa na ndugu na walilipwa na serikali ili kupisha Barabara ya Kilwa Road na mabaki yakaenda kuzikwa tena huko Tuangoma.
 
Mungu anisamehe lakini tulifanya sana matusi na kuroga kwenye hayo makaburi miaka ileee
 
"............kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ndugu yangu aliyelazwa.........." kwani anaendeleaje?
 
Huko diko kuvunjwa kwenyewe
MAKABURI ya Mbagala hayakuvunjwa, yalichimbuliwa na ndugu na walilipwa na serikali ili kupisha Barabara ya Kilwa Road na mabaki yakaenda kuzikwa tena huko Tuangoma.
 
Serikali ilishafunga makaburi ya kinondoni kwa sababu kumejaa na kuhamishia ununio kwa kondo. Kinachofanyika ni uhuni, ukienda na pesa yako ndefu wanakuuzia unapata sehemu ya kuzika
Anayekua anauza ni nani mkuu? na hiyo hela inakua inaingia kwa nani?
 
Mhm ningependa kufahamu zaidi kuhusu hili tafadhali
huyo Marehemu alikuwa mtu maarufu sana na alipenda kusaidia watu hasa masikini, alipofariki kama kawaida ya ukoo wa Mobutu walipenda kuzikana na mali kwa mfano kaburi la mama yake Mobutu lilipambwa na dhahabu na hata mke wa Mobutu alizikwa na vito vya thamani
hivo basi huyu Maboti alipofariki nae alizikwa na ma cheni na pete za dhahabu na makaburi yalilindwa,mwaka 1997 Mobutu alipokimbia waasi walifika kwenye makabuli ya ndugu zake na kuanza kuiba na walifanikiwa kweli kwenye makabuli yote kuwatoa marehemu ila kaburi la Maboti ndio hivo ikashindikana maana risasi ya kwanza tu kufyatuliwa kwenda kwenye kaburi ilirudi,mpaka leo hakuna aliyegusa hilo kaburi.nitaweka picha badae
 
Inatakiwa watu muwe na viwanja au mashamba na umejenga ,kuzikwa manispaa ni aibu ,unatakiwa uzikwe kwenu ,au kwako Kama wachaga na Kanda ya kaskazini wanavyofanya
 
tunakaribia kufika kwenye makaburi ya kupangisha.
 
Ulienda kuangalia maendeleo ya ndugu yako alizikwa hapo sio? Anaendeleaje?
 
Sisi wamasai zamani mtu alikuwa akifa tunampaka mafuta ya kondoo na anapelekwa vichakani huko analiwa na fisi habari yakw inakuwa imeisha (Au mnaishia zetu makazi mapya mnamwacha hapo)
 
Asante sana[emoji1545][emoji1545]nasubiri picha
 
Kifupi jiji la dar Lina eneo kubwa zuri sana la makaburi liko kunduchi linaitwa kwa kondo nendeni kuzika huko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…