Inasikitisha! Ona taarifa zetu za benki zinavyotumika kufungia vitafunwa

Inasikitisha! Ona taarifa zetu za benki zinavyotumika kufungia vitafunwa

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Ku-share data/taarifa binafsi imekuwa muhimu katika kufanya kazi zetu za kila siku na kushirikiana na watu wengine katika jamii.

Mwingiliano wetu na mashirika na taasisi mbalimbali unahusisha ubadilishanaji wa data/taarifa binafsi.

Hizi data/taarifa binafsi ni taarifa yoyote inayokuhusu, iwe inahusiana na maisha yako binafsi, kitaaluma, au ya umma (Mfano: majina, namba za simu, anwani n.k)

Sasa basi, ni mara ngapi unakutana na taarifa za watu wengine katika mazingira ambayo hukupaswa kukutana nazo? Kama ni mara nyingi, basi huenda hata taarifa zako zinazagaa mahali wakati huu bila wewe kujua.

Kwa mfano: Hapa chini ni vielelezo vinavyoonesha nyaraka zenye taarifa binafsi za watu. Yaani unanunua vitumbua, vinakuja na taarifa za watu. Si sahihi. Hizi taarifa zinapaswa kuwa ni siri miongoni mwa wahusika.

Si taasisi binafsi tu ambazo hazioni umuhimu wa kutunza taarifa za watu kwa usiri mkubwa, bali hata taasisi za umma/mamlaka za serikali.

So, nimepiga picha hizo karatasi kwa masikitiko makubwa. Zilitumika kama vifungashio vya chakula.

Kwakweli kunahitajika mwongozo wa jinsi data/taarifa za watu zinapaswa kukusanywa, kushughulikiwa na kuhifadhiwa kulingana na unyeti na umuhimu wake.

4.jpg
22.jpg
111.jpg

111.jpg
photo_2021-11-17_08-08-27.jpg
 
Hapo usishangae ni haohao watumishi wa bank wana vijiwe vyao vya vitafunio wanaamua kuchukua hizo karatasi zenye taarifa za wateja kwenda kufungia vitafunwa
 
Unajua hizo karatasi zinauzwagwa tena ni hela nzuri tu, sasa usijekuta mtumishi mmoja wa bank lunch time amekosa anatoa kilo zake mbili akapime mchana mwema upite
Duh! Kwahiyo ukute kuna ninja mmoja anasema "msichome hizi, nina kazi nazo"
 
Ni balaa aisee!
Pongezi nyingi kabisa The Sheriff kwa kutumia busara ya hali ya juu na kuziba sehemu sensitive za document zisionekane. Hongera sana kwani watu wenye upeo kama wewe ni wachache kwa Bongo. Ukiondoa hilo jambo la kijinga kabisa la kutotunza siri za wateja, bado kuna tatizo la kiafya. Chakula kinakuwa contaminated na wino au uchafu mwingine kwani hizi karatasi zilipitia kwenye mikono mingi na mazingira machafu pia.
 
Pongezi nyingi kabisa The Sheriff kwa kutumia busara ya hali ya juu na kuziba sehemu sensitive za document zisionekane. Hongera sana kwani watu wenye upeo kama wewe ni wachache kwa Bongo. Ukiondoa hilo jambo la kijinga kabisa la kutotunza siri za wateja, bado kuna tatizo la kiafya. Chakula kinakuwa contaminated na wino au uchafu mwingine kwani hizi karatasi zilipitia kwenye mikono mingi na mazingira machafu pia.
Shukrani sana, ndugu yangu.

Upo sahihi kabisa. Madhara ni makubwa. Nadhani bado wengi hatujaona umuhimu wa ulinzi wa taarifa binafsi.
 
Unajua hizo karatasi zinauzwagwa tena ni hela nzuri tu, sasa usijekuta mtumishi mmoja wa bank lunch time amekosa anatoa kilo zake mbili akapime mchana mwema upite
Itakua aiseee...mm nishakutana na za CRDB aisee i was suprised..maana ni account za namba za watu/makampuni,...kiasi cha pesa na jina..tena zimepangwa kwa wingi wa pesa sio vi account vya watu masikin masikin.....yn sikuamini
Zimetengenezewa bahasha....
 
Back
Top Bottom