Inawezekana 'Herd Immunity' na hali ya hewa (Mazingira) ndio vitu vinavyotuokoa Watanzania dhidi ya COVID-19

Inawezekana 'Herd Immunity' na hali ya hewa (Mazingira) ndio vitu vinavyotuokoa Watanzania dhidi ya COVID-19

Kabisa zaidi ya mwaka na nusu watu wanaranda randa tu bila ya kujikinga maana yake wengi walishaugua COVID na kunatengeneza herd immunity.

Watakuwepo wagonjwa wa hapa na pale, lakini kwa maamuzi ambayo yalikuwa reckless mwaka jana ya kusema liwalo na liwe COVID aiwezi kuwa tishio Tanzania, watu wengi mpaka sasa itakuwa walishapata sema ugonjwa wenyewe hauna madhara as that.

Wimbi la pili serikali ilipeleka mitungi ya Gas hospitali kubwa zote zikajiandaa hao wagonjwa awakutokea ilibeba tu mapadre ambao wanaishi kwa kujitengeka. Mmoja awakaingizia Corona ikafanya yake kama ilivyofanya ikulu; lakini kwenye jamii sasa hivi kuna herd immunity ya ugonjwa.

Hiyo report mbona aisemi hospitali zina wagonjwa wangapi wa COVID leo.

Ukiona JK havai barakoa na anaingia mitaani jua mambo shwari yule kuna watu wanamtonya hali ikiwa tete mahospitalini.
 
Pamoja na kutokuzingatia miongozo yoyote ya kupambana na Corona watu hawafi kama nchi nyingine.
Umejuaje kuwa watu hawafi kama nchi nyingine?Yaani umetumia kitu gani kujua kuwa Tanzania watu hawafi kama nchi nyingine?
 
Umejuaje kuwa haina effect kubwa?Yaani umetumia nini kujua kuwa Tanzania Corona haina effect kubwa?

easy! tuko kwenye mikusanyiko january to january, no masks, no sanitizers, no vaccines! effect ya corona tanzania ni almost zero, but najua tanzania inapokea wageni na wenyeji pia, so i said ALMOST ZERO sjasema exactly ZERO
 
Kwanza niweke wazi kuwa mimi si daktari na wala sina utaalamu wa magonjwa ya kuambukiz bali nimetumia tu common sense na elimu ya kusoma vyanzo mbalimbali na hatimae ku-arrive at this conclusion:

Tuanze kwa kutazama herd community ni mini.

Herd immunity ni kinga inayotokana na sehemu kubwa ya jamii kuugua ugonjwa husika na baadae kujenga kinga dhidi ya ugonjwa huo au ni kinga kwa jamii baada ya sehemu kubwa ya jamii kuwa imepata chanjo hivyo kupunguza uwezekano wa watu wachache ambao hawana kinga katika jamii hiyo kuambukizwa ugonjwa huo.

Mtandao wa Wikipedia umeelezea hivi kuhusu herd immunity;

Herd immunity is a form of indirect protection from infectious disease that can occur with some diseases when a sufficient percentage of a population has become immune to an infection, whether through vaccination or previous infections, thereby reducing the likelihood of infection for individuals who lack immunity.

Kwanini inawezekana hali kuwa n hivyo kwa watanzania?

Jibu ni rahisi tu nalo ni kwamba hatuchukua tahadhari za kutosha mlipuko unapotokea na matokeo yake wengi tunaugua ns baadae kupona na wengine kupata maambukizi bila kuonyesha dalali kutokana na uimara wa kinga zao ila mwisho wa siku sehemu kubwa ya jamii inakuwa imetengeneza kinga( herd immunity).

Kinachotokea ni watu wengi kupata maambukizi huku baadhi wakiugua na kupona na wengine kutoonyesha kabisa dalili huku wachache(hasa wazee na wenye matatizo fulani fulani ya kiafya)wakifariki na ushahidi wa kimazingira wa hali hii ni kipindi ambao vifo huwa vingi kuliko kawaida tena vikionekana ni vifo vya ghafla kwa walio wengi.

Nini hutokea baada ya hapo(herd immunity kuwa developed)?

Kwa mtazamo wangu, kwakuwa kinga hii huwa si ya Kudumu, basi kuna wakati kinga hii huisha ila virusi vinakosa mazingira ya kuviwezesha kuendelea kutushambulia mpaka kipindi fulani cha mwaka(probably January to March) kijirudie ndio hali ya hewa huwa conducive kwa virusi hawa ku-survive na kutushambila na ndio maana kwa miaka hii miwili ya 2020 na 2021, milipuko na ongezeko la vifo vilijitokeza zaidi katika kipindi hicho kwa hii miaka miwili mfululizo.

Tusubiri tena kuanzia mwezi January mpaka mwezi March mwakani(2022) ili tuweze kujiridhisha na wakati huo huo tuombe kirusi kitachokuwa kimejibadilisha na kusubiri conducive environment kisiwe hatari kulik virusi vilivyopita.

Kwahiyo ni imani yangu si maombi,nyungu, malimao, pilipili wala tangawizi ndio vinavyotusaidia, badala yake ni herd immunity na hali ya hewa(mazingira) ndio vinavyotusaidia na si vinginevyo.

Vile vile ushahidi wa kimazingira unatuonyesha mazingira ya baridi sio factor kabisa kama inavyodaiwa kwani kipindi cha January mpaka March, si kipindi cha baridi kwa maeneo mengi ya nchi yetu, ila mlipuko huwa juu kipindi hicho. Hivyo, labda hali ya hewa ya joto ndio inaweza kuchangia kwani kwa mkoa kama wa Dar-es-Salaam kipindi hicho joto huwa kali zaidi.

Ni mtazamo wangu ingawa naamini utafiti unahitajika kupata ukweli na mambo mengine kuhusu hili gonjwa hapa nchini na mwenendo wake na hasa utafiti utaolenga kujua nini hutokea katika kipindi cha January mpaka March kinachopelekea (maambukizi)ugonjwa huu kuonekana unaongezeka.
Siyo daktari lakini wewe Ni mtu makini. Andiko lako zuri
 
Umejuaje kuwa haina effect kubwa?Yaani umetumia nini kujua kuwa Tanzania Corona haina effect kubwa?
we jamaa unaonekana unatamani sana corona iingie tz. nakuona unavo lazimishi ionekane tz kuna corona...ila ukweli ni kua hakuna corona tz. sisi huku mbeya tuna saranda tu mitaani tena kwa kujiachia kabisa lakini hakuna mtu anae umwa
 
we jamaa unaonekana unatamani sana corona iingie tz. nakuona unavo lazimishi ionekane tz kuna corona...ila ukweli ni kua hakuna corona tz. sisi huku mbeya tuna saranda tu mitaani tena kwa kujiachia kabisa lakini hakuna mtu anae umwa
Nimekuuliza swali dogo sana,wewe ulipaswa kujibu swali hilo badala ya kufanya personal attack.Kwa hiyo kama Mbeya hakuna mtu anaeumwa Corona hilo linathibitisha kuwa nchi nzima hakuna anaeumwa?
 
Naposema herd immunity,maana yake ni asilimia 80 ya watu wawe wameugua au wamepata maambukizi pasipo kuonyesha dalili lakini waka-develop kinga. Kwahiyo, kitendo cha kuongelea tu herd immunity, maana yake ugonjwa umefikia aailimia 80 ya watu katika jamii yetu.
well said
 
easy! tuko kwenye mikusanyiko january to january, no masks, no sanitizers, no vaccines! effect ya corona tanzania ni almost zero, but najua tanzania inapokea wageni na wenyeji pia, so i said ALMOST ZERO sjasema exactly ZERO
Kwa nini hujibu swali langu la msingi?Nimekuuliza kuwa umetumia kigezo gani kujua kuwa effect ya Corona Tanzania ni almost zero?Yaani umejuaje?
 
MAOMBI.
rais wacnchi kujitokeza hadharani na kutamka kuwa JANGA LA CORONA ANAMUACHIA MUNGU.
si Jambo dogo.wengi tulimuona amechanganyikiwa.
SASA MUNGU AMEAMUA KUTUKOSOA.
kuwa yeye yupo na ukimtegemea kwenye Jambo lolote anakujibu.
 
Mtoa mada una akilia nyingi Sana,wanaokubeza na kukupinga wana akilia mgando.
Kwanza kuumiza kichwa TU na kuja na wazo lako Ni mwanzo wa utafiti(research) Tosha.
Na kuanzia Hapo wengine wanaweza kuongeza kwa kwenda deep zaidi
Tatizo la Wachangiaaji wengi humu na husussani Watanzania huwa tunaviamini Sana vitu vikivyokwisha kamilika na hasa vilivyokamililishwa na wazungu.
Bila kujali hata hao wazungu inawezekana walipata wazo kutoka kwa Mtu mmoja great thinker kama wewe.Ndipo hao mabingwa wakaendeleza alipoishia mtoa wazo.
Kitu kingine Cha kushangaza kwa wachangiaaji wengi,badala ya kujadili mada wanajadili kosa la herufi.spelling wakati tayari wameshajua au walishaelewa kuwa ulitaka kusema Nini au ulimaanisha Nini,lakini ukakosea herufi TU.
Kosa la herufi bila kujua pengine ulikua umekusudia kuandika meno Fulani ukakosea kubonyeza herufi husika.

Hata hivyo mada yako inafikiriaha.
Iweje Nchi jirani na baadhi ya Nchi watu wanakufa kama kuku wa kideri lakini sisi so hivyo?
 
Brother Corona bado haijaisha duniani, tumuombe Mungu atuepushe na kikombe hiki..Hata India huko nyuka hawakuwaza siku moja italipuka vile ilivyo...walikuwa salama kama sisi.... hatujui kesho itakuwa zamu ya nani...

Covid 19 huwa inalipuka tu kama mzaha, mpaka sasa ziko nchi nyingi ambazo hazijawahi kuexperience madhara ya Covid19 lakini hii sio guarantee kwamba ndio wako salama hapana...
 
Back
Top Bottom