Inawezekana hili la mahindi lilikuwa namna ya kutafuta pakupotezea wadadisi wa mambo

Inawezekana hili la mahindi lilikuwa namna ya kutafuta pakupotezea wadadisi wa mambo

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Kuna mshkaji mtaani tulikua tunajadili changamoto iliyopo kwenye zogo la mahindi baina ya Kenya na Tanzania, akanipa uwezekano wa wazo fulani, naifahamu sana Serikali yangu ya Kenya ikitaka kuficha kitu kwanza huwa na mazoea ya kuibua jambo lingine litakalosababisha migongano ya baina yetu kwenye mitandao ya kijamii, tukianza kulumbana hapo fursa inapatikana ya kufanya walichotaka kufanya au kuficha hadi tunapomaliza kulumbana walishafanya yao.

Nimewaza hili la mahindi na kujiongeza, mahindi yaliyopakiwa kwenye malori ya kutokea Tanzania, haya mahindi tunayakula kila siku, mbona ghafla ndani ya wiki hizi mbili ndio pameibuka hili, na kusababisha migongano baina ya Wakenya na Watanzania kwenye mitandao ya kijamii, kipi hicho tunafichwa kinachohusu hizi nchi mbili.

Maana hili la mahindi limeibua mapovu kote, kuanzia Youtube, Twitter, Facebook, mpaka huku JF tunalumbana kwa kwenda mbele, na uwezekano mkubwa upo zikiisha siku 14 au 20 tutaambiwa wamesuluhisha palikua na sintofahamu fulani tu lakini wameweka sawa.

Haya bana sitahoji zaidi, ila kama ni kweli basi wakuu mngetafuta kingine cha kutumia, hili la mahindi mlikosa ubunifu maana mtasababishia watu hasara. Uzuri wa kwetu hapa tuna uhuru wa maoni.

Wana Afrika mashariki bado natoa tahadhari, corona ipo na inapukutisha, vaa barakoa muda wote ukiwa nje, nawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, epuka misongamano, ukihisi dalili zinazofahamika, nenda kwenye kituo cha afya mara moja, acheni hayo mambo ya sijui matangawizi na malimau, hayo yafanye wakati uko mzima ili kuendelea kujichimbia na kuongeza kinga, ila ukihisi kimepenya, kimbilia kwenye kituo cha afya, kunazo dawa za kawaida ambazo zinakipiga vita hiki kirusi.
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.
Mnaenda kula mahindi yaliyokuwa yalishe nguruwe kule Mexico!
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.

Inawezekana hilo la mahindi ya Mexico kuwa kweli.

Inawezekana kweli mahindi ya Watanzania yana sumu.

Lakini pia inawezekana hilo la mahindi limeandaliwa kufunika tetesi za kiongozi wa Afrika kutibiwa huku kimya kimya.
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.
I also thought the same too
 
Viongozi wetu hapa Afrika Mashariki akili zao wanazijua wenyewe, nawahakikishia mahindi ya Tanzania kenya yatauzwa vizuri tu hayana hata mwezi mmoja mtajionea, ni sawa na unieleze mimi nikose sabuni ya jamaa, au mafuta ya vaseline au lotion ile ya AMARA FOR MEN au nikose Big G original hapo hatutaelewana.
 
Vizazi vya vijana wa Afrika Mashariki tusikubali kurithi akili za hii mizee, lazima tuwe na wivu kuona namna region nyingine hasa west wanavochanga mbuga huku sisi tukikubali mgawanyo miongoni mwetu hapana
 
Halafu East Africa ni Kenya na Tanzania, na Uganda kwa mfano Kenya na Tanzania sisi tunataniana kupita maelezo ndio maana utaona Geza ulole ( ina maana ya Subiri Uone) akileta picha za miradi ya Tanzania, huku unaona MK254 nae anaita wenzake kusema Bongo lalaz huku wabongo wkisema manyangau basi tunasonga kiivo wala sio ugomvi.
 
Viongozi watuunganishe na Biashara mara zote unaanza kufanya na jirani ndio wengine huvutiwa kufika kutafuta biashara na wewe, nimeshangaa Burundi nae eti hataki mahindi yetu nimeona kakutupuka maana ukiangalia migogoro yetu Kenya na Tanzania kwanza wananchi wenyewe ndio hua tunaanza kuungana baadae viongozi wanajiona wamebaki peke yao wanaamua tu kutatua migogoro yao maisha yanasonga
 
Inawezekana hilo la mahindi ya Mexico kuwa kweli...
Inawezekana kweli mahindi ya Watanzania yana sumu...
Lakini pia inawezekana hilo la mahindi limeandaliwa kufunika tetesi za kiongozi wa Afrika kutibiwa huku kimya kimya...
Nawewe unaaminini huyo jamaa yupo huko kutibiwa? Yule jamaa yuko radhi afe lakini si kutibiwa kee.
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.
Kina Ruto wamefanya yao!
 
Nawewe unaaminini huyo jamaa yupo huko kutibiwa? Yule jamaa yuko radhi afe lakini si kutibiwa kee.

Sijui unazungumza kuhusu nani, ila ninavyofahamu hakuna mwenye jeuri dhidi ya kirusi cha kolonya, kikitia kambi kwako lazima ukubali yaishe na utakubali upelekwe popote na kwa yeyote, kunao wanakunywa hadi sanitizer, yaani kinatesa binadamu hadi unatamani hata ufe tu.

Halafu poleni sana Watz naona kwenu imekua mwendo wa tanzia tu TANZIA - Kanali Fabian Massawe, aliyekuwa RC Kagera afariki dunia
 
Sijui unazungumza kuhusu nani, ila ninavyofahamu hakuna mwenye jeuri dhidi ya kirusi cha kolonya, kikitia kambi kwako lazima ukubali yaishe na utakubali upelekwe popote na kwa yeyote, kunao wanakunywa hadi sanitizer, yaani kinatesa binadamu hadi unatamani hata ufe tu.

Halafu poleni sana Watz naona kwenu imekua mwendo wa tanzia tu TANZIA - Kanali Fabian Massawe, aliyekuwa RC Kagera afariki dunia
Kupoa tumeshapoa ila nakuhakikishia jamaa hawezi kukubali kutibiwa kwa manyang'au. Wanachofanya sasahivi ni kama walichofanya kenya ishu ya mahindi tu wanatengeneza attention ili wafanye jambo lao, huyu jamaa ataibuka na kuanza kusema msisikilize wapinzani hao ni wapuuzi tu.
 
Mimi naona ni kama wanasiasa walikuwa tayari wameagiza mahindi kutoka Mexico kwa ajili ya kutafuta pesa ya kupiga campaign. Sasa kwa sababu meli inakaribia kuwasili basi inabidi waondoe mahindi kutoka TZ na UG ili wapate nafasi ya kuuza mahindi yao. Ni mawazo yangu tu based on past experience lakini naweza kuwa wrong.
Wacha wee

Yale mahindi wanayolima kwa ajili ya farasi na ng'ombe kule Mexico ndo wamewaagizia.
 
Inawezekana hilo la mahindi ya Mexico kuwa kweli.
Inawezekana kweli mahindi ya Watanzania yana sumu.
Lakini pia inawezekana hilo la mahindi limeandaliwa kufunika tetesi za kiongozi wa Afrika kutibiwa huku kimya kimya.
Hivi niulize Kenya haikuwa na wakemia miaka yote hiyo leo ndo inao?

Miaka yote hiyo mahindi ya tz mnakula walikua hawayachunguzi na kujua hiyo so called sumu ila this week ndo wakagundua?

Je walishindwa kukaa chini meza moja wakafikia muafaka kwamba kama mnataka tuendelee kununua fuateni procedure hizi na hizi tupate mahindi salama.na wakifuata mnayapima yako salama biashara inaendelea.

Je, kwa uagizaji kutoka mexico hudhani kwamba gharama itakuwa juu zaidi?

Gunia lako la mahindi from namanga na gunia la mahindi from Mexico?

Siasa mpaka kwenye maisha ya watu.
 
Back
Top Bottom