Inawezekana kulima ngwara kipindi cha kiangazi?

Inawezekana kulima ngwara kipindi cha kiangazi?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Wazo hili limezaliwa kutokana na michango ya wazoefu waliomo humu JF wa kilimo cha zao tajwa. Kwa kuwa wazo limezaliwa humu, nimeamua kulirejesha humu ili lipate ukosoaji wenye tija.

Kwa mujibu wa wazoefu, inaonekana ngwara ni zao lisilohitaji maji mengi. Hulimwa
mwishoni mwa msimu wa mvua.

Ikiwa ndivyo, haiwezekani kulilima kipindi cha kiangazi?

Maadam linahitaji unyevunyevu tu utakaosaidia kuchipua, kwa nini lisimwagiliziwe kwa maji ya kisima, mto, n.k.?

Kwamba, labda mkulima anaamua kuandaa utaratibu wa kusomba maji kutoka mtoni kwa kichwa, gari, n.k. kwa ajili ya kuloanisha ardhi wakati wa kupanda, kisha baada ya hapo, anamwagilizia mara moja kwa wiki mpaka mazao yake yatakapokomaa.

1. Utaratibu huo utafaa?

2. Kwa wastani, shina moja la ngwara linahitaji maji kiasi gani kwa siku?

3. Kama mtu ataamua kufanya kilimo cha ngwara kipindi cha kiangazi, atapaswa kumwagilizia mara ngapi kwa wiki?

🙏🙏🙏
 
Ngwara ni zao gani tena?[emoji849]

Lina matumizi gani?

Lipoje hata kapicha tupia.
Mkuu, hufahamu ngwara😀

Ni mazao jamii ya kunde. Yana rangi nyeusi.

Ni "matamu" sana, yanapatikana kwa wingi Arusha na Manyara.

Wakenya wanayapenda mno. Ni "matamu" na yana utajiri wa virutubisho muhimu kwa afya.
 
Mkuu, hufahamu ngwara😀

Ni mazao jamii ya kunde. Yana rangi nyeusi.

Ni "matamu" sana, yanapatikana kwa wingi Arusha na Manyara.

Wakenya wanayapenda mno. Ni "matamu" na yana utajiri wa virutubisho muhimu kwa afya.
Ngwara ilikua 2012-2017 1kg 5000+ ukipiga trip Moja Kenya ukirudi lazima ufanye jambo!
 
Sidhani kama ni sahihi sana kulima kiangazi mara nyingi hua wanapanda mbegu mwezi wa nne mwishoni au tano mwanzoni issue siyo mvua tu apana Kuna hali ya hewa

Ngwara inachukua miezi minne mpaka mitano hadi uvune, kwa maeneo yanayolima ngwara mwezi wa nne mpaka nane hali ya hewa ni ya baridi sana na mvua za rasha rasha zikistop tu hali ya hewa inakua joto/jua kali ndo ngwara zinakauka vzr tayar kwa mavuno

Ukisema ulime kiangazi means utalima Kati ya mwezi wa 8 au tisa itakua kuharibiwa na mvua za October mwishoni, November na December
 
Sidhani kama ni sahihi sana kulima kiangazi mara nyingi hua wanapanda mbegu mwezi wa nne mwishoni au tano mwanzoni issue siyo mvua tu apana Kuna hali ya hewa

Ngwara inachukua miezi minne mpaka mitano hadi uvune, kwa maeneo yanayolima ngwara mwezi wa nne mpaka nane hali ya hewa ni ya baridi sana na mvua za rasha rasha zikistop tu hali ya hewa inakua joto/jua kali ndo ngwara zinakauka vzr tayar kwa mavuno

Ukisema ulime kiangazi means utalima Kati ya mwezi wa 8 au tisa itakua kuharibiwa na mvua za October mwishoni, November na December
Lakini mkuu, kukimwagiliziwa alau mara moja au mbili kwa mwezi itakubali?

Wakati mwingine ninakuwa na "kaubishi" kazuri, kuamua kufanya jambo tofauti na ilivyozoeleka.

Mwakani, nitajaribisha kulima eneo dogo kwenye mwezi wa Sita hivi au mwishoni mwa mwezi May. Kwa kuwa mvua huanza mwezi wa kumi, zitakuta zimeshavunwa.

Nitalima kwa lengo la kujibu kwa vitendo swali nililolileta humu jukwaani!

Tutaona😀
 
Lakini mkuu, kukimwagiliziwa alau mara moja au mbili kwa mwezi itakubali?

Wakati mwingine ninakuwa na "kaubishi" kazuri, kuamua kufanya jambo tofauti na ilivyozoeleka.

Mwakani, nitajaribisha kulima eneo dogo kwenye mwezi wa Sita hivi au mwishoni mwa mwezi May. Kwa kuwa mvua huanza mwezi wa kumi, zitakuta zimeshavunwa.

Nitalima kwa lengo la kujibu kwa vitendo swali nililolileta humu jukwaani!

Tutaona😀
Its good kua mbishi, lakn om the flip side, jaeibu kuangalia maelezo ya jamaa kwa kina,
Ngwara n jamii ya maharage, na maharage hayapendi maji mengi.
So technically unaeza kulima kweli kwa hyo njia yako, yes yatastawi vzur lakn yatakapokomaaa ready kuvunwa ndo mvua zitakua zmeanza so possibility ni kubwa yataozea shambani.
Ni mtazamo tu.
 
Its good kua mbishi, lakn om the flip side, jaeibu kuangalia maelezo ya jamaa kwa kina,
Ngwara n jamii ya maharage, na maharage hayapendi maji mengi.
So technically unaeza kulima kweli kwa hyo njia yako, yes yatastawi vzur lakn yatakapokomaaa ready kuvunwa ndo mvua zitakua zmeanza so possibility ni kubwa yataozea shambani.
Ni mtazamo tu.
Mkuu, nimemwelewa mjibu hoja na wadau wengine pia. Ninachotaka kufanya ni jaribio, kuona kitakachotokea. Naamini "uwanja" wa majaribio ungali wazi. Na kwa kuwa ni majaribio, matokeo yo yote nitakayoyapata yatakuwa majibu sahihi.
 
Back
Top Bottom