Inawezekana mfumuko wa bei Tanzania ni wa kutisha, idara ya Takwimu wametupiga chenga ya mwili kwa takwimu za Januari, ila nimewagundua

Kama ni hivi tutaona mengi sana.. maana kila mahali wanaongopa data.. Ndo ile unaambia uchumi unakuwa halafu life bado lipo tight
Hongera kwa jicho lako la utambuzi, yote haya ni kwa sababu ya hofu, kila mtu hataki kumkwaza bwana yule, wanaishi naye kama unavyoishi na mtoto anaye deka.
 
Magu hataki kusikia habari ya mfumuko wa bei na watakwimu wanamridhisha kwa takwimu za kupikwa
Bati imepanda na kufikia 27000_mwezi huu
Umeona sasa.. data zao na huku ground mambo yapo tofauti sana.. hususani hicho ulichosema kuhusu bei ya bati
 
Usiwe mwepesi wa kuandika halafu ukawa mvivu wa kusoma.

1. Unaanza kwa kusema eti market basket inabadilika kila mwaka wakati nimekuonesha data za kuanzia January 2018 ambapo ilikuwa sawa mpaka December 2020.. soma ndo ujibu usikurupuke

2. Inflation kwa developing countries kama Tanzania inasababishwa zaidi na supply side factor na sio monetary phenomena kama unavojaribu kusema.. kwa hiyo kama kuna inflation Tanzania usidhanie supply ya pesa itakuwa ni kubwa kwenye uchumi... Kwa kukusaidia, money supply growth ipo chini sana sasahivi kuliko kipindi kingine chochote ndani ya miaka kumi iliyopita.

3. Sijaongea mambo ya more Taxation.. elewa hoja ndo uandike acha kukurupuka.

4. Poor purchasing power haisababishi watu wa import zaidi..

Kijana naona kichwani umeweka theory nyingi mbovu za uchumi.. kuwa mtulivu ujifunze uchumi utauolewa.

Ila ukiendelea kuandika kwa sababu tu una bando.. my friend utapotea sana
 
I choose to ignore you after this post nisiharibu uzi wako.

What will happen kama serikali isipoweka limitations za import quotas kwenye mafuta ya kupikia, sukari na sehemu zingine ambazo wazalishaji wandani wanalindwa kwanza. Na kwanini baadhi ya bidhaa sokoni serikali inapanga price floor kwa kuzingatia production cost za wazalishaji wa ndani.

Ndugu gharama za kuzalisha Tanzania zipo juu na hiko ndio kinavutia imports ya products nyingi, umeshaona kodi za imported finished goods na bado maduka yamejaza bidhaa zinazozalishwa nje? Kwanini hao waagizaji wasianzishe viwanda? Mbona imported agricultural products zinazotumika viwandani hakuna kodi?

Kubishana na kiazi kama wewe kuhusu uchumi I can see from the start ni kupoteza muda wangu, market basket inachaguliwa na serikali and it is never constant after a few years it usually changes; you should know that as you claim to be an economist.
 
Ni kwamba wanajidanganya tu kwa sababu kwa bahati mbaya sana ni kwamba masuala ya uchumi huwa hayaishii tu kwenye makaratasi bali huwa reflected kwenye maisha halisi huku mtaani.

Yaani kama wanadanganya kwenye makaratasi kuwa mfumko wa bei ni sifuri watashangaa kuna siku watu wapo barabarani kwa sabu chumvi pakiti moja imekuwa TZS 10,000/= na sukari kilo moja imekuwa TZS 50,000/=!Ni punguani peke yake ndiye anaweza kupoteza muda wake kudanganya masuala ya uchumi kwenye karatasi kwa sababu masuala haya hayaishii tu kwenye karatasi.
 
mbona una hasira hivi!!!

ni mfumuko wa bei au una mengine mkuu??
 
Nchi hii inaongozwa na waongo sana Kama corona tunaambiwa haipo na inaua watu watashindwaje kudanganya kuhusu mfumuko wa bei
 
Magu hataki kusikia habari ya mfumuko wa bei na watakwimu wanamridhisha kwa takwimu za kupikwa
Bati imepanda na kufikia 27000_mwezi huu
swali ni moja yananunulika au yameganda store!!!

maana ukiona bidhaa inapanda bei,kuna factor nyingi, lakini kubwa kuliko zote, ni uzalishaji hautosherezi mahitaji.
 
Nimekusoma na kukuelewa. Nasubiri waje watupe majibu ya hizo mambo ulizowaachia.
Huwa hawajibu hoja,wataanza Ku attack personality ya mtoa mada.Ndivyo walivyoelekezwa,kupotosha ukweli na kuaminisha Watanzania kwamba wapo salama chini ya CCM.
Ile CCM ya enzi za Mwl.Nyerere ambapo kusema kweli daima ilikuwa moja ya Imani zake imefwariki ndiyo maana tunashuhudia Intarahamwe's doing.
 
Na mimi nimeshangaa japo taaluma yangu sio mchumi lakini hapo aliposema kuna Money supply kubwa nimeshangaa sana how? Kama serikali ndiye main distributor na fedha yake kwa asilimia kubwa inaenda kwa International Contractors na sisi tunabaki na kiduchu, Pesa imeongezekaje? Awamu hii ni kubana Matumizi tu pesa imeongezekaje?

hoja ya kusema watu wana Purchasing power ndogo ndo maana tuna import sana nayo ina ukakasi kidogo, japo vitu vya nje vinaweza kuwa bei nafuu lakini hiyo purchasing power ndogo inawezaje ku cover kupata fedha za kigeni sasa?
 
Ni bora u choose kuni ignore.. maana unaongelea mambo ambayo yapo nje ya mada kabisa.. Na mimi huwa sipendi kubishana na watu wanacheza nje ya key!

Unaanza kuongelea sijui import quotas kwenye mafuta na sukari.. sijui price floor.. mi mada yangu wala haipo huko.. nilidhani utasema rationale ya kuongezeka kwa bidhaa kwenye basket lakini naona unajaribu kuongea jargons za kiuchumi kwa kudhani kwamba ndo utaonekana unajua!!!!

Stick kwenye point.. na useme hoja yako ikajulikana acha papara..

Halafu unaanza kuzungumzia masuala ya kodi na bla bla nyingine..

Jenga hoja ya kitu unachotaka kuzungumza vinginevo utaonekana mkurupukaji..
 
Huyo jamaa ni mkurupukaji wa uchumi wa kati.. anaongea mambo hayaeleweki halafu anaweka jargons za kiuchumi anadhani ndo ataonekana anafahamu sana..
 
Hakuna adui mkubwa wa watawala sasa hivi kama TAKWIMU SAHIHI.

Hebu jaribu hata kufanya utafiti wa kiwango cha ukosefu wa ajira Tanzania uone kama utatoka salama.
 
swali ni moja yananunulika au yameganda store!!!

maana ukiona bidhaa inapanda bei,kuna factor nyingi, lakini kubwa kuliko zote, ni uzalishaji hautosherezi mahitaji.
Sasa hicho unachokisema kwamba bei inapanda .. ndo kinatakiwa kiwe reflected kwenye inflation na sio serikali kujarivu kuficha ukweli...
 
Hakuna adui mkubwa wa watawala sasa hivi kama TAKWIMU SAHIHI.

Hebu jaribu hata kufanya utafiti wa kiwango cha ukosefu wa ajira Tanzania uone kama utatoka salama.
Hilo la ajira ndo bomu...
 
Hilo la ajira ndo bomu...
Yaani sasa hivi amani yao ni ukimya wa matatizo kama hivi.

Case study check Corona, as long as haitangazwi wala hawapimi wana assume haipo.

Style za kufukia kichwa cha mbuni ardhini wakati kichwa chote kiko nje
 
Wameona food inflation inawaumbua.. na vile weight yake ni kubwa impact yake pia kwenye inflation ni kubwa.. kwa hiyo itakuwa wamepunguza weight yake ili kuhakikisha inflation hairuki kwenda popote
Inflation ni pana sana, Hakuna anaeweza kucheza na asili yake. Serikali inacheza na namba kuaminisha raia hakuna ongezeko la Inflation

Bahati mbaya au Nzuri watanzania wengi hatupewi knowledge kuhusu maswala ya uchumi, tungekua nayo wengi wangeshtuka na kuishukia serikali kama mataifa yaliyoendelea lakini tumeamriwa kusoma historia ya Tanzania may be itatusaidia kupunguza inflation 😢
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…