Inawezekana siasa za nchi hii ndio somo gumu kwa watanzania kuliko hata Hesabu(Mathematics)

Inawezekana siasa za nchi hii ndio somo gumu kwa watanzania kuliko hata Hesabu(Mathematics)

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Katika nchi yetu na pengine duniani kote,hesabu ndio somo linalotajwa kuwa gumu(wengi wanashindwa kulielewa) kuliko masomo mengine mengi, ila binafsi naona kwa nchi yetu siasa za nchi hii ndio somo gumu zaidi kueleweka kwa watanzania walio wengi.

Inawezekana kabisa hata wale ambao ni "magwiji"wa hesabu, baadhi yao ndio wakawa vilaza wakubwa katika kuelewa siasa za nchi hiii.

Hali hii ya watu kushindwa kuelewa siasa za nchi yetu,ndio msingi wa wanasiasa kuwarubuni watu na kuwafanya kama wajinga kiasi kwamba hata wakifanya mambo ya kijinga na kipuuzi, bado kuna watu watawatetea na hata wakitimiza wajibu wao, kuna watu watawatukuza kama miungu watu.

Kwa mfano,hivi sasa kuna mwanasiasa mmoja mwenye madaraka makubwa tu kaamua kufanya mambo yasiyofaa yenye muelekeo wa chuki,ubaguzi,uonevu,n.k, ila kuna watu kutokana na siasa kwao kuwa ni somo gumu, haya yote hawayaelewi ingawa wanayoana kisa tu Bwana yule anafanya baadhi ya mambo mengine yanayoonekana kuwa ni mazuri lakini ambayo ndio wajibu wake kwa nafasi yake.

Kutokana na uelewa mdogo wa watu katika kuwapima wanasiasa kwa matendo na kauli zao,watu wanashindwa kuelewa kuwa huyu bwana ndio chanzo kikuu cha yote haya na badala yake utawasikia baadhi ya wenzetu wakilaumu wasaidizi wake eti ndio wanamshauri vibaya na kwamba hao ndio wanampotosha!!!

Mfano mwingine ni mwanasiasa mmoja machachari aliewahii sema kuwa kuna kiongozi fulani aliwahi ishi kwa "uongouongo" jambo ambalo ukilichunguza utagundua ni kweli kwa baadhi ya mambo(mfano lile swala la kuunganisha nchi "A" na nchi "B") ila mwanasiasa huyo alishambuliwa sana kwa kauli yake hiyo na ukichunguza utagundua hii ni kutokana na siasa kuwa ni somo gumu sana kueleweka kwa walio wengi na ndio maana watu wanadanganyika sana na wanasiasa.

Uzuri mzee wa watu kwa heshima na busara zake, aliwahi kukiri hadharani kuwa katika zama zake, kuna mambo ya kijinga yalifanyika, ila watu wanashindwa kuelewa kuwa hili la kuunganish nchi "A" na nchi "B" ni moja ya hayo makosa aliyoyafanya enzi zake(mchakato mzima ulivyofanyika).

Na bahati mbaya sana kwa sasa amepatikana yule anaetumia uelewa mdogo wa watu katika mambo ya siasa kutaka kufanya karibu kila mtu ni kilaza wa siasa za nchi hii ila msishangae akawapata wengi maana siasa limekuwa somo gumu sana katika Taifa hili na wengi wataendelea kufeli hili somo mpaka kwenye vyumba vya kupigia kura na kutugharimu tusiohusika na ujinga huu.
 
Umerudi Mkuu ulipotea sana"

Weekend yote hii mpaka mwaka mpya mwendo wa kula bia mpaka mwaka upite...

Wacha nitulie siasa za nchi hii ukizijua wala hazitakusumbua.

Wewe unaumia mwenzio yupo chato anakula bata mpaka mwaka mpya...

mwingine nimeona anakiri na kuacha siasa good

Maisha yenyewe mafupi aya kujipa stress na kuzeeka haraka yanini?

Nchi hii kama una pesa kipindi kama iki unaenda zako Uturuki, France- au Dubai unajipumzikia tu mpaka mwaka mwingine uanze.

ukiachana na siasa uchwara zinazoleta stress Tanzania ilikuwa nchi bora kabisa duniania ya kuishi na ukatulia.
 
Mkuu siasa za tz, zinaendeshwa na njaa.
Mchochezi wewe....😂😂😂😂
Njaa ina kanuni ya kuua uwezo wa kufikiri na kukosa umakini na msimamo, hivyo mtu mwenye njaa sio mtu wa kuaminika (mwepesi kumuuuliza) katika maneno na matendo yake kwa kuwa anachosema na anachofanya kina dhamira moja tu ya kuweka chakula mezani....kwa muktadha huu siasa za Tz. hazitokuja kueleweka kamwe kwa kuwa zimefungamanishwa na njaa. Kinachotokea mwanasiasa anatafuta namna bora ya kula, mwananchi anatafuta namna ya kula (hata kidogo) hatma yake wanakutana kwenye temporary goal. Hivyo usishangae aliyechafuliwa mwaka jana leo anakuwa msafi hadi unajiuliza amesafishika lini, aliyeshinda akiwa CDM ndo huyo huyo anashinda CCM
 
Wakati mwingine kiongozi mmoja akisema yeye ni rafiki wa wanyonge, huwa najiuliza wanyonge wa tz au wanyonge wa chama chake, na zaidi akisema msemakweli ni mpenzi wa Mungu, pia huwa najiuliza mungu wa chama chake au Mungu wa wote!.

Sent using Jamii Forums mobile app
Anajua siasa(hadaa za kisiasa) ni jambo ambalo baadhi ya watanzania wenzetu wameshindwa kulielewa hivyo anatumia udhaifu huo kuwahadaa na wao wanamuamini na kumuona ni mzalendo.
 
Umerudi Mkuu ulipotea sana"

Weekend yote hii mpaka mwaka mpya mwendo wa kula bia mpaka mwaka upite...

Wacha nitulie siasa za nchi hii ukizijua wala hazitakusumbua.

Wewe unaumia mwenzio yupo chato anakula bata mpaka mwaka mpya...

mwingine nimeona anakiri na kuacha siasa good

Maisha yenyewe mafupi aya kujipa stress na kuzeeka haraka yanini?

Nchi hii kama una pesa kipindi kama iki unaenda zako Uturuki, France- au Dubai unajipumzikia tu mpaka mwaka mwingine uanze.

ukiachana na siasa uchwara zinazoleta stress Tanzania ilikuwa nchi bora kabisa duniania ya kuishi na ukatulia.
Mkuu nipo tu ila sio mara kwa mara.
 
Back
Top Bottom