Inawezekana tatizo la ajira likawa la ukanda

Inawezekana tatizo la ajira likawa la ukanda

MKEHA

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
716
Reaction score
1,143
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wabunge wengi waliochangia kamati ndogo ya sheria na ajira kuna kubebana sana kwenye SECRETARIAT ya ajira. Wabunge wamesema siku hizi kuna kanda watu wake hawaajiriwi kabisa.

Kuna vimemo vinawataka wabunge watie mkono ili ajira zitoke. Je NEPOTISM inatokea ndani ya secretariat yenyewe ama mfumo ndo unaamua yupi apate ajira.

Mbunge wa Simanjiro bwana Ole Sendeka ameenda mbali sana kwa kutoa taarifa kuwa suala la ajira limegawa nchi katika vipande. Kuna ukanda unapata ajira sana huku wengine wakiishia kwenye usaili tu

Amesema hapo zamani serikali ililiona hilo chini ya Mwalimu Nyerere na kuamua kila mkoa kuwa na pass mark zake ili kuweka usawa katika nchi.

Wengine wamesema serikali iige jinsi majeshi yetu yanavyo ajiri kwani kila wilaya huwa na nafasi zake maalum na hivyo kuwa na uwoano mzuri kwenye ajira zaajeshi japo wamesema askari wengi huingiza watoto wao, ndugu zao na.marafiki zao kwenye ajira hizi.
 
Ni kweli kabisa kama watendaji wa kata, vijiji watumishi wengine aisehh wengi ni Wasukuma kabisa... Juzi juzi nilienda home nikakuta ni wao tuuu tena ajira mpya. Mimi nadhani sasa hilo liangaliwe upya serikali ifanye re-allocation kabisa watawanye watawanye ili msawaziko uwepo

Mfano kwenye kazi, yaani huwaambii chochote kumhusu Mwenda zake mpaka nikawa wananitisha ila cha ajabu wana mchukia mama Samia huwezi amini.
 
Ni kweli kabisa kama watendaji wa kata, vijiji watumishi wengine aisehh wengi ni Wasukuma kabisa... Juzi juzi nilienda home nikakuta ni wao tuuu tena ajira mpya. Mimi nadhani sasa hilo liangaliwe upya serikali ifanye re-allocation kabisa watawanye watawanye ili msawaziko uwepo

Mfano kwenye kazi, yaani huwaambii chochote kumhusu Mwenda zake mpaka nikawa wananitisha ila cha ajabu wana mchukia mama Samia huwezi amini.
Hilo nalo mkalitazame
 
Ni kweli kabisa kama watendaji wa kata, vijiji watumishi wengine aisehh wengi ni Wasukuma kabisa... Juzi juzi nilienda home nikakuta ni wao tuuu tena ajira mpya. Mimi nadhani sasa hilo liangaliwe upya serikali ifanye re-allocation kabisa watawanye watawanye ili msawaziko uwepo

Mfano kwenye kazi, yaani huwaambii chochote kumhusu Mwenda zake mpaka nikawa wananitisha ila cha ajabu wana mchukia mama Samia huwezi amini.
Wapo wengi sana makazini watu type hio
 
Back
Top Bottom