Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Kwa nchi kama Tanganyika na nchi zote za Afrika, ambayo mipaka yake iliamuliwa na Wazungu kwa kutumia rula kwenye mkutano wa Berlin 1884-1885, sahau kupata maendeleo ya kweli. Mataifa ya kizungu yapo kikabila zaidi, lakini kwa Afrika mataifa yamebaki na mipaka ileile ya Berlin Conference ya 1884-1885 hadi leo ambapo nchi moja ina makabila 100 na zaidi.
Mkuu nikuulize, kukaa kwao kikabila kumewasaidiaje na kukaa kwetu pamoja makabila mseto kumetukwamishaje? Chukulia baadhi ya makabila yanayokaa pamoja mpaka sasa kama Wamasai, Wasandawe, Wabarbaig n.k., kumekuwa na msaada wowote kwao tofauti na makabila mengine?
 
Nini? Soko la Kariakoo lilijengwa na Mjerumani? Ni kweli mkuu?

Sikuwa nafahamu hilo. Kama ndivyo, Mjerumani alikuwa ni mkoloni mzuri japo inasemekana alikuwa mkali sana na mbabe mno.
Someni historia zipo wandugu.

Wakati wa utawala wa wajerumani walijenga hilo jengo na likawa ni ofisi zao, walitaka wawe watumia kwa shughuli kama ghafla na sherehe.

Baadae walipokuja waingereza wakapageuza kuwa ni soko kwa wakazi wa Dar-es-Salaam.
 
Lakini pamoja na mipaka ilowekwa na Berlin Conference 1884-1885 bado zipo nchi barani Afrika zina maendeleo makubwa tu Botswana, Namibia, Rwanda (baada ya vita iloisha 1994) ni mfano wa nchi zinoonyesha kuwa kukiwa na nia na malengo thabiti, basi maendeleo huja kwa kasi.

Sasa sisi hadi leo twahangaika na soko moja tu la Kariakooo lilijengwa na wajerumani na tumeshindwa kujenga masoko mengine makubwa katika kila mkoa au wilaya na wananchi wapanga bidhaa zao ardhini na pembezoni mwa barabara.
Bora umezitaja hizo nchi tatu, maana ni mataifa ambayo idadi ya raia ni chache sana ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika, lakini pia hizo nchi zina makabila machache. hapo ndiyo utaona sababu mambo yao yanaenda vizuri relatively speaking.
 
🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Ingelikuwa ni maamuzi yangu, hayo mawazo yangeingia kwenye utekelezaji haraka sana.
Suala na kodi na maendeleo huwa haya mijadala hata kama huna fedha za kulipa kodi itatafutwa namna ulipe.

Ndo maana kwa wenzetu kila mtoto anezaliwa tayari data huingizwa kwenye mfumo. Akifika miaka 16 waanze kumwambia awez akupiga kura na akifika 18 huambiwa ajiandae kulipa kodi maana tayari anakuwa amepewa ile namba ya bima.
 
Mkuu nikuulize, kukaa kwao kikaba kumewasaidiaje na kukaa kwetu pamoja makabila mseto kumetukwamishaje? Chukulia baadhi ya makabila yanayokaa pamoja mpaka sasa kama Wamasai, Wasandawe, Wabarbaig n.k., kumekuwa na msaada wowote kwao tofauti na makabila mengine?
Kitaifa mshikamano unakuwa siyo harmonious sababu tofauti zinakuwa kubwa zaidi ya umoja kwa huu utaifa feki wa kubuni wa Utanzania ukilinganisha na nchi za Ulaya ambapo utaifa unaendana na ukabila.
 
Someni historia zipo wandugu.

Wakati wa utawala wa wajerumani walijenga hilo jengo na likawa ni ofisi zao, walitaka wawe watumia kwa shughuli kama ghafla na sherehe.

Baadae walipokuja waingereza wakapageuza kuwa ni soko kwa wakazi wa Dar-es-Salaam.
🙏🙏🙏
 
Bora umezitaja hizo nchi tatu, maana ni mataifa ambayo idadi ya raia ni chache sana ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika, lakini pia hizo nchi zina makabila machache. hapo ndiyo utaona sababu mambo yao yanaenda vizuri relatively speaking.
Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.

Tunaweza sema Mtwara iimarishwe ili isaidie Lindi, au Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Katavi isaidie mikoa yote ya kusini kimandeleo.

Ukiangalia nchi yetu mikoa mingi ina fursa kubwa ya kiuchumi ila tatizo lipo kwenye usimamizi wa uchumi na vyanzo vya mapato.
 
Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.

Tunaweza sema Mtwara iimarishwe ili isaidie Lindi, au Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Katavi isaidie mikoa yote ya kusini kimandeleo.

Ukiangalia nchi yetu mikoa mingi ina fursa kubwa ya kiuchumi ila tatizo lipo kwenye usimamizi wa uchumi na vyanzo vya mapato.
Kwa hilo, nakubaliana nawe mkuu.
 
Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.

Tunaweza sema Mtwara iimarishwe ili isaidie Lindi, au Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Katavi isaidie mikoa yote ya kusini kimandeleo.

Ukiangalia nchi yetu mikoa mingi ina fursa kubwa ya kiuchumi ila tatizo lipo kwenye usimamizi wa uchumi na vyanzo vya mapato.
Nakubaliana na wewe. Mikoa ya Tanzania kwa kiasi kikubwa ndiyo kigezo kikubwa cha kutofautisha mipaka ya makabila nchini. Mikoa ingepewa hadhi ya majimbo yajitawale kiuchumi na kisiasa kama ilivyo Nigeria na USA. Hizi ni nchi mbili zenye very diverse population kama Tanzania.
 
Usije ujatamka hayo mbele ya Trump. Alishawahi kutoa kejeli mbaya sana ya kibaguzi dhidi ya Bara la Afrika.

1. Aliziita nchi za Kiafrika "Shithole countries"

2. Alizitukana nchi za Kiafrika kwa kusema "Afrika inatakiwa itawaliwe tena"
Olay, we unaonaje kwa upande, alikuwa right or wrong
 
Kuna mwamba alisema Afrika hasa kusini mwa jangwa la sahara tukihamishiwa nchi za Ulaya nao wakaletwa kuishi hapa Afrika... Kwamba baada ya miaka 5 tutakuja kuomba msaada nilicheka sana... Ila ni kama. Kuna ukweli ndani yake

By the way... Kwanini wanafunga ubalozi wao!??
Naked truth
Yaani itokee tuhamishwe waafrika tupelekwe ulaya na marekani halafu wazungu wake Africa, wakati wa kuhama hamna unachochukua zaidi ya nguo ulizovaa
Baada ya miaka mitano,ni sisi ambalo tutaomba viza na kulia ubarozini ili tukubaliwe kuingia tena Afrika
 
Watu wameshaanza kuamka. Sasa ni tofauti kidogo na zama za ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI. Si unaona hata wewe mwenyewe unavyokwazika?

Mimi naamini, siku za mbeleni, tena siyo mbali saana, hali itakuwa tofauti sana. Fikra mpya na chanya zinaendelea kuibuka.
Shida ni kwamba walio kwenye nafasi za maamuzi asilimia 98 wapo kwa ajili ya matumbo yao, na baada ya wao kutoka wana tengeneza watu watakao kuja kuendelea kulinda maslahi yao, ndio mfumo walio uweka, ukija ukataka kuwapinga na kufuata haki na kua muadilifu na muwajibikaji utaondoka bila kupenda
 
Denmark ni nchi kubwa na kongwe kuliko Tanzania- cheki history na facts.

Leo ki eneo Tanzania ni kubwa kuliko, Uingereza lakini miaka 70 iliyopita, Uingereza ilikuwa I atawalaye 25% ya nchi za uliwengu.

Hivyo Ukubwa na ukuu wa nchi hauko katika eneo/ardhi.
 
Denmark inatarajia kuufunga ubalozi wake nchini Tanzania ifikapo 2024. Ni kati ya nchi ambazo zimekuwa zikiipa Tanzania misaada, tokea ikiitwa Tanganyika hadi sasa ikiwa inajulikana kwa jina adhimu, Tanzania.

Lakini Denmark ni nchi ya namna gani?

Ukifanya ulinganisho, Tanzania imeizidi kwa mambo mengi isipokuwa ujinga na umaskini. Ina rasilimali nyingi sana kuizidi, na hata idadi ya watu tumeipita mbali sana.

Denmark, ni kanchi kadoogo, kenye ukubwa wa kilomita za mraba 42,920 lakini inaizidi kiuchumi Tanzania, nchi Kuubwa kieneo, yenye kilomita za mraba 945,087.

Denmark, ni kanchi kadoogo kenye watu milioni tano lakini inaipa misaada nchi kuubwa, Tanzania, yenye watu milioni sitini na moja.

Ni nini siri ya kanchi kadogo kuizidi nchi kubwa kama Tanzania? Imekuwa ikiisadia Tanzania tokea 1963, enzi hizo ikiitwa Tanganyika, lakini hakuna taarifa ya Tanzania ambayo ni nchi kubwa kuisaidia Denmark kanchi kadogo.

Imewezekanaje kwao lakini kwetu ikashindikana?

Mwingine anaweza kusema ni kwa sababu ya ukoloni, lakini hilo halina mashiko. Hata Korea Kusini ilishawahi kuwa koloni la Japan, lakini kwa sasa wanatukimbiza kiuchumi.

Ni nini walichogundua hao watu weupe ambao weusi wa Tanganyika na Zanzibar hawajagundua?

Angalia, hata eneo la Korea Kusini ni dogo sana ukililinganisha na ukubwa wa Tanzania. Ina kilomita za mraba 100,210 na watu milioni hamsini na moja.

Inawezekanaje kanchi kadoogo, Denmark, kuipa misaada nchi kuubwa, Tanzania?
Baadhi ya Viongozi wa Bara la Afrika ni mafisadi wala rushwa wezi Majambazi na wezi Unafikiri kweli tutaendelea kichumi?
 
Magufuli alipotaka kuigeuza Tanzania iwe sawa na nchi za Ulaya mlimfanyaje? Mnataka maendeleo lakini hamtaki namna ya kuyafikia hayo maendeleo. Maendeleo ni malengo, nidhamu, kujitoa mhanga (self sacrifice), bidii ya kazi, uadilifu na kutambua vipaji na ubunifu na kuvitumia ipasavyo. Ulaya wameweza kuviunganisha hivyo vyote kufikia hapo walipo. Sisi hapa bado tunajitafta na akija mwenye mawazo kama hayo bado hatumwelewi. Tutachelewa sana.
kupora mali za watu nakuua hakuwezi kuleta maendeleo
 
Mkiacha wizi, kudai Rushwa kama za mama zao, kuwa na moyo wa kujituma na kufanya kazi bila kusubiri hongo ama kweli mtawapita hao mnaowaita kanchi

Siku hela zote zitatumika zote kwenye sehemu zilikoelekezwa bila kuiba basi mjue mmekaribia pepo

Majizi lini yakafika mbali?
 
Nimekubali! Una akili sana mkuu!!!
Hata maelezo yako yanatanabaisha hilo. Yaelekea ulikuwa mzuri sana kwenye debate!

Unajua jinsi ya kujenga hoja kutetea kile ulichokidhamiria, hata kama sicho unachomaanisha.

Ni kweli? Usijibu hapa watu wasije wakakuona wewe ni kigeugeu, lakini imeshafahamika kuwa una akili sana bila kujali rangi ya ngozi yako.

Kongole kwako mkuu!
Sifa ulizonimwagia ni mtego mkuu🤣.
Anyways nina akili za kutosha kuvukia barabara ila hazifikii za wazungu🤣.
Ningekua nina akili kama.za wazungu ningefanya jambo nchi yangu iwe kama Denmark.
Asante kwa pongezi lakini
 
Back
Top Bottom