GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
- Thread starter
-
- #401
Mkuu nikuulize, kukaa kwao kikabila kumewasaidiaje na kukaa kwetu pamoja makabila mseto kumetukwamishaje? Chukulia baadhi ya makabila yanayokaa pamoja mpaka sasa kama Wamasai, Wasandawe, Wabarbaig n.k., kumekuwa na msaada wowote kwao tofauti na makabila mengine?Kwa nchi kama Tanganyika na nchi zote za Afrika, ambayo mipaka yake iliamuliwa na Wazungu kwa kutumia rula kwenye mkutano wa Berlin 1884-1885, sahau kupata maendeleo ya kweli. Mataifa ya kizungu yapo kikabila zaidi, lakini kwa Afrika mataifa yamebaki na mipaka ileile ya Berlin Conference ya 1884-1885 hadi leo ambapo nchi moja ina makabila 100 na zaidi.
Someni historia zipo wandugu.Nini? Soko la Kariakoo lilijengwa na Mjerumani? Ni kweli mkuu?
Sikuwa nafahamu hilo. Kama ndivyo, Mjerumani alikuwa ni mkoloni mzuri japo inasemekana alikuwa mkali sana na mbabe mno.
Bora umezitaja hizo nchi tatu, maana ni mataifa ambayo idadi ya raia ni chache sana ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika, lakini pia hizo nchi zina makabila machache. hapo ndiyo utaona sababu mambo yao yanaenda vizuri relatively speaking.Lakini pamoja na mipaka ilowekwa na Berlin Conference 1884-1885 bado zipo nchi barani Afrika zina maendeleo makubwa tu Botswana, Namibia, Rwanda (baada ya vita iloisha 1994) ni mfano wa nchi zinoonyesha kuwa kukiwa na nia na malengo thabiti, basi maendeleo huja kwa kasi.
Sasa sisi hadi leo twahangaika na soko moja tu la Kariakooo lilijengwa na wajerumani na tumeshindwa kujenga masoko mengine makubwa katika kila mkoa au wilaya na wananchi wapanga bidhaa zao ardhini na pembezoni mwa barabara.
Suala na kodi na maendeleo huwa haya mijadala hata kama huna fedha za kulipa kodi itatafutwa namna ulipe.🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Ingelikuwa ni maamuzi yangu, hayo mawazo yangeingia kwenye utekelezaji haraka sana.
Kitaifa mshikamano unakuwa siyo harmonious sababu tofauti zinakuwa kubwa zaidi ya umoja kwa huu utaifa feki wa kubuni wa Utanzania ukilinganisha na nchi za Ulaya ambapo utaifa unaendana na ukabila.Mkuu nikuulize, kukaa kwao kikaba kumewasaidiaje na kukaa kwetu pamoja makabila mseto kumetukwamishaje? Chukulia baadhi ya makabila yanayokaa pamoja mpaka sasa kama Wamasai, Wasandawe, Wabarbaig n.k., kumekuwa na msaada wowote kwao tofauti na makabila mengine?
🙏🙏🙏Someni historia zipo wandugu.
Wakati wa utawala wa wajerumani walijenga hilo jengo na likawa ni ofisi zao, walitaka wawe watumia kwa shughuli kama ghafla na sherehe.
Baadae walipokuja waingereza wakapageuza kuwa ni soko kwa wakazi wa Dar-es-Salaam.
Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.Bora umezitaja hizo nchi tatu, maana ni mataifa ambayo idadi ya raia ni chache sana ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika, lakini pia hizo nchi zina makabila machache. hapo ndiyo utaona sababu mambo yao yanaenda vizuri relatively speaking.
Kwa hilo, nakubaliana nawe mkuu.Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.
Tunaweza sema Mtwara iimarishwe ili isaidie Lindi, au Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Katavi isaidie mikoa yote ya kusini kimandeleo.
Ukiangalia nchi yetu mikoa mingi ina fursa kubwa ya kiuchumi ila tatizo lipo kwenye usimamizi wa uchumi na vyanzo vya mapato.
Nakubaliana na wewe. Mikoa ya Tanzania kwa kiasi kikubwa ndiyo kigezo kikubwa cha kutofautisha mipaka ya makabila nchini. Mikoa ingepewa hadhi ya majimbo yajitawale kiuchumi na kisiasa kama ilivyo Nigeria na USA. Hizi ni nchi mbili zenye very diverse population kama Tanzania.Ni kweli, lakini kama nilivyosema hapo juu ukiamua kwamba mikoa ijitegemee kama "pilot project" na uangalie "progress" utaona kwamba waweza kufanikiwa.
Tunaweza sema Mtwara iimarishwe ili isaidie Lindi, au Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Katavi isaidie mikoa yote ya kusini kimandeleo.
Ukiangalia nchi yetu mikoa mingi ina fursa kubwa ya kiuchumi ila tatizo lipo kwenye usimamizi wa uchumi na vyanzo vya mapato.
Olay, we unaonaje kwa upande, alikuwa right or wrongUsije ujatamka hayo mbele ya Trump. Alishawahi kutoa kejeli mbaya sana ya kibaguzi dhidi ya Bara la Afrika.
1. Aliziita nchi za Kiafrika "Shithole countries"
2. Alizitukana nchi za Kiafrika kwa kusema "Afrika inatakiwa itawaliwe tena"
Acha tu mkuu! Jibu ninalo ila silipendi. Bora nikae kimya!!!Olay, we unaonaje kwa upande, alikuwa right or wrong
Naked truthKuna mwamba alisema Afrika hasa kusini mwa jangwa la sahara tukihamishiwa nchi za Ulaya nao wakaletwa kuishi hapa Afrika... Kwamba baada ya miaka 5 tutakuja kuomba msaada nilicheka sana... Ila ni kama. Kuna ukweli ndani yake
By the way... Kwanini wanafunga ubalozi wao!??
Shida ni kwamba walio kwenye nafasi za maamuzi asilimia 98 wapo kwa ajili ya matumbo yao, na baada ya wao kutoka wana tengeneza watu watakao kuja kuendelea kulinda maslahi yao, ndio mfumo walio uweka, ukija ukataka kuwapinga na kufuata haki na kua muadilifu na muwajibikaji utaondoka bila kupendaWatu wameshaanza kuamka. Sasa ni tofauti kidogo na zama za ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI. Si unaona hata wewe mwenyewe unavyokwazika?
Mimi naamini, siku za mbeleni, tena siyo mbali saana, hali itakuwa tofauti sana. Fikra mpya na chanya zinaendelea kuibuka.
Haya, kiongoziAcha tu mkuu! Jibu ninalo ila silipendi. Bora nikae kimya!!!
Mkuu, nashukuru kwa kunielewa.Haya, kiongozi
Baadhi ya Viongozi wa Bara la Afrika ni mafisadi wala rushwa wezi Majambazi na wezi Unafikiri kweli tutaendelea kichumi?Denmark inatarajia kuufunga ubalozi wake nchini Tanzania ifikapo 2024. Ni kati ya nchi ambazo zimekuwa zikiipa Tanzania misaada, tokea ikiitwa Tanganyika hadi sasa ikiwa inajulikana kwa jina adhimu, Tanzania.
Lakini Denmark ni nchi ya namna gani?
Ukifanya ulinganisho, Tanzania imeizidi kwa mambo mengi isipokuwa ujinga na umaskini. Ina rasilimali nyingi sana kuizidi, na hata idadi ya watu tumeipita mbali sana.
Denmark, ni kanchi kadoogo, kenye ukubwa wa kilomita za mraba 42,920 lakini inaizidi kiuchumi Tanzania, nchi Kuubwa kieneo, yenye kilomita za mraba 945,087.
Denmark, ni kanchi kadoogo kenye watu milioni tano lakini inaipa misaada nchi kuubwa, Tanzania, yenye watu milioni sitini na moja.
Ni nini siri ya kanchi kadogo kuizidi nchi kubwa kama Tanzania? Imekuwa ikiisadia Tanzania tokea 1963, enzi hizo ikiitwa Tanganyika, lakini hakuna taarifa ya Tanzania ambayo ni nchi kubwa kuisaidia Denmark kanchi kadogo.
Imewezekanaje kwao lakini kwetu ikashindikana?
Mwingine anaweza kusema ni kwa sababu ya ukoloni, lakini hilo halina mashiko. Hata Korea Kusini ilishawahi kuwa koloni la Japan, lakini kwa sasa wanatukimbiza kiuchumi.
Ni nini walichogundua hao watu weupe ambao weusi wa Tanganyika na Zanzibar hawajagundua?
Angalia, hata eneo la Korea Kusini ni dogo sana ukililinganisha na ukubwa wa Tanzania. Ina kilomita za mraba 100,210 na watu milioni hamsini na moja.
Inawezekanaje kanchi kadoogo, Denmark, kuipa misaada nchi kuubwa, Tanzania?
kupora mali za watu nakuua hakuwezi kuleta maendeleoMagufuli alipotaka kuigeuza Tanzania iwe sawa na nchi za Ulaya mlimfanyaje? Mnataka maendeleo lakini hamtaki namna ya kuyafikia hayo maendeleo. Maendeleo ni malengo, nidhamu, kujitoa mhanga (self sacrifice), bidii ya kazi, uadilifu na kutambua vipaji na ubunifu na kuvitumia ipasavyo. Ulaya wameweza kuviunganisha hivyo vyote kufikia hapo walipo. Sisi hapa bado tunajitafta na akija mwenye mawazo kama hayo bado hatumwelewi. Tutachelewa sana.
Sifa ulizonimwagia ni mtego mkuu🤣.Nimekubali! Una akili sana mkuu!!!
Hata maelezo yako yanatanabaisha hilo. Yaelekea ulikuwa mzuri sana kwenye debate!
Unajua jinsi ya kujenga hoja kutetea kile ulichokidhamiria, hata kama sicho unachomaanisha.
Ni kweli? Usijibu hapa watu wasije wakakuona wewe ni kigeugeu, lakini imeshafahamika kuwa una akili sana bila kujali rangi ya ngozi yako.
Kongole kwako mkuu!