Injini ya Airbus ya Air Tanzania ilipata hitilafu ikiwa angani Februari 24, 2024

Injini ya Airbus ya Air Tanzania ilipata hitilafu ikiwa angani Februari 24, 2024

View attachment 2919531
Abiria 122 wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wamenusurika kifo wakiwa safarini baada ya ndege waliokuwa wamepanda kupata hitilafu kwenye moja ya injini zake.

Ilikuwa Jumamosi Februari 24, 2024, ndege ya ATCL Airbus A220-300 iliyoruka kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya iliponusurika kushika moto baada ya moja ya injini kupata hitilafu na kuanza kutoa moshi.

ATCL imesema tukio hilo limetokea dakika 25 baada ya ndege kuruka na kwamba, marubani na wahudumu walidhibiti hali hiyo na ndege kurejea na kutua salama jijini Dar es Salaam.

Abiria aliyekuwa ndani ya ndege hiyo aliyeomba jina lake lisitajwe, amesema baada ya kuruka umbali wa futi anazokadiria kuwa 12,000 walianza kuhisi harufu ya kitu kinachoungua.

MWANANCHI
Hayo matengenezo yake sasa . huu kama sio mchongo sijui!?
 
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limesema tukio lililotokea katika ndege yake aina ya Airbus A220-300 iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam kwenda jijini Mbeya kupata hitilafu kwenye moja ya injini zake kuwa ni dogo na la kawaida.

Ndege ya shirika hilo namba 106 iliyoanza safari saa 12 jioni Jumamosi Februari 24, mwaka huu, ililazimika kukatisha safari na kurejea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam baada ya injini yake moja kupata hitilafu na kusababisha moshi ndani ya ndege.

“Kuna injini moja ilipata joto sana na ikawa na mafuta mengi ndiyo yaliyosababisha moshi ambao, uliingia kwenye mifumo ya hewa (AC) na ndiyo sababu moshi huo ukawafikia abiria sio ndege kuungua moto kama ilivyoelezwa,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladslaus Matindi alipozungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi, Februari 29, 2024 jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya Mhandisi Matindi inakuja baada ya Mwananchi kuripoti tukio la injini ya ndege hiyo kupata hitilafu na kusababisha taharuki kwa abiria waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.

Baadhi ya abiria waliozungumza na Mwananchi, walieleza kuwa moshi huo ulisababisha taharuki, lakini baadaye marubani na wahudumu wa ndege walifanikiwa kudhibiti na hali kurejea kawaida.

Hata hivyo, ndege hiyo ililazimika kurejea Dar es Salaam na baada ya saa chache baadhi ya abiria waliendelea na safari huku wengine wakibadili tarehe ya safari.
 
Hio ni kawaida sana ?!!! Wapi Huko ?

Kama hii ni kawaida inabidi warekebishe isiwe kawaida
 
Hawa jamaa hawana Akili kabisa.
Nairobi wanapeleka Bombardier then Songwe inaenda Airbus...
 
Ingekua Precision ndo moshi umeonekana wangesema ndege mbovu.
 
Walioahirisha safari Itakuwa walikuwa Makini sana kujua itafika Mbeya salama?
 
  • Mshangao
Reactions: BRB
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limesema tukio lililotokea katika ndege yake aina ya Airbus A220-300 iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam kwenda jijini Mbeya kupata hitilafu kwenye moja ya injini zake kuwa ni dogo na la kawaida.

Ndege ya shirika hilo namba 106 iliyoanza safari saa 12 jioni Jumamosi Februari 24, mwaka huu, ililazimika kukatisha safari na kurejea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam baada ya injini yake moja kupata hitilafu na kusababisha moshi ndani ya ndege.

“Kuna injini moja ilipata joto sana na ikawa na mafuta mengi ndiyo yaliyosababisha moshi ambao, uliingia kwenye mifumo ya hewa (AC) na ndiyo sababu moshi huo ukawafikia abiria sio ndege kuungua moto kama ilivyoelezwa,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladslaus Matindi alipozungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi, Februari 29, 2024 jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya Mhandisi Matindi inakuja baada ya Mwananchi kuripoti tukio la injini ya ndege hiyo kupata hitilafu na kusababisha taharuki kwa abiria waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.

Baadhi ya abiria waliozungumza na Mwananchi, walieleza kuwa moshi huo ulisababisha taharuki, lakini baadaye marubani na wahudumu wa ndege walifanikiwa kudhibiti na hali kurejea kawaida.

Hata hivyo, ndege hiyo ililazimika kurejea Dar es Salaam na baada ya saa chache baadhi ya abiria waliendelea na safari huku wengine wakibadili tarehe ya safari.
Jambo la kawaida halikuwa na sababu ya ndege kurudi Dar, ingeendelea tu na safari, na moshi ndani ya ndege nao ni kawaida mbona kwenye mzinga wa nyuki kunapuliziwa moshi na nyuki hawafi ndivyo hali ilivyokuwa kwa abiria, hawakufa.
 
Kwa kweli. Kutumia injini pungufu maanayake ni emergence na siyo kawaida. Kwani hata kutua kwao waliomba emergency na siyo kawaida
Wenzetu hilo swala wanaitwa waliotengeneza hiyo Engine na kutoa maelekezo ambayo wao wanapewa baada ya kuuliza na si kutoa majibu kama vile iliyogoma ni Engine ya Treni ya mizigo...
 
Hiyo ndege istaafishwe kwa manufaa ya umma imekua na majanga mengi yasiyo tabirika
 
Kweli mkuu, nilikuwa very disappointed last Wednesday flight ya kutoka NBO - Dar ilikuwa Bombardier kelele nyingi sana kwa kweli.
Halafu unasikia Airbus inaenda Songwe.

ATCL ni ngumu sana kupambana na KQ kwenye hili anga la Afrika Mashariki kwasababu wana very poor strategies.
Japo KQ na wao yale ma Embraer yao yanayokuja TZ yamechoka tu.
 
Back
Top Bottom