FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
-
- #101
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 23
SONGA NAYO............
“Niseme kwamba nashukuru sana wazazi wangu kunilea kwenye maadili yaliyokuwa bora na ndiyo yamenifanya mpaka nikakamilisha ndoto yangu ya kuweza kuusomea udaktrai ambao niliuota nikiwa tangu mdogo sana na nilitamani kuweza kuiishi ndoto hiyo siku zote. Pale tunapo ishi kwa pembeni kidogo kuna nyumba moja hivi ambayo yenyewe ni nzuri kiasi kuizidi nyumba yetu, kwenye ile nyumba alikuwa anaishi bibi mmoja ambaye alikuwa mara nyingi sana anakaa nje ya geti kwa sababu palikuwa na mti mkubwa na hapo alipenda kakaa kupumzika akiwa anawasimulia hadithi watoto wachache ambao walikuwa wamemzoea sana wakiwemo na wadogo zangu wote wawili walikuwa wakimpenda sana.
Yule bibi alinizoea sana kwa sababu mara nyingi sana mimi nilikuwa nikimsaidia baadhi ya kazi kama Kwenda sokoni au kwa chochote ambacho yeye alikuwa anakihitaji hivyo ilifanya kwa kiasi kikubwa yeye kuweza kuyajua maisha ya familia yangu hivyo akawa kama mtu wa kunipa ushauri sana ikiwa pomoja na kuwa makini sana na hii dunia hususani wanaume ambao alisema kwamba hawana huruma kabisa na mtoto wa kike hasa yule ambaye wanajua hana msaada kabisa. Baada ya kukata tamaa ya kusoma kabisa nilianza kulipambania lile genge ili familia yangu iweze kuishi angalau kwa kupata uhakika wa chakula, kuna siku akawa ananiuliza maswali mengi sana kuhusu elimu yangu kwani aliona nikiwa kama binti mdogo ambaye nilikuwa na majukumu mazito sana lakini hata hivyo nilitakiwa kuwa shule kwa ule wakati basi sikuwa na namna zaidi ya kumpa maelezo yote pamoja namaamuzi ambayo mimi nilikuwa nimeyachukua baada ya kuona kwamba sina namna nyingine ya kuweza kugharamikia kusoma.
Baada ya maelezo yangu aliniuliza swali moja tu ambalo nadhani lilienda kuikamilisha ndoto yangu hiyo
“Unapenda kusoma?”
“Ndiyo tena sana natamani sana niwe kwenye orodha ya watu wasomi nchini”
“Unataka kusoma nini na wapi?”
“Kwa sasa siwezi tena ili nilitamani sana nisomee udakitari Mhimbili”
“Masomo yao ya mhula huu yanaanza lini?”
“Walianza juzi jumatatu kwa sababu ndio muda ambao ilitakiwa nifanyiwe usahili lakini sina pesa”
“Jiandae kesho tunaenda na mimi”
“Wapi?”
“Wewe si umesema unataka kusoma?”
“Ndiyo bibi ila mimi sina pesa ya kufanyia hivyo” aliijua hofu yangu alitabasamu na kuitoa simu yake kwenye kimkoba chake kidogo kisha akavaa miwani, alikuwa ni bibi lakini cha ajabu alikuwa na simu ya kisasa kabisa, aliipiga mahali ambapo sikujua kwamba ni wapi
“Joseph kesho nakuja na mwanangu hapo hospitalini anakuja kuanza masomo, sio muda sana nakutumia taarifa zake zote hakikisha unaandaa kila kitu pesa nakuingizia baadae ya ada na kingine sitaki kuja kusikia huyu binti anasumbuliwa mchukulie kama mdogo wako na hakikisha unampa kila anacho kitaka anapokuwa anasoma na nisije nikasikia kitu chochote cha kijinga kimempata utajuta” alitoa maelezo ambayo mimi yaliniacha mdomo wazi kwa sababu sikuwahi kufikiria kama bibi huyo ana mamlaka sehemu yoyote ile kwa namna alivyokuwa akiishi maisha ya kawaida sana, baada ya kukata simu yeye ndiye aliye nishtua kwenye mshangao ambao mimi nilikuwa nimemezwa nao mpaka wakati huo, kwangu kila kitu kilikuwa kama ndoto ambayo haikuwa ya kweli.
“Haya jiandae mjukuu wangu uyaanze maisha ya ndoto zako na hakikisha ukienda huko haufanyi ujinga wowote ule, naona kwa siku zangu chache ambazo nimebakisha naweza nikakusaidia ukatimiza ndoto zako nahisi nitafurahia sana kama hilo litatimia kabla ya mimi kufa” alitamka huku akiwa ananishika kichwani kama kunipa baraka, wakati wote huo nilikuwa nimepiga magoti nikiwa nalia sikuamini kama naweza kupata neema kubwa sana kama hiyo kwenye maisha yangu ambayo sikuitegemea kabisa kutoka sehemu yoyote ile
“Bibi hivi unacho kiongea kina ukweli wowote ule?” niliuliza nikiwa nina hamu kubwa sana isiwe alikuwa ananitania maana kwa namna nilivyokuwa ninamuona sikudhani kama angeweza kunilipia ada ya kusoma sehemu kama mhimbili, kwa mwaka ada tu ilikuwa ni kama milioni tano za kitanzania ukitoa na vitu vingine kama usafiri na chakula.
“Nilipokuwa binti mdogo kama wewe niliyaishi maisha ambayo yalinipa somo kubwa sana kwenye maisha yangu, wanaume walinitumia watakavyo wao kwa sababu sikuwa na chochote kitu, kwa sababu waliamua kunifanya mimi sehemu ya kupumzikia hivyo namimi niliamua kuwatumia wao ili nifanikiwe, nilichagua wanaume wenye pesa tu ndio ambao nilikuwa tayari kufanya kila ambacho walikuwa wakihitaji kunifanyia, sio kwamba nilipenda hapana bali kwa maisha ambayo nilikuwa naishi yalikuwa yamejaa dharau, dhihaka, kuonewa na kudhalilishwa hivyo niliamua kuutafuta utajiri kwa namna yoyote ile huku nikiwa na hasira sana na maisha haya ya kudhalilishwa kila siku. Hiyo ilinifanya nitumike sana unaweza ukahisi kwamba nilikuwa pekeyangu ila nilikuwa na ndugu wa kutosha tu na wengine walikuwa nauwezo hata wa kunisaidia lakini hawakufanya hivyo walinifungia vioo vyao kwamba hawaniju namimi niliamua kuishi kama vile nipo mwenyewe hapa duniani”
“Kwenye shughuli zangu za kuutafuta utajiri nilifanikiwa kukutana na mwanaume mmoja ambaye alikuwa tajiri mkubwa sana, huyo mwanaume alinipenda sana, alinifanyia kila kitu na kunifanya nijutie kuyaishi maisha yale ya nyuma na huyo ndiye ambaye alikuja kuwa mume wangu wa ndoa kabisa na tulibahatika kupata watoto wawili wa kike mmoja na wa kiume mmoja, huwa sipendi sana kukumbuka kuhusu wanangu ila wote wametangulia mbele za haki pamoja na mume wangu hivyo kwa sasa nipo mimi na wajukuu zangu watatu ambapo wawili ni wa kike na mmoja ni wa kiume na wote wapo nje ya nchi wanasoma huko nadhani baada ya miaka miwili watakuwa wamemaliza hivyo watarudi tena kuungana na mimi. Mume wangu wakati anakufa aliniacha na utajiri mkubwa sana ambao mpaka hivi sasa ninavyo ongea na wewe upo wa kutosha ila nimewaandalia wajukuu zangu ndio maana nimewasomesha kwa nguvu sana ili kila mtu awe na uwezo mkubwa wa kuuendesha utajiri wake nikifa”
“Wewe hapo siyo mjukuu wangu ila nikikuona hauna tofauti sana na wajukuu zangu hivyo kwa mazingira ambayo umeyapitia imeniuma sana ndiyo maana nimetamani sana nikusaidie utimize walau ndoto zako za kuwa msomi mkubwa na kama nipo hai hata baada ya kumaliza masomo yako basi utasema unataka kuajiriwa wapi na siku hiyo hiyo utapata kazi ila zingatia sana masomo na tabia njema kwa sababu tabia yako nzuri ndiyo iliyo nivutia sana kuweza kukusaidia, wewe ni binti mwenye moyo wa pekee sana upo tayari ukose ili wenzako wapate umenivutia sana nadhani kwa sasa nitakuweka kwenye orodha ya wajukuu zangu na siku moja wakirudi muonane wakutambue kama ni moja ya ndugu yao ili hata nikiondoka utakuwa mikono salama maana watakusaidia kwa vitu vingi sana, haya nimechoka mimi njoo ndani huku uchukue kiasi ambacho kitawasaidia wazazi wako pindi utakapokuwa shule huko na ukirudi kama siku ukiwa na muda ndipo utakuwa unaenda kufanya hiyo biashara yako ya genge” aliongea na kuanza kuondoka pale alipokuwa amekaa, kiukweli nilibaki pale nimeduwaa sana kwanza sikuwahi kuamini kwamba bibi kama huyo angekuwa mtu tajiri kama yeye alivyokuwa anasema, nilimfuata ndani nikiwa na furaha kubwa sana na hiyo ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza kuweza kuingia ndani ya nyumba yake hiyo, ilikuwa ni ya kawaida sana kwa nje ila kwa ndani ilikuwa imepambwa kwa thamani za gharama sana, kuna swali ambalo nilitamani sana nilipatie majibu kwa wakati ule hivyo ilinilazimu kumuuliza
"Bibi sasa kwanini umechagua kuja kuishi sehemu ya kawaida kama hii” baada ya lile swali alitabasamu sana huku akiwa ananikabidhi bahasha yenye pesa
“Mjukuu wangu kwenye haya maisha kabla mimi sina pesa niliwahi kuamini pesa ndiyo kila kitu, ni kweli kama una maisha ,magumu pesa ni kila kitu kwako kwa sababu unaihitaji kuliko hata unavyo uhitaji uhai wako lakini siku ukiwa una pesa ndiyo unakuja kujua kwamba pesa siyo kila kitu kwa sababu furaha ndiyo inakamilisha sehemu ya maisha yote ya mwanadamu, baada ya kuwa na pesa za kutosha na kuanza kuyaishi maisha ya kitajiri hususani baada ya mume wangu kufa niligundua kwamba pesa haikuwa sehemu ya furaha kubwa kwenye maisha japo kama nisingekuwa na pesa bado nisingeishi kwa furaha hivyo hiyo inakuhakikishia kwamba hakikisha una pesa kwanza ndipo mengine yafuate. Hiyo ndiyo sababu niliwalea wajukuu wangu kwenye maisha mazuri sana na ndio waliokuwa wananifanya nakuwa na furaha muda wote wakiwa karibu yangu, walivyokuwa wanaenda shule niliona kabisa maisha yangu yatakuwa magumu sana kwa sababu niliona nitakosa mtu wa kuwa naye karibu ndiyo maana niliamua kuitafuta furaha yangu mwenyewe sehemu ambayo naweza nikapata nafasi ya kukutana na watu kirahisi sana hususani watoto wadogo”
“Maisha yangu ya kuishi masaki yalinifanya muda mwingi sana niwe nashinda ndani tu au Kwenda hotelini au kufurahi mara moja moja lakini licha ya pesa zote hizo bado nilikuwa nipo mpweke sana muda mwingi ndipo nilipo amua kuhamia eneo kama hili ambalo nimefanikiwa mpaka kukutana na nyie” maelezo yake yalinipa funzo kubwa sana na huo ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kuipata elimu ambayo mpaka sasa ninayo. Yule bibi alinisomesha kwa miaka mitano yote na sikutoa kitu chochote kile kwenye kuipata ile elimu kwangu alikuwa ni mtetezi na mkombozi wa maisha yangu.
Nilifanikiwa kumaliza masomo yangu kwa hiyo miaka mitano huku nikiwa nasaidiwa kila kitu na yule bibi hata pale kwenye familia yetu yeye ndiye aliyekuwa anatusaidia sana, aliwaanzisha mpaka shule wadogo zangu, shule ambazo kidogo zilikuwa na unafuu na kwa miaka yote ile mitano pale nyumbani kidogo palikuwa na unafuu mkubwa sana kwa sababu yake na hiyo kiasi fulani ilirejesha tumaini jipya la maisha, alifanikiwa kunikutanisha na hao wajukuu zake ambao kiukweli hawakuwa wema sana kwa sababu nadhani kwa sababu ya ubinafsi wao na kwakweli sijawahi kuwalaumu kwa sababu zilikuwa ni mali zao. Nilivyo maliza masomo yangu hali yake haikuwa nzuri sana kiafya na alikuwa amerudi Masaki ambako ndiko walikokuwa wanaishi wajukuu zake, akiwa huko niliwasiliana naye mara moja tu ambapo kwa mwezi unao kuja alinihakikishia kwamba nilitakiwa kuanza kazi pale pale mhimbili kuna vijana wake wengi sana hivyo akiwa sawa basi atawasiliana nao nikaanze kazi, nilikuwa namuombea sana nadhani kuliko hata ndugu zake na nilikuwa naenda kuikamilisha ndoto yangu na kuisaidia familia yangu kutoka kwenye yale maisha ya taabu ambayo tuliyapitia kwa miaka kadhaa baada ya kuchukuliwa kila kilichokuwa cha kwetu.
Bahati mbaya sana ilikuwa upande wangu, ikiwa imebakia wiki moja ili ufike muda ambao aliniambia atawasiliana na vijana wake nianze kazi pale mhimbili ambao kiuhalisia zaidi ya yule Joseph ambaye alinitambulisha kama kijana ambaye aliwasaidia sana wazazi wake kufanikiwa kwenye maisha yao ndiyo maana yule kijana alikuwa anamheshimu sana hata mimi kwenda kusoma pale ilikuwa ni kwa sababu huyo kijana alikuwa anamheshimu sana yule bibi, kijana ambaye alibahatika kupata ajira pale akiwa bado ni kijana mdogo sana, ilikuwa ni usiku was aa 7 ambao nilipokea sms kutoka kwa moja ya wajukuu zake ambaye alinipa taarifa kwamba bibi yao alikuwa amekufa ila alinionya kwamba nisije nikasogea kwenye familia yao maana zile mali hazinihusu kabisa ilikuwa ni haki yao, nilimuomba nihudhurie tu msiba ya yule bibi lakini ilishindikana ilifika mahali nilitishiwa mpaka kuuliwa na sikuwa nikijua msiba ungefanyikia wapi kwa sababu hata Masaki ambapo nilipajua kwamba ni nyumbani kwake ukiacha pale Mbagala sikuweza kumkuta mtu yeyote hivyo mimi na ile familia tukawa tumeishia pale kufanya mawasiliano kwani hata ile nyumba ya Mbagala waliiuza baada ya wiki moja na sikuwahi kuwaona tena licha ya kuwatafuta sana.
Ndoto zangu za kupata kazi zilianza kuyeyuka sana na hata maisha ya nyumbani yalianza kuwa magumu kama mwanzo baada ya yule bibi kufariki, nilijaribu sana Kwenda pale mhimbili kukutana na Joseph cha ajabu naye alinikataa kama hanijui kabisa vinginevyo alidai kwamba nikae kwake kwa wiki moja nimpe mwili wangu ili nipate kazi, hiyo kwangu ilikuwa ni zaidi ya udhalilishaji nilimkataa kabisa na hapo ni kama niliharibu sana maana alienda kunichafulia jina langu kwenye hospitali nzima maana hata wale watu ambao nilijuana nao kipindi nasoma walinikataa kabisa. Wadogo zangu waliacha shule kwanza ili nipambane na maisha ya mtaani kama ninaweza kupata ada zao na tegemeo langu kubwa ilikuwa ni kupata kazi kwanza hiyo ingenifanya niwe na uhakika wa kuwasomesha lakini ilishindikana, nimezunguka kwenye taasisi nyingi sana kwa mwaka mzima lakini kote nimeishia kuona unyanyasaji mkubwa kwa sababu wanahitaji kwanza hongo ya penzi ndipo kaz itolewe cha ajabu hata wanawake wenzangu nao wananibania mpaka imefika hatua nimeamua kukata tamaa ya kazi. Nilirudi kwenye lile genge la mama la zamani lakini kwa wakati huu hakuna biashara ambayo inaenda hivyo imefanya maisha kuwa magumu sana kwa upande wetu kwa sasa hata wadogo zangu hawasomi tena juzi ulipo nipatia ile pesa nimeenda kuliboresha genge pamoja na kununua mahitaji mengine ya mhimu ya nyumbani kidogo hali imekuwa angalau niombe nikushukuru tena kwa hilo.
Mimi sijawahi kuwa jasiri sana mpaka kumwambia mwanaume maneno kama niliyo kwambia siku ile ila nilivutiwa sana na upole wako machoni na usoni ndiyo maana nilikuja kukuongelesha vile nikihisi huenda ulikuwa upo pale kuwaangalia wanawake hata hivyo sikuwa na maana kwamba ungefanya mapenzi na mimi ila nilitaka nifanye namna yoyote ile ili nipate pesa japo sikuwa tayari kuutoa mwili wangu maana siku ile mdogo wangu alikuwa anaumwa sana na sikuwa na chochote mfukoni hivyo nilitaka nitumie akili ili kuzipata pesa naomba unisamehe sana na namshukuru sana MUNGU kwa kukuleta kwenye maisha yangu” hadithi ndefu yenye kusikitisha sana ya maisha ya Nairah waweza kumuita Nurryat aliihitimisha na kilio kizito sana ambacho kilimfanya ampe kazi Jason ya kuanza kumbembeleza mwanamke huyo.
Vipi kuna tukio gani baya au hali gani ya kusikitisha ya maisha ambayo umewahi kuipitia hata iweje hauji kuisahau kabisa kwenye maisha yako yote mpaka unakufa?
Sehemu ya 23 sina la ziada tena tukutane wakati ujao ndani ya INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
Wasalaam
Bux the storyteller.
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 23
SONGA NAYO............
“Niseme kwamba nashukuru sana wazazi wangu kunilea kwenye maadili yaliyokuwa bora na ndiyo yamenifanya mpaka nikakamilisha ndoto yangu ya kuweza kuusomea udaktrai ambao niliuota nikiwa tangu mdogo sana na nilitamani kuweza kuiishi ndoto hiyo siku zote. Pale tunapo ishi kwa pembeni kidogo kuna nyumba moja hivi ambayo yenyewe ni nzuri kiasi kuizidi nyumba yetu, kwenye ile nyumba alikuwa anaishi bibi mmoja ambaye alikuwa mara nyingi sana anakaa nje ya geti kwa sababu palikuwa na mti mkubwa na hapo alipenda kakaa kupumzika akiwa anawasimulia hadithi watoto wachache ambao walikuwa wamemzoea sana wakiwemo na wadogo zangu wote wawili walikuwa wakimpenda sana.
Yule bibi alinizoea sana kwa sababu mara nyingi sana mimi nilikuwa nikimsaidia baadhi ya kazi kama Kwenda sokoni au kwa chochote ambacho yeye alikuwa anakihitaji hivyo ilifanya kwa kiasi kikubwa yeye kuweza kuyajua maisha ya familia yangu hivyo akawa kama mtu wa kunipa ushauri sana ikiwa pomoja na kuwa makini sana na hii dunia hususani wanaume ambao alisema kwamba hawana huruma kabisa na mtoto wa kike hasa yule ambaye wanajua hana msaada kabisa. Baada ya kukata tamaa ya kusoma kabisa nilianza kulipambania lile genge ili familia yangu iweze kuishi angalau kwa kupata uhakika wa chakula, kuna siku akawa ananiuliza maswali mengi sana kuhusu elimu yangu kwani aliona nikiwa kama binti mdogo ambaye nilikuwa na majukumu mazito sana lakini hata hivyo nilitakiwa kuwa shule kwa ule wakati basi sikuwa na namna zaidi ya kumpa maelezo yote pamoja namaamuzi ambayo mimi nilikuwa nimeyachukua baada ya kuona kwamba sina namna nyingine ya kuweza kugharamikia kusoma.
Baada ya maelezo yangu aliniuliza swali moja tu ambalo nadhani lilienda kuikamilisha ndoto yangu hiyo
“Unapenda kusoma?”
“Ndiyo tena sana natamani sana niwe kwenye orodha ya watu wasomi nchini”
“Unataka kusoma nini na wapi?”
“Kwa sasa siwezi tena ili nilitamani sana nisomee udakitari Mhimbili”
“Masomo yao ya mhula huu yanaanza lini?”
“Walianza juzi jumatatu kwa sababu ndio muda ambao ilitakiwa nifanyiwe usahili lakini sina pesa”
“Jiandae kesho tunaenda na mimi”
“Wapi?”
“Wewe si umesema unataka kusoma?”
“Ndiyo bibi ila mimi sina pesa ya kufanyia hivyo” aliijua hofu yangu alitabasamu na kuitoa simu yake kwenye kimkoba chake kidogo kisha akavaa miwani, alikuwa ni bibi lakini cha ajabu alikuwa na simu ya kisasa kabisa, aliipiga mahali ambapo sikujua kwamba ni wapi
“Joseph kesho nakuja na mwanangu hapo hospitalini anakuja kuanza masomo, sio muda sana nakutumia taarifa zake zote hakikisha unaandaa kila kitu pesa nakuingizia baadae ya ada na kingine sitaki kuja kusikia huyu binti anasumbuliwa mchukulie kama mdogo wako na hakikisha unampa kila anacho kitaka anapokuwa anasoma na nisije nikasikia kitu chochote cha kijinga kimempata utajuta” alitoa maelezo ambayo mimi yaliniacha mdomo wazi kwa sababu sikuwahi kufikiria kama bibi huyo ana mamlaka sehemu yoyote ile kwa namna alivyokuwa akiishi maisha ya kawaida sana, baada ya kukata simu yeye ndiye aliye nishtua kwenye mshangao ambao mimi nilikuwa nimemezwa nao mpaka wakati huo, kwangu kila kitu kilikuwa kama ndoto ambayo haikuwa ya kweli.
“Haya jiandae mjukuu wangu uyaanze maisha ya ndoto zako na hakikisha ukienda huko haufanyi ujinga wowote ule, naona kwa siku zangu chache ambazo nimebakisha naweza nikakusaidia ukatimiza ndoto zako nahisi nitafurahia sana kama hilo litatimia kabla ya mimi kufa” alitamka huku akiwa ananishika kichwani kama kunipa baraka, wakati wote huo nilikuwa nimepiga magoti nikiwa nalia sikuamini kama naweza kupata neema kubwa sana kama hiyo kwenye maisha yangu ambayo sikuitegemea kabisa kutoka sehemu yoyote ile
“Bibi hivi unacho kiongea kina ukweli wowote ule?” niliuliza nikiwa nina hamu kubwa sana isiwe alikuwa ananitania maana kwa namna nilivyokuwa ninamuona sikudhani kama angeweza kunilipia ada ya kusoma sehemu kama mhimbili, kwa mwaka ada tu ilikuwa ni kama milioni tano za kitanzania ukitoa na vitu vingine kama usafiri na chakula.
“Nilipokuwa binti mdogo kama wewe niliyaishi maisha ambayo yalinipa somo kubwa sana kwenye maisha yangu, wanaume walinitumia watakavyo wao kwa sababu sikuwa na chochote kitu, kwa sababu waliamua kunifanya mimi sehemu ya kupumzikia hivyo namimi niliamua kuwatumia wao ili nifanikiwe, nilichagua wanaume wenye pesa tu ndio ambao nilikuwa tayari kufanya kila ambacho walikuwa wakihitaji kunifanyia, sio kwamba nilipenda hapana bali kwa maisha ambayo nilikuwa naishi yalikuwa yamejaa dharau, dhihaka, kuonewa na kudhalilishwa hivyo niliamua kuutafuta utajiri kwa namna yoyote ile huku nikiwa na hasira sana na maisha haya ya kudhalilishwa kila siku. Hiyo ilinifanya nitumike sana unaweza ukahisi kwamba nilikuwa pekeyangu ila nilikuwa na ndugu wa kutosha tu na wengine walikuwa nauwezo hata wa kunisaidia lakini hawakufanya hivyo walinifungia vioo vyao kwamba hawaniju namimi niliamua kuishi kama vile nipo mwenyewe hapa duniani”
“Kwenye shughuli zangu za kuutafuta utajiri nilifanikiwa kukutana na mwanaume mmoja ambaye alikuwa tajiri mkubwa sana, huyo mwanaume alinipenda sana, alinifanyia kila kitu na kunifanya nijutie kuyaishi maisha yale ya nyuma na huyo ndiye ambaye alikuja kuwa mume wangu wa ndoa kabisa na tulibahatika kupata watoto wawili wa kike mmoja na wa kiume mmoja, huwa sipendi sana kukumbuka kuhusu wanangu ila wote wametangulia mbele za haki pamoja na mume wangu hivyo kwa sasa nipo mimi na wajukuu zangu watatu ambapo wawili ni wa kike na mmoja ni wa kiume na wote wapo nje ya nchi wanasoma huko nadhani baada ya miaka miwili watakuwa wamemaliza hivyo watarudi tena kuungana na mimi. Mume wangu wakati anakufa aliniacha na utajiri mkubwa sana ambao mpaka hivi sasa ninavyo ongea na wewe upo wa kutosha ila nimewaandalia wajukuu zangu ndio maana nimewasomesha kwa nguvu sana ili kila mtu awe na uwezo mkubwa wa kuuendesha utajiri wake nikifa”
“Wewe hapo siyo mjukuu wangu ila nikikuona hauna tofauti sana na wajukuu zangu hivyo kwa mazingira ambayo umeyapitia imeniuma sana ndiyo maana nimetamani sana nikusaidie utimize walau ndoto zako za kuwa msomi mkubwa na kama nipo hai hata baada ya kumaliza masomo yako basi utasema unataka kuajiriwa wapi na siku hiyo hiyo utapata kazi ila zingatia sana masomo na tabia njema kwa sababu tabia yako nzuri ndiyo iliyo nivutia sana kuweza kukusaidia, wewe ni binti mwenye moyo wa pekee sana upo tayari ukose ili wenzako wapate umenivutia sana nadhani kwa sasa nitakuweka kwenye orodha ya wajukuu zangu na siku moja wakirudi muonane wakutambue kama ni moja ya ndugu yao ili hata nikiondoka utakuwa mikono salama maana watakusaidia kwa vitu vingi sana, haya nimechoka mimi njoo ndani huku uchukue kiasi ambacho kitawasaidia wazazi wako pindi utakapokuwa shule huko na ukirudi kama siku ukiwa na muda ndipo utakuwa unaenda kufanya hiyo biashara yako ya genge” aliongea na kuanza kuondoka pale alipokuwa amekaa, kiukweli nilibaki pale nimeduwaa sana kwanza sikuwahi kuamini kwamba bibi kama huyo angekuwa mtu tajiri kama yeye alivyokuwa anasema, nilimfuata ndani nikiwa na furaha kubwa sana na hiyo ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza kuweza kuingia ndani ya nyumba yake hiyo, ilikuwa ni ya kawaida sana kwa nje ila kwa ndani ilikuwa imepambwa kwa thamani za gharama sana, kuna swali ambalo nilitamani sana nilipatie majibu kwa wakati ule hivyo ilinilazimu kumuuliza
"Bibi sasa kwanini umechagua kuja kuishi sehemu ya kawaida kama hii” baada ya lile swali alitabasamu sana huku akiwa ananikabidhi bahasha yenye pesa
“Mjukuu wangu kwenye haya maisha kabla mimi sina pesa niliwahi kuamini pesa ndiyo kila kitu, ni kweli kama una maisha ,magumu pesa ni kila kitu kwako kwa sababu unaihitaji kuliko hata unavyo uhitaji uhai wako lakini siku ukiwa una pesa ndiyo unakuja kujua kwamba pesa siyo kila kitu kwa sababu furaha ndiyo inakamilisha sehemu ya maisha yote ya mwanadamu, baada ya kuwa na pesa za kutosha na kuanza kuyaishi maisha ya kitajiri hususani baada ya mume wangu kufa niligundua kwamba pesa haikuwa sehemu ya furaha kubwa kwenye maisha japo kama nisingekuwa na pesa bado nisingeishi kwa furaha hivyo hiyo inakuhakikishia kwamba hakikisha una pesa kwanza ndipo mengine yafuate. Hiyo ndiyo sababu niliwalea wajukuu wangu kwenye maisha mazuri sana na ndio waliokuwa wananifanya nakuwa na furaha muda wote wakiwa karibu yangu, walivyokuwa wanaenda shule niliona kabisa maisha yangu yatakuwa magumu sana kwa sababu niliona nitakosa mtu wa kuwa naye karibu ndiyo maana niliamua kuitafuta furaha yangu mwenyewe sehemu ambayo naweza nikapata nafasi ya kukutana na watu kirahisi sana hususani watoto wadogo”
“Maisha yangu ya kuishi masaki yalinifanya muda mwingi sana niwe nashinda ndani tu au Kwenda hotelini au kufurahi mara moja moja lakini licha ya pesa zote hizo bado nilikuwa nipo mpweke sana muda mwingi ndipo nilipo amua kuhamia eneo kama hili ambalo nimefanikiwa mpaka kukutana na nyie” maelezo yake yalinipa funzo kubwa sana na huo ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kuipata elimu ambayo mpaka sasa ninayo. Yule bibi alinisomesha kwa miaka mitano yote na sikutoa kitu chochote kile kwenye kuipata ile elimu kwangu alikuwa ni mtetezi na mkombozi wa maisha yangu.
Nilifanikiwa kumaliza masomo yangu kwa hiyo miaka mitano huku nikiwa nasaidiwa kila kitu na yule bibi hata pale kwenye familia yetu yeye ndiye aliyekuwa anatusaidia sana, aliwaanzisha mpaka shule wadogo zangu, shule ambazo kidogo zilikuwa na unafuu na kwa miaka yote ile mitano pale nyumbani kidogo palikuwa na unafuu mkubwa sana kwa sababu yake na hiyo kiasi fulani ilirejesha tumaini jipya la maisha, alifanikiwa kunikutanisha na hao wajukuu zake ambao kiukweli hawakuwa wema sana kwa sababu nadhani kwa sababu ya ubinafsi wao na kwakweli sijawahi kuwalaumu kwa sababu zilikuwa ni mali zao. Nilivyo maliza masomo yangu hali yake haikuwa nzuri sana kiafya na alikuwa amerudi Masaki ambako ndiko walikokuwa wanaishi wajukuu zake, akiwa huko niliwasiliana naye mara moja tu ambapo kwa mwezi unao kuja alinihakikishia kwamba nilitakiwa kuanza kazi pale pale mhimbili kuna vijana wake wengi sana hivyo akiwa sawa basi atawasiliana nao nikaanze kazi, nilikuwa namuombea sana nadhani kuliko hata ndugu zake na nilikuwa naenda kuikamilisha ndoto yangu na kuisaidia familia yangu kutoka kwenye yale maisha ya taabu ambayo tuliyapitia kwa miaka kadhaa baada ya kuchukuliwa kila kilichokuwa cha kwetu.
Bahati mbaya sana ilikuwa upande wangu, ikiwa imebakia wiki moja ili ufike muda ambao aliniambia atawasiliana na vijana wake nianze kazi pale mhimbili ambao kiuhalisia zaidi ya yule Joseph ambaye alinitambulisha kama kijana ambaye aliwasaidia sana wazazi wake kufanikiwa kwenye maisha yao ndiyo maana yule kijana alikuwa anamheshimu sana hata mimi kwenda kusoma pale ilikuwa ni kwa sababu huyo kijana alikuwa anamheshimu sana yule bibi, kijana ambaye alibahatika kupata ajira pale akiwa bado ni kijana mdogo sana, ilikuwa ni usiku was aa 7 ambao nilipokea sms kutoka kwa moja ya wajukuu zake ambaye alinipa taarifa kwamba bibi yao alikuwa amekufa ila alinionya kwamba nisije nikasogea kwenye familia yao maana zile mali hazinihusu kabisa ilikuwa ni haki yao, nilimuomba nihudhurie tu msiba ya yule bibi lakini ilishindikana ilifika mahali nilitishiwa mpaka kuuliwa na sikuwa nikijua msiba ungefanyikia wapi kwa sababu hata Masaki ambapo nilipajua kwamba ni nyumbani kwake ukiacha pale Mbagala sikuweza kumkuta mtu yeyote hivyo mimi na ile familia tukawa tumeishia pale kufanya mawasiliano kwani hata ile nyumba ya Mbagala waliiuza baada ya wiki moja na sikuwahi kuwaona tena licha ya kuwatafuta sana.
Ndoto zangu za kupata kazi zilianza kuyeyuka sana na hata maisha ya nyumbani yalianza kuwa magumu kama mwanzo baada ya yule bibi kufariki, nilijaribu sana Kwenda pale mhimbili kukutana na Joseph cha ajabu naye alinikataa kama hanijui kabisa vinginevyo alidai kwamba nikae kwake kwa wiki moja nimpe mwili wangu ili nipate kazi, hiyo kwangu ilikuwa ni zaidi ya udhalilishaji nilimkataa kabisa na hapo ni kama niliharibu sana maana alienda kunichafulia jina langu kwenye hospitali nzima maana hata wale watu ambao nilijuana nao kipindi nasoma walinikataa kabisa. Wadogo zangu waliacha shule kwanza ili nipambane na maisha ya mtaani kama ninaweza kupata ada zao na tegemeo langu kubwa ilikuwa ni kupata kazi kwanza hiyo ingenifanya niwe na uhakika wa kuwasomesha lakini ilishindikana, nimezunguka kwenye taasisi nyingi sana kwa mwaka mzima lakini kote nimeishia kuona unyanyasaji mkubwa kwa sababu wanahitaji kwanza hongo ya penzi ndipo kaz itolewe cha ajabu hata wanawake wenzangu nao wananibania mpaka imefika hatua nimeamua kukata tamaa ya kazi. Nilirudi kwenye lile genge la mama la zamani lakini kwa wakati huu hakuna biashara ambayo inaenda hivyo imefanya maisha kuwa magumu sana kwa upande wetu kwa sasa hata wadogo zangu hawasomi tena juzi ulipo nipatia ile pesa nimeenda kuliboresha genge pamoja na kununua mahitaji mengine ya mhimu ya nyumbani kidogo hali imekuwa angalau niombe nikushukuru tena kwa hilo.
Mimi sijawahi kuwa jasiri sana mpaka kumwambia mwanaume maneno kama niliyo kwambia siku ile ila nilivutiwa sana na upole wako machoni na usoni ndiyo maana nilikuja kukuongelesha vile nikihisi huenda ulikuwa upo pale kuwaangalia wanawake hata hivyo sikuwa na maana kwamba ungefanya mapenzi na mimi ila nilitaka nifanye namna yoyote ile ili nipate pesa japo sikuwa tayari kuutoa mwili wangu maana siku ile mdogo wangu alikuwa anaumwa sana na sikuwa na chochote mfukoni hivyo nilitaka nitumie akili ili kuzipata pesa naomba unisamehe sana na namshukuru sana MUNGU kwa kukuleta kwenye maisha yangu” hadithi ndefu yenye kusikitisha sana ya maisha ya Nairah waweza kumuita Nurryat aliihitimisha na kilio kizito sana ambacho kilimfanya ampe kazi Jason ya kuanza kumbembeleza mwanamke huyo.
Vipi kuna tukio gani baya au hali gani ya kusikitisha ya maisha ambayo umewahi kuipitia hata iweje hauji kuisahau kabisa kwenye maisha yako yote mpaka unakufa?
Sehemu ya 23 sina la ziada tena tukutane wakati ujao ndani ya INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
Wasalaam
Bux the storyteller.