STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 20
SONGA NAYO............
Jason baada ya kufika nje ya Ikulu, kulikuwa na gari moja ya bei ghali sana yenye namba za Ikulu ilikuwa ikimsubiri yeye ili impeleke mahali ambapo alitakiwa Kwenda kupumzika usiku wa siku hiyo, aliingia humo ndani ambamo kulikuwa na dereva mmoja tu ila hakuwa tu dereva alikuwa ni komando ambaye alipewa kazi ya kuhakikisha anamfikisha mwanaume huyo salama sehemu yoyote ambayo angetakiwa Kwenda kwa muda wowote ule.
“Nadhani umeambiwa sehemu ambayo unatakiwa kunipeleka” aliongea Jason kwa sauti yake nzito sana
“Ndiyo mheshimiwa” mwanaume huyo aliyekuwa naye kwenye suti nzito nyeusi alijibu huku akiwa anaiwasha gari hiyo na kuanza kuondoka lakini aliombwa kusimamisha gari hiyo baada ya Jason kuona simu yake inaita na namba ilikuwa ni ngeni, aliiangalia kwa sekunde thelathini baada ya kuona inaendelea kuita tu aliamua kuipokea.
“Hello” sauti ya mtume ilisikika upande wa pili, sauti isiyokuwa na hatia yoyote ndani ya ulimwengu, ni sauti laini sana ambayo iliweza kumsulubu Samson akasahau kwamba kuna siri hakutakiwa kuzitoa, ni lafudhi ambayo haikuwa ikiumiza masikio pale mtu yeyote anapo pata bahati ya kuisikia, Jason alitulia baada ya kuisikia sauti hiyo ya kike ambayo ilikuwa na utulivu mkubwa sana ndani yake.
“Naongea na nani?” mwanaume alitamka baada ya kuwaza sana lakini hakuweza kuitambua sauti hiyo
“Nayrah” hili jina lilimfanya aumize ubongo wake haraka haraka ili aweze kuona kama anaweza kukumbuka mahali alipokutana na mwanamke mwenye jina kama hilo, ndipo ubongo ulipo msafirisha mpaka maeneo ya Mbagala wakati ameenda kuonana na ASP Bakari Zalimo alitabasamu kwa mbali.
“Ooooh nambie Nayrah”
“Samahani naweza kukuona?”
“Muda huu?”
“Ndiyo”
“Ok nipe nusu saa nakuja nitakuwa pale uwanjani nilipo kukuta siku ile ndani ya huo muda”
“Sawa” alishusha pumzi ndefu sana kisha kaangalia saa yake
“Kuna sehemu ambayo tunaweza kupata nguo za kawaida kwa muda huu?” alimshtua dereva huyo kwa sauti hiyo nzito.
“Ndiyo kiongozi kuna maduka yatakuwa wazi bado mapema sana saivi Kariakoo hapo hata njiani zinapatikana”
“Basi naomba tupite huko ukanichukulie nguo za kawaida kisha wewe utaniacha hiyo sehemu baada ya kunipa hizo nguo”
“Lakini mheshimiwa ameniambia nihakikishe ulinzi wako na kuhakikisha unafika salama sasa nitamweleza nini akiniuliza”
“Mwambie mimi ndiye niliyekupa maagizo uniache mwenyewe sihitaji kuwa na mtu yeyote yule kwa huu muda”
“Sawa kiongozi” Basi safari ilianza kuelekea Kariakoo ambapo gari yao ilikuwa ipo taratibu sana ili wahakikishe wanafanikiwa kuzipata nguo hizo kama Jason alivyokuwa ameagiza, kabla hata ya kufika kuna duka moja njiani waliona kwa ndani kuna suruali jeans za wanaume, tshirt na Laba, Jason aliomba gari isimamishwe hapo pangewafaa kuweza kumaliza hilo tatizo. Alitoa pesa mfukoni lakini mwanaume huyo alitikisa kichwa kukataa hiyo bili angemalizana nayo mwenyewe, basi alipewa vipimo na aina ya nguo za Kwenda kubeba kisha akatoka kwenye hiyo gari, ndani ya dakika 10 za kuhesabu alikuwa amesha maliza manunuzi, alirudi akiwa na mfuko uliokuwa umejaa.
Jason alibadilisha nguo humo humo ndani ya gari, mwilini alibakia na jeans, laba nyeupe na prova ambayo ilikuwa imeufiti mwili wake vyema na kumfanya kuonekana kama miongoni mwa vijana wa kisasa, nguo hizo kiasi chake zilisaidia kuuficha mwili wake ambao ulikuwa umejikata sana kwa mazoezi makali mno ila kwa kumuangalia ungehisi kwamba ni kijana mlegevu ambaye alikuwa anapenda kunyanyua tu vyuma vya kawaida kwa sababu mwili wake haukuwa umeumuka sana ulikuwa mwili wa kawaida ila ambao kila nyama ilikuwa imapangwa vyema sana mahali pake.
“Hiyo suti unaweza ukaitumia mwenyewe na kama haikufai basi waweza mpa hata rafiki yako, safari yako inaishia hapa niseme tu nashukuru mno kwa wema wako nina imani haitakuwa mwisho wa sisi kukutana ipo siku tunaweza kuja kukutana tena, uwe na usiku mwema” Jason aliongea kumpa mtu huyo maelekezo huku akiwa anaiweka vyema kofia yake kichwani na alikuwa amesha anza kuondoka ndani ya hilo eneo.
“Sawa kiongozi kuwa makini” baada ya kuisikia sauti hiyo alitabasamu kwa mbali huku akimnyooshea mwanaume huyo mkono wa kwaheri bila kugeuka, alitembea kwa dakika tano kuna tax aliiona ikiwa inapita aliipa mkono nayo ikaitikia na kusimama, akamuelekeza dereva tax huyo sehemu ambayo alitakiwa kuwepo na muda ambao ulitakiwa kutumika mpaka kuweza kufika ndani ya hilo eneo.
Dakika ishirini na tano ziliwatosha kufika Mbagala karibu kabisa na eneo ambalo Jason alikuwa amekusudia kufika japo zilibaki kama hatua hamsini ili aweze kutokekezea kwenye uwanja wa eneo ambalo ndipo alipanga kumkuta mrembo huyo, alilipa pesa yake na kuangalia muda ambao ulikuwa umesoma dakika 50 tangu aondoke ndani ya Ikulu maana yake kwa muda ambao alikuwa amemuahidi mrembo huyo alikuwa amevusha dakika 20, alijisonya mwenyewe kwa hasira kwa sababu alikuwa anachukia sana kwenda nje na muda ambao yeye mwenyewe alikuwa akijiwekea. Akiwa anaangaza huku na huku na kuanza kutembea kwenye njia ya chocho ambayo aliona itakuwa ni mkato wa kutokezea kwenye hiyo sehemu yenye uwanja mkubwa kirahisi alihisi kama nyuma yake kulikuwa na mtu, ni kweli baada ya kugeuka aliona kuna vijana sita ambao walikuwa na mapanga kwenye mikono yao haikumpa shaka kwamba hao walikuwa ni vibaka ambao huwa wanatumia mabavu kuweza kujichumia pesa alisikitika sana na kuanza kuondoka hapo.
“Acha dharau kabla hatujakupunguza kipande cha mkono wako mbwa wewe yaani unatuona na unajifanya kama vile hakuna kitu hautujui vizuri sio?” kuna sauti moja ya uvundo ambao ndani yake ilionekana kulikuwa na ugoro ulitoka kuliwa sio muda sana ilisikia masikioni kwa mwanaume ikamfanya kusimama, lilikuwa ni kosa kubwa sana kibaka kama huyo kumuita yeye mbwa na kuamrishwa mtu ambaye hata raisi wa nchi anaongea naye kistaarabu na kumuomba pale anapo mhitaji afanye jambo fulani, aligeuka akiwa ana hasira sana nadhani hata huyo kibaka kama angejua kwamba mwanaume huyo hiyo siku alitoka kumzika kaka yake wa damu basi asingethubutu kumuongelesha mtu wa namna hiyo.
“Kati yenu hapo ni nani ambaye amepata hicho kiburi cha kuniita mimi mbwa?” aliuliza kwa hasira huku akiwa anarudi walipo vijana hao ambao nao walikuwa wanamfuata, walidhani kwamba wamempata mwanaume mshamba ambaye walikuwa wanaenda kubeba kila alichokuwa nacho kwenye mwili wake, kabla hajafanya chochote simu yake ilianza kuita, aliitoa mfukoni na kuiangalia namba iliyokuwa inapiga ni ile ile ya Nayra, aliirudisha simu hiyo kwenye mfuko wake, simu ilikuwa ya gharama sana japo ilikuwa ni usiku wanaume hao walizidi kupata tamaa. Aliyekuwa mbele yao alijibu kwa kujigamba huku akiwa anasogea kwa kumkimbilia Jason alipokuwa akiwa ameunyanyua upanga wake mkononi.
“Ni mimi hapa ms***** wewe unasemaje?” alijibu kwa jeuri akiwa anaushusha upanga huo kwenye bega la Jason alihitaji kuutengenisha mkono huo kwa sababu waliona kama anawaletea jeuri watoto wa mjini, mkono wake alihisi huenda ni mfupi kwa sababu hakujua mwanaume huyo alimfikia saa ngapi, mkono wake ulidakwa kwenye kifundo chake ulivutwa na kuvunjwa kwa kutumia mkono mmoja tu, alipiga makelele sana upanga ulimponyoka mkononi lakini haukudondoka chini ulidakwa na Jason aliuzungusha na kumpiga kijana huyo na ubapa wa upanga kwenye shingo yake, hakutamka neno lolote lile alibaki ameganda kama ulikuwa mti hapo mwanaume akamsukumia pembeni na kulitupa panga hilo chini.
“Nisije nikawakuta kwenye haya maeneo tena wapuuzi nyie hamjui hata namna ya kuyatumia haya mapanga yenu halafu mnawakazia sauti watu na kuwapora, mbebeni mwenzenu ataamka keshokutwa na akiamka apelekwe hospitali maana mkimchelewesha atakufa, nitakaye mkuta tena sitakuwa na msamaha mwingine nitamuua” aliongea kwa hasira na kuwafanya vijana hao watano ambao walishuhudia hilo tukio la kutisha waanze kutetemeka, walimbeba mwenzao na kukimbia sana huku wakipiga kelele za kuyatete maisha yao, aliitoa simu yake mfukoni na kuipiga kwa mwanamke huyo ambaye alimuomba samahani kwa kuchelewa na kuhitaji amueleze ni wapi alipokuwa kwa wakati huo.
Nayrah baada ya kumuona mwanaume huyo alimkimbilia na kumkumbatia, kwake alikuwa anamuona mwanaume bora sana, mkarimu na mwenye moyo wa huruma sana ila kama angejua namna huyo binadamu anavyo ogopwa basi huenda hata kuwa na namba yake tu angejutia kwenye maisha yake.
“Kwanini umeniita na usiku saivi?” mwanaume huyo aliuliza wakiwa wamekaa kwenye tairi kubwa wakiwa wanaangalia namna watu walivyokuwa wanapishana mtaani hapo.
“Nimekuitia hapa kwa mambo matatu, jambo la kwanza nataka niseme kwamba asante sana kwa msaada wako wa siku ile kwa sababu sio rahisi sana mtu ambaye hakujui kabisa kukupa msaada kama ule sina cha kukulipa ila nina imani MUNGU atanilipia hilo, jambo la pili ni siku ile baada ya kunipa ule msaada zile pesa ilibidi nimfikishie na mama yangu ambaye aliniuliza nimepata wapi pesa zote kama zile ilibidi nimwelekeze kilicho tokea lakini hakuweza kabisa kuniamini mimi hivyo akawa anaomba kwamba anahitaji akuone ili ahakikishe awe na amani maana anakuwa kwenye wakati mgumu sana kutumia pesa ambazo hata hajui zinatoka wapi na malipo yake ni nini. lakini jambo la tatu nataka nikuombe msamaha sana kwa kile nilicho kifanya pale mbele yako siku ile kwa kujirahisisha kwamba najiuza na pia nahitaji kukupatia historia ya kweli kabisa ya maisha yangu” Nayrah aliongea kwa sauti yake ya kistaarabu sana ambayo ilimfanya aonekane kama ni mwanamke bora sana kwenye macho ya kila mwanaume ambaye angekuwa anamtazama kwa wakati huo.
Siku hiyo Nayrah alikuwa ni tofauti kidogo, alikuwa amevaa nguo za heshima sana huku kichwa chake kikiwa kimefunikwa na mtandio safi sana, Jason alikuwa makini sana kumsikiliza mwanamke huyo.
“Huogopi kukutana usiku kama huu na mwanaume ambaye hata humjui kwa sababu tu alikusaidia vipi kama anahitaji kukufanyia kitu kibaya? Huoni kama itakuwa ni tatizo kubwa sana kwako?” Jason alimuuliza Nayrah swali ambalo lilimfanya ainame chini kwa aibu, kwa namna walivyokuwa wanaongea ungehisi kwamba ni watu ambao walikuwa wamejuana kwa muda mrefu sana na hata kwa mtu ambaye angewaona angehisi watu hao walikuwa ni wapenzi wa muda mrefu sana bila kujua kwamba siku hiyo ilikuwa ni mara ya pili kukutana kwenye maisha yao.
“Kama ungekuwa na lengo baya namimi basi siku ile ile ambayo nilijirahisisha kwako ungeitumia kunifanya kile ambacho ungeona inafaa kwa upande wako lakini ulionyesha kwamba wewe ni mwanadamu wa tofauti sana ndiyo maana nikakuamini sana tangu siku ile” aliongea kistaarabu sana mwanaumke huyo kitu ambacho kilikuwa kinampeleka mbali sana Jason na kujikuta anatabasamu sana.
“Usiwaamini sana wanadamu kwenye maisha yako hata mimi usije ukaniamini tena kuanzia sasa, sina muda mrefu sana wa kukaa hapa ila mambo ya mhimu ni mawili tu hilo la asante unapaswa kumshukuru MUNGU na sio mimi, jambo la kwanza nahitaji unipe hiyo historia yako wewe na pia nitajitahidi sana niweze kwenda kuwaona wazazi wako kabla sijaondoka jappo sitakaa sana huko” Mwanaume huyo alijibu kwa sauti kavu sana kitu ambacho kilimfurahisha sana mrembo huyo kwa sababu alitamani sana kuaminika sana kwa wazazi wake hususani mama yake ambaye alikuwa akijielewa ukiachana na baba yake ambaye alikuwa ana ugonjwa wa ukichaa lakini pia alihitaji mama yake aweze kumuona mwanaume huyo ambaye kwake alikuwa kama shujaa kwake.
Je mwanamke huyu historia yake ina mambo gani ambayo yamejificha? Kwanini anahitaji mwanaume huyu aweze kuifahamu? Jason ni maamuzi gani aliyachukua?
Sehemu ya 20 inafika tamati panapo majaaliwa tukutane tena wakati ujao.
Wasalaam
Bux the storyteller.