Innocent Killer (The Revenge)

Innocent Killer (The Revenge)

STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 17

SONGA NAYO............
Mkuu wa majeshi baada ya kutoka pale nje akiwa mwenye hasira sana alienda moja kwa moja ndani, alitamani afanye maamuzi magumu lakini kuna nafsi ambayo ilikuwa inamsuta kumuua kijana huyo kwake halikuwa chaguo la kwanza lakini kwa mambo ambayo yalikuwa yameongelewa na kijana huyo basi ilimtosha sana kwenye maisha yake kuendelea kuwa kimya juu ya hilo jambo, huenda ni kweli kijana huyo alikuwa kachanganyikiwa kwa kuipoteza familia yake sawa lakini sasa vipi kuhusu mambo nyeti sana ambayo alionekana kuwa anayajua kiundani mno? Hakuona haja ya kulifumbia macho hilo jambo ilimhitaji yeye kujipa uhakika juu ya hilo jambo kama je lilikuwa ni la kweli kama kijana huyo alivyokuwa analisema mbele yake au ni kijana huyo tu ambaye aliyaunganisha matukio yake kutokana na uwezo wa kichwa chake? Alivua suti yake akabakia uchi kabisa ndani ya chumba chake ambacho kwenye kioo kulikuwa na picha ya Malaika sio yule aliye omba dafu kwenye zali la mentali la professor J Hapana bali ni sura moja ambayo ilikuwa imenyooka kama maandiko yanavyokuwaga yana maana ya moja kwa moja na mrembo huyo ilikuwa ni zawadi na kiburudisho kikubwa sana kwa mzee huyo wakati anapokuwa kwenye mawazo mazito sana.

Aliinyanyua simu yake na kubonyeza akiwa anatafuta namba ya mlengwa wake ambaye alikuwa amepanga kumpigia kwa huo wakati, Lusubilo Mtindiga ndilo jina ambalo lilionekana kwenye kioo cha simu yake, hakusubiri zaidi ya kuruhusu kitufe cha kupigia, simu iliita kwa muda mrefu sana wakati anajiandaa kuikata ndipo ilipo sikika sauti upande wa pili huyo alikuwa ni IGP rafiki yake wa damu ambaye walikuwa wamefikia hatua ya kuwa ndugu na kwa sasa walikuwa wamebaki wao wawili tu basi wenzao watatu walikuwa wametangulia mbele za haki.

“Saa saba hii ndugu yangu kuna tatizo mpaka tunaamshana saivi unajua tangu asubuhi sijapata hata sekunde moja ya kupumzika kutokana na matatizo mazito ambayo yamelikumba taifa letu? Tuongee kesho tafadhali nimechoka sana” mheshimiwa IGP alijibu kwa sauti ya uchovu sana na kukereka kwa mwenzake kumtafuta majira kama hayo ambayo yeye binafsi alihitaji kuyatumia kupumzika kwa sababu kesho yake alijua kwamba itakuwa ni siku ndefu sana hata hivyo CDF aliguna kidogo na kujikohoza hiyo ilikuwa ni ishara kwamba huyo mtu alikuwa anatakiwa kumpa wasaa kadhaa kwa ajili ya kumsikiliza muda huo hata kama alikuwa amechoka vipi hilo jambo lilikuwa na umuhimu mkubwa sana basi hakuwa na namna zaidi ya kuweza kumsikiliza rafiki yake kipenzi.

“MD hivi mheshimiwa raisi kuna siri ambazo amekufa nazo labda nawewe ulikuwa unazijua ila mkaamua kutufumba sisi wawili na Mark, huenda ni kwa lengo zuri la kuliendeleza taifa lakini je kuna chochote kile ambacho mimi sikijui nawewe unakijua ndugu yangu?” alikuw akimuita MD ikiwa ni herufi mbili za jina la Lusubilo kwenye neno MTINDIGA alizichukua herufu mbili na kumpachika jina hilo rafiki yake kwa sababu alikuwa ni mtu ambaye alikuwa anapenda kuonekana kama kiongozi wa kila anacho kifanya ndipo akampa kifupi hicho kinacho maanisha Managing Director.

“Mhhh ni usiku sana unaanza kunipa habari za kunishtua sana namna hii, nadhani unanijua tangu nikiwa mdogo hakuna kitu nilikuwa naweza kukifanya nawewe usikijue sasa kama kuna taarifa za siri na za mhimu unahisi ningezifanyiaje kazi bila kukuomba ushauri wako?” alimjibu kwa kumuuliza lakini CDF hakujibu kitu aliguna tu na kuendelea.

“Hivi utakuwa na taarifa kuhusu mkurugenzi wa usalama wa taifa ni nani? kwa sababu huyu ndiye mtu ambaye alikuwa anatakiwa ahakikishe usalama wa mheshimiwa raisi muda wote kuanzia ndani ya Ikulu mpaka sehemu yoyote ile anayo Kwenda ikiwemo kukusanya taarifa za sehemu ambayo mheshimiwa anakuwepo, kutojulikana kwake kunatufanya sisi hapa tuanze kupata lawama ambazo hata hazituhusu sasa kama mimi mkuu wa majeshi nalaumiwa raisi kuvamiwa na kupigwa risasi inanihusu nini hiyo wakati kuna watu ambao ndio wana hakikisha usalama wa raisi?” aliongea huku akiwa anamsogelea mrembo wake ambaye sasa alikuwa amejilaza kitandani akiwa uchi kabisa tena akiwa amelala kifudi fudi kumsubiria mheshimiwa akate simu aende kulifaidi tunda lake, mzee huyo aliendelea kuziminya minya nyama alizokuwa amebarikiwa mwanamke huyo huku akiendelea kuongea na simu yake kama ilivyokuwa kawaida akisubiri jibu kutoka upande wa pili.

“Kwenye kikao cha mwisho ambacho tulikutana wote uliwahi kuuliza hilo swali mbele ya raisi nadhani unakumbuka alivyokuwa amekujibu kwamba hizo ni taarifa ambazo hataki mtu yeyote azijue wala kujulikana popote mpaka pale atakapo ona inafaa na akaahidi kwamba kama ikatokea kuna tatizo basi kuna watu wawili ambao ndio watakuwa na taarifa za huyo mtu hata kama yeye hatakuwepo leo na kesho na ukaridhika kabisa siku ile hukuuliza tena sasa leo nakushangaa unakuja kuniuliza mimi wakati siku ile tulijibiwa wote watatu pamoja na Mark sasa mimi nitajulia wapi na nahusiana nini na mkurugenzi wa usalama wa taifa?. Kuhusu suala la kwamba wewe unahusishwa ujue ndugu yangu kuna kitu ambacho hukielewi hivi wewe hapo ukiulizwa ile video uliikuta wapi utajibu nini? nimezikuta sms zako kwenye simu ya Mark nimeamua kumezea tu japo imeniuma sana, sasa kama tu ndugu yako unanipa ukakasi utashindwa vipi kuhisiwa na mtu ambaye atapata hizo taarifa? Mimi mwenyewe hapa kuna maswali ambayo unatakiwa unijibu baada ya msiba” IGP alimpa jibu ambalo hakulitegemea yeye mwenyewe alikuwa hamjui huyo mkurugenzi wa usalama wa taifa na wala hata kwenye hili tukio hakuonekana kabisa suala ambalo lilianza kuwapa shaka watu hawa wawili hata hivyo IGP alimweleza kwamba alikuwa naye bado hamuelewi ndugu yake huyo na mipango yake ambayo alikuwa nayo.

“Tuachane na mengine tuongelee ambalo limenifanya nimekupigia simu wakati huu, umesema kwamba raisi alidai kwamba kuna watu wawili walikuwa na taarifa za huyu mtu na ukimtoa yeye watu ambao alikuwa anatuamini sana tulikuwa watatu, mimi, wewe na Mark, sasa kama ni hivyo lazima watu hawa wawili walikuwa wanatoka ndani yetu maana yake unaweza kuwa ni wewe na Mark na kama sio hivyo hata kama alikuwa na mtu mwingine nje ila lazima mmoja wetu anajua yule hawezi kutuficha ndugu zake alikuwa anatuamini sana”

“Mhhh usijichanganye sana kaka, mtu kuwa ndugu yako au kuwa rafiki yako wa damu haikuhakikishii kwamba anakuamini hilo usije ukaliweka sana kwenye akili yako, dunia inabadilisha sana watu hususani wakizishika pesa wanakuwa tofauti sana na yule alikuwa ni raisi wa nchi unahisi kwamba kila kitu anaweza akakiweka wazi kama unavyohisi wewe kwa sababu wewe ni ndugu yake ndo ujue kila kitu? hakuna kitu cha hivyo duniani tena usije ukakuta katika watu ambao alikuwa anawaamini sana hayupo hata mmoja kati yetu sisi sasa unajihakikishia vipi kwamba lazima kuna mtu anajua? Ni vyema kama angeliweka hilo wazi mapema amekufa nalo kwenye moyo wake kuja kulijua tena ni hadithi nyingine hiyo kwa hapo sina msaada wowote maana mimi mwenyewe nimechanganyikiwa”

“Mhhhhhh nadhani makamu wa raisi anaapishwa asubuhi sana, yule mtu inabidi tuwe naye karibu sana maana kiofisi ndiye mtu wake wa karibu zaidi hivyo huenda kuna taarifa nyingi sana yeye anazo ambazo hata sisi hapa hatuna”

“Ok, vipi una swali lingine mimi nahitaji kulala ndugu yangu”

“Unautolea wapi usingizi na mambo yalivyokuwa mazito hivi?”
“Ok tuachane na hayo nambie hicho unacho taka kuniambia”

“Who is he (yeye ni nani)?” aliongea kwa mafumbo ila mheshimiwa IGP alimuelewa vizuri sana

“Umekutana naye?”
“Ndiyo maana nimekuuliza”

“Ulivyo kataa kukutana naye mimi nilikusisitiza ukutane naye nadhani ulikuwa naye hapo si ungemuuliza yeye mwenyewe kwamba ni nani ili akujibu, sasa mtu ulikuwa naye saivi unaanza kuniuliza mimi tena nina jibu gani zaidi ya kukwambia kwamba ni mtoto wetu au mdogo wa rafiki yetu, kwa ninavyo kumbuka namna tulivyo mlea Jason kwa upendo tukiwa wote sina jibu lingine la uhakika zaidi ya kusema ni mtoto wetu, vipi umelewa mpaka unaniuliza swali kama hilo?”

“Mimi huwa silewi na hizi pombe za kubahatisha, ningekuwa kwenye sehemu ya starehe jibu lilikuwa ni ndiyo ila nikiwa nyumbani huwa nakunywa kistaarabu sana na unalijua hilo, amekuja hapa na kuanza kuongea mambo ya ajabu ambayo nimemshangaa sana mpaka nimeshindwa kumuelewa mpaka ilifika hatua nilitaka nimtie adabu maana alianza kunikosea heshima akisahau kabisa kwamba mimi ni baba yake mkubwa unajua watoto wa siku hizi wamekuwa wa hovyo sana”

“Mhhhhhhh wewe hapo ndo ulihitaji kumpiga yule mtoto?”
“Ndiyo nilitaka kufanya hivyo kwa sababu niliona kama anakosa heshima kabisa mbele yangu sema nafsi yangu imenisuta hata Mark asinge niangalia vizuri huko aliko nadhani angejisikia vibaya sana kusikia nimemfanyia hivyo yule mtoto akiwa hata hajamzika”

“Hilo lingekuwa ni moja ya makosa makubwa sana ambayo wewe ungewahi kuyafanya kwenye maisha yako na ungejutia maisha yako yote mpaka unakufa”

“Una maanisha nini kuweza kuniambia hivyo mbona kama unaanza kunitisha, kumbuka unaongea na mkuu wa majeshi hapa sio raia wa mtaani na kingine mbona unaonekana kama unamuogopa sana huyo mtoto kuna nini?”

“Mhhhhhhh ndiyo maana vitu vingi ulikuwa unamtegemea sana Mark, ujue kuna muda huwa huna akili kabisa, yaani wewe hapo unaanza kunitambia mimi cheo chako siyo? Nimekuambia ungejutia kwa sababu hata mimi siwezi kukuacha salama kama ukimgusa huyo mtoto. Tumeishi na kufikia hapa kwa sababu ya akili ya kaka yake ndiyo maana mpaka leo hapa una mpaka kiburi cha kujisifia wewe ni mkuu wa majeshi, huyo mtoto amebakia ili sisi tumlinde kwa gharama yoyote ile kama kumuenzi ndugu yetu wewe kipuuzi tu kisa unajijua unatulizwa na hao malaya zako unataka kushusha mkono wako kwa huyo bwana mdogo? Kama unataka kunijua rangi yangu kamguse huyo mtoto hata kibao nione kama utaendelea kukaa kwenye hiyo nafasi yako ya ukuu wa majeshi ambao unajisifia sana.

Siwezi kumuogopa huyo mtoto ambaye kwangu ni mwanangu na mdogo wangu pia, nchi nzima inamtazama yeye saivi kama mkiwa pale alipo hata akili yake haiko sawa yupo kama amechanganyikiwa kutokana na kitu ambacho kimetokea na wewe unataka kuyazua mengine ebu jaribu nikuone, kuna muda uwe unafikiria kama mtu mzima yaani kunipigia kote na usiku huu nikajua una jambo la maana sana kumbe ndo huo utumbo ulikuwa unahitaji kuniambia mimi? Kama kumuona anateseka ndiyo furaha yako iambie serikali isitishe misaada yote ambayo imepanga kumsaidia baada ya msiba wa kaka yake na kama hauna ishu ya maana ya kuongea namimi usije ukanipigia tena” mheshimiwa IGP alikereka sana na mazungumzo ya mwenzake, yalimfanya akajisikia vibaya sana mtu huyo alifikia mpaka hatua ya kuanza kuwatishia moja ya watu waliokuwa wanaiunda hiyo familia yao alimpa makavu yake na kumkatia simu na kuizima kabisa maana aliona kama mwenzake huyo haeleweki kabisa alikuwa akimtia hasira tu.

Mkuu wa majeshi alibaki anaongea pekeyake, alichukia sana baada ya kugundua kwamba simu hiyo ilikuwa imekatwa, alisonya kwa nguvu na kuibamiza simu hiyo kwa hasira akiwa ameikunja ndita ya uso wake, mrembo ambaye alikuwa kitandani aliielewa hali ya mtu wake ambaye ndiye alikuwa anampa jeuri ya kuishi maisha ya ndoto za warembo wengi mjini hivyo kumuweka kwenye furaha mwanaume huyo ilikuwa moja ya majukumu yake, alinyanyuka na kumfuata mwanaume huyo na kuanza kuutambaza ulimi kwenye maeneo mbali mbali ya mwili huo mpaka alipo kolea walizama kwenye bahari moja ya chini sana kina kirefu kiliwafanya wazisahau shida zinazo patikana kwenye uso wa dunia ilikuwa ni muda wao kuweza kuzila raha ambazo zilikuwa ni furaha kubwa sana kwa wanadamu wengi ulimwenguni.

Sehemu ya 17 inafika mwisho tukutane kwenye sehemu inayo fuata.

Wasalaam

Bux the storyteller.
 
Habari ya Jumapili? Ni matumaini yangu wote mpo salama.

Nilipotea siku mbili hizi, nilimuwa namalizana na simulizi hii, ambayo nimeandika mpaka mwisho. Ina kurasa 135.

Leo tunasoma kurasa mbili.

Wasalaam.
 
Habari ya Jumapili? Ni matumaini yangu wote mpo salama.

Nilipotea siku mbili hizi, nilimuwa namalizana na simulizi hii, ambayo nimeandika mpaka mwisho. Ina kurasa 135.

Leo tunasoma kurasa mbili.

Wasalaam.
tupia basi mkuu
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 18

SONGA NAYO............

“You can dance”
“You can jive”
“Having the time of your life”
“This is the rhythm of the night”

Utulivu wa akili ulikuwa amemzamisha mbali sana na hiyo ndiyo mistari mitamu sana ambayo ilikuwa inajirudia sana kwenye kichwa chake, hakutamani siku hiyo kama ingekuwa imeisha kwenye kichwa chake ni miongoni mwa siku ambazo yeye alijifungia rasmi kwenye dunia ya mapenzi, ni siku ambayo yeye na mpenzi wake walikuwa wametoka Kwenda kwenye club moja kwa ajili ya Kwenda kufurahi na marafiki zao pamoja na kuyafurahia mapenzi yao.

Akiwa katikati ya viunga vya chuo cha HAVARD bibie Monalisa au waweza kumuita Lisa ndiye ambaye alikuwa na haya mawazo kichwani, na siku ambayo alikuwa anaikumbuka sana na alifanikiwa kuisikia mistari hiyo adimu sana ilikuwa ni moja ya siku bora sana kwa upande wake baada ya kufanikiwa kuanza mahusiano na Jason walitoka pamoja na marafiki zao Kwenda kwenye hiyo club ili kufurahi na mistari hiyo ilikuwa ikipatikana kwenye moja ya wimbo ambao yeye alikuwa akiupenda sana na ndio ambao ulikuwa ukichezwa wakati ule alikuwa ameshikwa kiunoni na Jason wakiwa wamezama mbali sana kwenye ulimwengu wa huba.

Monalisa kwa madai yake ni kwamba hakuwahi kabisa kupenda kwenye maisha yake mpaka pale alipokuja kukutana na Jason ndipo rasmi moyo wake ulipokuja kumsaliti kabisa, alijaribu sana kuukatalia moyo wake lakini ulimgomea na kuamua kumzomea kwa sababu alishindwa kabisa kuweza kufaulu mtihani wa kuweza kupambana na moyo wake mwenyewe na ndipo hapo ambapo alijikuta anaangukia kwenye huba zito sana na mwanaume huyo Jason. Monalisa hakumaanisha kwamba alimpenda kijana huyo kwa sababu alikuwa ndiye mwanaume wake wa kwanza lahasha huo ungekuwa ni uongo kwa sababu aliwahi kuwa na wanaume wengine kadhaa kwenye maisha yake lakini kwa Jason alikubali kuwa Rose akiwa anamsubiri Jackie apone kwenye ajali ya kutisha sana ya TITANIC, aliogopa mno kwamba huenda Jack wake asirudi ila alijipa matumaini kwa sababu yeye hakuwa Rose aliamini Jason wake atamtia kwenye mkono wake tena.

Hapo alikuwa amekaa na mawazo hayo yalikuwa yameenda mbali sana kwa sababu mpenzi wake aliondoka ghafla sana baada ya kupata taarifa ambayo ilionekana kutokuwa sawa kwa upande wake yeye, hilo halikuwa tatizo lakini kilichokuwa kinampa wasiwasi sana ni namna mtu huyo alivyo ondoka bila kumpatia yeye maelezo ya kutosha na hata namna ya uondokaji wake alikuwa kama mtu ambaye amepotea na sio mtu ambaye alikuwa ameondoka kwa amani. Wasi wasi wake mkubwa ulihamia upande wa Professor Michael ambaye yeye mwenyewe alidai kwamba alikuwa anafundishwa pia na Professor huyo, swali lake moja rahisi sana lilikuwa ni kwanini mara tu baada ya Jason kupata tatizo aende kumuona Professor huyo? Na hata kama walikuwa ni marafiki na alienda kumuaga napo alitengeneza maswali mawili tofauti kweye kichwa chake.

Kwanza je professor ana umuhimu mkubwa kwenye maisha ya Jason kuliko yeye? Kwa sababu yeye ndiye alikuwa mpenzi wake na ndiye ambaye angetakiwa kumpatia faraja kipindi ambacho yeye asingekuwa sawa kabisa sasa kwanini yeye aambiwe juu juu tu na mtu huyo akaondoka au hamwamini? Hakuwa na mtu wa kumjibu. Swali lake la pili ambalo alikuwa anajiuliza yeye mwenyewe ni kwamba kama alienda kwenye ile ofisi kwa ajili ya kuhitaji ushauri au msaada sasa kivipi aingie mle ndani na hakutoka tena mpaka baadaye ambapo yeye mwenyewe alikutana na professor huyo ambaye alimwambia kwamba mtu wake kwa muda huo alikuwa ndani ya ndege akiwa anarudi Tanzania sasa alikuwa anajiuliza sana kwamba hilo suala linawezekanaje? Majibu yake alitakiwa kukutana na professor Michael au kuwasiliana na Jason mwenyewe ambaye namba aliyokuwa akiitumia akiwa huko Marekani ilikuwa haipatikani kabisa hicho ndicho kitu ambacho kilimpa wasi wasi sana binti huyo na kumfanya asiwe na uhakika na Jason kwamba kwanini alikuwa akimficha sana mambo hayo hata taarifa za familia yao hakuwa akimwambia kuna nini?

Alikuwa amekaa kwa zaidi ya masaa Matano akiwa amezama ndani ya mawazo mazito sana na ndipo hapo alipo amua kuondoka na kurudi nyumbani mida ya jioni. Alifika nyumbani kwake alipokuwa amepanga hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa amewahi au kuingia kwenye nyumba hiyo, hata Jason alikuwa hajawahi kabisa kukanyaga hapo na hata Jason mwenyewe hakuwahi kabisa kuuliza au kuhitaji kufika kwa mwanamke huyo sehemu ambayo alikuwa akiishi kwa sababu ambazo alikuwa nazo yeye mwenyewe.
Ulikuwa ni muda mrefu sana akiwa hajaingia kwenye mtandao wake tangu Jason awepo huko Marekani, alifunga milango yote na madirisha yote baada ya dakika tano alitoa godoro kwenye kitanda chake na kukutana na kioo cha shaba ambacho kilikuwa kimewekwa kama pambo hapo, alisogeza jicho lake zikatokea namba, alibonyeza tarakimu kadhaa pakafunguka, aliitoa laptop yake na kuiwasha, baada ya kuwaka tu alikutana na picha ambayo ilikuwa imechorwa alama ya X katikati na kuandikwa “DEAD” lakini kabla hajaipekua vizuri picha hiyo alikutana na picha nyingine nayo ilikuwa imechorwa X kama ya kwanza napo ikiwa imeandikwa “DONE” alitabasamu japo alishtuka sana alikuwa na muda mrefu mno bila kuingia kwenye mtandao wake wa siri huo au mtandao wowote ule hivyo kwake aliona kama ni mzembe sana kuweza kuchelewa kuzipata taarifa kama hizo ambazo zilionekana kuwa nyeti sana.

Alinyanyuka haraka haraka na Kwenda kuiwasha televisheni kubwa ya ukutani hapo ndipo alipo pigwa na butwaa japo butaa hizo zilimfanya afurahi huenda kwake zilikuwa ni taarifa njema, alitabasamu sana japo alishangaa hizo taarifa zilikuwa zimesambazwa kwenye kila chombo cha habari, swali aliloweza kujiuliza kwanini taarifa kubwa kama hizo hakuweza kusikia watu wakizijadili ndipo hapo alipokumbuka kwamba yeye na Jason mara nyingi hawakuwa watu wa kujichanganya sana na hata Jason tangu aondoke hakuwa amekutana na mtu mwingine yeyote maana hakupokea simu ya rafiki yake yeyote yule hata chuo akienda alikuwa anaenda kupumzika peke yake kwenye viunga vya bustani nzuri sana ambavyo aliona kwamba vilikuwa vinamtuliza mawazo yake.

Watu ambao walikuwa wanatangazwa kupoteza maisha alikuwa ni mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania pamoja na mheshimiwa jaji mkuu wa Tanzania ni vifo ambavyo viliushitua sana ulimwengu na kilicho washtua watu wengi zaidi ni baada ya video ambayo inaonyesha mheshimiwa raisi anauliwa kuweza kuwekwa hadharani, jaji mkuu kifo chake nacho kiliwaacha watu midomo wazi kwa sababu baada tu ya kutoa hukumu kwa mtu ambaye walimhisi kama mhusika hakuchukua muda sana aliweza kuuawa nayeye, watu wengi walikuwa wakiyatoa maoni yao kwa kuhusisha tukio hilo na matukio ya kigaidi huku wengine wakisema kwamba ni wapinzani walikuwa wanaona wivu kwa watu hao, maneno yalikuwa mengi sana lakini ni kama Monalisa alishtuka kuhusu kitu kimoja kwanini Jason amerudi kipindi hiki ambacho haya matukio yalikuwa yametokea? Hakupata jibu.

Alisoma vizuri sana historia ya mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania jina lake halikuwa likiendana kabisa na Jason, ikamlazimu kuzipitia upya taarifa za jaji mkuu kwa sababu alionekana kwamba alikuwa na taarifa zao mapema sana alikuta kuna taarifa kwamba mtu huyo alikuwa na ndugu yake mmoja tu na walizaliwa wawili tu basi, bahati mbaya sana ndugu yake huyo kwenye huo ukurasa ambao ulikuwa unatunza taarifa za watu mashuhuri kulikuwa na picha zake za utotoni tu basi akiwa na tabasamu hafifu usoni pake, alijaribu sana kuzitafuta picha za ukubwani za mdogo wake na jaji mkuu hakuzipata na hapo ndipo alipo angalia jina la mdogo wake na jaji mkuu, JASON JAPHARY ndilo jina ambalo lilikuwa limeandikwa hapo. Alivuta kumbu kumbu siku ambayo aliwahi kumuuliza Jason wake yeye aliye mwambia anaitwa JASON MUHAN kwamba ni kwanini alikuwa na jina la ubini wa kihindi wakati yeye ni mtanzania kwa asilimia miamoja? Jason alimjibu kwamba babu yake alikuwa ni mtu ambaye aliishi India sana na huko India alikutana na mwanaume mmoja ambaye ndiye aliye msaidia kwenye maisha yake na kumpa maisha mazuri na mwanaume huyo alikuwa anaitwa MUHAN RAWAR na ndipo baadaye babu yake alipokuja kuoa aliamua kumuita mtoto wake huyo wa kiume jina la huyo rafiki yake kama kumuenzi na huyo aliye itwa hilo jina ndiye baba yake na Jason, hayo ndiyo majibu ambayo aliwahi kujibiwa na Jason.

Pale kwenye ule ukurasa jina lilikuwa ni Jason Japhary hivyo moja moja akajua kwamba watu hao walikuwa na mfanano wa majina yao ya kwanza ila walikuwa ni watu tofauti kitu ambacho aliamua kujidanganya yeye mwenyewe bila kujua na haikujulikana sana kwamba ni sababu ipi ambayo iliweza kumfanya Jason akamdanganya mwanamke ambaye yeye mwenyewe alikiri kwamba alikuwa anampenda sana kwa moyo wake wote na hata huyo mwanamke hakuelewa kwamba ni kwanini alikuwa akifurahia sana baada ya kuona watu hao wawili wakiwa wamekufa na haikujulikana ni nani aliyekuwa amemtumia picha hizo na kwa dhumuni lipi.

Taarifa ambayo ilikuwa inampa amani ni baada ya kuona habari kwamba muda sio mrefu sana walikuwa wanajiunga moja kwa moja kwenye mazishi ya watu hao wawili wa mhimu sana ndani ya taifa la Tanzania, alishangaa taarifa hiyo kwa sababu ilikuwa ni mapema sana mtu kama raisi hawezi kuzikwa kwa haraka sana namna hiyo ilitakiwa watu wamuage na taratibu zingine ziendelee lakini cha kushangaza ilidaiwa kwamba muda sio mrefu sana watakuwa live kwenye mazishi ya mheshimiwa raisi pamoja na jaji mkuu wake ambaye yeye mwenyewe alimteua na taarifa nyingine ya kushtua ni kwamba kulikuwa na sababu gani mpaka watu wasiruhusiwe kuweza kumuaga raisi wao mpendwa? Hakuwa akihusika sana kwa sababu kwa wakati huo ilibidi asubirie hizo taarifa maana kwa huo muda walikuwa wanamuapisha mheshimia makamu wa raisi kuichukua nafasi ya raisi ambayo ilikuwa imeachwa na marehemu ambaye alitakiwa kuzikwa punde tu makamu wa raisi atakapo apishwa na kuwa raisi rasmi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kwa marekani ilikuwa ni usiku tayari na alitumia muda wa kutosha kuweza kuangalia taarifa hizo lakini kwa Tanzania ndo kulikuwa kumepambazuka na kilichokuwa kimetawala mtaani sio mishe mishe za wale watu ambao wamezoea kuhangaika kwa ajili ya kujipatia chochote kitu kwa ajili ya kuhakikisha matumbo yao yanakuwa na shibe bali vilitawala vilio vya watu ambao walikuwa wanalia sana kuwapoteza wapendwa wao wawili na hawakupata hata nafasi ya kuweza kuwaaga. Makamu wa raisi aliapishwa rasmi kama raisi mteule wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na sasa alitakiwa kuongoza mazishi ya watu hao wawili ndani ya nchi na kuelezea sababu za kuto ruhusu watu hao waagwe.

Sababu kubwa alisema kwamba yalikuwa ni mambo ya kiusalama kutokana na aina ya vifo ambavyo watu hao walikuwa wamekufa, alisema kwamba hawakutaka kuzua taharuki kwa wananchi na walitakiwa kuwa wapole kwa kuwapumzisha kwa amani wapendwa wao ambao hawakuwa na hatia yoyote ile lakini ni husda za watu ambao walikuwa hawapendi maendeleo ya nchi ya Tanzania ndio ambao walikuwa wamefanya hayo yote ili kuwarudisha nyuma.

Alitoa rai kwa wananchi kuwa watulivu na kufuata sheria za nchi huku akiahidi kwamba kwa yeyote yule ambaye alikuwa amehusika na hayo matukio basi atatafutwa kwa nguvu zote na kupewa adhabu ambayo ilikuwa inaenda kutoa funzo ulimwenguni, alisistiza kwamba aliye muua mheshimiwa raisi alikuwa amenyongwa lakini aliamini kwamba lazima mtu huyo alikuwa ana watu wake ambao walikuwa wanamsaidia kwenye hilo tukio hivyo hao watatafutwa usiku na mchana jeshi la polisi halitalala kuanzia siku hiyo ambayo walikuwa wanaenda kuwapumzisha wapendwa wao na kuongeza kwamba hata wale ambao walimuua jaji mkuu mtukufu na familia yake huku hiyo familia akipona mtu mmoja tu pekee hawataachwa hivi hivi watatafutwa na kupatiwa adhabu kali sana.

Aidha kabla ya kuhitimisha hotuba yake fupi kama mheshimiwa raisi alisema kwamba kwa ajili ya mambo ya kiusalama basi ndugu wa mheshimiwa raisi pamoja na mdogo wake jaji mkuu ambaye alikuwa anaishi nje ya nchi hawatawekwa wazi ili wasije na wao wakafanyiwa kama vile ndugu zao walivyo fanyiwa kwani hawajui lengo la hao wauaji ni nini ila serikali itakuwa nao bega kwa bega katika wakati huu mgumu na watapatiwa kila msaada ambao utakuwa unahitajika kwa upande wao ili kuweza kuwapa Faraja, baada ya hapo alisisitiza kwa makini kwamba misiba hiyo itaonyeshwa moja kwa moja ila itahudhuriwa na watu maalumu ambao wamealikwa kwa ajili ya usalama wa nchi yake” alimaliza hotuba yake na kupigiwa makofi sana huku tukio hilo likiwa linarushwa moja kwa moja ulimwenguni kote.


Mmoja wa watu ambao walikuwa wanaliangalia tukio hilo alikuwa ni Monalisa, alitabsamu sana baada ya kusikia taarifa hizo, alichukua simu yake na kutuma sms fupi tu “KUDOS” kwenye private namba ambayo alikuwa anaiijua yeye mwenyewe, ulikuwa ni muda wake wa kufurahi sana, aliifuata pombe kwenye friji lake akaimimina kwenye glass huku akiwa mwingi wa tabasamu akianza kuishusha taratibu huku akiweka mziki mkubwa na kuanza kukatika akiimba kwa sauti kubwa, dunia ya faraja na amani kwa wakati huo ilikuwa ipo upande wake sasa angemhofia nani?

Monalisa ni nani hasa? Kuna nini kipo kwenye maisha yake, Professor Michael ni nani na hawa watu wanafichana nini kwenye uhalisia wao?

Sehemu ya 18 inafika mwisho, panapo majaaliwa tukutane tena sehemu inayo fuata.

Wasalaam

Bux the storyteller.
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 19

SONGA NAYO............
Siku ilikuwa ni ndefu sana lakini hatimaye ilikuwa imeisha, mazishi yalifanyika kwa amani sana, ndugu wa marehemu na wahusika wote walipewa maelekezo kwamba walikuwa wanahitajika Kwenda Ikulu baada ya hayo mazishi kuweza kufanyika ili wakapate pole za dhati kutoka kwa raisi mpya ambaye alikuwa ameapishwa siku hiyo ndani ya nchi ya Tanzania. Jason alikuwa kwenye suti moja nyeusi ambayo ilikuwa imempendeza sana lakini sura yake haikuwa kwenye furaha yoyote kwa siku hiyo ambayo ilikuwa ni ndefu sana kwa upande wake, baada ya kushuka ndani ya eneo hilo ambalo ni eneo la ndoto za kila mtu ndani ya nchi yoyote ile duniani kama sio kwa kuingia kwenye madaraka basi hata walau kupewa mwaliko wa kuweza kuingia ndani la hayo majengo ya ikulu, baada tu ya kushuka hapo alifuatwa moja kwa moja na watu ambo walimwambia kwamba mheshimiwa raisi alikuwa anahitaji kuongea naye basi wala hakuwa na shida ikabidi awafuate watu hao kuelekea hilo eneo ambalo alikuwa yupo mheshimiwa na muda huo alikuwa anajiandaa kuanza kuwapokea wageni ila kwake mtu wa mhimu zaidi kabla ya kuongea na wageni ambao walikuwa wengine ni maraisi na viongozi wakubwa kutoka nchi mbali mbali duniani wengine wakiwa wametuma wawakilishi wao hata hivyo Jason lilikuwa chaguo lake la kwanza.

“Jina lake anitwa Jason Japhary, ni mdogo wake wa damu na marehemu Markvelous Japhary ambaye alikuwa ni jaji mkuu wa nchi ya Tanzania. Ana umri wa miaka 28 kwa sasa akiwa ana shahada ya uzamili katika mambo ya uhandisi na kwa sasa anajiendeleza ili kuwa daktari wa falsafa kwenye uhandisi ambao ndio ameuishi tangu akiwa ni kijana mdogo. Elimu zake za awali nadhani inajulikana maeneo ambayo amesomea, elimu yake ya juu ameanzia hapo Kenya ambapo alisomea ndani ya chuo kikuu cha Kenyatta, baada ya hapo alienda kusomea udhamiri wa shahada yake ya kwanza ndani ya chuo cha Cambridge University kule nchini Uingereza na baada ya hapo ndipo alijiunga na chuo kikubwa zaidi duniani HAVARD UNIVERSITY ambako ndiko anasoma mpaka muda huu tunavyo zungumza.

Hajawahi kukatisha hata kidogo kwenye kusoma kwake na ni miongoni mwa wanafunzi walioweza kupokea tuzo nyingi sana za nidhamu na taaluma kwenye kila sehemu ambayo ameweza kupita, ni kijana ambaye hajawahi kukutwa na hatia yoyote au kosa lolote lile la kinidhamu iwe ni ndani au nje ya chuo hivyo ni moja kwa moja kwamba ni kijana mmoja msafi sana kwenye taarifa zake” ndani ya Ikulu katika chumba kimoja ambacho alikuwa amekaa mkuu wa majeshi na mwana historia mkuu wa Ikulu alikuwa anahitaji taarifa za kijana huyo kwa sababu mwana historia huyo alikuwa ni mtu ambaye alikuwa anaizitunza historia zote za nchi ya Tanzania pamoja na taarifa za viongozi ambao waliwahi kupita kwenye madaraka yao pamoja na familia zao kwa ujumla. Kwa tukio ambalo lilikuwa limetokea mkuu wa majeshi alimuomba mtu huyo ampe taarifa hizo ambazo alidai kwamba zitawasaidia sana kwenye kuweza kumtafuta mhusika wa mauaji ya mheshimiwa raisi lakini pia namna ya kuweza kuwalinda wana familia wa marehemu wa pande zote mbili hivyo alitaka jambo hilo mzee huyo kuliweka kuwa siri sana hakuhitaji hata raisi mpya aweze kuzipata kabisa taarifa hizo ndiyo maana aliiweka kama siri yao wenyewe.

Mkuu wa majeshi alilazimika kuzitafuta taarifa za kijana huyo ili kama kulikuwa kuna kitu ambacho hukukijua kuhusiana na kijana huyo aweze kukifahamu lakini hakukuwa na tatizo lolote lile juu ya Jason na kwa taarifa zake alikuwa ni kijana mmoja mlaini sana basi CDF aliamua kuamini kwamba huenda kijana huyo aliongea naye vile kwa sababu ya hasira na mawazo mazito ya msiba.

“Una uhakika hakuna taarifa yoyote nyingine ambayo inamhusu huyu kijana na haijulikani?” aliuliza akiwa anamwangalia mzee huyo ambaye alikuwa amefanya kazi ndani ya ikulu hiyo kwa muda mrefu sana.

“Nimekaa Ikulu kwa awamu nne tofauti tofauti najua mambo mengi pengine kuliko hata mtu ambaye anasimama kama raisi wa nchi, kama kungekuwa na taarifa za ziada kuhusu huyu kijana basi ningekuwa nimeshazipata muda mrefu sana kwani alikuwa ni mdogo wa mtu mkubwa sana ambaye pia ni familia ya mheshimiwa raisi hivyo taarifa zake haziwezi kujificha”

“Sawa kama kuna taarifa za mhimu zozote ambazo utazipata basi naomba usisite kunipa hiyo taarifa haraka sana maana saivi kuna taharuki kubwa sana hivyo inatakiwa tuhakikishe kwamba ulinzi na usalama vinaboreshwa ili kuhakikisha tunawalinda hawa watu lakini pia hata raia wa nje wasije wakapata matatizo na sisi tupo kama tulivyoweza kushindwa kuwalinda ndugu zetu”

“Sawa mkuu” CDF alitabasamu baada ya mzee huyo kutamka hivyo kisha akatoka ndani ya chumba hicho. Baada ya yeye kutoka mzee huyo alifunga mlango na kuchukua simu yake kisha akaipiga mahali, iliita kwa muda mfupi tu na kupokelewa.

“Nina wageni wengi sana hivyo nikiwa na muda nitakutafuta mwenyewe kama kuna jambo la mhimu la kuongea nawewe” ilisikika sauti upande wa pili baada ya simu hiyo kuweza kupokelewa.

“Mheshimiwa amekuja kumuulizia Jason” aliongea kwa sauti ndogo sana ambayo hakutaka kusikika na mtu yeyote yule.

“Whaaaaat” Upande wa pili wa simu ulionekana kushtuka sana
“Yes, alikuwa anazihitaji taarifa za historia ya Jason tangu azaliwe?”

“Ni nani ambaye amefanya hicho kitu?”

“Mkuu wa majeshi”

“Umemwambiaje?”

“Nimempa zile taarifa za siku zote”

“Safi, kakwambiaje baada ya wewe kumwambia hivyo?”

“Amesema kwa taharuki ambayo imezuka kwa sasa wanahitaji kufanya uchunguzi mkubwa sana juu ya tukio lililo tokea hivyo alikuwa anahitaji taarifa za Jason ili aweze kumlinda maana mpaka sasa hawana imani na usalama wake ndiyo maana wanataka kuwa na taarifa zake zote ili waweze kumlinda na lisitokee kosa lingine kama lile ambalo limefanyika kwa kaka yake”

“Ni bora ufe ila hizo taarifa hazitakiwi kumfikia mtu yeyote yule, kwa watu ambao tupo hai, tulikuwa wawili tu mpaka pale ambapo niliamua kukushirikisha wewe hapo tumekuwa jumla watatu ndio ambao tuna taarifa za huyo mtoto hivyo kama ikivuja hata sentensi moja basi hakutakuwa na mwingine zaidi ya sisi watatu ambaye ndiye atakuwa amevujisha hizi habari hivyo hicho kitu hakikisha unakufa nacho kwenye kifua chako yule ndiye future ya nchi na mambo mengi yanamtegemea yeye ili hii nchi iwe sawa nadhani unanielewa”

“Ndiyo mheshimiwa nakuelewa vizuri”

“Nikimaliza vikao nitakutana na wewe baadaye”
“Sawa mheshimiwa” alionekana kwamba alikuwa anaongea na mtu ambaye yeye binafsi alikuwa akimheshimu sana kwa jinsi alivyokuwa mnyenyekevu mbele ya mtu huyo, alihema baada ya kukata simu yake na kuchora ishara ya kutoa shukrani kwa muumba wake.


Ndani ya chumba ambacho alikuwa amekaa mheshimiwa raisi, mlango ulifunguliwa aliingia mwanaume ambaye uso wake ulikuwa na ndevu nyingi ambazo zilichongwa vyema, baada ya kuufunga mlango huo mwanaume huyo alizibandua ndevu zake hizo usoni kwake, Jason ndiye ambaye alikuwa ameingia humo ndani, tangu asubuhi ya siku hiyo alikuwa ndani ya hizo ndevu ilikuwa sio rahisi kuweza kumtambua kama ni yeye ndiye ambaye alikuwa kwenye hiyo hali, mheshimiwa alinyanyuka kutoka kwenye kiti chake na Kwenda kumkumbatia kijana huyo akiwa anampiga piga mgongoni mwake.

“Pole sana pole sana mwanangu, nisamehe mno tangu umefika sijapata hata bahati ya kuweza kukutana na kuongea nawewe najua ni maumivu makali sana ambayo unayapitia mpaka wakati huu ila kwa mimi nipo bega kwa bega na wewe”

“Asante sana mzee”

“Kwanini leo umeamua kuwa kwenye mwonekano wa hivyo?”
“Unayajua maisha yangu vizuri kwamba mimi ni mtu ambaye sitakiwi kujulikana sana hivyo sina namna nyingine ndiyo maisha ambayo mmesha nichagulia, leo vyombo vya habari vilizagaa sana sura yangu ingetambulika kiwepesi kila sehemu”

“Daaah pole sana, unajua kuna muda inaniuma sana kuona unaishi hivi ila hakuna namna kwa ajili ya usalama wa hili taifa inakulazimu kuwa hivyo tu, siku ya kwanza ya kukujua kwamba wewe ni nani nilikuonea huuruma sana kwa sababu ulikuwa umepewa majukumu mazito sana ungali bado kijana mdogo tu ambaye ulitakiwa kuendelea kuzipambania ndoto zako na sijajua kwanini ulikubali kufanya kazi za kutisha kama hizo na umri wako huo” mheshimiwa raisi aliongea hayo maneno akiwa anamimina wine kwenye bilauri mbili zilizokuwa juu ya meza ghali ya vioo hiyo huku akiendelea kuongea na kijana wake.

“Na ndiyo maana hata baada ya kukubali sikuwahi kuruhusu kaka yangu aweze kuyajua haya mambo maana angechukia sana na asidhani kama angemsamehe mheshimiwa raisi au baba mkubwa ambaye ni mmoja kati ya wale ndugu zake ndiye mwenye taarifa zangu zote. Mimi nilichagua kazi hii kwa sababu napenda ninacho kifanya na hata kama kufa nipo tayari muda wowote ule, kilicho nifanya nikawa na moyo wote wa kuifanya hii kazi ni pale ambapo raisi alikuwa tayari kunipa kazi kubwa kama ile wakati sikuwa na taaluma yoyote ile na baada ya kunieleza kwamba wananihitaji mimi sikuwaza mara mbili japo kwa wakati ule nilikuwa bado mdogo ila niliamua kuikubali na kufa na ile siri kwenye kifua changu hata kaka yangu amekufa akiwa hamjui mdogo wake ambaye amemlea yeye mwenyewe kwa mikono yake” Jason alijibu huku akiwa anashushia bilauri yake hiyo ya wine.

“Na hilo ndilo jambo ambalo nilikuwa naliogopa mpaka leo kwamba vipi kama Mark angejua angetuchukia sana kukuingiza kwnye hatari kubwa kama hiyo mtu ambaye akili yake ilikuwa inatumika kuliongoza taifa, niseme tu MUNGU amlaze mahala pema huko aliko”

“Sina imani kama kaka yangu anaweza kupumzika kwa amani kama hawa watu wanaendelea kuishi”

“Mhhhh nalielewa hilo lakini si unajua kwamba watu wa namna hii lazima watakuwa na nguvu na kila kitu ndiyo maana kirahisi tu wamepata mpaka kiburi cha kuweza kumuua mkuu wa nchi, hili ni jambo la kutisha sana saivi nchi nyingi duniani zinahoji sana kuhusu hilo na hata umoja wa mataifa wanahoji kwamba nchi itachukua uamuzi gani ili kama tuna uhitaji na msaada wao basi watusaidie”

“Kuhusu hilo jambo la kuwatafuta hawa watu niachie mimi mwenyewe nitaifanya hiyo kazi na hao wanao hoji waambie kama taifa tunawatafuta hao watu na muda wowote kuanzia sasa watapatikana”

“Sasa wasipo patikana?”

“Mhhhh hakuna mtu anayeweza kupona katika hili kama tu aliingiza mkono wake na akaonyesha uhusika wake iwe moja kwa moja u hata kwa kugusia tu”

“Unataka kufanya nini?”
“Nikitoka hapa kuna mtu nitawasiliana naye yupo CANADA kwa sasa kesho ataingia nchini, baada ya hapo nitataka anihakikishie kitu fulani kama ni cha kweli basi nitatoa muda kwa hao watu ambao wamehusika waje wenyewe mbele ya vyombo vya habari, kwa atakaye jitokeza basi atahukumiwa kwa sheria ila kwa wale ambao watapuuza basi hii nchi itakuwa sehemu mbaya sana kwao kwa ajili ya maisha yao”

“Una uhakika gani kama watu hao watajitokeza?”

“Ndiyo maana nimesema wasipo jitokeza basi mimi nitafanya maamuzi yangu mwenyewe”

“Mhhhh unataka kuanza kuua tena”

“Yes”

“Hapana hapana, hawa watu naomba tuwakamate tu wateswe vikali na kufungwa au kunyongwa kwa sheria, kama utaua mtu hata mmoja basi utawafanya wananchi waishi maisha ya hofu sana maana kile kiwango cha mauaji kama kuna mwananchi akiona au marehemu akipigwa picha kuna mtu atatamani kuishi nchi hii kweli? Hapana Hapana huko ni mbali mno” mheshimiwa raisi aliyapinga sana mawazo ya Jason ambaye haikueleweka huwa anauaje mpaka mheshimiwa anaogopa sana kuweza kumruhusu kufanya hayo maamuzi yake.

“Ndiyo maana nimesema nitatoa muda, miezi sita inatosha sana kwa watu hao kujifikiria na kujitokeza na kwa huo muda hawatakuja kunisikia kabisa ila kama utapita huo muda wakadharau na wakagoma kujisalimisha kwenye vyomba vya habari basi itabidi niwatafute mimi mwenyewe”

“Mhhhhhh mimi biafsi huwa sitaki hata kuona mwili wa mtu ambaye umempiga inanitisha sana sasa ukirudi kwenye uuaji hii nchi haitakuwa sehemu salama kwa kuishi”

“Nimefanya uzembe raisi wa nchi amekufa, kama ningebaki hapa hapa nchini hakuna mtu ambaye angekuwa na jeuri ya kufanya hayo yote lakini kuondoka kwangu tu sijajua imekuwaje mpaka uzembe mdogo sana namna hiyo unafanyika, hao wajinga hawajaishia hapo wameenda na kuigusa familia yangu sasa hapo nitawaachaje mheshimiwa? Huruma yangu ni kwa huo muda ambao nitautoa ila baada ya hapo itabidi watu waijue sehemu yangu ambayo inaishi gizani ninapokuwa nashika kalamu ya wino pamoja na hizi nguo nzuri ambazo nakuwa nazivaa”

“Mkuu wa majeshi amekuja kuzitafuta taarifa zako”

“Huyo usijali kuhusu yeye nitamalizana naye mimi mwenyewe”

“Una uhakika na usalama wako? kama inawezekana uwe unatembea na vijana?”

“Hao watoto ndo wanilinde mimi hapa?”
“Nadhani itafaa zaidi kule kuna watu wana uwezo sana”

“Hao nitawapa tu majukumu ya kuweza kuendelea kukusanya taarifa za wahusika”

“Ni lini utaruhusu wakujue?”

“Kama nikiondoka kwa huo muda ambao nitawapa nafasi watu hao kujitokeza kama hawatajitokeza basi nikirudi vijana watanifahamu” Jason alijibu huku akiwa anasimama ili kuweza kutoka humo ndani.

“Kuwa makini sana” Mheshimiwa raisi aliongea huku akiwa anamtazama kijana huyo ambaye alikuwa anaishia mlangoni. Jason baada ya kutoka hapo aliichukua simu yake na kupiga mahali.

“Alphonce, i need you by tomorrow, location Dar es salaam” aliongea kifupi tu na kukata simu hiyo kisha akatoka na kuondoka kabisa ndani ya Ikulu.

Huyu Jason ni nani? ni mtu wa aina gani?

19 nafika tamati sehemu inayofuata inaweza kutupatia majibu ya maswali yetu.

Wasalaam

Bux the storyteller.
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 19

SONGA NAYO............
Siku ilikuwa ni ndefu sana lakini hatimaye ilikuwa imeisha, mazishi yalifanyika kwa amani sana, ndugu wa marehemu na wahusika wote walipewa maelekezo kwamba walikuwa wanahitajika Kwenda Ikulu baada ya hayo mazishi kuweza kufanyika ili wakapate pole za dhati kutoka kwa raisi mpya ambaye alikuwa ameapishwa siku hiyo ndani ya nchi ya Tanzania. Jason alikuwa kwenye suti moja nyeusi ambayo ilikuwa imempendeza sana lakini sura yake haikuwa kwenye furaha yoyote kwa siku hiyo ambayo ilikuwa ni ndefu sana kwa upande wake, baada ya kushuka ndani ya eneo hilo ambalo ni eneo la ndoto za kila mtu ndani ya nchi yoyote ile duniani kama sio kwa kuingia kwenye madaraka basi hata walau kupewa mwaliko wa kuweza kuingia ndani la hayo majengo ya ikulu, baada tu ya kushuka hapo alifuatwa moja kwa moja na watu ambo walimwambia kwamba mheshimiwa raisi alikuwa anahitaji kuongea naye basi wala hakuwa na shida ikabidi awafuate watu hao kuelekea hilo eneo ambalo alikuwa yupo mheshimiwa na muda huo alikuwa anajiandaa kuanza kuwapokea wageni ila kwake mtu wa mhimu zaidi kabla ya kuongea na wageni ambao walikuwa wengine ni maraisi na viongozi wakubwa kutoka nchi mbali mbali duniani wengine wakiwa wametuma wawakilishi wao hata hivyo Jason lilikuwa chaguo lake la kwanza.

“Jina lake anitwa Jason Japhary, ni mdogo wake wa damu na marehemu Markvelous Japhary ambaye alikuwa ni jaji mkuu wa nchi ya Tanzania. Ana umri wa miaka 28 kwa sasa akiwa ana shahada ya uzamili katika mambo ya uhandisi na kwa sasa anajiendeleza ili kuwa daktari wa falsafa kwenye uhandisi ambao ndio ameuishi tangu akiwa ni kijana mdogo. Elimu zake za awali nadhani inajulikana maeneo ambayo amesomea, elimu yake ya juu ameanzia hapo Kenya ambapo alisomea ndani ya chuo kikuu cha Kenyatta, baada ya hapo alienda kusomea udhamiri wa shahada yake ya kwanza ndani ya chuo cha Cambridge University kule nchini Uingereza na baada ya hapo ndipo alijiunga na chuo kikubwa zaidi duniani HAVARD UNIVERSITY ambako ndiko anasoma mpaka muda huu tunavyo zungumza.

Hajawahi kukatisha hata kidogo kwenye kusoma kwake na ni miongoni mwa wanafunzi walioweza kupokea tuzo nyingi sana za nidhamu na taaluma kwenye kila sehemu ambayo ameweza kupita, ni kijana ambaye hajawahi kukutwa na hatia yoyote au kosa lolote lile la kinidhamu iwe ni ndani au nje ya chuo hivyo ni moja kwa moja kwamba ni kijana mmoja msafi sana kwenye taarifa zake” ndani ya Ikulu katika chumba kimoja ambacho alikuwa amekaa mkuu wa majeshi na mwana historia mkuu wa Ikulu alikuwa anahitaji taarifa za kijana huyo kwa sababu mwana historia huyo alikuwa ni mtu ambaye alikuwa anaizitunza historia zote za nchi ya Tanzania pamoja na taarifa za viongozi ambao waliwahi kupita kwenye madaraka yao pamoja na familia zao kwa ujumla. Kwa tukio ambalo lilikuwa limetokea mkuu wa majeshi alimuomba mtu huyo ampe taarifa hizo ambazo alidai kwamba zitawasaidia sana kwenye kuweza kumtafuta mhusika wa mauaji ya mheshimiwa raisi lakini pia namna ya kuweza kuwalinda wana familia wa marehemu wa pande zote mbili hivyo alitaka jambo hilo mzee huyo kuliweka kuwa siri sana hakuhitaji hata raisi mpya aweze kuzipata kabisa taarifa hizo ndiyo maana aliiweka kama siri yao wenyewe.

Mkuu wa majeshi alilazimika kuzitafuta taarifa za kijana huyo ili kama kulikuwa kuna kitu ambacho hukukijua kuhusiana na kijana huyo aweze kukifahamu lakini hakukuwa na tatizo lolote lile juu ya Jason na kwa taarifa zake alikuwa ni kijana mmoja mlaini sana basi CDF aliamua kuamini kwamba huenda kijana huyo aliongea naye vile kwa sababu ya hasira na mawazo mazito ya msiba.

“Una uhakika hakuna taarifa yoyote nyingine ambayo inamhusu huyu kijana na haijulikani?” aliuliza akiwa anamwangalia mzee huyo ambaye alikuwa amefanya kazi ndani ya ikulu hiyo kwa muda mrefu sana.

“Nimekaa Ikulu kwa awamu nne tofauti tofauti najua mambo mengi pengine kuliko hata mtu ambaye anasimama kama raisi wa nchi, kama kungekuwa na taarifa za ziada kuhusu huyu kijana basi ningekuwa nimeshazipata muda mrefu sana kwani alikuwa ni mdogo wa mtu mkubwa sana ambaye pia ni familia ya mheshimiwa raisi hivyo taarifa zake haziwezi kujificha”

“Sawa kama kuna taarifa za mhimu zozote ambazo utazipata basi naomba usisite kunipa hiyo taarifa haraka sana maana saivi kuna taharuki kubwa sana hivyo inatakiwa tuhakikishe kwamba ulinzi na usalama vinaboreshwa ili kuhakikisha tunawalinda hawa watu lakini pia hata raia wa nje wasije wakapata matatizo na sisi tupo kama tulivyoweza kushindwa kuwalinda ndugu zetu”

“Sawa mkuu” CDF alitabasamu baada ya mzee huyo kutamka hivyo kisha akatoka ndani ya chumba hicho. Baada ya yeye kutoka mzee huyo alifunga mlango na kuchukua simu yake kisha akaipiga mahali, iliita kwa muda mfupi tu na kupokelewa.

“Nina wageni wengi sana hivyo nikiwa na muda nitakutafuta mwenyewe kama kuna jambo la mhimu la kuongea nawewe” ilisikika sauti upande wa pili baada ya simu hiyo kuweza kupokelewa.

“Mheshimiwa amekuja kumuulizia Jason” aliongea kwa sauti ndogo sana ambayo hakutaka kusikika na mtu yeyote yule.

“Whaaaaat” Upande wa pili wa simu ulionekana kushtuka sana
“Yes, alikuwa anazihitaji taarifa za historia ya Jason tangu azaliwe?”

“Ni nani ambaye amefanya hicho kitu?”

“Mkuu wa majeshi”

“Umemwambiaje?”

“Nimempa zile taarifa za siku zote”

“Safi, kakwambiaje baada ya wewe kumwambia hivyo?”

“Amesema kwa taharuki ambayo imezuka kwa sasa wanahitaji kufanya uchunguzi mkubwa sana juu ya tukio lililo tokea hivyo alikuwa anahitaji taarifa za Jason ili aweze kumlinda maana mpaka sasa hawana imani na usalama wake ndiyo maana wanataka kuwa na taarifa zake zote ili waweze kumlinda na lisitokee kosa lingine kama lile ambalo limefanyika kwa kaka yake”

“Ni bora ufe ila hizo taarifa hazitakiwi kumfikia mtu yeyote yule, kwa watu ambao tupo hai, tulikuwa wawili tu mpaka pale ambapo niliamua kukushirikisha wewe hapo tumekuwa jumla watatu ndio ambao tuna taarifa za huyo mtoto hivyo kama ikivuja hata sentensi moja basi hakutakuwa na mwingine zaidi ya sisi watatu ambaye ndiye atakuwa amevujisha hizi habari hivyo hicho kitu hakikisha unakufa nacho kwenye kifua chako yule ndiye future ya nchi na mambo mengi yanamtegemea yeye ili hii nchi iwe sawa nadhani unanielewa”

“Ndiyo mheshimiwa nakuelewa vizuri”

“Nikimaliza vikao nitakutana na wewe baadaye”
“Sawa mheshimiwa” alionekana kwamba alikuwa anaongea na mtu ambaye yeye binafsi alikuwa akimheshimu sana kwa jinsi alivyokuwa mnyenyekevu mbele ya mtu huyo, alihema baada ya kukata simu yake na kuchora ishara ya kutoa shukrani kwa muumba wake.


Ndani ya chumba ambacho alikuwa amekaa mheshimiwa raisi, mlango ulifunguliwa aliingia mwanaume ambaye uso wake ulikuwa na ndevu nyingi ambazo zilichongwa vyema, baada ya kuufunga mlango huo mwanaume huyo alizibandua ndevu zake hizo usoni kwake, Jason ndiye ambaye alikuwa ameingia humo ndani, tangu asubuhi ya siku hiyo alikuwa ndani ya hizo ndevu ilikuwa sio rahisi kuweza kumtambua kama ni yeye ndiye ambaye alikuwa kwenye hiyo hali, mheshimiwa alinyanyuka kutoka kwenye kiti chake na Kwenda kumkumbatia kijana huyo akiwa anampiga piga mgongoni mwake.

“Pole sana pole sana mwanangu, nisamehe mno tangu umefika sijapata hata bahati ya kuweza kukutana na kuongea nawewe najua ni maumivu makali sana ambayo unayapitia mpaka wakati huu ila kwa mimi nipo bega kwa bega na wewe”

“Asante sana mzee”

“Kwanini leo umeamua kuwa kwenye mwonekano wa hivyo?”
“Unayajua maisha yangu vizuri kwamba mimi ni mtu ambaye sitakiwi kujulikana sana hivyo sina namna nyingine ndiyo maisha ambayo mmesha nichagulia, leo vyombo vya habari vilizagaa sana sura yangu ingetambulika kiwepesi kila sehemu”

“Daaah pole sana, unajua kuna muda inaniuma sana kuona unaishi hivi ila hakuna namna kwa ajili ya usalama wa hili taifa inakulazimu kuwa hivyo tu, siku ya kwanza ya kukujua kwamba wewe ni nani nilikuonea huuruma sana kwa sababu ulikuwa umepewa majukumu mazito sana ungali bado kijana mdogo tu ambaye ulitakiwa kuendelea kuzipambania ndoto zako na sijajua kwanini ulikubali kufanya kazi za kutisha kama hizo na umri wako huo” mheshimiwa raisi aliongea hayo maneno akiwa anamimina wine kwenye bilauri mbili zilizokuwa juu ya meza ghali ya vioo hiyo huku akiendelea kuongea na kijana wake.

“Na ndiyo maana hata baada ya kukubali sikuwahi kuruhusu kaka yangu aweze kuyajua haya mambo maana angechukia sana na asidhani kama angemsamehe mheshimiwa raisi au baba mkubwa ambaye ni mmoja kati ya wale ndugu zake ndiye mwenye taarifa zangu zote. Mimi nilichagua kazi hii kwa sababu napenda ninacho kifanya na hata kama kufa nipo tayari muda wowote ule, kilicho nifanya nikawa na moyo wote wa kuifanya hii kazi ni pale ambapo raisi alikuwa tayari kunipa kazi kubwa kama ile wakati sikuwa na taaluma yoyote ile na baada ya kunieleza kwamba wananihitaji mimi sikuwaza mara mbili japo kwa wakati ule nilikuwa bado mdogo ila niliamua kuikubali na kufa na ile siri kwenye kifua changu hata kaka yangu amekufa akiwa hamjui mdogo wake ambaye amemlea yeye mwenyewe kwa mikono yake” Jason alijibu huku akiwa anashushia bilauri yake hiyo ya wine.

“Na hilo ndilo jambo ambalo nilikuwa naliogopa mpaka leo kwamba vipi kama Mark angejua angetuchukia sana kukuingiza kwnye hatari kubwa kama hiyo mtu ambaye akili yake ilikuwa inatumika kuliongoza taifa, niseme tu MUNGU amlaze mahala pema huko aliko”

“Sina imani kama kaka yangu anaweza kupumzika kwa amani kama hawa watu wanaendelea kuishi”

“Mhhhh nalielewa hilo lakini si unajua kwamba watu wa namna hii lazima watakuwa na nguvu na kila kitu ndiyo maana kirahisi tu wamepata mpaka kiburi cha kuweza kumuua mkuu wa nchi, hili ni jambo la kutisha sana saivi nchi nyingi duniani zinahoji sana kuhusu hilo na hata umoja wa mataifa wanahoji kwamba nchi itachukua uamuzi gani ili kama tuna uhitaji na msaada wao basi watusaidie”

“Kuhusu hilo jambo la kuwatafuta hawa watu niachie mimi mwenyewe nitaifanya hiyo kazi na hao wanao hoji waambie kama taifa tunawatafuta hao watu na muda wowote kuanzia sasa watapatikana”

“Sasa wasipo patikana?”

“Mhhhh hakuna mtu anayeweza kupona katika hili kama tu aliingiza mkono wake na akaonyesha uhusika wake iwe moja kwa moja u hata kwa kugusia tu”

“Unataka kufanya nini?”
“Nikitoka hapa kuna mtu nitawasiliana naye yupo CANADA kwa sasa kesho ataingia nchini, baada ya hapo nitataka anihakikishie kitu fulani kama ni cha kweli basi nitatoa muda kwa hao watu ambao wamehusika waje wenyewe mbele ya vyombo vya habari, kwa atakaye jitokeza basi atahukumiwa kwa sheria ila kwa wale ambao watapuuza basi hii nchi itakuwa sehemu mbaya sana kwao kwa ajili ya maisha yao”

“Una uhakika gani kama watu hao watajitokeza?”

“Ndiyo maana nimesema wasipo jitokeza basi mimi nitafanya maamuzi yangu mwenyewe”

“Mhhhh unataka kuanza kuua tena”

“Yes”

“Hapana hapana, hawa watu naomba tuwakamate tu wateswe vikali na kufungwa au kunyongwa kwa sheria, kama utaua mtu hata mmoja basi utawafanya wananchi waishi maisha ya hofu sana maana kile kiwango cha mauaji kama kuna mwananchi akiona au marehemu akipigwa picha kuna mtu atatamani kuishi nchi hii kweli? Hapana Hapana huko ni mbali mno” mheshimiwa raisi aliyapinga sana mawazo ya Jason ambaye haikueleweka huwa anauaje mpaka mheshimiwa anaogopa sana kuweza kumruhusu kufanya hayo maamuzi yake.

“Ndiyo maana nimesema nitatoa muda, miezi sita inatosha sana kwa watu hao kujifikiria na kujitokeza na kwa huo muda hawatakuja kunisikia kabisa ila kama utapita huo muda wakadharau na wakagoma kujisalimisha kwenye vyomba vya habari basi itabidi niwatafute mimi mwenyewe”

“Mhhhhhh mimi biafsi huwa sitaki hata kuona mwili wa mtu ambaye umempiga inanitisha sana sasa ukirudi kwenye uuaji hii nchi haitakuwa sehemu salama kwa kuishi”

“Nimefanya uzembe raisi wa nchi amekufa, kama ningebaki hapa hapa nchini hakuna mtu ambaye angekuwa na jeuri ya kufanya hayo yote lakini kuondoka kwangu tu sijajua imekuwaje mpaka uzembe mdogo sana namna hiyo unafanyika, hao wajinga hawajaishia hapo wameenda na kuigusa familia yangu sasa hapo nitawaachaje mheshimiwa? Huruma yangu ni kwa huo muda ambao nitautoa ila baada ya hapo itabidi watu waijue sehemu yangu ambayo inaishi gizani ninapokuwa nashika kalamu ya wino pamoja na hizi nguo nzuri ambazo nakuwa nazivaa”

“Mkuu wa majeshi amekuja kuzitafuta taarifa zako”

“Huyo usijali kuhusu yeye nitamalizana naye mimi mwenyewe”

“Una uhakika na usalama wako? kama inawezekana uwe unatembea na vijana?”

“Hao watoto ndo wanilinde mimi hapa?”
“Nadhani itafaa zaidi kule kuna watu wana uwezo sana”

“Hao nitawapa tu majukumu ya kuweza kuendelea kukusanya taarifa za wahusika”

“Ni lini utaruhusu wakujue?”

“Kama nikiondoka kwa huo muda ambao nitawapa nafasi watu hao kujitokeza kama hawatajitokeza basi nikirudi vijana watanifahamu” Jason alijibu huku akiwa anasimama ili kuweza kutoka humo ndani.

“Kuwa makini sana” Mheshimiwa raisi aliongea huku akiwa anamtazama kijana huyo ambaye alikuwa anaishia mlangoni. Jason baada ya kutoka hapo aliichukua simu yake na kupiga mahali.

“Alphonce, i need you by tomorrow, location Dar es salaam” aliongea kifupi tu na kukata simu hiyo kisha akatoka na kuondoka kabisa ndani ya Ikulu.

Huyu Jason ni nani? ni mtu wa aina gani?

19 nafika tamati sehemu inayofuata inaweza kutupatia majibu ya maswali yetu.

Wasalaam

Bux the storyteller.
shukran Sana chief.

be blessed
 
Nimehangaika nayo, hatimaye imeisha yote[emoji106]
Screenshot_20230508-142622_WhatsAppBusiness.jpg
 
Back
Top Bottom