Innocent Killer (The Revenge)

Innocent Killer (The Revenge)

STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
TELLER: Bux the story teller
WhatsApp: 0621567672
Email: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
SONGA NAYO................

Jaiwelo Makupi Makubilo CDF wa nchi ya Tanzania alikuwa kwenye wakati mgumu sana, usiku kwa upande wake ulikuwa ni mgumu na mrefu sana, alijaribu mno kujilazimisha ili alale siku ipite lakini ilishindikana. Siku ya kesho yake alikuwa anasubiri kumpokea bintiye kipenzi ambaye alikuwa nje ya nchi akiisomea sheria ambayo aliahidi kwamba akirudi tu Tanzania basi ataanza kuifanyia kazi haraka sana, Asharose ndilo lilikuwa jina lake huyu ndiye alikuwa dada wa pekee kwa Oden mtoto wa kiume wa CDF, akiwa ndani ya jengo lake la kifahari hilo akili ilimkatalia kabisa kuweza kuendelea kukaa kitandani hapo ambapo aliishia tu kumwangalia mrembo ambaye kila siku alikuwa hapo kumpatia burudani pale alipo ihitaji. Alinyanyuka na kuelekea kwenye chumba cha nguo alivaa suti safi sana nyeusi na kiatu chake cheusi na kuitoa simu yake mfukoni, alipekua namba kadhaa kwenye simu yake baada ya kuipata ambayo yeye alikuwa akiihitaji aliipiga ambayo iliita karibia dakika nzima ndipo ikapokelewa.

“Mheshimiwa naomba unisamehe sana tena sana kwa kukusumbua mapema yote hii ambayo usingizi huwa unakuwa mtamu sana kwa ajili ya kuitafuta alfajiri lakini nakuomba sana nikutane nawewe muda huu nina jambo la mhimu sana nahitaji kuongea nawewe muda huu” aliongea kwa sauti ya upole na unyenyekevu ndani yake akimuomba mtu wa upande wa pili kisha akaikata simu hiyo baada ya kulipata jibu ambalo huenda alikusudia kulipata. Hakukaa tena alitoka nje moja kwa moja na kuingia kwenye gari yake ambayo alimkuta dereva wake akiwa ndani ya gari hiyo tena akiwa macho kabisa.
“Mhhhhh sijawahi kupata kijana mchapakazi kama wewe haujalala mpaka muda huu? kuna haja kubwa sana ya kukuongezea mshahara” aliongea akiwa anakaa vizuri na kuiweka tai yake vyema
“Kazi yangu ni kukupeleka popote unapo hitaji kwa muda wowote ule na nitahakikisha hilo nalikamilisha kwa asilimia zote bosi wangu” kijana huyo ambaye kwenye mwili wake alikuwa amevaa vazi la jeshi alijibu huku akiwa anasogeza gari getini.

“Nipeleke Ikulu na tunatakiwa kufika mapema sana kwa sababu ni dharura ila mheshimiwa kaniruhusu niweze Kwenda haraka” aliongea na kumfanya kijana huyo aelewe kwamba kumbe ilikuwa ni safari ya Kwenda kukutana na mkubwa wa nchi, hakuwa na neno ilikuwa ni kazi yake kumuendesha bosi wake huyo japo siku hiyo alishangaa sana kuona mzee huyo anatoka bila ulinzi wowote ule japo hakutaka kabisa kuuliza kwani haikuwa biashara yake. Walifika Ikulu mwanaume huyo alishuka na kumtaka derva wake abaki humo humo ndani ya gari angerudi baada ya kumaliza kikao na mheshimiwa, aliiweka suti yake vizuri na kujinyoosha kisha akaanza safari ya kuelekea kwenye chumba cha mkutano ambako angeweza kufanya maongezi na mheshimiwa raisi mpya wa Tanzania, baada ya kufika aliambiwa asubiri hapo ,mheshimiwa anapigiwa simu, baada ya kama dakika tano alipita kwenye machine moja ambapo aliacha silaha zake hapo na kuhakikisha hana chochote kwenye mwili wake, huu ulikuwa ni utaratibu mpya wa Ikulu ambao hata yeye aliushangaa sana kwani kwa mara ya kwanza kwa watu wenye vyeo kama yeye walikuwa wanaingia tu kama wapo kwao.

Mheshimiwa alikuwa ndani ya chumba hicho akiwa anamsubiri mkuu wa majeshi ambaye alimkurupua usiku huo kwamba alikuwa ana shida ya mhimu sana ya kuweza kuogea naye.

“Nisamehe sana bosi kwa kukuweka hapa muda huu nikakupa na adhabu ya kusubiri” aliongea huku akiwa anasogeza kiti hicho pembeni kidogo ili apate nafasi ya kukaa ili aongee na raisi wa nchi.
“Unajua zamani sana nilikuwa namuonea sana wivu mtu yeyote yule ambaye anakuwa kwenye ngazi za juu kwa sababu nilikuwa nahisi kwamba wao ndio wanao faidi sana haya maisha kuliko mtu yeyote yule lakini cha ajabu baada ya kuja kuwa makamu wa raisi nilielewa mizigo mizito ambayo maraisi wanayo, kwanza muda wa kulala ni mdogo sana kwa sababu unakuta unataka kupumzika muda huo unapigiwa simu kuna dharura ya mkutano, mara wanasubiri tamko lako na unakuwa huna namna kwa sababu umeapa kuwapigania wananchi wako kwa hali yoyote na kwa muda wowote hivyo hauna haja hata ya kuniomba msamaha kwa sababu ni moja ya majukumu yangu kufanya hivi kwa moja ya wananchi wangu” hayo maelezo namna yalivyoweza kuhitimishwa ni kama hayakumfurahisha sana CDF sura ilibadilika ghafla kisha akarudi kwenye hali yake na kutabasamu.

“Asante sana kwa kuwa moja ya viongozi bora sana na nikupe hongera kwa kuboresha baadhi ya vitu vya ulinzi hapa japo ni kimya kimya mheshimiwa” CDF alikuwa anachombeza kuweza kujua nini sababu ya vyote hivyo kufanyika ghafla sana namna hiyo

“Nadhani umeniambia una mazungumzo ya mhimu sana ndiyo maana nimeacha kila kitu changu nipo hapa kukusikiliza sasa sijaelewa kama unataka hadithi za ulinzi au unataka kuniambia kilicho kuleta hapa”mwanaume huyo ambaye umri ulikuwa umeenda lakini alikuwa imara sana kwa mwonekano alimjibu mheshimiwa Jaiwelo ambaye alionekana kutaka kuzidisha mazoea na mtu ambaye hakutakiwa kumzoea kwa namna yoyote ile kwenye maisha yake zaidi ya kumheshimu na kumtumikia.
“Ernesto Steven ndilo jina lako mheshimiwa, jina lako ndilo lililo nifanya nikavutiwa sana na wewe ndiyo maana nikatamani sana kuweza kukujua kiundani na ndilo nilipo yapata makablasha mengi sana yaliyo andikwa kuhusu maisha yako, kilicho nivutia zaidi kwenye simulizi ya maisha yako na hilo neno Ernesto ni jina ambalo ni maarufu sana kwenye dunia ya wapambanaji na wapambania haki lakini pia kwa masocialist(majamaa) kama baba yako mzazi mzee Steven yahaye Mdumila. Hilo ni jina la Guevarra Ernesto Chegue Vara mwanaume ambaye mpaka leo dunia haijui kaburi lake liko wapi, huyo ni mtu ambaye alizaliwa Argentina huko lakini alisaidia sana kupigania uhuru wa nchi nyingi mno ikiwemo Cuba na hata Congo hapa Jirani na kwetu, nilitamani sana kujua kwanini baba yako kakupa hilo jina badala ya kukuita Enest ya kawaida ndipo niligundua alikuwa mwana mapinduzi japo hakujulikana na baadae aliishia kuuawa lakini alikupa hilo jina ili wewe uje kuendeleza yale ambayo mwanaume huyo aliwahi kuyafanya huko duniani mwenye hilo jina na tangu hapo sijawahi kabisa kuwa na wasiwasi na uongozi wako hata ulipokuwa makamu wa raisi nilijua hapa nchi imepata mtu mwenye maono makubwa sana kuhusu nchi yetu na nilijivunia sana kwa hilo” mkuu wa majeshi alitulia kidogo baada ya kuongea hayo maneno na kuliweka sawa koo lake huku akiwa na uhakika kwamba mtu aliyekuwa mbele yake alikuwa akimsikiliza kwa umakini sana.

“Licha ya mambo mengi sana ambayo umepitia kwa kulelewa na mama wa kambo pamoja na mihogo ya kuchoma pale Kawe ila baadae ukafanyika kuwa kiongozi bora wa nchi na nina imani una malengo makubwa sana ya kuweza kuifikisha nchi hii mbali na ili uifikishe nchi mbali unatuhitaji sasa sisi ambao tutakuwa tunetekeleza kazi nyingi sana zinazohusu ulinzi wako, ulinzi wa mipaka ya nchi lakini hata usalama wa raia pamoja na mali zao kwa kushirikiana na hizi taasisi zetu nne, hapa namaanisha Ikulu, jeshi la nchi, jeshi la polisi pamoja na taasisi ya usalama wa taifa, tukiwa na nguvu moja nina imani kubwa sana tutaweza kuirejesha amani kubwa sana ya nchi kama ilivyokuwa hapo mwanzo na tunaweza kulifanyia kazi haraka sana hili jambo ambalo limetokea la aibu sana la kumpoteza mkuu wa nchi pamoja na jaji mkuu wa nchi kwa kupata kitu cha kuwaambia wananchi kuhusu kilicho tokea lakini kuna muda mimi huwa napata sana ukakasi kwa sababu kuna baadhi ya viongozi wangu wa taasisi zingine za usalama siwajui hili jambo kila nikiwaza sana huwa linafikia hatua ya kunichanganya sana akili ndiyo maana leo nilivyo wakumbuka wale rafiki zangu wawili ambao wamekufa basi nimeshindwa kabisa kulala” Jaiwelo Makubilo alihema kwa nguvu na kujipa nafasi kidogo ya kupumua maana alikuwa anaongea kwa hisia sana kisha akaendelea.

“Ni miaka mingi sana imepita mimi tangu nipate nafasi kwenye jeshi mpaka mwisho wa siku nikaja kuwa mkuu wa majeshi lakini kuna changamoto moja kubwa sana ambayo nadhani nilikuwa naiona ya kawaida ila haijawahi kuwa ya kawaida ndiyo maana leo nikaamua kukupigia simu kuhitaji msaada wako kwa sababu ni mhimu sana kwa taifa letu, raisi wa nchi kwa sasa ni wewe hapo nakujua vizuri kabisa, IGP ni rafiki yangu tangu utotoni namjua vizuri sana, mkuu wa majeshi ni mimi hapa mwenyewe na ninajijua vizuri sana lakini ni muda mrefu sana tangu abadilishwe yule mzee ambaye alipotea pasipo kujulikana kwamba ameenda wapi sijawahi kabisa kumjua mkurugenzi wa usalama wa taifa wa nchi yangu, hili jambo naona linaenda kuwa ni tatizo kubwa sasa, wewe ni mheshimiwa raisi kwa sasa najua unajua kila kitu kuhusu hili hivyo nakuomba sana nikutanishe na mtu huyo au uniambie kwamba ni nani kwa sababu kuna muda huwa tunahitaji msaada pia hususani mambo ya upelelezi pamoja na mawasiliano lakini huwa tunashindwa kwa sababu hatujui hata wa kumfuata ni nani, mimi ni kiongozi mkubwa tena wa usalama nastahili kuwajua wenzangu wote nadhani hiyo ni namna sawa kabisa ya kuifanya nchi yetu kuwa vizuri naomba sana unisaidie bosi wangu” kilichokuwa kimemleta mheshimiwa mkuu wa majeshi ilikuwa ni kuhitaji kumjua mkurugenzi wa usalama wa taifa baada ya siku ile kuongea na rafiki yake Lusubilo Mtindika ambaye yeye ndiye alimjibu kwamba hata yeye hajui chochote kile leo alikuwa anategemea kupata jibu kutoka kwa mheshimiwa ambalo lingemsaidia kumjua kiongozi huyo wa moja ya taasisi kubwa sana nchini.

Mheshimuwa Ernesto Steven kama alivyokuwa ametambulisha alimsikiliza mwanaume mwenzake huyo ambaye alikuwa chini yake kimadaraka, hakuwa na haraka kabisa juu ya meza ambayo walikuwa wamekaa kulikuwa na sehemu ya kupikia hapo kulikuwa na birika ambalo lilikuwa na chai ndani yake ikiendelea kuchemka kidogo kidogo, alimimina kwenye vikombe viwili kimoja alikishika na kimoja akamsukumizia mtu huyo, alipiga mafunda mawili na kuyafumba macho yake ilionyesha kwamba chai ilikuwa ni ya moto sana, alipitisha kitambaa mdomoni na kujifuta kisha akayainua macho yake na kumuangalia mkuu wa majeshi kwa umakini sana ambaye hakuwa hata amegusa kikombe cha kahawa hiyo.
“Unahisi kwanini umeona kwa sasa ndiyo muda bora zaidi wa wewe kulijua hilo?” alimuuliza akiwa amemkazia macho
“Huko nyuma aliyekuwa anatawala kwangu hakuwa ni raisi tu bali alikuwa ni ndugu yangu na kama familia yangu, tuliishi kwa uwazi sana wote wanne hivyo sikutaka kumuuliza sana licha ya kumuuliza mara kadhaa na jibu lake halikuwa la kuridhisha sana, lengo la kuto mlazimisha sana kuniambia ni kwa sababu nilijua yule muda wowote angekuja kuniambia kama angekuwa tayari lakini kwa bahati mbaya sana wamekufa nikiwa hata sijapata neno lolote kutoka kwake kuhusu hilo jambo na kwa mambo ambayo yametokea tunatakiwa kufanya uchunguzi mkali na huo uchunguzi unatakiwa kuanzia kwenye hiyo taasisi kwa sababu ndio wanao husika na mheshimiwa raisi na usalama wake kuanzia Ikulu mpaka anako elekea” alijibu kiume naye akiwa amekaza sana sura yake, alihitaji sana kuweza kuujua huo ukweli ambao alihisi ana haki kabisa ya kuujua lakini ni kama alikuwa anafichwa mno.
“Mimi sina jibu lolote la kukupatia na leo wala sitahangaika sana kukuhoji kuhusu suala la wewe kunifuatilia sana maisha yangu kiasi hicho, kama ni kunikubali kikazi nadhani kuna watu wengi sana ambao wamefanya makubwa kwenye hii nchi nadhani ungeanza nao hao hivyo tafuta sababu nzuri ya kunipatia kwanini umenichimbua mimi na baadhi ya taarifa ambazo hata mwana historia wa nchi na Ikulu hana. Kama unahitaji kumjua mtu huyo mtafute IGP kama atakuwa anajua basi atakwambia ila kama hajui basi itakuwa ndiyo mwisho wa kukujibu hili swali, IGP ndiye mtu ambaye anapaswa kukujibu kwa sababu umesema nyie ni zaidi ya marafiki mmefikia hatua ya kuwa familia sasa mimi siwezi kuingilia kwenye mambo ya familia yenu kamalizaneni wenyewe” mzee huyo aliongea kama masiara ila ndivyo alikuwa amemaliza na kunyanyuka hapo ili aondoke hiyo hali hata mkuu wa majeshi ilimshtua mno.

“Mkuu samahani sijakuelewa”
“Kipi ambacho hujakielewa hapo kwenye lugha rahisi sana namna hiyo?”
“Una maanisha nini kusema nimfuate IGP? Kwa sababu nina uhakika yule hajui lolote lile wala chochote kuhusu hili jambo?”
“Mhhhh wewe hapo una uhakika gani kwamba hajui lolote? Wanadamu mnakufa kwa kukosa akili yaani nafsi ya mtu mwingine wewe ndiye ambaye unaithibitishia? Naenda kulala mchana nina mikutano ambayo inabidi niishughulikie nikutakie siku njema na usije ukanipigia simu tena kuniambia jambo la kipuuzi kama hili mida kama hii” mheshimiwa huyo aliongea na kuondoka Kwenda kulala kama alivyokuwa amekusudia lakini hayo yote hata hayakuingia kabisa kwenye kichwa cha mkuu wa majeshi yeye alichokuwa anakiwaza mpaka muda huo kwake lilikuwa ni swali kwamba ni kivipi aambiwe akamuulize IGP ambaye juzi yake tu hapo alimwambia hajui lolote?

Dunia ni kama ilikuwa inamdanganya sana, alinyanyuka hapo na kujifuta jasho kwenye uso wake, alitoka ndani kuelekea kwenye gari sura yake ikiwa imejikunja sana kwa hasira, safari yake alihitaji Kwenda kwa IGP muda huo ili akamwambie kwanini anamjua mkurugenzi wa usalama wa taifa na anamficha? Aliapa rafiki yake huyo ilikuwa ni lazima akauseme ukweli iwe ni kwa nguvu au kwa kutaka ikiwa ni pamoja na kuitoa sababu ya kwanini aliamua kumficha kuhusu hilo jambo.

Ni kweli IGP anamjua huyo mtu? Ni kweli atamtajia huyo mtu? Na kama ikitokea kweli anamjua ipi sababu ya kumficha huyo mtu?..33 inafika mwisho tukutane ndani ya sehemu inayo fuata.

Wasalaam

Bux the storyteller.
FB_IMG_1685786432842.jpg
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 34

SONGA NAYO............
“Huko mbweni ni baridi sana hauhitaji hata feni”, ni moja ya mistari maarufu sana ambayo watu wengi hupenda kuitaja pale wanapokuwa wanaitaja Mbweni, huko ndiko kulikuwa nyumbani kwa Lusubilo Mtindiga, familia yake yote ilikuwa ikiishi huko na huko ndiko kulikuwa nyumbani kwake ambako mara nyingi asipokuwa na majukumu ya kazi alikuwa akipatikana, Jaiwelo Mkupi Makubilo alihitaji Kwenda huko baada ya kutoka Ikulu ili akakutane na rafiki yake ambaye walikuwa wanaitana ndugu wa damu ili akamueleze ni mambo yapi ambapo alionekana kuyajua na akaamua kuyakumbatia kwenye kifua chake bila kuweza kumshirikisha mwenzake huyo, hilo jambo lilimfanya aghafilike sana kwenye moyo wake alihisi mwenzake huyo huenda kuna mambo mengi sana ambayo huwa anamficha na hataki yeye aweze kuyajua kabisa kwenye maisha yake. Baada ya kutoka nje ya Ikulu alipanda kwenye gari na kumtaka dereva wake huyo aondoke haraka sana maeneo hayo, cha ajabu baada ya kufika nje tu alimwambia dereva huyo ashuke kwenye gari na aende kwake siku hiyo alitaka kuendesha mwenyewe lilikuwa ni jambo la hatari sana kumuacha kiongozi wa ngazi ya juu kabisa ya jeshi kufanya jambo la hatari kama hilo kwenye maisha yake lakini hakuwa na namna baada ya kuambiwa kwa ukali sana ikamlazimu kushuka akiwa anasikitika huku akiwa anamuaga bosi wake huyo kwa macho na kwa aina ya spidi ambayo aliondoka nayo pale.

Lusubilo Mtindiga alikuwa kwenye chumba chake cha mazoezi ndani ya chumba chake ambacho kilijengwa kwa vioo tu na kumfanya mtu ambaye angekuwa nje kama kusingefunikwa kitu chochote basi angeshuhudia kila ambacho mtu wa ndani ya chumba hicho angekuwa anakifanya na alikuwa akifanya hivyo makusudi kwa miaka mingi sana, chumba hicho kilikuwa ndani ya uzio mkubwa wa fensi ndefu ambayo pia ilikuwa na ulinzi mkali sana. Akiwa ndani ya chumba hicho alikuwa ameshika Upanga kwenye mkono wake na nguo nyepesi zikiwa kwenye mwili wake, alipenda sana kufanya mazoezi na upanga tangu akiwa kijana mpaka uzee ulikuwa unamnyemelea na kwa mbali kabisa juu ya ghorofa ya pili alikuwa amesimama mwanamama ambaye umri wake ulikuwa umemtupa mkono kiasi uzee ulikuwa unamuita kwa kasi sana, alikuwa kwenye tabasamu pana sana kumuona mwanaume huyo akiwa anafanya mazoezi hapo ni zoezi ambalo amelishuhudia kwa idadi ya miaka mingi sana mpaka leo kila mwanaume huyo alipokuwan anaenda kufanya mazoezi basi ilikuwa ni lazima aache chumba hicho wazi bila kufunika mapazia makubwa ambayo yalikuwa yamewekwa kwa ndani ili kumuwezesha mwanamke huyo kuweza kuona kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani.

Akiwa anaendelea kufanya hayo mazoezi ambayo alikuwa anaishia kujisonya mwenyewe kwa sababu kuna vitu alikuwa anatamani kuvifanya ila mwili ulikuwa unakataa kutokana na mifupa kukomaa kupitiliza kulingana na umri Kwenda sana hivyo kuna vitu vilikuwa vinamkera hali hiyo inapo mtokea ila hakuwa na namna, alisikia mlio wa honi ambao ulikuwa unapigwa kwa fujo sana, alisikitika wala hakuhangaika kugeuka kuangalia getini. Geti lilifunguliwa na mtu huyo akaingiza gari lake ndani hata hakukumbuka kulizima alishuka kwa haraka mno akiwa mwingi wa hasira kwenye uso wake, walinzi waliokuwa hapo walikuwa wanampa heshima yake kwa sababu alikuwa ni kiongozi mkubwa mno ndani ya nchi hata hivyo hakujibu salamu ya mtu yeyote yule safari yake ilienda kuishia ndani ya chumba ambacho alikuwa anafanya mazoezi ndugu yake.

“Sijui lini utaacha kuwa kwenye hali kama hiyo kiongozi mkubwa kama wewe haupaswi kuwa namna hiyo utajikuta umefanya maamuzi ya hovyo sana ambayo yanaweza kuleta maafa makubwa kwa vijana wako na kwa taifa pia” IGP aliongea baada ya kumuona mwenzake kaingia kwa hasira sana huku akimrushia upanga ambao ulikuwa umewekwa kwenye ala yake ukutani na mwanaume huyo aliudaka akiwa kwenye suti yake safi.

“Ungekuwa unajali kuhusu hilo usingekuwa mtu wa kuanza kunizunguka mimi” aliongea kwa hasira akiwa anamfuata rafiki yake huyo kwa kasi, mkewe na IGP baada ya kuona shemeji yake kaja hakuendelea kukaa pale alitoka na kuwaacha wanaume hao wapigane, ni mara nyingi huwa inakuwa hivyo pale wanapokutana kwenye mazingira kama yale na yeye huwa hapendi kabisa kushuhudia watu hao wakiwa wanacheza na maisha yao kimasiara sana namna hiyo wakiwa na mapanga ya kweli kwenye mikono yao. IGP alikwepa upanga kwa kujigeuza haraka na kutua nyuma alisogea kwa kasi sana na kumfikia mkuu wa majeshi ambaye aliinama kidogo upanga ukapita juu kidogo ya kichwa chake na kupukutisha nywele kadhaa kichwani.

“Kipi hicho ambacho unasema nakuzunguka ndugu yangu? mbona mimi nawewe hatujawahi kuzungukana kwa lolote” IGP alijibu huku akiuingiza upanga wake kwenye ala yake kwani mwenzake huyo aliutupa chini kwa hasira alizokuwa nazo hakuhitaji waendelee kupigana tena kwa sababu sicho kilichokuwa kimemleta siku hiyo na nje kulikuwa kumepambazuka kabisa na wasakatonge walikuwa wanaendelea na mambo yao kama ilivyokuwa kawaida ya siku zote.

“Nina swali ambalo ni dogo na ni fupi sana ila ni la mhimu sana tena sana nadhani huwa unanielewa ninapokuwa ninaweka msisitizo kwenye mambo yangu”
“Ok uliza unachotaka kukisema”
“Naomba uniambie mkurugenzi wa usalama wa taifa ni nani na kwanini mmeamua kunificha kuhusu hili swala?” baada ya kuongea IGP alimtazama mwenzake huyo bila wasiwasi
“Unamaanisha nini kusema hivyo?”
“MD usitake kupoteza muda kwa jambo ambalo linaeleweka hivi ninavyo ongea nawewe nimetoka kwa mkuu wa nchi nimembana sana aniambie kwanini mtu wa mhimu kama mimi kwenye taifa nafichwa mambo nyeti kama haya halafu rafiki zangu wamekufa? Mimi natakiwa kushirikiana na hao usalama wa taifa kuhakikisha mhusika anakamatwa halafu nafichwa nawewe hapo unajua kila kitu na bado unanikalia kimya kabisa kana kwamba hujui lolote hebu nambie ni hilo tu mimi nitaondoka” kwa maelezo ambayo aliyatoa IGP hakuona sehemu ya kukwepea, alimuongoza mtu huyo wakatoka hapo na Kwenda nje kwenye bustani sehemu ambayo ilikuwa imejengwa kwa ajili ya kupumzika, kulikuwa na meza ndogo ambayo juu yake kulikuwa na vitabu walikaa hapo haukupita muda mke wa IGP aliwaletea kahawa na kumsalimia shemeji yake huyo kisha akawapisha wanaume wayajenge huku wakiendelea kushushia kahawa kuyapasha matumbo yao.

“Ndiyo hicho tu basi unachotaka kukijua?”
“Yes, ni hicho ila ndani yake kina mambo mawili kwanza nahitaji kujua hizi taarifa unazo tangu lini lakini pia nahitaji kujua kwamba kwanini hizi taarifa zinalindwa kwa siri sana namna hii?” aliongea huku akiwa anaiweka suti yake vizuri na kunyanyua kikombe cha kahawa, alipiga mafunda matatu na kutulia ulikuwa ni muda mwafaka wa kumjua mkuu wa idara ya usalama wa taifa

“Jason Markvelous Japhary” IGP alitamka kwa msisitizo sana macho yake yakiwa makavu lakini mwenzake ni kama aliona mwenzake anafanya mzaha kwenye mambo ambayo yalikuwa yanahitaji taarifa zinazo eleweka
“Hahahahahah hahahah hahah, sasa ndugu yangu naona nawewe umeanza kuwa na ugonjwa wa akili, mimi nimekuuliza kuhusu mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa sijakuuliza mdogo wa ndugu yetu Mark hahahhah sasa huyu mtoto anaingiaje kwenye hizi maada za kikubwa? Ebu nijibu nilicho kuuliza niwahi mahali leo binti yangu anafika nataka niwepo nyumbani atakapokuwa anafika atajisikia vibaya sana kama asipo nikuta au nikichelewa kukutana naye kwa muda ambao atakuwepo hapa Tanzania” mheshimiwa alicheka sana huku akikinyanyua kikombe chake cha kahawa tena akiwa ameweka miguu nne kabisa hakuwa na shaka leo alikuwa analipata jibu lake ambalo lilikuwa linamchanganya sana akili.

“Huyo ndiye mkurugenzi wa usalama wa tai………” IGP hakumalizia kauli yake CDF mkono wake ulikuwa ukitetemeka sana baada ya kuisikia hiyo kauli kutoka kwenye mdomo wa ndugu yake kabla hata hajamaliza kikombe hicho kilimponyoka kwenye mkono wake na kahawa hiyo yote iliishia kwenye mapaja yake, hata hakushtuka alibaki ameganda mdomo ukiwa wazi licha ya kahawa hiyo kuwa ya moto sana, kikombe kilijipigiza chini na kupasuka hiyo hali ilimshtua mpaka mke wa IGP alitaka kuja lile eneo kufanya usafi lakini IGP alimzuai kwa mbali kwa mkono hayo mazungumzo walitakiwa kuyamaliza wenyewe hawa ndugu wawili, usoni kwake IGP alikuwa yupo siriasi sana kuliko anavyokuwa siku zote mdomo wa CDF ulikuwa ukitetemeka na kucheza cheza akiwa kama vile anasimuliwa hadithi za nchi zinazo dhaniwa kwamba zitatokea lakini hazitokei.

“You must be kidding MD! (utakuwa unatania MD)” aliongea kwa shida mdomo wake ukiwa unatetemeka sana
“Hilo ndilo jibu sahihi la swali ambalo wewe umeniuliza” IGP uso wake haukuwa na masihara hata kidogo wakati anamjibu rafiki yake
“Hapana yule mtoto aaaaaagr Hapana Hapana, yule amekua mimi namuona mpaka anapelekwa huko nje kusoma, kwanza ni mdogo yule hiyo nafasi kaipataje pataje na kaipatia wapi? Hapana Hapana naomba uniambie kwamba ulikuwa unanitani” mheshimiwa huyo bado nafsi yake ilikuwa inagoma kabisa kuamini kile ambacho mwenzake alikuwa akimwelekeza hapo hakuhitaji kuziamini hizo habari kwamba eti zilikuwa ni za kweli kivipi yani? Nafsi iligoma kabisa.

“Nakujibu swali la pili na la tatu, ni kwamba hizo taarifa namimi nimezipata usiku huu lakini pia sijui kwanini hizi taarifa zilikuwa zinafichwa sana namna hii nadhani mhusika mwenyewe anaweza kuwa na majibu sahihi zaidi” IGP alikuwa anaongea kiwepesi mno kiasi kwamba mpaka mwenzake huyo alibaki anamshangaa tu, CDF aliingiza mkono kwenye mfuko wa mbele koti lake la suti alitoa tablet ndogo na kuingia kwenye mtandao. Aliandika jina la Jason zilikuja taarifa zile zile ambazo yeye alisimuliwa na mwana historia wa Ikulu alitabasamu lakini kwa hasira mno.

“MD who is this kid? Na imekuwaje mpaka akapewa nafasi kama hiyo mtoto laini sana namna hii? Hakuna watu kwenye nchi yetu mpaka mtoto kama yule ndiye anapewa nafasi kubwa sana namna hii? How mbona mnataka kuichanganya sana akili yangu namna hii” aliongea kwa jazba sana huku akili yake ikiwa inapingana yenyewe kuna sehemu ya akili yake ilikuwa kama inataka kukubali hilo jambo lakini sehemu nyingine ilikuwa inagoma.

“Wewe hapo ndo unamuita yule bwana mdogo ni laini laini?” IGP aliuliza kistaarabu huku akipata kahawa yake na kutulia
“Sio mara ya kwanza unaonyesha viashiria vya kumuogopa huyo bwana mdogo ebu naomba nijibu maswali yangu niliyo kuuliza hapo juu kabla hujatoa hilo neno” aliongea akiwa anajifuta futa ile kahawa ambayo ilimdondokea kwenye mapaja yake.

“Ulitakiwa kwanza kujiuliza kwanini kijana mdogo kama yule alikuwa anajiamini sana kuja mpaka nyumbani kwako muda kama ule na kuongea na wewe kijasiri sana namna ile, huyo ambaye wewe unamuita mlaini sana sidhani kama umewahi hata kuona namna anavyofanya mauaji nafikiri ungekuwa haumtaji taji kiwepesi sana namna hii, yule ndiye mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa ila hata hao majasusi wenyewe na vijana wote ndani ya idara hawamjui na kuna sababu za msingi za yeye kuto julikana. Yule ni mtu wa kutisha kuliko hata neno lenyewe linavyo tamkwa na ni mtu ambaye huwa haongei mara mbili kwenye maisha yake anapokuwa huko kwenye ulimwengu wake ndiyo maana huwa unamuona hapendi kubishana kabisa huwa anaamua kukaa kimya kwenye mambo mengi sana na hiyo ndiyo silaha yake kubwa anayo itumiaa kuuhadaa ulimwengu wa watu wasio mjua na kuwaaminisha kwamba yeye ni dhaifu na ni laini sana”

“Uhatari wake ni upi huo ambao wewe unauzungumzia?”
“Mbali na kuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa yule ni kiongozi wa kundi moja la hatari sana linalo itwa “Five poisoned serial killers (Wauaji watano waliotiwa sumu mfululizo)” wote ni vijana wadogo sana na inasemekana hili ndilo kundi la hatari zaidi kuwahi kutokea kwenye historia nzima ya taifa hili, wanapopewa amri na kiongozi wao kwamba lifanyike jambo fulani hata wakiwa wawili tu basi hiyo sehemu inageuka kuwa kama uwanja wa mauaji kwa jinsi walivyo, ubaya wa hawa vijana hawajulikani na mtu yeyote yule zaidi yake yeye mwenyewe Jason na hata ambao wanajua siri zake baadhi hawawajui vijana hawa hata mmoja ila kwa mimi namjua mmoja tu pekee kati yao. Kumjua ninako maanisha mimi sio kwamba nimewahi kumuona au nalijua hata jina lake la kuzaliwa hapana ila nimewahi kusikia kwamba anafanyia kazi kwenye moja ya vyuo bora sana kwenye nchi hii, kinatumia maandishi matatu tu NIT kikiwa ni kifupisho cha National Institute of Transpot, hiki ndicho chuo pekee cha usafirishaji kinachotegemewa Afrika ya mashariki na kati lakini pia kwa Afrika inasemekana vipo viwili tu basi, ni chuo kidogo kwa mwonekano ila kina sifa kubwa sana ndani yake na kinatajwa kuwa miongoni mwa vyuo bora zaidi ambavyo vinaenda kuokoa tatizo la elimu na usafirishaji kwenye bara ya Afrika kwa miaka kumi ijayo. Sasa ndani ya hicho chuo ndiko aliko mmoja wa hawa vijana watano tena nasikia ni mlinzi wa kawaida sana unaweza kumuita mgambo tu ambaye kaajiriwa na mshahara wake wa laki mbili kwa mwezi una…….” IGP alitaka kuendelea lakini alikatishwa na ndugu yake huyo.

“Haya mambo unayo niambia hapa ni mambo ambayo yapo kwenye hii nchi au umetunga hadithi zako za kwenye movie ili ionekane kwamba umenijibu nilicho kuuliza?” CDF alikuwa anapewa mambo ya ajabu ambayo hata yeye kama mkuu wa majeshi hakuwahi kuyafikiria wala kukutana nayo sasa alishangaa mwenzake huyo alikuwa anayatoa wapi mambo ya kutisha sana namna hiyo alibaki ameduwaa.

Huo ndio ulimwengu wa watu wenye mabavu, unadhani eti inawezekana kweli huyu huyu Jason ambaye tumemsoma ndiye mkurugenzi wa usalama wa taifa? Eti ndiye mtu wa kutisha sana tena anamiliki kundi la hatari sana namna hii na hilo kundi ni la nini? Mimi bado siamini kama kuna ukweli kutoka kwenye mdomo wa IGP niseme tu sehemu ijayo huenda ikatufungua kidogo.

Wasalaam
Bux the storyteller.
FB_IMG_1685786432842.jpg
 
Back
Top Bottom