Intelligensia juu ya Mabomu ya Arusha

Kwa mtazamao wangu,hii ni vita ya kibiashara sisi na jirani yetu,kwanini kila mara iwe na Arusha au Znz?baada ya wao kuboronga Mombasa na Nairobi sasa wanataka kuwaaminisha wageni kuwa hata Tz siyo salama.

TISS watizame nje ya siasa na dini

Tha's is the bulldog institution let's put it out of the equation
 

Wakenya washindwe kwao waweze tz? Basi adui wa Tz na kenya ni mmoja. kwa sababu, kenya wanashambuliwa na alshababu ili wayatoe majeshi yao Somalia. Lakini nani alianza kumshambulia mwenzake? Ni alshababu ndipo kenya ikapeleka majeshi somalia kuwasaka alshababu.

Aidha, ni nchi nyingi zenye vikosi vyao huko somalia.mfano,Djibout, Ethiopia, Uganda na Burundi mbona huko kwao hakuna harakati za alshababu? Kama hoja itakuwa ni ufikivu, Ethiopia pia imeunga mpaka na Somalia.

Kama ni ushindani wa kibiashara, Kenya yawapasa washindane si kwenye utalii pekee bali na kwenye gesi, mafuta, ukubwa wa ardhi ya tz, jina la tz kujiuza lenyewe. Hulka ya watz kupenda na kuenzi amani.Jeshi la tz limetukuka duniani(syschelis,Comoro,Mozambique,Uganda,DRC,Darfur,Lebanon)

Milipuko ya tz CCM wanaijua vilivyo chanzo,sababu na mikakati yake. Viweje polisi watumie masaa 24 kuwanasa wauaji wa faru jacq; watumie masaa 24 kuwakamata wauaji wa mama wa kichina; watumie wiki kuwatia mbaroni wauaji na waporaji kituo cha polisi kimanzichana LAKINI polisi hao hao tena wakishirikisha FBI washindwe kuwakamata wauaji wa padri, walipua mabomu Soweto?...!!!
 
Yote yanawezekana na sidhani kama dawa yake ipo karibu.

Ila mabomu ya tz hayawafaidishi majirani tu.
 
Bila kubaini wahalifu, bila kuachana na kauli za kisiasa na tusipotegemea taaluma katika kukabiliana na uhalifu huu, hali itazidi kuwa mbaya tena na tena.
 
That has to be the most pointless per thoughts pored into it because no matter how hard you think, and no matter how hard you try to convince people, and no matter how passionately you believe
Kaka uko sahihi tena sana. Kwani hujaona mtu anasoma sana, halafu kwenye mtihani anafikiri sana. Majibu yakitoka ameambulia 5 ya 100. Sasa imagine asingesoma na kufikiri sana angepata nn. Sijaona thread ya hovyo humu jf kama ya huyo jamaa
 

Mkuu Tety, Rais wetu Dr.Dr. Dr. Dhaifu katika kuhakikisha polisi wa Tz. wasiolipwa vizuri, wanailinda ccm kwa nguvu zote. Amechilia Karibu kila polisi wa Tz. ajipandishie mshahara wake kwa kutwa kucha, kuwatafutia raia makosa ya kuwadai rushwa. Kwa sasa hakuna polisi anayefanya kazi kwa weledi bali wanafanya kazi kiccm, ccm. Acha mabom yaendelee kutularua pengine yatatuamsha waTz. kadia tuwe na jeshi la polisi linalofanya kazi kwa weredi.
 
Tusimlaumu mleta mada amefikiria na akataka tuyaangalie maoni yake. Tunachoilaumu serikali ni ukimya wake kuhusu mabomu haya pamoja na mambo mengine mazito mazito ambayo tulitegemea akiwa kama amiri jeshi mkuu angetujuza iwe kwenye hotuba za mwisho wa mwezi au kwa kuzungumza na wazee wa Dar. Lakini tunapoona kimya na mabomu yanaendelea tunakuwa na mashaka na uongozi wa huyu mkuu wa nchi au mpaka asikie ndugu au rafiki yake wa karibu ameuawa na haya mabomu? Hao TISS wanafanya nini kama wanafanya kazi kisirisiri basi matatizo yasingeendelea! Hii serikali kwa kweli inakifu kwa sababu wao na upinzani tuu; basi turudi kwenye serikali ya chama kimoja!
 
Kwa mtazamao wangu,hii ni vita ya kibiashara sisi na jirani yetu,kwanini kila mara iwe na Arusha au Znz?baada ya wao kuboronga Mombasa na Nairobi sasa wanataka kuwaaminisha wageni kuwa hata Tz siyo salama.

TISS watizame nje ya siasa na dini

Mkuu umenena , mimi pia nauliza why Arusha and Zanzibar only ? Kisa ni utalii ili watalii watakapokuja wakute hali ni tete maeneo yote ya kibiashara east africa . Then watafikiria kusitisha kuja Tanzania na kusuburi hali itengemae na kurudia destination yao ya kawaida KENYA. Vinginevyo hali ya usalama ikiwa nzuri kwa maeneo ya Tanzania watalii wataanza kupita na kusahau kenya. Ambapo itakuwa pigo kwao.
 
Mkuu sijataja Kenya kwenye comment yangu!.
Wakenya walilipua uzinduzi wa Kanisa Katoliki ili wapate manufaa gani ktk eneo ambalo moja ya Wageni walio kuwa wamehudhuria ni Viongozi wa Kanisa toka Kenya??
 
Suala la milipuko ya mabomu Tanzania hasa Arusha na Zanzibar, kuna 0.87 probability wameungana Serikali ya Rwanda na Kenya, na Uganda ikiwezekana Uganda imeshirikishwa, 0.13 tunawaachia vyombo vya usalama vifanye kazi yake na kupata majibu.
0.87 uhalisia wake ni huu
Kama ilivyoelezwa na vyombo vya usalama na bahadhi ya wadau kuwa aina ya mabomu yanayotumika katika matukio haya yanafanana. Hii inadhihilisha kuwa ni kikundi kimoja au muunganiko wa makundi tofauti yanayoshirikiana.

Mosi Rwanda(Paul Kagame), kwa suala la M23 ambao wanaaminika kuwa ni wanyarwanda (Nyuma ya Kagame). ‘
Paul Kagame ana tabia ya kujihami mapema sana pale anapokuwa amefanya tukio baya au anapotarajia kufanya. Tukumbuke kuwa mara tu baada ya M23 kuanza harakati zake kagame alikanusha vikali kuhusika kwake huku jumuiya ya kimataifa(UN) na wengine wakithibitisha kuhusika kwa kagame juu ya M23, Siku chache zilizopita Kagame alieleza kupitia vyombo vya habari kuwa “……Tanzania na Rwanda ni ndugu na haina haja ya kuwatenga ndugu hawa………” huku kesho yake akijua kuwa anakutana katika kikao cha northen corridor kilichofanyika Kigali ambapo walikutana Kagame, Kenyatta, Museven na raisi wa Sudan kusini. Kulikuwa na ulazima gani wa kutamka maneno hayo kama si kujihami kabla ya tukio lililotarajiwa kufanyika siku inayofuata.
Pili, Kenya(Kenyatta)
Serikali ya kenya baada ya bandari zao kudorola pamoja na vita ya Utalii kuhusu wageni wanaokuja Arusha kwa ajili ya mbuga zilizo karibu, Kama tunavyofahamu Mlima kilimanjaro upo TZ lakini watalii wengi wakigeni huja kuona mlima huo wakipitia Kenya tusisahau hata ndege za kenya sasa zinaandikwa mount kilimanjaro kwa wao kujitangaza zaidi. Inawezekana ni vita ya mapato ya utalii kuweka milipuko ya mabomu wakilenga kuwafanya watalii waogope kuja Tanzania. Kwa nini milipuko iwe tu Arusha na Zanzibar isiwe Ukerewe, Mbeya ama Nanyumbu? Lah asha kuna kitu nyuma ya pazia.
Uganda(Museveni),
Inawezekana anashirikishwa kutokana na ukaribu mkubwa wa yeye na Kagame, hata M23 ambao kagame anahusishwa nao, baada ya kushindwa na majeshi ya UN(Tanzania ikiwemo) waasi wa M23 wanadaiwa kukimbilia Uganda, Je srikali ya Uganda haijui, hii inadhihirisha wazi ukaribu wake na Kagame.

Suala la kujiuliza kuna ajenda gani ya siri inayowafanya Kagame, Kenyatta na Museveni kukutana mara kwa mara na kutoihusisha Tanzania kwenye vikao hivyo? Tusisahau pia kauli ya Kagame aliyowahi kuitoa kuwa Akipewa Tanzania kuiongoza bandari pekee inatosha kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tajiri, Je ni wivu wa kiuchumi wanaotaka kufanya ili kuwaaminisha wafanyabiashara wa nje na ndani ya Afrika kuwa Tanzania si mahali salama?
“Watanzania tunaipenda nchi yetu wala hatuhitaji uhasama na nchi yoyote, tunapenda tuendelee kuwa na amani hatuhitaji mabomu, watuachie Tanzania yetu na watanzania tutakuwa wa mwisho kuikana nchi yetu”
 
Nakuunga mkono.

Yanayotokea Arusha ni Vita ya Utalii.

Kenya wameamua tukose wote.
 
Nakuunga mkono.

Yanayotokea Arusha ni Vita ya Utalii.

Kenya wameamua tukose wote.

Wa Tgk kwa visingizio.

Ilipokuwa inatokea kule Znz mlisema UAMSHO. Je huko Arusha mnarudikusingizia wakenya.

Poleni sana msitafute mchawi wachawi ni nyie wenyewe
.
 
Kwa mtazamao wangu,hii ni vita ya kibiashara sisi na jirani yetu,kwanini kila mara iwe na Arusha au Znz?baada ya wao kuboronga Mombasa na Nairobi sasa wanataka kuwaaminisha wageni kuwa hata Tz siyo salama.

TISS watizame nje ya siasa na dini

Upeo duni kabisa na fikra hafifu......hivi unaposema kenya wanahusika na mabomu unamaanisha kenya kama kenya nchi ndio imeleta watu kulipua mabomu. Au unamaanisha wakenya yaani wafanyabiashara binafsi wameamua kupiga mabomu? ............hebu jaribu kufikiria zaidi hivi serikali ya kenya inaweza kutuma mtu au kutuma usalama wao kurusha vibomu na bodaboda......wa tz tuache kujitia aibu na mawazo duni
 
Wa Tgk kwa visingizio.

Ilipokuwa inatokea kule Znz mlisema UAMSHO. Je huko Arusha mnarudikusingizia wakenya.

Poleni sana msitafute mchawi wachawi ni nyie wenyewe
.
mkuu hata pale Arusha kwenye mkutano wa chadema Lukuvi aliitangazia dunia kuwa wapinzani wamejiripua ili kupata huruma ya wana nchi hivyo hiyo tume huru wanayoitaka iundwe kuchunguza haitahundwa, jamani milipuko na tindikali ni miradi ya ccm, kitulacho kipo nguoni mwetu kabla hatujatoka nje tujiangalie kwanza.
 
Nina hofu kuwa mabomu ya Arusha na Zanzibar yana harufu ya kubalance biashara ya utalii na Kenya baada ya al-shabab kuiandama biashara ya utalii Kenya kwa mabomu na mauaji. Juzi nilimsikia mtangazaji wa BBC raia wa Kenya kipindi cha focus on Africa akihanikiza uhusiano wa mabomu ya Arusha ya juzi na Serengeti na utalii. Hebu tuungane tuelekeze pua, masikio na macho yetu kuelekea mpaka na Kenya na watu wake tunaweza kutagundua kitu.
 
Mkuu sijataja Kenya kwenye comment yangu!.

Mkuu wangu sawa hukusema ni Kenya,umesema ni majirani. Majirani wanapata faida gani kulipua mkutano wa CDM na Kanisa?

Ukiondoa bomu la Soweto haya mengine ni ya kienyeji kwa maana yametengenezwa majumbani kwa teknolojia duni. Ni kazi ya Majirani?

Bomu limelipuka Mwanza ktk Kanisa la KKKT na huko walikua Majirani? Watanzania tuache visingizio vya kijinga,haya mabomu ni kazi yetu wenyewe!
 

Unashindwa kuelewe kitu gani kujua mahusiano ya Arusha na Vivutio vya Utalii kama Serengeti,Ngorongoro,Kilimanjaro,nk? Hii elimu duni inasababisha watu wavivu kufikiri.
 

Nadhani upo ktk makambi ya Wakimbizi ukichochea uhasama kati ya nchi yetu na majirani. Hivi unaelewa kwa mfano Arusha Night Park moja ya Wateja wao wakubwa ni Watanzania,Wakenya,Waganda,Warundi na Wanyarwanda wanaoitembelea Arusha kikazi,kibiashara na wale wanao fanya kazi Arusha ktk Taasisi za Kimataifa na Makampuni kama Mabenki nk? Sasa walipue eneo kama hilo ili kuua wananchi wao??
 
Wa Tgk kwa visingizio.

Ilipokuwa inatokea kule Znz mlisema UAMSHO. Je huko Arusha mnarudikusingizia wakenya.

Poleni sana msitafute mchawi wachawi ni nyie wenyewe
.

Mkuu nakubaliana nawe kwa asilimia 100 mchawi na wachawi ni sisi wenyewe. Chukulia mfano mzuri kabisa bomu la Soweto ambako mashuhuda waliowaona Polisi wakimwokoa mrushaji wa bomu na kumkimbiza. Leo wamesahau eti majirani! Akili na kumbukumbu za Nyumbu hizi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…