Intelligensia juu ya Mabomu ya Arusha

Intelligensia juu ya Mabomu ya Arusha

umewasilisha ugorou umetumwa udivert mada, mbona hutaki kumnyooshea kidole raisi wako jk alipokataaa kuunda tume ya kiuchunguzi ya kimahakama badada ya cdm kudai wanao ushahidi jinsi polisi na ccm walivyohusika na ulipuaji bomu pale soweto kwenye mkutano??

hakuna cha m23 wala Malawi ni ccm ndo mnajifanyia ugaidi kwa malengo ambayo ambayo kila mtu anayajua,

nyie ccm mnacho mnadhani kila mtanzania ni mjinga , watu wenu wa mikakati ya kisiasa wamefeli, yaani mnatumia mbinu za mwaka 1947
Let us think inside the box, outside the box and trash the box and think without a box as well.

Inside the box

CCM wamepanga njama ya kulipua bomu kwenye mkutano wa CHADEMA ili wananchi waogope kuhudhulia mikutano ya chadema. Tuhuma hizi zinakuzwa na maneno ya Mwigulu Nchemba ambaye katika mikutano yake alionya kwamba watakaohudhulia mikutano ya chadema watakufa pamoja.Pia vifo vilivyofanya na polisi kwenye mikutano ya CHADEMA huko morogoro na iringa pamoja na utekwaji na uteswaji wa Ulimboka na wengineo vinafanya watu wengi ikiwamo viongozi wa CHADEMA waamini kuwa CCM ilitumia polisi kufanya hujuma hizi.

LAKINI, kwanini yalipuliwe siku ambayo ni mwisho wa kampeni?Lengo lingekuwa ni kuwatisha wananchi wasihudhulie mikutano ya chadema basi bila shaka bomu lingelipuliwa mwanzoni kabisa mwa kampeni.

Outside the box

Kuna wengine wanaamini CHADEMA wamejilipua wenyewe ili kutafuta umaarufu na huruma ya wapiga kura pamoja na kuipaka matope serikali ya CCM pamoja na jeshi lake. Fikra hii inachukuliwa kwa uzitio kwani hata katibu mwenezi wa CCM Nape Mnauye katika tarifa yake kwa vyombo vya habari anatuaminisha hivyo.

LAKINI, kiongozi gani yupo tayari kumwaga damu kwani tunaambiwa bomu lililipuka jirani na jukwaa kuu na miongoni mwa waliokufa ni kiongozi wa CHADEMA. Isitoshe kulikuwa na mpango wa kutengeneza mlipuko mkubwa zaidi ambao ungeleta madhala zaidi kwani Tenki la mafuta la gari la matangazo lilikutwa limepigwa risasi kwa mategemeo lingelipuka.

Trash the box and think without the box

Mimi nafikiri kuna mtu/ kikundi cha tatu ambacho tunatakiwa tukiweke kwenye tafakari zetu wakati tunamtafuta mchawi katika hili. Kikundi hiki kinaweza kuwa ndani ya nchi ama hata nje ya nchi. Tujiulize je ndani ya nchi kuna kikundi kinapenda kuona CHADEMA na CCM kwenye malumbano? Je kuna kikundi ama mashirika ndani ya nchi hakipendi kuona watanzania tunaishi kwa amani? Je kuna Vikundi vya nje ama nchi za nje ambazo hazipendi kuona watanzania tunaishi kwa amani? Je kuna nchi ama vikundi tuna uhasama navyo?

Ndai ya nchi sina uhakika kama kuna kikundi ama chama cha siasa kisichopenda kuona CCM na CHADEMA wakilumbana ama kinachopenda tuingie kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe, labda TISS watakuwa wanajua. Kuhusu vikundi nchi za nje ambavyo vina uadui na Tanzania, nina uhakika na M23. Kikundi hiki cha wanamgambo wanaopigana Congo ambao inaaminika wanafadhiliwa na serikali za Rwanda na Uganda havijafurahishwa na hatua ya serikali ya Tanzania kupeleka majesi yake kwenda kulinda amani Congo. Sijui vikundi vingine nadhani TISS wana idadi ya ya vikundi tulio na uadui navyo.

Kuhusu nchi pia nina uhakika kwamba tuna uadui na Malawi kutokana na mgogoro wa mipaka kule ziwa nyasa. Pia nina uhakika tuna uhasama na Rwanda na Uganda kwakuwa tumeingilia Maslahi yao kwa kupeleka majeshi Congo. Sina uhakika na nchi nyingine ila nadhani TISS watakuwa wanajuia nchi ambazo tuna uhasama nao kwasababu ndio kazi yao , ingawa Kenya lazima tutakuwa na uhasama nao kwenye masuala ya kibiashara.

Kwanini natilia mashaka vikundi vya nje ya nchi ama nchi majirani zetu?

Kwasababu aina ya bomu lililolipuka katika kanisa la Joseph mfanyakazi Olasiti ni ile ile iliyolipuka katika mkutano wa kufunga kampeni wa CHADEMA. Ni bomu la kiwandani na limetengenezwa China. Mabomu haya ni kwaajili ya majeshi sio polisi. Ikumbukwe kipindi kile bomu lilipolipuka kanisani , kulikuwa na Tension kubwa sana kati waislam na wakristo. Motive ya mlipuaji ilikuwa ku spark vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya wakristo na waislam. Hii ilishindikana baada ya wakristo kuendelea kuonyesha uvumilivu pia ilikuja gundulika kwamba mtu aliyerusha bomu ni mkristo mwenzao. Nadhani dhamira ya kikundi ama nchi iliyotaka tuingie katika Mapambano ya wenyewe kwa wenyewe ili fail.

Wakati huu ambapo kulikuwa na Tension kubwa kati ya mahasimu wa siasa CCM na CHADEMA hapa Arusha tunaona hali hii inajirudia. Motive ni ile ile ya kutaka tuingie kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe, wakati huu katu ya wafuasi wa CHADEMA na CCM.
Viongozi wetu wanatakiwa wawe makini sana wanapotoamatamko yao kwani tukianza kuuana hakuna atakayepona. Kwamfano kakukuwa na haja ya Mh Lukuvi ama Nape kutoa matamko ya namna ile ama jeshi la polisi kuzuia wafuasi wa CHADEMA kufanya maombolezo ya wafuasi wao waliouawa katika mlipuko.

Halikadhalika hakukuwa na sababu ya viongozi wa CHADEMA kuwatuhumu polisi moja kwa moja kabla ya kuwa na uhakika wa kinachoendelea kwani wakati wa matukio kama ya uchaguzi polisi huwa wanaletwa toka kila kona ya Tanzania kwahiyo sio rahisi polisi walio katika scene kujuana, kitu kinachoweza kutoa mwanya kwa wahalifu ku camouflage kama police na kutekeleza adhma yao(kumbuka tunaambiwa polisi walimtorosha mrusha bomu je tuna uhakika ni polisi wetu, ama ni agents wa maadui zetu?).
NB; Rejea maneno ya rais wa Rwanda baada ya hizi kash kash aliposema Kikwete Kikwete anajidai kupatanisha nchi za wenzake wakati kwake kumshinda.

Pia bomu la kanisani lililipuka pindi tu askari wetu walipokuwa deployed kwenda rwanda;Rejea maneno ya M23 kwenye mitandao yao ;ikumbukwe kenyan hawafurahishwi na our mega development projects kama za ujenzi na upanuaji wa bandari zetu, na reli utajiri wa gas, ujenzi wa bomba na impact zake katika uchumi hapo baadae n.k.


Sina Chama

Naomba kuwasilisha.
 
Mikoa hii ndioyo inayoongoza kwa wahamiaji haramu, ukiwa Arusha wasomali wengi, wazungu uchwara wengi, wakenya wamasai wengi, wakenya wanojifanya watanzania hasa kutoka musoma silali, tukija zanzibar waarabu omani wengi ukizingatia wana koo zao huko uarabuni, wangazija kibao kwa hiyo mabomu hayaepukiki kutokana na jiografia.
 
Kwa comment yako hiyo ya mwisho umejivua nguo na kubaki uchi; huna chama, so what! Hii yako ni red herring kwani swala la nani walihusika liko wazi wala halina mjadala!
Hana chama....lakini anaongelea CHADEMA na CCM.

huyu yupo ndani ya tank wala sio ndani ya box.
 
Upeo duni kabisa na fikra hafifu......hivi unaposema kenya wanahusika na mabomu unamaanisha kenya kama kenya nchi ndio imeleta watu kulipua mabomu. Au unamaanisha wakenya yaani wafanyabiashara binafsi wameamua kupiga mabomu? ............hebu jaribu kufikiria zaidi hivi serikali ya kenya inaweza kutuma mtu au kutuma usalama wao kurusha vibomu na bodaboda......wa tz tuache kujitia aibu na mawazo duni

kwani kufanya recruitment ni kazi ngumu?anaefundishwa atapewa sababu nyingine ila wao wana other motives,usiwe mvivu kufikiria na kurusha critics bila kutoa maoni yako, idiot!
 
Mbona wakati anazungumzia mauaji ya mpeketoni na Nairobi hakutaja habari za masaimara, utalii na huduma za bandari kuwa na uwezekano wa kuathiriwa na mabomu? kwanini iwe serengeti na mabomu? kuwa paranoid ni muhimu maishani kwa usalama wa mtu na mali zake. Nahisi wewe ni Mkenya

Una kichwa kigumu kuelewa hata issues ndogo ndogo unakimbilia kunipachika uKenya! Mpeketoni ipo Pwani ya Kenya. Ilipolipuliwa Watalii waliondolewa Mombasa. Milipuko ya mabomu ya Nairobi inakuwa na athari ktk mbuga ya Masai Mara na baadhi ya Mbuga zetu ziliziko Kaskazini.

Sisi tunaathirika na mabomu ya Nairobi kwasababu Watalii wengi wanao kuja nchini wanatua kwanza Nairobi. Mbuga za Serengeti,Ngorongoro,Mlima Kilimanjaro,Tarangire nk wanaathirika na mabomu ya Arusha kwasababu Watalii karibu wote wanaanzia safari zao Arusha! Sasa mtu akisema ukweli ooh hatupendi!
 
Tatizo la mabomu halihusiani na udhaifu wa serikali, kwani mabomu yanalipuliwa hata Marekani, Uingereza na kwingineko ambako usalama ni imara, usipotoshe hoja ya mtoa mada

Wakati nakubaliana nawe kwamba nchi yeyote yaweza lipuliwa na mabomu lakini wote uliowataja hapo juu walishughulikia milipuko ktk nchi zao kwa umakini mkubwa sana kwa kuwatafuta wahusika na kuwafikisha ktk mkono wa sheria. Sisi hakuna umakini wowote na ni kama watawala hawajali pengine wakilipuliwa wao na vimada wao. Mlipuko kama wa Soweto walifikia hatua mbaya ya kuwakejeli waanga wa mlipuko kwasababu tu ya itikadi za kisiasa.
 
Wakati nakubaliana nawe kwamba nchi yeyote yaweza lipuliwa na mabomu lakini wote uliowataja hapo juu walishughulikia milipuko ktk nchi zao kwa umakini mkubwa sana kwa kuwatafuta wahusika na kuwafikisha ktk mkono wa sheria. Sisi hakuna umakini wowote na ni kama watawala hawajali pengine wakilipuliwa wao na vimada wao. Mlipuko kama wa Soweto walifikia hatua mbaya ya kuwakejeli waanga wa mlipuko kwasababu tu ya itikadi za kisiasa.
Well said!!!!!!
 
Wakati nakubaliana nawe kwamba nchi yeyote yaweza lipuliwa na mabomu lakini wote uliowataja hapo juu walishughulikia milipuko ktk nchi zao kwa umakini mkubwa sana kwa kuwatafuta wahusika na kuwafikisha ktk mkono wa sheria. Sisi hakuna umakini wowote na ni kama watawala hawajali pengine wakilipuliwa wao na vimada wao. Mlipuko kama wa Soweto walifikia hatua mbaya ya kuwakejeli waanga wa mlipuko kwasababu tu ya itikadi za kisiasa.

Ha ha ha wewe, kwahiyo wewe unataka serikali ikamate na kuua kila mtu wakati ikitafuta walipua mabomu kama vile Marekani ilivyofanya wakati ikimtafuta "Osama"?
 
Nasema hivyo kwasababu polisi hawajawahi kushindwa kuwakamata wahalifu,siku zote majambazi wanapofanya matukio kesho yake utasikia yamekamatwa mahali Fulani,hata milipuko ya majuzi tayari wameshakamata washukiwa,lakini wale waliolipua mkutano Wa chadema mwaka Jana,hadi leo bado hawajawakamata mtu yeyote,eti wanategemea chadema wawape ushahidi sijui ndiyo waanze uchunguzi au kwakuwa wanahusika wauharibu.

Ikiwa mlipuko Wa juzi tayari washukiwa wameshawadaka,inakuwaje kwa Wa olesiti?Hii inanifanya niamini kuwa wahusika walikuwa ni polisi .
 
Ni wakati wa kufikiri nini cha kufanya ktk mazingira kama hayo (mauaji ya Mwangosi, Bomu O:lesty/Arusha). CDM isijisahau juu ya hayo. Walinia mabaya juu yake...na mbinu zilizotumika kutaka kuiangamiza ni za kighaidi. Hazijawaifanyika ktk siasa za Tanzania.
 
Mbona hata mwanangu wa chekechea anatambua hivyo?
 
Hata hawa walokamatwa kuna walakini
Tujiulize kwa nini Arusha tu?
Jee ni siasa ?
Je ni kukosa surpot na warusha na jimbo linatakiwa?
Jee ni mbinu za adui koidhoofisha utalii wetu?
Masuali ni mengi kwa nini arusha tu.
Tunaweza kukamata watu fulani fulani kuwafurahisha watu fulani juu ya ugaidi.
Kitu kimoja lazima tukubali vikosi vilivopata mafunzo ya kupambana na ugaidi yamepata kwa muelekea wa marekani bila kujali uhalisia bali chuki ..islamophobia wale walopata mafunzo wengine ------------ beberu ni beberu tu habadiliki kuwa rafiki anacheka uongo tu.
Tunaona kenya keo vikosi hivyo vinaua masheikh kwa kushtukiza na sasa sio masheikh tu hata waislam wenye uwezo na sote tunashuhudia kenya ilibo sasa.
Hapa kuna amri ua wale wote adui wa usa bila kufata sheria nchi ikiharibika potelea mbali sana sana tutatoa travel advise raia wetu wasikaribie
Tufunue vichwa vyetu nchi yetu isiharibiwe
Huvi hatuna uwezo wa kufundisha askari wetu sisi wenyewe?
Kuwapeleka nje ni kuhatarisha usalama wetu..
 
Hata hawa walokamatwa kuna walakini
Tujiulize kwa nini Arusha tu?
Jee ni siasa ?
Je ni kukosa surpot na warusha na jimbo linatakiwa?
Jee ni mbinu za adui koidhoofisha utalii wetu?
Masuali ni mengi kwa nini arusha tu.
Tunaweza kukamata watu fulani fulani kuwafurahisha watu fulani juu ya ugaidi.
Kitu kimoja lazima tukubali vikosi vilivopata mafunzo ya kupambana na ugaidi yamepata kwa muelekea wa marekani bila kujali uhalisia bali chuki ..islamophobia wale walopata mafunzo wengine ------------ beberu ni beberu tu habadiliki kuwa rafiki anacheka uongo tu.
Tunaona kenya keo vikosi hivyo vinaua masheikh kwa kushtukiza na sasa sio masheikh tu hata waislam wenye uwezo na sote tunashuhudia kenya ilibo sasa.
Hapa kuna amri ua wale wote adui wa usa bila kufata sheria nchi ikiharibika potelea mbali sana sana tutatoa travel advise raia wetu wasikaribie
Tufunue vichwa vyetu nchi yetu isiharibiwe
Huvi hatuna uwezo wa kufundisha askari wetu sisi wenyewe?
Kuwapeleka nje ni kuhatarisha usalama wetu..
Waliokamatwa ni vijana wa kiislam ambao walishawahi kusafiri kwenda yemen ndicho kigezo polisi walichotumia
 
Back
Top Bottom