Ipi bora? Lipa namba ya CRDB/NMB au Lipa ya Vodacom/tigo?

Ipi bora? Lipa namba ya CRDB/NMB au Lipa ya Vodacom/tigo?

Upepo wa Pesa

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2015
Posts
21,600
Reaction score
35,158
Je kwa biashara ni ipi bora kati ya Lipa ya voda na lipa za mabenki kama CRDB au NMB?

Ni ipi haina makato makubwa kwa mteja (wakati wa malipo) na mfanyabiashara (wakati wa kutoa ela)?

Naomba kujua ili nifanye maamuzi.
 
Zipo kawaida tu unahitaji unafanya Biashara gani? Km sio mfanyabiashara huwezi kupata hizo ni kwa ajili ya wafanyabiashara tu
Ukilipa laki moja gharama shs ngapi???
 
Sijawahi ata sikia hii.
Zipo
Screenshot_20250313_181625.jpg
 
Natumia lipa namba ya voda iko vizuri, natumia pia ya airtel.

Uzuri wa voda hata kulipana kati ya lipa namba to lipa namba ni free.

Ndio maana hata kwenye kazi yangu ya kubeti naitumia hii.
Yaani mimi sikatwi thumuni wakati wa kudeposit, sikatwi 10% maana nimechagua bookie ambao hawakati. Nikishinda nalipwa pesa ileile bila makato kisha natoa bure kwenye lipa namba.
 
Natumia lipa namba ya voda iko vizuri, natumia pia ya airtel.

Uzuri wa voda hata kulipana kati ya lipa namba to lipa namba ni free.

Ndio maana hata kwenye kazi yangu ya kubeti naitumia hii.
Yaani mimi sikatwi thumuni wakati wa kudeposit, sikatwi 10% maana nimechagua bookie ambao hawakati. Nikishinda nalipwa pesa ileile bila makato kisha natoa bure kwenye lipa namba.
Muwekaji kwema huko.
 
Muwekaji kwema huko.
Wakala wa bookie mfano mrusi (888starz au melb) ana lipa namba tofauti ikiwemo voda.
Kwa hiyo mimi nalipia kupitia voda lipa yake free kabisa.
Na nikishinda nikitoa namwambia aweke kwenye lipa namba yangu kama ni 100,000 ananiwekea yote hakatwi.
Na mimi naenda kwa wakala natoa free.

Kwa hiyo nakuwa nimefanya mizunguko yote bila kukatwa hata 10.
 
Sahivi lipa imeanza kuwa na makato?? Au makato yameanza na mimi 🙄
 
Back
Top Bottom