Ipi faida ya Mzee Alli Hassan Mwinyi kuwepo Dodoma kama Baba wa Taifa aliyebakia?

Ipi faida ya Mzee Alli Hassan Mwinyi kuwepo Dodoma kama Baba wa Taifa aliyebakia?

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Upo uwezekano kuwa mzee wetu Alli Hassan Mwinyi alipewa uongozi wa nchi bila kuwa na upeo imara wa kiuongozi.

Tofauti kabisa na wazee wenzake, huyu amekuwa hata haelewi umuhimu wa uwepo wa katiba Tanzania. Haelewi maana ya uongozi wa katiba katika nchi.

Ni aibu kwa mzee kama Mwinyi ambaye anatazamwa kama kiongozi baba wa nchi aliyebakia akihimiza eti katiba iende likizo kwa muda ili jambo ambalo kimsingi hata halina maana lifanyike.

Ni aibu kubwa kumpa jukwaa huyu mzee kisha anaongea haya huku ikiaminiwa kuwa aliwahi kuwa Rais wa nchi tena chaguo la Mwalimu Nyerere. Ndiyo maana huwa nabakia kujiuliza sana uko wapi umakini wa baba wa taifa tunaoaminishwa kama tu alituletea mrithi wa hovyo kama mzee Mwinyi.

Ni katika utawala wake tuliwahi kuwa na naibu waziri mkuu asiyetambulika kikatiba. Hivyo sina wasiwasi kuwa anamaanisha ayasemayo. Huyu mzee ni heri asiwe anapewa kipaza sauti kuongea, aachwe apumzike na uzee wake!
 
Yaaani mtoto wake kupitishwa na Magufuli kugombea uraisi Zanzibar anaona basi taifa lote tumtunuku magufuli kwa kumzawadia miaka mitano zaidi. This is very stupid kwa kweli.

Hadi wajumbe wa CCM walianza kumshangaa na walikuwa wananong’ona sana. Kama anakata kumshukuru Magufuli kwa kumpitisha mtoto wake kwenda kugombea Zanzibar basi amshukuru peke yake sio Eti kushauri taifa tuvunje katiba.

Kwa mara ya kwanza niliona hadi Magufuli alijishtukia akachomekea mzee amalize kuongea.
 
Hata alipokuwa akiongoza alikuwa anaongoza kwa mawazo ya walio nyuma ya pazia. Nyerere alimuweka maana ilikuwa rahisi kwake kumuagiza afanye atakalo.
Kama kitu hujui, ni vyema ukasoma comments tu. Inaonesha wewe wa baada ya 70s. Hakuwa ni chaguo la mwalimu ila baada ya kuukwaa ilibidi mwalimu amsaidie kwa karibu
 
Mkuu, huyu Mzee ni wa kumsamehe bure tu, kwa kuwa alitamka hivyo kwa kusukumwa na mhemuko uliotokana na mwanaye kuweza kuchaguliwa kuwa mpeperusha bendera wa nafasi ya uraisi kwa upande wa Tanzania Visiwani. Hili lilikuwa ni tamanio lake la muda mrefu, na hivyo kuona kuwa amepewa upendeleo mkuu.

Pia ukweli ni lazima uwekwe wazi, ktk michakato ambao CCM iliweza kutuletea viongozi pasipo kuchukua tahadhari yoyote ile, ilikuwa ni kipindi cha awamu ya kwanza na hatimaye Mzee Mwinyi akaingia madarakani. Na pia katika kipindi cha awamu ya nne na hatimaye Mheshimiwa wa sasa akaingia madarakani.

Lakini jambo moja linanishangaza na kunifanya niweze kutafakari kwa kina zaidi. Majina ya kwanza ya Rais wa awamu ya kwanza lilikuwa ni Julius, awamu ya nne lilikuwa ni Jakaya, na awamu hii ya tano ni John. Japo mimi si mpiga ramli, lakini huu mfanano wa herufi za kwanza za herufi "J" ktk majina yao, zinatupa "general rule" kuwa hawapo makini kusimamia vyema michakato ya kutuletea warithi wazuri wa nafasi za pale wanapostaafu. Kwa pengine hata kwa John tutegemee mambo kama hayo.
 
Back
Top Bottom