Kuna sehemu nimeongelea masuala ya lugha aisee au umenichanganya na mtu mwingine 😳😳Lugha gani tena? Hapo umeambiwa nchi 54, au unataka kusema Kenya wanazungumza zaidi kiingereza kuliko Uganda, Zambia, Zimbabwe, ghana, nigeria?
Tutafute sababu halisi
Tanzania kuna potential kubwa sana kiutalii sema focus yetu imekua tu sehemu ndogo .......wakenya na vivutio vichache ila wameweza kuvitumia, bongo ukiacha kaskazini huku kwingine kumesahaulika sanaNdugu yangu siku hizi kuna kitu kinaitwa 'cultural tourism' have you ever heard about it? Hii ni muhimu sana na inaleta pesa nyingi sana kwa wamasai.
Pia Kuna sex tourism wenzetu hapo Lamu na Malindi imeshamiri sana beach boys wanakula wamama wa kizungu kwa malipo naona Zanzibar imeanza hii.
Kuna agricultural tourism etc yani Ile sabasaba day inatakiwa wageni wajae Tanzania kuja kuangalia what do we in the market!
Kuna vitu tumezubaa ndio maana wenzetu wanatupiga bao sehemu ndogo sana.
Sisi tuna vivutio vingi zaidi Ila hatujajiongeza kuvifanya viafahamike kwamba tunavyo ili tuexplore hizo fursa.
Wakisema wanazo fursa tunaanza kukasirika all we have to offer is Kilimanjaro and Serengeti huu no ujinga wakenya hata Kilimanjaro wameacha kuitaja siku hizi.
We have to be proactive.
BET Awards Red Carpet...
Pamoja na mambo mengine, usikute Diamond hapo alidhani alikuwa anaitangaza Tanzania lakini kwa wale ambao ilikuwa ndo mara yao ya kwanza kumuona/kumsikia basi, kwa hiyo dressing code, majority aliwaaminisha yeye ni Mkenya!!
Nini hiyo dressing code, hata Kiswahili huko mbele majority wanadhani Kenya ndo "wenyewe"!!
Ingawaje kwa mbaaaaaaali hivi sasa kidogo inapungua lakini zamani kuitambulisha Tanzania ipo wapi ilikuwa ni kazi ngumu kweli kweli hususani kama HUTAKI kuitaja Kenya kwa sababu the only way kuitambulisha kirahisi ilikuwa uitaje Kenya manake hata ukitaja Mt Kilimanjaro, usishangae ukaambiwa "Oh! So, you mean it's Kenya"!
Bila shaka hapo utakuwa umepata jibu!!
In short, Ujamaa wa Mwalimu ulitufanya Watanzania kuwa mazombi and less aggressive! Na vile hatutaki hata kuwashtua CCM physically, ndo kabisa coz' in Africa, if you don't have something good to showcase, just showcase your unpleasant side!
Ni kweli, unajua kwa mfano ziwa Tanganyika ndio ziwa lenye kina kirefu barani afrika na kuna utalii wa kutosha ziwani ikiwemo scuba diving, ziwa nyasa Kuna Mbuga Kama Mikumi, Katavi nk ambazo Zina wanyama na vivutio vingi zaidi.Tanzania kuna potential kubwa sana kiutalii sema focus yetu imekua tu sehemu ndogo .......wakenya na vivutio vichache ila wameweza kuvitumia, bongo ukiacha kaskazini huku kwingine kumesahaulika sana
Lugha inawabeba wenzetu sana ni Wakati sasa wa kuanza kufundisha Lugha ya Dunia kuanzia Primary mpaka Chuo kikuu, Hili Swala la kukumbatia kiswahili tu. Kwa kweli linatukosesha Kuwa linked na Ulimwengu tembea hata Platform nyingi uone wakenya wanavyo ji brand ila sisi watz tunakwama kwa ajili ya Lugha pia
KENYA ILIJITANGAZA KWA MDA MREFU SANA DUNIANI TOFAUTI NA TANZANIA,TUNASHUKURU MAMA #SSH AMELIONA HILI NA ANAKWENDA NALO SAMBAMBA MUNGU AMBARIKI SANA MAMA HUYU,JAPO NI GHALI KUFANYA HILI LAKINI HAKUNA NAMNA,HATA KAGAME YUPO BIZE KWENYE HILI,RWANDA NAYO INAWEZA KUWA NEXT TO KENYA,LAKINI KWA BIDII HIZI ZA MAMA "AT NO LONGER WE SHALL BE NUMBER ONE"Nilikuwa naangalia video flani YouTube inahusu capital city za nchi 54 za Africa. Sasa nikaenda sehemu ya comments kusoma nikajionea watu wengi kutoka mataifa mbalimbali dunia wakiisifia Kenya kuwa ndo favourite country yao lakini kiuhalisia ni dhahiri tumewazidi vivutio (Sina haja ya kuvitaja vinajulikana) pamoja na utamaduni tuna makabila mengi ambayo wazungu labda wangetamani kuja kwetu kujifunza Mila za makabila pia tuna amani hatuna historia mbaya ya kumwagana damu kugombana kubwa zaidi tuna eneo kubwa la ardhi mapori yasiyofanyiwa chochote yameachwa tu hivyo ni rahisi kuwekeza tofauti na Kenya ambapo ardhi inashikiliwa na wachache.
Sielewi kwanini wazungu waipende kenya tukisema kwamba sababu ni ina maendeleo sio kweli maana hata kwao ulaya huko wako vizuri tu hawawezi kuja kushangaa magorofa ya Nairobi hapo na hata hivyo kama kutupita kiuchumi hawajatupita sana ni gap fulani la kawaida.
Ingawa pia nilianza kuhisi labda comments hizo zaweza kuwa ni za Wakenya wenyewe wameamua tu kujimwambafy; si mnajua walivyo makanjanja kwenye kujipaisha.
Video yenyewe iko hapo chini search YouTube nenda upande wa comments.
View attachment 2104557