demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Asanteni sana Bodi ya Ligi kwanza kabisa ya kukubali Maombi ya Dar es Salaam Young Africans SC ya kubuni trophy jipya la kuendana na Msimu wao mpya wa kurudi kwenye Mataji Rasmi.
Pili shukrani ziwafikie kwa maandalizi ya kipekee mliyo yafanya pale Sokoine. Nilikuwa na kiongozi mmoja wa Simba SC akasema “Shamra shamra hizi hazikuwahi kutokea”.
Tatu, Napenda kuwapa matumaini watani zangu wa Jadi kuwa wasijione wanyonge. Ofcourse Dar es Salaam Young Africans SC imekuwa ni klabu pekee yenye ushawishi mkubwa katika LIGI Kuu kuliko klabu yeyote katika historia, lakini hiyo sababu isiwafanye mjione WANYONGE.
Wengi wenu hamjapendezewa na muonekano mpya wa kombe Jipya ambalo ujio wake unatokana na Mapendekezo ya Klabu ya Dar es Salaam Young Africans SC.
Sio tu mashabiki bali hata sehemu kubwa ya viongozi wa Simba SC nao hawajafurahishwa kabisa na muonekano wa Kombe Jipya. Nadhani kwa upande wetu sisi Viongozi na Mashabiki wa Dar es Salaam Young Africans SC tumekuwa na mapokezi chanya kutokana na sisi ndio tulio dau mabadiliko hayo.
USHAURI:-
Ninawashauri Viongozi wa Klabu ya Simba SC kugomea kushiriki msimu mpya wa LiGI KUU Tanzania Bara utakao anza 2022/23.
Ni matumaini yangu kuwa kama wakigoma kushiriki kama misimu miwili mitatu mfululizo basi huenda Body ya Ligi wakata na muundo mpya wa trophy ambao utaendana na matamanio ya klabu ya simba sc.