Ipo siku tutajenga sanamu ya Hayati Magufuli na kufungua Maktaba yake ili vizazi vijifunze Uzalendo

Ipo siku tutajenga sanamu ya Hayati Magufuli na kufungua Maktaba yake ili vizazi vijifunze Uzalendo

Mungu wewe unachukua majabali una chukua wanaume ambao kweli jando lao halikuwa la ganzi. Wanaume wenye misuli ya Imani na uwezo wakuona kesho kwa Imani na matendo. Kwa Tanzania Ulitupa Hayati Joseph Pombe Magufuli. Kijana alie zaliwa ktk ufukara ila ukampa kukikalia kiti cha Jamuhuri ya watu Wa Tanzania na kweli akatupa darasa ambalo kamwe kwa tulio Baki hatuto msahau.

Kama ilivyo kwa mzazi alituchapa na alituadabisha akiwa na ndoto za mzazi siku moja siku moja tutamkumbuka nakwenda ktk kaburi lake nakusema baba tunakukumbuka kama Mungu angetupenda basi angalau angekupa mwaka mmoja tu zaidi utuchape viboko ili tuwe na akili.

Jemedari huyu wa awamu ya Tano aliitikisa nchi ikatikisika alipambana na majangili mpaka wanyama Porini na miti maporini ikawa inamuombea kwa Mungu. Alilinda kwa mkono wa chuma mipaka na siri za serikali kiasi kila alie na siri aliona kuliko kuitoa Bora kunywa sumu.

Alimanisha alicho Maanisha na hakuwa na utani kwa kile alimanisha. Kwake dam na neno lake vilikuwa nijambo lakuchaguwa na hiyo ndio maana ya kiongozi. Wanafiki na mapandikizi walipata tabu sana maana aliwafanya wajione kama mapanzi mbele ya tai.

Hakuwa na mchezo hakuwa na masihara kwenye kitu kinaitwa hela ya serikali kama ulitaka kuona rangi ya mtawala huyu basi cheza na hela ya serikali. Watu walirudisha risiti na pesa ilio Baki. Watu waliogopa pesa ya serikali kiasi ilifika mahali TUNAKUTANA kwa Mama ntilie Yani mama ntilie alipanda thamani kuliko 5 star hotels.

Mbabe huyu alitufanya watu wawe na plan B ktk kila wakifanya na alifanya watu kuheshim mishara yao nikatika kipindi chake alifanya mageuzi makubwa na yaaina yake kwenye secta ya ajira sio hivyo tu alihakikisha masikini akiingia Ofisi ya serikali awe mfalme asikudanganye mtu masikini na mtu wa chini alikuwa mfalme maana ilikuwa akisikia mtu amedhulumiwa au akionewa na RC walile eneo hakufanyia kazi tatizo lake unakiwa kichwa bila notice. He was Iron Men. Acha chezea hii namba.

Hayati Magufuli hakuwa kiumbe cha kawaida hakuwa mwanadam au kiongozi wakawaida alipania na alikumbuka ahadi yake kwa Mungu na akiifanyia kaz kwa dam na jasho kwa ajili ya Tanzania. Moja maisha yalio watisha wengi nikufanya kaz usiku wakati mwingine usiku mzito sana the guy was not normal human being lazima watu wakaribu watasimulia maajabu ya huyu kiumbe.

Alilijuwa duka na alikuwa na kila siri ya duka na hili likiwatetemesha wengi japo wazalendo walio mpenda walisema Mungu Asante umetuletea mkombozi. Alizijuwa siri ambazo watangulizi wake uwenda hawakudhani angezijuwa na alisoma sana kila siri wakati mwingine files ZINGINE mezani mwake zilimtisha hata yeye mwenyewe na uwenda ndio maana alituacha ktk wakati hakuna aliamini angetuacha japo Yeye alishakiona kifo.

Mwamba ndio mwanaume alie Jenga hili Taifa kwenye miundo mbinu huwezi simulia miundombinu ya Taifa hili bila kumtaja Mwamba Magufuli. Alitandaza lami mpaka Malaika wa Mbinguni wakasema lazima utaliongoza hili Taifa. Wachambuzi wa mambo wanasema kama angekuwa kibaka uwenda ndio waziri angekuwa na ukwasi wakitisha ktk Taifa hili ila alikuwa wakawaida sana.

Ukikaa nakujiuliza why Kuna kundi lina mchukia sana jibu nimoja tu kitu alicho wafanyia na pin alizowawekea na makofuli aliwafungia milango yao ya ulaji kamwe hawatoweza kuifungua hata baada ya miaka 100 yani aliona zaidi yao mfano nani anapenda mradi wa bwawa la mwalim Nyerere kama unamacho ya mbali Yani huu mradi unawauma watu fulani sana Usiniulize kwanini.

Miaka inakuja Gemedari huyu atakuwa Habari ya Taifa na huwenda siku zinakuja kutakuwa na Magufuli day. Siku zinakuja kumdhihaki nakumsema huyu Mwamba vibaya unakosa kura siku zinakuja hata upinzani watamtaja kwa mema. Wajukuu watamuimba nakumsoma mashuleni. Maana ndie kiongozi alie sema moyoni mwake kuliko kuishi nakupigiwa mizinga 21 na heshima na kukaa ktk magorofa nakula Pepo za Dunia ni Bora kufa nikiacha alama ambayo kila mtu hatoangalia mabaya yangu ila mema yangu.
Hayati Magufuli ni nyota iliozima wakati wa mchana ila lijapo giza atamulika kwa milele. Asante Baba Asante Mzee Magufuli umetufundisha Uzalendo wa kweli kwa Taifa letu. Amen
MAGUFULI HAKUWA MZALENDO acheni kumpa Sifa za Kiccm
 
Mwamba JPM, alitikisa Dunia, nayo Dunia ilitikisika. Mwamba aliwika na ssuti yake ilisikika haswaa.
Mwamba aliipenda Tanzania na Watanzania wote.
Mwamba alikuwa tishio kwa mabeberu, walarushwa, wezi na wazembe katika kazi za umma.

Ushujaa wa pekee aliotuonesha Mwamba ni pale alipojua kabisa kwamba Kiongozi yeyote wa Afrika kujaribu kutetea Rasilimali za Nchi yake ni sawa kabisa na kuvaa kitanzi shingoni mwake, lakini yeye hakurudi nyuma hata kidogo.

Kwa kifupi kabisa ni kwamba, JPM alipambana mpaka tone lake la mwisho bila kusalimu amri.

Ndo maana utakuta lile GENGE la mafisadi linajaribu kupambana naye, lakini unafika wakati wanashindwa, kwani Mungu hawapendi wanafiki.
 
Mwamba JPM, alitikisa Dunia, nayo Dunia ilitikisika. Mwamba aliwika na ssuti yake ilisikika haswaa.
Mwamba aliipenda Tanzania na Watanzania wote.
Mwamba alikuwa tishio kwa mabeberu, walarushwa, wezi na wazembe katika kazi za umma.

Ushujaa wa pekee aliotuonesha Mwamba ni pale alipojua kabisa kwamba Kiongozi yeyote wa Afrika kujaribu kutetea Rasilimali za Nchi yake ni sawa kabisa na kuvaa kitanzi shingoni mwake, lakini yeye hakurudi nyuma hata kidogo.

Kwa kifupi kabisa ni kwamba, JPM alipambana mpaka tone lake la mwisho bila kusalimu amri.

Ndo maana utakuta lile GENGE la mafisadi linajaribu kupambana naye, lakini unafika wakati wanashindwa, kwani Mungu hawapendi wanafiki.
Labda dunia ya kwenu Burundi
 
Mkuu ni kweli huenda kuna kumbukumbu ya mazuri yake. Lakini vipi yakipimwa kwa kulinganisha na mabaya yake. Ndiyo! Alikuwa ni kipenzi cha maendeleo ya vitu, na tena kwa amri katili ya kikatiba kuendana na mamlaka ya kirais aliyokuwa nayo katika enzi zake.

Vipi kuhusu upande wake wa pili! Ule wa madhila hasi kwa wale wote aliowatendea udhalimu kwa ajili ya manufaa yake binafsi ya kisiasa. Ili kumtendea haki yote, kila jiwe itapaswa ligeuzwe ili mazuri yote na mabaya yake yakapate kudhihirika.

Yeye alikuwa ni binadamu kama mwingine yeyote yule. Hatuwezi kuficha mabaya yake eti kisa alikuwa Rais wa JMT, na alikuwa na kinga ya kutokushtakiwa akiwa hai kwa yale aliyoyafanya akiwa Rais. Ni lazima avune alichokipanda, hii ni kanuni ya maisha, hapa duniani katika maisha ya kimwili, na hata mbele ya mamlaka ya mbingu katika maisha ya umilele ya kiroho.
Umenena vyema kabisa
 
Nilikaa na Waziri Bashe anaongelea uwekezaji katika umwagiliaji wa kiasi cha dola milioni 16.

Yeye mwenyewe akiziona hela nyingi hizo.

Wakati dola milioni 16 ni thamani ya nyumba moja tu hapo Malibu.

Nikasema Jiwe alitupiga na kitu kizito sana katika ununuzi wa zile ndege.

Tena ndege zenyewe zimenunuliwa kijinga, nyingine zikisafiri nje zinakamatwa kufidia madeni ya nchi.

Ujinga mtupu.

Tumenunua Dreamliner 4 za dola za Marekani milioni 726, halafu kilimo cha umwagiliaji nchi nzima tunawekeza dola milioni 16.


Halafu ndiyo unaambiwa mzalendo huyo!

Ukiwasikia hawa majuha wanaongelea kuhusu huyu mtu wao unaweza hisi alikuwa na akili kumbe upupu mtupu!!

Alipoteza hela nyingi tu za wananchi kwa sifa za kijinga kabisa!! Watanzania wangapi sasa hiv wanaopandanhizo dreamliner?

Na uwanja wa mamilioni kajenga chato!!

Hawa wasukuma wa kupuuza tu, akili kichwani hamna!!
 
Uzalendo mavi, na mapesa yote alioenda ficha china!! Hiv wasukuma mnaumwa ugonjwa gani?
Mkuu usiunganishe kabila zima lenye mamilioni ya watu na ujinga wa watu wachache.

Wasukuma wengi tu tumempinga Magufuli tangu siku nyingi sana na mpaka leo tunaendelea kupinga siasa zake.

Tafadhali ondoa kauli za kuchochea ukabila JF.

Wasukuma wangekuwa na ujinga wa ukabila hii nchi isingekuwa na amani hivi.

Well, isingekuwa na kukosa vita hivi, maana amani haina.
 
Mitume tunayoisoma kwenye vitabu vya dini ilikataza masanamu, Mtanzania wa leo anajenga masanamu.

Aliyeshauri kujengwe sanamu apige hesabu mitume walibomoa masanamu miaka mingapi nyuma, atajieleaankuws yupo nyuma kwa miaka mingapi.

Kwa watu wenye fikra zilizo nyuma kwa miaka hiyo tutegemee maendeleo? Mawee!
 
Mimi kama mimi, kwa heshima yake yeye kama yeye, ambaye aliaminiwa kuishika nafasi ya Rais wa nchi yetu katika awamu ya 5, kesho sintakuja jukwaani kwa ajili ya maoni yoyote yule kuhusu yeye.

Nathamini nafasi ya familia katika maombolezo, kumbukizi na hata kusheherekea mazuri yake kama mume, baba wa familia, mjomba, baba mkubwa, baba mdogo, kaka, mpwa, rafiki, jamaa wa karibu, mwana jumuiya, muumini, mteja, mpangaji, mlipa kodi, kiongozi wa CCM, dikteta, muimla, dhalimu, fedhuli, amiri jeshi mkuu, Rais, Mwenyekiti Taifa wa CCM, jirani, mchepuko, na sifa nyingine yoyote ile aliyokuwa nayo kama binadamu wa kawaida mwenye sifa ya kuwa "possessed to many societies" na jina ake kubadilika kutokana na matakwa ya wakati.
 
Mimi kama mimi, kwa heshima yake yeye kama yeye, ambaye aliaminiwa kuishika nafasi ya Rais wa nchi yetu katika awamu ya 5, kesho sintakuja jukwaani kwa ajili ya maoni yoyote yule kuhusu yeye.

Nathamini nafasi ya familia katika maombolezo, kumbukizi na hata kusheherekea mazuri yake kama mume, baba wa familia, mjomba, baba mkubwa, baba mdogo, kaka, mpwa, rafiki, jamaa wa karibu, mwana jumuiya, muumini, mteja, mpangaji, mlipa kodi, kiongozi wa CCM, dikteta, muimla, dhalimu, fedhuli, amiri jeshi mkuu, Rais, Mwenyekiti Taifa wa CCM, jirani, mchepuko, na sifa nyingine yoyote ile aliyokuwa nayo kama binadamu wa kawaida mwenye sifa ya kuwa "possessed to many societies" na jina ake kubadilika kutokana na matakwa ya wakati.
Mimi kesho nitashinda hapa Picnic bar Arusha napiga K-vant
 
Mungu wewe unachukua majabali una chukua wanaume ambao kweli jando lao halikuwa la ganzi. Wanaume wenye misuli ya Imani na uwezo wakuona kesho kwa Imani na matendo. Kwa Tanzania Ulitupa Hayati Joseph Pombe Magufuli. Kijana alie zaliwa ktk ufukara ila ukampa kukikalia kiti cha Jamuhuri ya watu Wa Tanzania na kweli akatupa darasa ambalo kamwe kwa tulio Baki hatuto msahau.

Kama ilivyo kwa mzazi alituchapa na alituadabisha akiwa na ndoto za mzazi siku moja siku moja tutamkumbuka nakwenda ktk kaburi lake nakusema baba tunakukumbuka kama Mungu angetupenda basi angalau angekupa mwaka mmoja tu zaidi utuchape viboko ili tuwe na akili.

Jemedari huyu wa awamu ya Tano aliitikisa nchi ikatikisika alipambana na majangili mpaka wanyama Porini na miti maporini ikawa inamuombea kwa Mungu. Alilinda kwa mkono wa chuma mipaka na siri za serikali kiasi kila alie na siri aliona kuliko kuitoa Bora kunywa sumu.

Alimanisha alicho Maanisha na hakuwa na utani kwa kile alimanisha. Kwake dam na neno lake vilikuwa nijambo lakuchaguwa na hiyo ndio maana ya kiongozi. Wanafiki na mapandikizi walipata tabu sana maana aliwafanya wajione kama mapanzi mbele ya tai.

Hakuwa na mchezo hakuwa na masihara kwenye kitu kinaitwa hela ya serikali kama ulitaka kuona rangi ya mtawala huyu basi cheza na hela ya serikali. Watu walirudisha risiti na pesa ilio Baki. Watu waliogopa pesa ya serikali kiasi ilifika mahali TUNAKUTANA kwa Mama ntilie Yani mama ntilie alipanda thamani kuliko 5 star hotels.

Mbabe huyu alitufanya watu wawe na plan B ktk kila wakifanya na alifanya watu kuheshim mishara yao nikatika kipindi chake alifanya mageuzi makubwa na yaaina yake kwenye secta ya ajira sio hivyo tu alihakikisha masikini akiingia Ofisi ya serikali awe mfalme asikudanganye mtu masikini na mtu wa chini alikuwa mfalme maana ilikuwa akisikia mtu amedhulumiwa au akionewa na RC walile eneo hakufanyia kazi tatizo lake unakiwa kichwa bila notice. He was Iron Men. Acha chezea hii namba.

Hayati Magufuli hakuwa kiumbe cha kawaida hakuwa mwanadam au kiongozi wakawaida alipania na alikumbuka ahadi yake kwa Mungu na akiifanyia kaz kwa dam na jasho kwa ajili ya Tanzania. Moja maisha yalio watisha wengi nikufanya kaz usiku wakati mwingine usiku mzito sana the guy was not normal human being lazima watu wakaribu watasimulia maajabu ya huyu kiumbe.

Alilijuwa duka na alikuwa na kila siri ya duka na hili likiwatetemesha wengi japo wazalendo walio mpenda walisema Mungu Asante umetuletea mkombozi. Alizijuwa siri ambazo watangulizi wake uwenda hawakudhani angezijuwa na alisoma sana kila siri wakati mwingine files ZINGINE mezani mwake zilimtisha hata yeye mwenyewe na uwenda ndio maana alituacha ktk wakati hakuna aliamini angetuacha japo Yeye alishakiona kifo.

Mwamba ndio mwanaume alie Jenga hili Taifa kwenye miundo mbinu huwezi simulia miundombinu ya Taifa hili bila kumtaja Mwamba Magufuli. Alitandaza lami mpaka Malaika wa Mbinguni wakasema lazima utaliongoza hili Taifa. Wachambuzi wa mambo wanasema kama angekuwa kibaka uwenda ndio waziri angekuwa na ukwasi wakitisha ktk Taifa hili ila alikuwa wakawaida sana.

Ukikaa nakujiuliza why Kuna kundi lina mchukia sana jibu nimoja tu kitu alicho wafanyia na pin alizowawekea na makofuli aliwafungia milango yao ya ulaji kamwe hawatoweza kuifungua hata baada ya miaka 100 yani aliona zaidi yao mfano nani anapenda mradi wa bwawa la mwalim Nyerere kama unamacho ya mbali Yani huu mradi unawauma watu fulani sana Usiniulize kwanini.

Miaka inakuja Gemedari huyu atakuwa Habari ya Taifa na huwenda siku zinakuja kutakuwa na Magufuli day. Siku zinakuja kumdhihaki nakumsema huyu Mwamba vibaya unakosa kura siku zinakuja hata upinzani watamtaja kwa mema. Wajukuu watamuimba nakumsoma mashuleni. Maana ndie kiongozi alie sema moyoni mwake kuliko kuishi nakupigiwa mizinga 21 na heshima na kukaa ktk magorofa nakula Pepo za Dunia ni Bora kufa nikiacha alama ambayo kila mtu hatoangalia mabaya yangu ila mema yangu.
Hayati Magufuli ni nyota iliozima wakati wa mchana ila lijapo giza atamulika kwa milele. Asante Baba Asante Mzee Magufuli umetufundisha Uzalendo wa kweli kwa Taifa letu. Amen
Walamba asali wanatamani huu uzi ufutwe!
 
Back
Top Bottom