Iringa: Wanafunzi 400 wa Shule ya Msingi hatarini kuhara kutokana na changamoto ya choo kukosa maji

Mkuu wa mkoa yupo
Mkuu wa wilaya yupo
Mkurugenzi yupo
Katibu tawala yupo
Afisa elimu yupo
Mbunge yupo
Wazazi mpo
Jitahidini hamjashindwa kujenga hivyo vyoo
 
Ngoja tumalize kujenga kinyago ,tutakujuza mkuu
 
Halafu eti hela zinaenda kujenga sanamu ya mtu! Nyingine zinatumika kununulia Benzi la Rais Mstaafu, nyingine zinaenda kuwajengea Marais hao hao Wastaafu mahekalu ya kuishi!!

Yaani mtu amehudumu katika nafasi ya ubunge, uwaziri na baadae Urais kwa miaka lukuki, analipwa mafao ya 80% kila mwezi, halafu bado ananunuliwa gari, anajengewa nyumba ya kifahari na bado haitoshi, anajengewa mpaka sanamu!

Hakika Tanzania inahitaji Katiba Mpya haraka iwezekanavyo! Kuna mambo yanaleta sana maudhi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…