Is It Possible?

Ni ngumu kwa kweli hasa kama tuliachana katika hali ya mateso na manyanyaso.Tukiachana katika hali ya ugomvi mkubwa usitarajie ntakuwa rafiki yako..Kujifanya marafiki sitaweza kwani kila ninapokuona nitaanza kukumbuka mateso uliyonisababishia na muda ulionipotezea.Kama ni wa watoto utaenda nao matembezi kwa muda wako.
 
hahaha hapo ndo pagumu na ndo hupelekea kuongezeka zaidi madhara ya kuachana

Ha we acha kabisa haya mateso tuliyopitia wengine ni balaa kwa bahati mbaya alifariki baada ya miezi miwili (RIP G....) sifurahii kufariki kwake lakini nilipata amani maana ilikuwa ni balaa
 
Ha we acha kabisa haya mateso tuliyopitia wengine ni balaa kwa bahati mbaya alifariki baada ya miezi miwili (RIP G....) sifurahii kufariki kwake lakini nilipata amani maana ilikuwa ni balaa

pole sana dena kwa maswaibu yaliyokukuta ... lakini naamini watoto wanaendelea kufaidika na waliopo
 
Inawezekana. Its a matter of will, if you have a heart made of stone you can do that, but a heart like mine am not sure, inawezekana lakini.
Duh, ni kamtihani hakoo
 

Mbu nakumbuka sana topic yako
Maudhui yake na haya yanafanana sana
Kufanywa msukule wa mapenzi bila kujijua
 
Reactions: Mbu


Ndo maana hata mimi nawashauri, kama kweli hawataki kumegwa megwa kama ice cream za watoto wa shule waache mchezo wa kuendekeza mawasiliano na vikao na ma-ex wao!

 
Ukweli hii ni kukaribisha matatizo katika uhusiano mpya (kama upo), ni ngumu sana kuamini kaalikwa tu je hakuna jingine limejificha?
 

Usijali Maty,

Nawependa sana wajukuu zangu kiasi kwamba inaniuma kuona wanaingizwa mkenge...Ila ukikubali kuchezewa basi huko siyo kuchezewa tena bali ni kuchezeana!!
 
Ha we acha kabisa haya mateso tuliyopitia wengine ni balaa kwa bahati mbaya alifariki baada ya miezi miwili (RIP G....) sifurahii kufariki kwake lakini nilipata amani maana ilikuwa ni balaa

Pole sana AD,

Naona hii mioyo imebeba mazagazaga mengi sana,

Mshukuru mungu wako kwa kukuwezesha kumalizana na hilo timbwili...

Babu DC!
 
I think it is possible.... i Know mimi ni shahidi katika hilo.... but you need kujenga uaminifu kwa muda wa kutosha kwanza kuwa you have no interest ya kurudi where you were before..... You know some people can be good friends but not as husband and wife or life patners.
 
Wapendwa si kwamba nimewakimbia bali nawasoma na kuwaelewa vizuri. Aksanteni sana kwa mawazo yenu na ushauri. I will be with you shortly
 
Hili lisredi limenipitaje?

Kwangu mie:

Ni possible kama kutakuwa na mkakati wa kurudiana......... Yaani lazima yale ma SRM yakumbukwe na yafanyiwe kazi

Ila

Ni impossible kama vigezo na masharti ya yale ma SRM hayatazingatiwa.

Ushauri wangu: Bibiye, sahau yaliyopita. Piga moyo konde rudianeni na mzazi mwenzio. Maisha ya upweke yashakushinda, na moyo wako bado umeacha vipande kwenye moyo wake.Tii kiu yako. Acha penzi lionyeshe njia!

Na hili ndilo neno la ODM.
 
Asante wmaya maumivu yamenirudia upya baada ya kuona hii thread lakini maisha yanakwenda

DA amini kila kitu kina mwisho japo mwisho unaweza kuwa mzuri au mbaya kwa upande wako hivyo cha msingi ni kusimama kuanzia pale ulipo na kuangalia mbele na si kuangalia historia
 
Umenikumbusha AR kwa machalii na watani zangu.... kufungua lock ni kuzimua. Kwa hiyo kujipiga lock nadhani ni kujidunga na ulevi. Ukidadavua hapo with respect to love utakonkludi kuwa kurudiana na mzazi mwenzako eti "kiurafiki" zaidi ni ulevi wa kimapenzi.

Na hii ni hatari zaidi ya danger, hasa kwa mwanamke!
Kupigwa kimapenzi kunauma sana, lakini ogopa kupigwa mara ya pili na mtu yuleyule.
Msije mkasema sijawaambieni Yoooooo! IGWEEEEEEEEEEEEEEEEEE!!!
 


MJ1...fata moyo wako unavyosema, ghasia/shida/kutendwa etc unajua maumivu yake zaidi ya cc wengine, hakuna anaekufa na upweke n btw kwann uwe mpweke mpaka sasa?...mie cpendagi mambo ya kurudi nyuma, nadhani nina moyo wa kuacha kabisa bila kujutia, yaani ile nimeamua kufanya maamuzi bac ndio hayo hayo hata nani hawezi kuyatengua ninapoona ninayoyafanya ni kwa faida yangu...
 

ni kweli usemayo , maana halisi ya urafiki ni ukaribu na kuwepo uwezekano wa kujadili japo hata masuala mbali mbali ya kkimaisha na kijamii.. sasa sijui itawezekanaje wakati yawezekana umetenda au umetendewa ubaya .. naamini nafsi itakuwa inahukumu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…