Islam’s role in Tanzania’s freedom struggle

Nguruvi3.

Post yako uliotundikia sisi ukaweka CC;
 
Last edited by a moderator:
We Nguruvi3 bahati mbaya niko brbrn natumia tablet tu! Lkn kuna post nyingi tu umetoa kashfa wewe na yule swahiba yako Mag3 akitukana , wewe ukimpa support!
Sasa ukitaka majadiliano ya kistaarabu sisi tuko tayari! La we hodari ya kuwatungia mashairi wenzako ukawata MAKANJANJA! na sisi tumekulia kwenye mazingira kama ya kwako! Tunaweza na sisi kuuweka ustaarabu pembeni kidogo!
Sasa kabla hatujatoka kwenye mada!
Ulisema umeandaa vitu VIZITO SAANA!
AMBAVYO VITASABABISHA TUKIMBIE!
Leo jamaa yangi siku ya pili! Vipi!?
GOOGLE IMEKATAA??
au mgao wa umeme umeleta kero!?

Hayo ndio matatizo ya kukaa maeneo ya waislamu wengi! Mgao haupungui!
Ukihamia kwa wagalatia! Aaaaaah ! Mgao unauona kwenye tv tu!

Nakusubiri kabla sijaingia kazini!
Nipate kukimbia kabisa!!
 
Last edited by a moderator:

Nguruvi3.

Matumizi ya lugha yameanza kubadikika baada ya hii post yako.
 
Last edited by a moderator:

Unaweza kuandika historia ya kabila fulani, huwezi kuandika historia ya Tanganyika kwa kundi fulani.
Kufanya hivyo ni kupotosha ukweli.

Huwa unaandika pumba nyingi ili kuficha mchele ulio enguliwa.

Inawezekana wewe ni mtu ambae ili mradi ubishe kwa kuwa inakuuma kuona "kundi fulani" lina historia. Hilo "kundi fulani" kwanini kinakushinda kusema ni Waislaam? usiogope.

Tazama hizi historia za Mataifa makubwa, hawaogopi kuziandika na kuzisoma historia za "kundi fulani", kulikoni leo kwako iwe mwao kwa Tanganyika aka Tanzania tu?

1) Islam in America

2) BBC - Religions - Islam: History of Islam in the UK

3) Muslims in China - History of Islam in China

5) History of Islam in Russia | IslamDag.info

6) France and Islam from 732 AD to the 21 Century

7) History of Islam in Kenya

8) Islam in Ghana | Islam Story - Supervised by Dr. Ragheb Elsergany

9) How Islam Spread in India | Lost Islamic History

10) http://www.islamtanzania.org/nyaraka/islam_and_politics_in_tz.html


Huna pakukwepa Historia ya Uislaam kokote uendapo, nakuona wa ajabu sana ikiwa roho inakuuma inapoandikwa historia ya Uislaam na Waislaam wa Tanganyika /Tanzania.

Sijui kwanini roho ikuume kiasi hicho. Au unaumia zaidi unaposoma kuwa Nyerere alikuta watu tayari wako kwenye harakati na hata jina la TANU hakutunga yeye na lilikuwepo kabla ya ujio wake Dar?
 

mkuu umeeleza kwa kina na nikikusoma zaidi ninachokiona ni uzalendo mkubwa uliondani yako.
wasipoelewa na hapa;

cc Mohamed Said Mag3 THE BIG SHOW Gwalihenzi Nyakageni Eiyer
 
Last edited by a moderator:
Kwanza nikukumbushe kuwa haikuwa post yangu ya kwanza. Rekodi zipo wazi kabisa na nadhani umeamua kuweka hilo neno ya kwanza ili kuonyesha kuwa nilikuja na shari kinyume na ukweli.
Post ni hii hapa Hakuna mahali niliposema hamna akili kama ulivyodai.
Hakuna mahali niliposema mohamed kachanganyikiwa, kuna mahali nimesema ana frustration. Frustration haina maana ya kuchanganyikiwa unless tuna definition tofauti.

Lakini hili la frustration nina ushahidi kutoka nyuzi zake za nyuma ambapo amesema '' babu yake aliongoza miigomo ya reli na bandarini''. Akasema kuna watu hawakuwa na uwezo wakiwa UDSM lakini wanaendesha magari na nyadhifa kubwa kwasababu ya mfumo.

Mohamed aliendelea kusema kazi ya kupigania uhuru na historia yake ipo katika familia na si kama sisi tunaosimuliwa.
Ukiyasoma maneno hayo hakuna shaka MS ana frustration juu ya historia ya familia na nafasi yake katika taifa kwa sasa.

Nilimjibu kwa kumwambia kuwa hiyo ilikuwa personal frustration na hivyo asiifanye kama tatizo la kitaifa kama nilivyoandika tena hapo juu.

Hakuna shaka kuwa ninyi mnamtetea MS nashangaa mnakana ukweli huo. Kumtetea si dhambi lakini iwe kwa hoja na si kumdhalilisha kwa matusi kwasababu hata yeye anajisikia fedheha maandishi yake yakipambwa na lugha zenu ambazo nashindwa kuelewa ni kwa vipi mnazinasibisha na dini kwasababu hakika inatia dhalili.
Wapo wanaojiuliza hivi hawa ndio walivyo? Kama wasomi ni hivi vipi huko mitaani?

@Khataan, kuhusu mada ya kumwaga Mtama hakika mtama upo. Ninaweza kuweka hapa ili njiwa wa Ritz waushambulie. Busara zimeniongoza kuwa pamoja na kuwa na haki ni vema nisifanye hivyo. I chose not to write.
Nasisitiza mtama upo busara zinaniongoza sana nisifanye hivyo.

Na mwisho, mimi siwakatazi na wala sikuwa na nia ya kuwazuia kuendelea kuporomosha matusi.
Mumenitukana sana na nimekaa kimya kila mara nikiwanasihi kuwa hivyo sivyo.

Kilichonisukuma kuandika kuhusu lugha zenu ni baada ya kuona lugha hizo zinafungamanishwa na imani yenu, eti hata neno inshallah la kiarabu limekuwa sehemu ya imani.

Ndio maana nimeuliza je imani inawatuma mu behave katika hali dhalili na hovyo kama hiyo? Narudia katika hali dhalili na hovyo hivyo? Hebu rudini msome nyuzi zenu halafu mjiulize zimejaa dhalili kiasi gani kwenu na kwa jamii inayowahusu

Nikauliza,je mnaitendea haki jamii ya Watanzania, jamii zenu katika makundi ya kabila, koo na imani?
Je, kila mmoja anayesoma matusi yenu yakiwa katika mgongo wa imani anafurahia hilo?
Je, ndio mafunzo yaliyoelekezwa hayo? Na kwa lugha hiyo nani atasoma kile mlichokusudia au kuvutika na hoja zenu?
 
Last edited by a moderator:

Wewe utayaita matusi lkn nidhamu ya kuongea HUNA!.
Mimi sikujui wala wewe hunijui lkn sisi wote tunamfahamu Mohamed Said
Na kama wewe ni msema kweli kuwa sisi tumekutukana basi onyesha hayo matusi!

Ktk malumbano ukitoa kejeli unapewa kejeli! Na istoshe wewe unatetea BATILI bila ushahidi! Na kwa muungwana HILO NI TUSI KUBWA MNO!

Unatetea mtu aliyechoma nyumba ya babu yangu kwa kumlazimisha aende kuishi vijiji vya ujamaa PORINI?!
Halafu wewe unamtetea tena bila vigezo??

We unafahamu kuwa europe ukimtetea Hitler ni kosa la jinai??

Ok tuseme huyo baba yenu wa taifa hakufikia cheo cha kuitwa muuwaji wa halaiki!

Lkn je! Kauwa wasio na hatia au uongo??

Baba ya mwalimu wangu kafia kizuizini kwa sababu alikuwa against na CCM!

Watu chungu mzima wamefia majela bila kupitia mahakama kwa kufuata amri ya huyo nyerere!

We kumtetea na kumuita muungwana SIO MATUSI HAYO!??

Tell me! Mtu akutukane tusi la NGUONI KABISA! AU AMSIFU NA KUMTETEA ALIYE KUULIA BABA YAO! LIPI BORA HAPO??

Wacha bwana kuangalia upande mmoja!
Dhulma uifanyayo wewe ni kubwa mno!

Sasa mwaga mtama! Longalonga nyiingi inaumiza kichwa!
Kama kuna tusi llt kubwa hapa! Wahusika wanaona! Na watachukua hatua zinazo stahiki!

Mwaga mtama!
 
Last edited by a moderator:
Ahhh kama mtama wenyewe wa kuvizia namna hii mi naingia ofisini sasa!

Nakuomba tu Gurumvi3 utakapo mwaga huo mtama!

Mwaga kwa wingi ili hata kama njiwa wa shariff Ritz watakula! Na kuku wa hayaatollah CHAMVIGA na bata wa maulana gombesugu na ndege wa al habib Tayeb na wale tausi wa al mualim Boko haram
Na mimi nikienda break nikute japo kidogo!

Ahsanta
 
Last edited by a moderator:

Nguruvi3 wewe mwanga mtama wako wala hakuna tatizo lolote sisi tupo na njiwa wetu wanausubiri kwa hamu.

Nakushangaa umegeuka kuwa msemaji wa Mohamed Said. ghafla na kumtolea matamko, teh teh teh. Halafu Sheikh Mohamed Said, wala haitaji kutetea na mtu vitabu vyake ndiyo vinamtetea sijui umeipata wapi hii kuwa sisi tupo hapa kumtetea.

Nikipata wasaa tadadavua kiduchu kejeli zako na matusi yako kwetu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Boko haram heshima sana.

Mkuu wangu sijawahi kuwafananisha au kuwalinganisha Mohamed Said na Nguruvi3 hata siku moja labda utakuwa umenisoma ndivyo sivyo.Mo ni mzee wa gerezani maandishi yake yamejikita zaidi katika siasa za Dar na vitongoji vyake hasa hasa Gerezani akienda mbali hujikita kwenye box la dini ukimwondoa katika viwanja hivyo hana tofauti na kipofu.Nguruvi3 ni mwanajamvi mwenye uwezo wa hali ya juu sana wa kuchambua masuala mbali mbali kuanzia uchumi,siasa,utamaduni na ........Ni wazi hawa ni watu wawili wasiofanana majina wala mitazamo.Unaweza kuunga mkono hoja za Mo upendavyo lakini mwisho wa siku hata nafsi yako inajua fikra zake zikifuatwa hakika Tanzania na Afrika Mashariki haitobaki salama.Kila mara hoja za Mo zimejikita katika utengano sijawahi kusoma maandishi ya Mo yenye kuunganisha jamii ya waTanzania dhidi ya uporaji wa rasilimali zake kama dhahabu,Tanzanite,gesi,ardhi,misitu na nk.Hichi ndicho kilio cha waTanzania wenye akili nzuri,wenye kufahamu uporaji wa rasilimali zetu ni sababu kubwa ya umasikini ambao hauchagui wala haubagui dini,kabila au ukanda wa mtu.Ni ujinga wa hali ya juu Tanzania ya leo tukiamua kuegemea udini au ukabila na kuacha mambo ya maana yanayoamua mstakali wetu wa leo na vizazi vijavyo.




 
Last edited by a moderator:

Ngongo,
Mimi nimesoma Political Sience katika baadhi ya taaluma nilizokuwanazo.

Dini yangu naijua kwa kiasi changu lakini si bingwa katika somo la Uislam.
Kwa ajili hi basi sithubutu kuuzungumza Uislam hadharani kama hapa.

Unachokisoma katika maandishi yangu ni historia na ndani yake hamna suala la
dini kama ''doctronaire.''

Uislam humo unaingia kama unavyoingia Ukristo.

Angalia paper na mihadhara niliyopata kufanya ndani na nje ya nchi utalipata jibu.
 

Ritz,

Naona jamaa yangu anasema ati mie nina ''frustrations.''
Mdomo haumkatai bwana wake.

Anaweza kusema lolote alitakalo kuhusu mie na mdomo wake hautathubutu kumkataza.

''Frustrations'' ati kwa kuwa babu yangu Salum Abdallah hakutaja kwenye historia...
Hakutajwa kwenye historia hii ni kweli na hakuwa peke yake wengi waliondolewa katika
historia na mimi nikawarudisha.

Sasa hiyo ndiyo ''frustration?''

Kuhusu kupewa vyeo watu wenye elimu hafifu kwa kuwa tu wao ni Wakristo hili nikilisema wazi
bila kificho na nikawa maarufu kwa kutoogopa mtu.

Wanaonijua hili wanaweza wao wakalieleza vyema sana kuhusu hii hulka yangu.

Kama vile nilivyoserma Nyerere hakuasisi TANU Nyerere mwenyewe akiwa hai na hakuthubutu mtu
kujaribu kupambana na mimi katika ukweli huu kwa kuwa walikuwa wanajua wazee wangu ndiyo waasisi
wa TANU.

Huu ndiyo ukweli wenyewe na hivi ndivyo nilivyo.
Ikiwa yeye kaona hii ni ''frustation'' basi ni bahati mbaya.

Shariff Ritz niruhusu nikome hapa.
 

Nguruvi,

Mimi nalalamika?
Kulalamika kunatokana na ''ulalamishi.''

Mimi silalamiki mimi huandika kitabu au naandika paper.
Sijui kama huku ni kulalamika...

Unasikia nazungumza Nairobi...
Sasa hivyo si ndiyo viwanja vyangu?

Inakukera?
 
mkuu umeeleza kwa kina na nikikusoma zaidi ninachokiona ni uzalendo mkubwa uliondani yako.
wasipoelewa na hapa;

cc Mohamed Said Mag3 THE BIG SHOW Gwalihenzi Nyakageni Eiyer

Remote,
Maadam mtabaki humu JF bila ya kuandika huo ukweli upinge kitabu changu daima
mtabaki humu humu hamtaweza kutoka nje ya tundu hili.

Hili nimelisema sana kwenu.

Kitabu kinajibiwa na kitabu.

Kama mimi nisingekijibu kitabu cha CCM cha Historia ya TANU kwa kitabu changu
hakuna mtu angenijua na hii mialiko ya Afrika Kusini, Marekani, Ujerumani, Nigeria,
Kenya nk. isingekuwapo kamwe.

Nakusihini.
Andikeni kitabu.

PS:
Tanzania Muslim Professionals wanenitunikia nishani katika nyanja ya Utafiti na Uandishi mwaka huu wa 2013.
 

mzee wangu Mohamed heshima kwako....
Dhumuni langu lalakuku'mention ni kukuomba wewe ujibu zile hoja za nguruvi3 pale juu ambazo nimezi'qoute
 
Mkuu Ngongo umenichekesha sana unasema mzee MS siasa zake zimeegemea mitaa ya gerezani hili swali wakwanza kumuuliza alikuwa ni baba yako wa taifa kilimkimbiza nini kule butiama na kuja kwa wanywa kahawa wa gerezani tena akiwa kavaa kaptula.

Wazee wa gerezani kwa ustaarabu wao wakamshonea suruali mbili kiuno 30 paja 7 leo hii ndio hao wazee mnao wadharau na kufanyia "istiizai" na tashtiti kwao, wala mzee MS hayupo hapa kwa ajili ya udini yeye anatupa maalumati ambayo tulikuwa hatuyajui tulikuwa tulalishwa sumu/uranium.

Kuhusu udini mimi mpaka leo naamini "founder" wa udini ni Nyerere na ukitaka vielelezo viko vingi tu vya kuonyesha Nyerere alivyo andaa hili bomu la udini ambazo cheche zake ndio zinaanza kuruka sasa hivi.
 

Huyo Nguruvi3 hana cha kumwaga ila pumba tu. Nimempa moja kuhusu historia za Uislaam duniani na nikamuuliza nimuongeze? hana majibu, sasa hivi naichambuwa tena post yake na nnakuja na lingine. Nnakuhakikishia hana jibu, utaona atavyokuja na porojo zisizo na kichwa wala miguu.
 
Last edited by a moderator:
mzee wangu Mohamed heshima kwako....
Dhumuni langu lalakuku'mention ni kukuomba wewe ujibu zile hoja za nguruvi3 pale juu ambazo nimezi'qoute

Remote,
Niwekee hizo hoja za Nguruvi nizijibu Insha Allah kwa kadri ya uwezo wangu.
 

Akhiy, Mohamed Said, kuwaambia akina Remote, Nguruvi3, Mag3, Mzee Mwanakijiji, Yericko Nyerere waandike kitabu cha historia ni kama kuwataka mchwa watengeneze Mlima Kilimanajro badala ya kichuguu.

Hawawezi.

Tena waungane wote pamoja na bado hawatoweza.
 
Last edited by a moderator:


Al Murid THE BIG SHOW,

Hiki kigongo ulichomshindilia "jamaa yako",nina hakika hawezi kukujibu asilan!...si unaona kishaanza kukuwekea vikwazo ati atumie rationale,hapo anamaanisha atumie ule ubabaifu wake! Kwi! Kwi! Kwi!

Si unakumbuka yale mambo ya rationalize the Denominator,na ile vulgar fraction!? Kwi! Kwi! Kwi!

Ahsanta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…