Shemeji yangu Ritz
Aslaam aleykum
Sioni jinsi Nguruvi anavyoshambulia UISLAMU kama dini. Kifupi ni kwamba Article yake inawatanabahisha waislamu kujihadhahari na wenzao wanaogeuza madhila yao BINAFSI katika maisha na kuyageuga kuwa agenda ya UMMA wa KIISLAM. Kama hukubaliani na mtazamo wake huo hapo ndipo unatakiwa kumpinga kwamba madhila ya waislamu hao SIO KWELI na WALA HAWAJAWAHI kuwa na HIZO FRUSTRATION kisha utumwagie ILMU.
Article yake inagawa uwanja wa lawama kwa waislamu kuhangaika na marehemu Nyerere (14 yrs ago) huku wao wakikosa udiriki wa wakuenzi mashujaa wao wenyewe japo kwa kutumia majina ya mashujaa hao katika taasisi wanazounda. Binafsi nadhani hii changamoto ya kufanyiwa kazi. Lushoto kwa sasa kuna Sebastian Kolowa Memorial Univ. College, kama kumbukumbu ya askofu huyo (mlutheri) kwani shida iko wapi ile ya Morogoro ikiitwa Sheikh Amr bin Hassan Mem. University au Bibi Titi Memorial University au Sheikh Ponda University? kwani mpaka wawe marehemu? Lakini la maana zaidi kubadili majina pekee hakuleti mapinduzi ya ubora wa taasisi hizo kwa hiyo si vibaya mambo kama anayoyasema Nguruvi kuhusu Standard yakafanyiwa kazi. Nakukaribisha Tanga nitakutembeza wewe na utakaokuja nao kwa gharama zangu binafsi katika taasisi za kiislamu zenye shule za sekondari hapa mjini petu hadi lushoto kisha upime kama nasema uongo. Ni-PM unataka kuja lini niwaandalie mapokezi.
Hakuna ubaya kujua kuwa udhaifu wako uko wapi na kuufanyia kazi. Hawa wa Kirinjiko, Mudio, Buhongwa, na zingine zinazoanza kupanda chati wametambua kuwa kila jambo lazima lisimamiwe kwa taratibu zake ili liende vyema.
Shemeji, sioni dalili za Nguruvi kuubeza uislamu kama dini hapa na hata mimi kama mwislamu singekubaliana naye katika hilo. La maana sisi kama waislamu lazima tukubali kuwa hatuna mafuta wala mjomba wa kututoa katika hii DHIMA ila HARD WORK and good plans.
Wickama,
Salaam.
Bakhti njema hizo
sehemu takriban
zoote uzitajazo mimi binafsi
nazifahamu kwa utuvu na tuna familiy
history nazo na
Wazee wetu wakijuana na watu wengi wastaarabu na influential wa maeneo hayo.
Nafikiri utakumbuka niliwahi kukufahamisha yakuwa tulikuwa pale
Mazinde na
Mombo kwa shughuli za kilimo na biashara tangia yule khabith
Mjarumani hajatia maguu yake hapo
Tanganyika na mpaka yule
Nyerere alipoleta ile nakma aka
"Azimio la Arusha" na kuangamiza kila chema alichokikuta ndani ya nchi hiyo.
Kwa kifupi,napenda kugusia kiduchu hapo ulipoweka hayo maneno
"HARD WORK and
GOOD PLANS"! Kwi! Kwi! Kwi!...ni
rhetorical tamu mno!
Nina hakika umepitia huu mnakasha
post by post!?...kama ni hivyo mbona mimi binafsi nimejaribu kujibu/kuelezea suala hili!? Nafikiri tujiepushe kurejea kupeana au kuulizana majibu/maelekezo yaleyale!?
Kama ukiona
post yangu yoyote labda haijakidhi hayo uyatakayo,
nakusihi njoo nayo hapa na uniulize lolote utakalo,nami takujibu na pale nitakaposhindwa
Insha Allah nina hakika pana wengineo wenye
Ilm kubwa na wenye upeo mwingi hapa
jamvini.
Narejea tena;hiyo
argument yako mbona ni
dhaifu mno!
Maneno kama hayo hayo uyasemayo leo hapa jamvini,si ndo hayo hayo yalitumiwa/hutumiwa na wale Maharamia wa
Western Powers dhidi ya ndugu zetu
Afrikan Amerikans especiallyduring the
Civil Rights Movement!?
Arguments hizo hizo si ndo zilikua zikitumiwa na the
Apartheid Southern Afrikan regime dhidi ya wale ndugu zetu
Black South Afrikans!?
If you don't mind me expand a bit into
geopolitical arena...basi utathibitisha yakuwa hawa
Wazungu aka Mataifa ya Ki-magharibi mpaka kesho nao wanajaribu kupindisha
ukweli ulo dhahir kwa kutoa the so called
"facts" au arguments dhaifu na za kiharamia, kulinganisha ati "uzembe" na "upumbavu" wa
Blacks woote wa dunia nzima and/or Afrikans in particular na mataifa ya
Asia khasa China,South Korea,Singapore,Malaysia na kwingineko.
Huku waki-
discourage tena kwa makusudi
historical facts na baya zaidi ni ile kufanza mlingano kwenye two
different phenomenal.
Pia tunajua jinsi hao hao
Wazungu wanapojisifia na "kustaajabu" ya kwamba kwanini ati
Afrikans hawana maendeleo wala mipango tangia
"wamepewa"/wamegombania huo
"uhuru" wao!?
Nafikiri Wazungu pia hujitolea mfano wao mkubwa,kujinasib na kusifia mno nchi zao na
Wanachi wao ati kulinganisha tena bila ya soni na "uzembe"/"ujinga" wa
Waafrika!?...wanatolea hata mfano wa
WWII na mafanikio ya mataifa yao baada ya hapo!? Kwi! Kwi! Kwi!
Hili suali/hoja
Archbishop D. Tutu aliwajibu vizuri mno,Wazungu wanajisahau yakuwa baada ya WWII pamoja na misaada lukuki palikua pia na
ERP aka
Marshal plan!?
Afrika pamoja na
madhila yoote ya
centuries haijawahi/haitawahi kupata hata
thuluthi ya ile
Marshal plan kutoka kwa mtu/Taifa lolote ile!?
Sasa tukirejea kwenye
argument yako/hapo nyumbani;nafikiri utaona
similarities kwenye hayo kiduchu nilojaribu kukukumbusha!?
Au nawe unaamini yakuwa wale ndugu zetu pale
Haiti nao pia ni
"wazembe" na "wapumbavu" hawana
plans zozote kazi yao ni
kulalama kila kukicha!?.... kama unavyojaribu kudai kuhusu hao
Waislam wa hapo nyumbani!?
Nafikiri kwa yeyote mwenye kufahamu
madhila ya ndugu zetu wa
Haiti,hawezi asilan ati leo kukurupuka na kujaribu ku-
discourage and/or ku-disregard history walopitia, yenye madhilal na dhuluma ziso mipaka zilowapata kwa
centuries.... tangia ile
Haiti revolution dhidi ya wale washenzi
Polish troops aka
French Army na mangine mangi mno yaliofuatia/yanayozidi kuwasulubu mpaka kesho...kumbuka hapa sijagusia asilan hata ile
Christians Slave Trade aka
Atlantic Slave Trade.
Sasa ni vibaya mno na
unafiki wa kitaaluma na pia itakua ni
uzandiki ulokubuhu,kama leo sisi hatutafuatilia majambo kwa ile
historical context!
Itakuwaje leo hii nyinyi ndugu zetu
Wakristo muwe mstari wa mbele ati ku-
discourage historical facts, kwamba
Waislam walikuwa
systematical persecuted,oppressed,
marginalised and
allienated during both
colonial powers British and Dutch/Germany...na khalaf yake
Nyerere akafuatia na kufanza mangi yasio tafauti na yaleyale aloyakuta!
Khalaf,wewe
unakurupuka ndugu yangu unawaamabia ati watu waache "
uvivu" na wawe na "
mipango"!?
Hivi wewe unafikiri nyinyi
Wakristo kama mngepitia
nakma,
unyama,dharuba na dhuluma zoote walizopitia
Waislam hivi si mpaka leo mngalikua hizo
tongotongo za macho ndo zimekuzidini!?
Au hujui yakuwa
Wakristo walikua
systematicaly benefited toka kwa
Colonial Masters to the expense of almost all
Muslims and
others few with no religion!
Na
Nyerere ndo nae akapokea lile
jiti la maangamizi na kuendelea na huu
MfumoKristo unaondelea kututafuna mpaka kesho....yaani imekua kama vile
relay race! Kwi! Kwi!
Kwa maana hii huoni yakuwa
Wakristo na hayo
mafanikio mliyonayo;ni kuwa tayari walishatengenezewa platform aka
social engineering na wale mabwana zao wa Makanisa aka
Slave Masters/Colonists wao!?
Wallahi,naona
dhiki yakuwa kila siku
tunakufahamisheni haya haya nanyi mnarejea na yaleyale huku mkijifanza
vipofu!?
Pia naona unajaribu kumtetea
Nguruvi3 kiduchu,haina neno ni
vyema mno.
Lakini
argument yako bado
inalegalega mno!
Tatizo ni kwamba,hatuwezi hata siku moja kujaribu kuangalia dhulma na madhila waliyopata/wayapatayo
Waislam bila ya kumuhusisha yule
Nyerere.
Kumbuka yakuwa yule ndo alokua
Rais wa mwanzo hapo,na katika kile kipindi chake ndo pia
Waislamu walisulubiwa mno!....na kila
oppression dhidi ya Waislamu yeye ndie aliekua
Architect wa kila jambo..yaani ni sawa na kutaja ile nakma ya
WWII bila ya kumtaja Bwana
Adolf Hitler!?....si itakuwa ni
ubadhilifu wa kihistoria!? Kwi! Kwi! Kwi!
Sasa hizo
"plans" ujaribuzo kutufunza sisi
Waislam,tutawezaje kufanza bila ya kujua huko nyuma tulipotoka,yalotukuta na kurekebisha
makosa yetu kwa huko mbele tutarajiako kwenda!?
Sasa katika sisi kujitazama huko
ki-historia ndipo huyo
Nyerere aingiapo na hapa ndipo "ugomvi" na Bwana
Nguruvi3 unapoanza!? Kwi! Kwi! Kwi!
Kuhusu hayo maeneo unayojaribu kutaka kulinganisha na kusifia;yaani huko
Lushoto...ni sawa nakuomba uongezee na Mkoa wenu mpendao kulinganisha hayo muitayo ati ni
"maendeleo" ya
Waislam wa huko!
Nakhis madhumuni yako ni kuonyehsa labda
"uvivu" na "
uzembe" wa
Waislam wa huko ulikotaja na wale wa
mwambao!?
Hii album yenu ya
divide and rule mbona imeshapitwa na wakti ndugu yangu!?
Wewe binafsi,jaribu hata kuchungulia hayo mnayoita ati ni
"maendeleo" na hizo bidii za hao
Waislamu wa hayo maeneo na wale
Wakristo wa maeneo yaleyale,khalaf angalia hata ile
rate/mlinganisho ya hayo mafanikio...khalaf njoo hapa ndugu yangu tuzungumze kwa ustaarabu.
Mimi nayajua baadhi ya hayo maeneo na tuna family friends wengi na wa karibu mno tangia tuko wadogo...huko Mwanga,Vunjo,Mtae,Machame,Marangu,Soni, Lushoto na Bukoba, Mwanza,Mbeya na kwingineko.
Tatizo tunarejea palepale,kwa mfano hata tukichukulia yakuwa hao
Waislam wa huko labda ni kweli ndo wenye bidii na hawapendi kula wali na kucheza bao kulinganisha na labda wa
Zanzibar,
Bagamoyo,
Tabora,Mtwara na
Tanga... for the sake of argument nakubali ni kweli!?
Sasa itakua
historically hao wamefikia hapo walipo na kupata
nasra hiyo,kwa kuwa by
chance wametokea kuwemo ndani ya maeneo ambayo walipata ule
upendeleo makhsus wa
Wakoloni na hatimae kuendelezwa na yule
Nyerere chini ya huu
MfumoKristo!?
Kama nao pia wangekua kulekule kwenye
mainly Muslim inhabited areas ambako kulikua
systematically undermined,basi leo pia ingekua hiyo khadith/argument yako inawadhrau hata nao
!.....Hujawahi kusikia ile mithali yakuwa "mgagaa na upwa hali wali mkavu"!?
Niwie radhi kwa maandishi mangi mno.
Ahsanta.