Islam’s role in Tanzania’s freedom struggle

Nguruvi3.

Naona unaendelea kupiga ngumi hewani teh teh teh!

Hebu jisome tena ulichokiandika ndiyo utajua nani anajichanganya kati yako na Mujitahidi CHAMVIGA. unasema wanaotakiwa kulalamika kusema wameonewa wale waathirika, ndiyo maana tunakuambia wewe una chuki na Waislam kila dhulma walizofanyiwa na Nyerere kwako unaona sawa, wewe unamtaja Sheikh moja tu Hassan bin Amir kuna masheikh walikuwa mikoani Mwanza, Dodoma, Tabora, Kilwa, Tanga, walikamatwa wala hawakuwa wanasiasa nakutajia tena.

Baada ya kupatikana uhuru kilichofuatia ni kuwakamata hawa masheikh na kuwafunga jela, Sheikh Abdulkarim Abdulwahid, Maalim Popo Saleh, Sheikh Suleiman Masudi Mnoji, Sheikh Jumanne Bias, Sheikh Bilal Waikela, Ali Migeyo, Maalim Matar, Sheikh Nurdin Husein, Sheikh Ali Comorian, Sheikh Al Amin Mafta, Sheikh Hashimu Haji, Sheikh Abdalla Mwamba, Sheikh Amin Abdalla, Sheikh Maftaa, na wengine wengi.

Nguruvi3. sisi Waislam ndiyo waathirika wenyewe hivi unataka Masheikh wasemewe na nani kama siyo Waislam, nyie Maskofu wenu wakipatwa na matatizo wote mnanyanyua midomo yene tena wewe uliandika kuwa kuishambulia serikali ushahidi upo, Masheikh wakipata matatizo unasema wanaotakiwa kulalamika ni waathirika, eboo!! wewe mbona unakesha JF kumtetea Nyerere kwa nini usiwaachie kina Madaraka Nyerere, Makongoro Nyerere na watoto wengine wa Nyerere, wewe kweli kauzu.

Majanga.
 
Last edited by a moderator:
Tabia inayokuponza wewe ni kusema ukweli! My foot...

Kusema Mohamed Said alikuwa Bakwata ndiyo ukweli.

Nguruvi3 siku zote mtu mkweli huwa hana tabia ya majisifu na mikogo, jamii ndiyo inamsemea.
 
Last edited by a moderator:

Hakuna makosa kusema waliopigania walikuwa wazee wazalendo wa Kiislam, ambao walikuwa na mapenzi na Nyerere kama kijana wao wala hawakumbagua.
 
Mujitahid CHAMVIGA.

Mwaka 1958 kulitokea ugomvi Sheikh Suleiman Takadir aliwaonya Waislam haya yote mnayomfanyia Nyerere wachukuwe tahadhari atakuja kuwageuka, kama aliota.
 
Last edited by a moderator:

Anacho fanya hapa Jamvini Sheikh Mohamed Said vyote vinaangukia kwenye Fasihi andishi!

Unaweza ukawa hujuwi kusoma lakini basi hata LUGHA ya picha nayo ikushinde?!

Kama hutafahamu neno kwa neno na kisha kupata maana, bila shaka wewe utakua na kilema cha ufahamu!

Wewe Wickama, Nguruvi3 na Mag3 mtapata tabu sana kumfahamu ndugu yetu Sheikh Mohamed Said

CC : Dr. kahtaan, Sharrif Ritz, Al akhiy gombesugu Hayatollah CHAMVIGA Al ustaadh Boko haram na Hajjat FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:

Ujumbe wako maalim Tayeb uko waazi kabisa!
Wakikusikiliza hao vijana! Huenda wakafaidika.
 
Last edited by a moderator:

May be nimekuwa too prejudice kwako mapema sana hata kunipelekea kuwa na Paranoia dhidi yako. Sawa, lakini hebu jiulize kwa mfano unapotoa kauli ya kuwadhihaki wazanzibar au watu wa Tanga na kusema hawana maendeleo kwakuwa ni wavivu na watu wakupenda kukaa vibalazani na kunywa kahawa na kashata wakati huohuo historia inaonyesha Tanga ni miongoni mwa mikoa iliyokuwa mbele kimaendeleo, kama kuwapo kwa viwanda vingi ambavyo leo vimebakia magofu na muuwaji wa viwanda hivyo ni Nyerere mimi wa Tanga nitakuchukulia unanidhihaki/kejeli au unaniambia nini? Leo vijana kwakukosa kazi wamegeuka wauza unga na mateja wakati vyanzo vya ajira vimeuliwa makusudi na Nyerere je ukisema huyu ni mvivu ataichukulia kauli hii ni kejeli kwake au nini? Wewe unasema unasema unasimamia ukweli ambao sisi hatutaki kuusikia, labda nikuambie tu kuwa mimi nimuumini wa ukweli lakini ikiwa ni ukweli hasa. Wewe unakosa sifa ya kuaminiwa kwakuwa umekuwa kigeugeu (ndani ushahidi upo). Umesema hujamkeli mzee Mohamed Said na ushahidi tukakuwekea. Umesisitiza watu tusimamie ukweli na mimi nasisitiza hivyo pia kwani ukweli ndio pekee utakaotufikisha tunapotaka kama watanzania na kinyume chake itakuwa ni UNAFIKI. Turudi kwenye mada.
 
Last edited by a moderator:

Nimekusoma vizuri akhy Tayeb.
 
Last edited by a moderator:
Mujitahid CHAMVIGA.

Mwaka 1953 kulitokea ugomvi Sheikh Suleiman Takadir aliwaonya Waislam haya yote mnayomfanyia Nyerere wachukuwe tahadhari atakuja kuwageuka, kama aliota.

Shariff Ritz,
Lile onyo la Sheikh Suleiman Takadir kuhusu Nyerere ilikuwa ni mwaka 1958
siyo 1953.

Ilikuwa baada ya kurejea kutoka Mkutano wa Tabora wa 1958 uliojadili Kura Tatu.

Ndipo Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU na kupoteza uenyekiti wa Baraza
la Wazee na nafasi yake ikachukuliwa na Mzee Iddi Tulio.

Uongozi wa Baraza la Wazee chini ya Iddi Tulio ndiyo uliopewa taarifa ya kupigwa
marufuku baraza hilo pale Ukumbi wa Arnautoglo.

Si muda mrefu Mzee Tulio akagongwa na gari akafa na TANU hawakuwa na taarifa nae
akazikwa kimya kimya na nduguze Waislam.

Hapakuwa na rambirambi kutoka TANU wala hotuba za wasifu wake.

Na laiti kama Mohamed Said asingelimwandika katika kitabu chake hakuna ambae leo
angemtambua.

Sheikh Suleiman Takadir utabiri wake ulikuwa tawire.
 
Haya mzee Said, tumalize na la sigareti maana tumeshaona chanzo

Nguruvi,
Nimesoma maneno yangu na wala hayanipi shida naweza kuyaandika tena hivyo hivyo
neno kwa neno.

Ikiwa wewe unaona vinginevyo yawezekana labda sie sote tumeathiriwa na makuzi, mila
na malezi yetu.

Nakueleza makuzi yangu na uhusiano wangu na historia hii ya Soko la Kariakoo kwa kifujpi.

Mimi nimewasikia wazee wangu wakihadithia mambo haya kwa vizuri na huku wakikumbukia
zama wakicheka wala hapakuwa na chuki katika mazungumzo yao.

Nimewasikia wakinitania mimi kwa kushinda kwenye ubao wa biashara ya mjomba wangu wakati
wa likizo kwa sababu kutwa nzima nakula vyakula vya ubuge pale.

Akipita muuza kumbikumbi mjomba wangu ataninunulia, akipita muuza njugu za kuchemsha
nanunuliwa na mchana ananichukua hoteli kuninunulia sahani ya pilau nakula na ndizi mbivu.

Katika mazungumzo kama haya ndipo anapoingia babu yangu Sharif Mwamedi na anapoingia
Abdu Sykes, Mzee Abdallah na Shariff Abdallah Attas na uhusiano wao na Nyerere.

Sikupata hata siku moja kuhisi kuwa mazungumzo yale yalikuwa na nia ya kumdunisha Nyerere.

Mwisho sielewi kwa nini umelipenda sana hili jambo la sigara...
 
Nafyonza Ilm kutoka kwa Mzee Mohamed Said,
 
Last edited by a moderator:


Kwa hiyo Unataka kusema Nyerere na TANU ndiyo walimgonga siyo!
 
Kwa hiyo Unataka kusema Nyerere na TANU ndiyo walimgonga siyo!



Mkuu wacha hizo!

Unamuuliza au unamuwekea maneno mdomoni!?...wewe ndie unayeonekana umeshakuja na conclusion yako!?

Hiyo ni leading question...nafikri ingekua fair kwa unayemuuliza kama ungempatia open and/or closed question!?

Khalaf,kwa jinsi Serikali za Ki-Afrika na nyinginezo nyingi duniani zinavyoendeshwa,sioni hata sababu yawe ati kustaajabu kwalo!?

Ahsanta.
 



Sheikh Mohamed Said,

Asalaam Alaykum,Shukran na tunakusoma saana na kufuatilia hizi bayana zako kwa utuvu ulo mwingi.

Maneno kama hayo hayo alosema na kuusia Sheikh Suleiman Takadir...nami nilimsikia Al Marhum Sheikh Hussein Juma wa UTP akiyarejea kwa machungu mno.

Maana kuna wakti ilinilazim kujaribu kumuuliza kiduchu na kwa adabu ilo njema ili anijuzu kisa cha yeye kuwa UTP,basi ndo alifunguka kiduchu...nami mpaka leo kanacha mdomo wazi!

Ama kwa hakika tuna mafunzo makubwa/mangi mno sisi tuliopo leo hii, kutokana na yaliowasibu Wazee Wetu na dharuba walizostahamili...

Na ndo maana tumeapa/tunaapa, kwa yakini hatutarejea tena kule kwenye kudhalilishwa/kudhulumiwa kwa sababu tu ya uungwana na ustaarabu wetu!...abadan,asilan!!

Nipatia fursa nikuulize suali jingine kiduchu...hivi yule Brigadier Takadir alikua ni mtoto wa Sheikh Suleiman Takadir!?

Kama ndie yeye namfahamu uzuri mno,alikua ni sahib mkubwa mno wa Mzee wangu. Siku alipopatwa na ile "accident" pale junction ya St Peters nafikiri...Mzee wangu na Mzee Barongo aliekua TPDC,ndo waliokua watu wa mwanzo kufika Lugalo na kuthibitisha kifo chake maskini.

Kipata fursa pia tujuze sheikh Mohamed Said;je yule Bwana Idd Bin Khamis,alokua pale kona ya Udoe na Sikukuu,opposite na Sheikh Nurdin Hussein...nae alikua na shughuli zipi ndani ya ile TANU!?

Nini uhusiano/mchango wake ndani ya hizo harakati wakti huo hapo Mzizima!? Nae alikuwamo kati ya wale waliopata hiyo misukosuko kutoka kwa "Baba wa Taifa"!?

Niwie radhi
kwa hivyo visuali kiduchu...maana najaribu kuunganisha dots fulani kichwani mwangu,khalaf nituame.

Ahsanta.
 
Kwa hiyo Unataka kusema Nyerere na TANU ndiyo walimgonga siyo!

Hapa unauliza au unatoa ushauri!
Nyie watoto hizi elimu zenu za kata zimekuletee hasara kubwa sana!

Manake kwa elimu chafu mlizo pandikizwa kila ukifungua mdomo.

Badala ya kutengeneza! unachafua mazingira!!
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…