Mrengwa wa kulia
JF-Expert Member
- Mar 21, 2022
- 1,091
- 3,695
Wayahudi wana haki waliyopewa na Mungu kwa nchi hii. Kiongozi mmojawapo wa vyama viwili vya siasa kali za mrengo wa kulia, vinavyounga mkono walowezi, ambavyo Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alivileta katika muungano wake wa serikali baada ya uchaguzi wa 2022.
Smotrich anahudumu kama waziri wa fedha lakini pia ana wadhifa katika wizara ya ulinzi, ambao umemruhusu kufanya mabadiliko makubwa kwa sera za Israel katika Ukingo wa Magharibi.
Amewekeza kwa kiasi kikubwa fedha za serikali katika makazi ya walowezi, ikiwa ni pamoja na barabara mpya na miundombinu. Lakini pia amechukua mamlaka kutoka kwa jeshi, ili kuharakisha ujenzi wa makazi ya walowezi.
Katika matamshi yaliyorekodiwa kwa siri akiwaambia wafuasi wake, Smotrich alijigamba kuwa anafanya kazi kubadilisha DNA ya mfumo juu ya utanuzi wa makazi, na itakuwa rahisi kueleweka katika sheria na muktadha ya kimataifa.
Wazalendo wa kidini walikuwa pembeni mwa siasa za Israel kwa miongo kadhaa. Lakini itikadi yao polepole imekuwa maarufu zaidi. Katika uchaguzi wa 2022, vyama hivi vilichukua viti 13 katika bunge la Israel lenye viti 120 na kuwa katika muungano wa mrengo wa kulia wa Netanyahu.
Wanahakikisha vita vya gaza vinachukua muda muda mrefu ili kujihakikishia kuukalia ukingo wa magharibi bila bughudha kisha Israel waweze kuichukua palestina Yote.
Source BBC
Smotrich anahudumu kama waziri wa fedha lakini pia ana wadhifa katika wizara ya ulinzi, ambao umemruhusu kufanya mabadiliko makubwa kwa sera za Israel katika Ukingo wa Magharibi.
Amewekeza kwa kiasi kikubwa fedha za serikali katika makazi ya walowezi, ikiwa ni pamoja na barabara mpya na miundombinu. Lakini pia amechukua mamlaka kutoka kwa jeshi, ili kuharakisha ujenzi wa makazi ya walowezi.
Katika matamshi yaliyorekodiwa kwa siri akiwaambia wafuasi wake, Smotrich alijigamba kuwa anafanya kazi kubadilisha DNA ya mfumo juu ya utanuzi wa makazi, na itakuwa rahisi kueleweka katika sheria na muktadha ya kimataifa.
Wazalendo wa kidini walikuwa pembeni mwa siasa za Israel kwa miongo kadhaa. Lakini itikadi yao polepole imekuwa maarufu zaidi. Katika uchaguzi wa 2022, vyama hivi vilichukua viti 13 katika bunge la Israel lenye viti 120 na kuwa katika muungano wa mrengo wa kulia wa Netanyahu.
Wanahakikisha vita vya gaza vinachukua muda muda mrefu ili kujihakikishia kuukalia ukingo wa magharibi bila bughudha kisha Israel waweze kuichukua palestina Yote.
Source BBC