Israel yamuua kamanda wa kundi wa Islamic Jihad huko Gaza

Israel yamuua kamanda wa kundi wa Islamic Jihad huko Gaza

Exile

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2021
Posts
1,477
Reaction score
3,642
Shambulio la anga la Israel la mapema alfajiri limemuua kamanda mkuu wa kundi la Islamic Jihad (PIJ) na wanamgambo wengine wawili mjini Gaza.

Ndege ya kivita ilishambulia ghorofa ya tano ya jengo la makazi la Hamad , karibu na Khan Younis kusini mwa eneo hilo.

Siku ya Jumatano wanamgambo huko Gaza walirusha zaidi ya makombora 460 dhidi ya Israel.

Jeshi la Israel lilishambulia zaidi ya wapiganaji 130 huko Gaza, katika mapigano makali zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miezi tisa.

Watu 25 wameuawa huko Gaza tangu Jumanne asubuhi wakati Israeli ilipoanza operesheni yake dhidi ya PIJ, Wizara ya Afya ya Palestina huko inasema.

Waliouawa ni pamoja na raia wasiopungua 10 na makamanda wengine watatu wa PIJ.

Jeshi la Israel lilisema watu wanne, wakiwemo watoto watatu, wameuawa huko Gaza kwa roketi zilizoanguka, ingawa hii haijathibitishwa na vyanzo vya Palestina.

Source: BBC swahili
 
Watulie waache ugaidi la sivyo watauawa sana, haitokuja muifute Israel hata mkiungana.....kubwa lenu Iran huwa halina jeuri yoyote kwa Israeli.
 
Watulie waache ugaidi la sivyo watauawa sana, haitokuja muifute Israel hata mkiungana.....kubwa lenu Iran huwa halina jeuri yoyote kwa Israeli.
Israel inafundisha vitendo haramu na vya kigaidi duniani. Haipaswi kufumbiwa masikio.
 
Watu weusi na hizi Imani...zimeshaharibu bongo zao.....yaani anamuhurumia mwarabu aliyepo Palestine kuliko muafrika mwenzake wanaouwawa hapo Sudan
Na wewe why unaenda mbali wakti jirani yako DRC unajifanya umemsahau hadi urukie huko?

Alafu vita zote zinazungumzika so acha watu waongee ondosha ukuda wako kama jiwe
 
Wabarikiwe watoto wa Yakobo, mkono wa Jehova uwe juu ya wafilisti wote.
 
Back
Top Bottom