Israel yatoa ishara kuwa inapigana maeneo 7 huku Houthi wakifanikiwa kupenya ngome za mataifa 20 yanayoongozwa na Marekani

Israel yatoa ishara kuwa inapigana maeneo 7 huku Houthi wakifanikiwa kupenya ngome za mataifa 20 yanayoongozwa na Marekani

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Waziri wa ulinzi wa Israel amesema nchi yake iko vitani maeneo saba tofauti.Akaongeza kusema kuwa kutokana na hilo tayari wameshaanza kushambulia kwa nguvu maeneo sita kati ya hayo kulipiza kisasi.
Maeneo hayo aliyataja kuwa ni Iraq,Syria,Lebanon na Yemen.Mengine ni Gaza,ukiongo wa Magharibi na Iran.
Kwa upande wa wapiganaji wa Houth wa Yemen wamekuwa na hamasa za kupigana siku baada ya siku na kutokutishwa na muungano unaoongozwa na Marekani wenye nia ya kuwanyamazisha.
Hapo jana wanamgambo hao kutoka nchi maskini walifanikiwa kuipiga meli ya United VIII inayomilikiwa na shirika la MSC Mediterranean Shipping lenye uhusiano na Israel.Meli hiyo ilikuwa ikitokea Saudi Arabia kuelekea Pakistan.
Mbali na shambulio hilo la meli kiongozi wa kijeshi ya Yemen,Yahya Saree amesema vikosi vyake vilishambulia mji wa bandari wa Israel wa Eliat.Israel imekiri kupambana na makombora hayo kutoka Yemen bila kuweka wazi iwapo kulikuwa na hasara yoyote iliyosababishwa nayo.
Muungano wa kulinda bahari ya Red Sea umesema siku ya jana kudondosha droni 12,makombora 3 ya kupiga meli na makombora 2 ya kupiga mbali ambayo huenda yalikuwa yakielekea Israel.

Israeli minister hints at retaliatory actions taken in Iraq, Yemen, Iran

Yemen's Houthis claim responsibility for Red Sea container ship attack

 
Watajuana wenyewe huko na mambo yao, sasa hivi hakuna anaepigia kelele Yemen kuacha vita yakiwakuta makubwa ndio huruma zinaanza, dunia imekua kichaa kweli kweli
 
Watajuana wenyewe huko na mambo yao, sasa hivi hakuna anaepigia kelele Yemen kuacha vita yakiwakuta makubwa ndio huruma zinaanza, dunia imekua kichaa kweli kweli
Kwa fikra zako unadhani kila siku waislamu watapigwa tu na kwamba ubabe na uchokozi wa Israel utadumu.
Katika kuchokoza na kujifanya mbabe basi unadhoofika kidogo kidogo na mwishowe unapigwa na watoto au maskini ambao hata mlo wao wa siku hawaujui.
 
Kwamba mataifa saba ya kiislam yanapigana na nchi ndoogo ya Israeli...?

Hivi...! Kumbe Israel ni ndogo kiumbo tu eeh, ila inauwezo mkubwa kushinda mataifa mengi ya kiarabu na Kiislam..?
 
Kwamba mataifa saba ya kiislam yanapigana na nchi ndoogo ya Israeli...?

Hivi...! Kumbe Israel ni ndogo kiumbo tu eeh, ila inauwezo mkubwa kushinda mataifa mengi ya kiarabu na Kiislam..?
Mataifa saba yapi na yapi enhee tuanze na taifa la GHAZA tutajie rais wa hili taifa hem mara moja haya taifa la Hizbullah haya tutajie na rais wa hili taifa haya taifa la houthi tutajie na rais wa hili taifa
Israhell anapigana na hamas tu waliojikalia ukanda wa ghaza waache kulia lia
 
Ninyi wavaa vipedo na makobazi Mkiondoa makelele na propaganda uwezo wa kupigana vita hamna. Mmeua Wazayuni approx. 1,200 hiyo October 7,pamoja na wanajeshi 150 Toka vita ianze October 31.Lakini idadi ya waliokufa huko Gaza ni 22,000,Tena hapo Israel wanalenga maeneo yenye magaidi na miundombinu yao tu. Sasa kwa akili za ngumbaru tu nani anayepoteza watu wake wengi zaidi?
Kina Mahmoud Abasi wenye eneo lao wanalilia ceasefire, ninyi Waarabu wa kwa mtogole mnashabikia vita! 🤔
 
Kwa fikra zako unadhani kila siku waislamu watapigwa tu na kwamba ubabe na uchokozi wa Israel utadumu.
Katika kuchokoza na kujifanya mbabe basi unadhoofika kidogo kidogo na mwishowe unapigwa na watoto au maskini ambao hata mlo wao wa siku hawaujui.
Kuna sehemu nimeandika waislamu hapo 🤔🤔
 
Ninyi wavaa vipedo na makobazi Mkiondoa makelele na propaganda uwezo wa kupigana vita hamna. Mmeua Wazayuni approx. 1,200 hiyo October 7,pamoja na wanajeshi 150 Toka vita ianze October 31.Lakini idadi ya waliokufa huko Gaza ni 22,000,Tena hapo Israel wanalenga maeneo yenye magaidi na miundombinu yao tu. Sasa kwa akili za ngumbaru tu nani anayepoteza watu wake wengi zaidi?
Kina Mahmoud Abasi wenye eneo lao wanalilia ceasefire, ninyi Waarabu wa kwa mtogole mnashabikia vita! [emoji848]
Israhell ndio wanauwezo wakupigana vita bila ya shaka
Waliyapiga mataifa ya kiarabu kwamuda wa siku sita
Ila wanashindwa na wilaya moja ya hapa Mombasa
Wazayuni watu wa hovyo sana kuua watoto wanawake na propaganda ndio wanakuweza
 
Back
Top Bottom