IT kwa Tanzania ni kituko. Inakuwaje ni nadra kuwakuta waliotajirika? Hawazioni Fursa au ni watupu?

System hairuhusu startup kufanikiwa. Ukiona mtu ametoboa kwenye IT nchi hii ni yule ambaye yupo na financial support au connection ya kumwezesha kufika juu.

Kuna startup nipo nayo, lakini kila nikijaribu kuipush kuunganisha na system za fedha kama banks, mobile money wanahitaji a lot of documents ambazo kwa startup siwezi kuwa nazo au ili niwe nazo lazima mifuko itoboke kwa kiwango cha kutosha and they say ni matakwa ya BOT.

Ili tuweze kufanikiwa kwenye Tech industry kwa Tanzania, ni lazima tuwe na systems zinazo support maendeleo ya startups kuanzia kwenye policy, financial support, tech-minded leaders na sio wazee ambao they know nothing or they don't have any exposure to technology.

ahsanteni.
 
IT ni kama taaluma nyingine kama U daktari, Uhandisi au Ualimu

Wenyewe haukufanyi uwe tajiri. Hao kina Mark Zuckerberg na Bill Gate ulio watazama kama mifano, moja hawakusomea IT kama Taaluma, na mbili sio IT iliyofanya wawe matajiri bali ni Entrepreneurship iliyochukua fursa ya soko la Personal computer (kwa Bill Gate) na technology ya World wide web (kwa Zuckerberg)

Pia tambua kuwa kuja na idea ni kitu kimoja, na kuifanya idea yako iwe product iliyofanikiwa sokoni ni kitu kingine

Wenzetu wana ecosystem nzuri mno ya kukuza kampuni changa / startups

Kuna startups marekeni zinapewa pesa nyingi ya kujiendesha kuliko pesa walizotoa DP Worlds kununua bandari zetu hapa

Na wana uwezo wa kuendelea kui support miaka mingi bila Faida

Hapa Tanzania kuna aina hio ya Ecosystem? Nani ni Angel investor hapa? Venture capital?

Jambo jingine, IT industry ya Marekani ni profitable kuliko nchi yoyote ile, so demand ya IT ni kubwa, hivyo mshahara wao ni mkubwa kuliko huku ambapo demand sio kubwa

The reason huku demand sio kubwa ni kwa sababu wafanyabishara wa huku hawaja ona value kubwa kwenye sekta ya IT, biashara zao bado ni Local

Mo anauza Juice na vibiriti.


Halafu hata logic yako bado ni ya kijinga, kutaka IT wa Tanzania wawe na mafanikio sawa na IT wa Marekani

Naweza tumia logic yako kusema Matajiri wa Bongo ni kituko, mbona hawapo top 100 ya Forbes?


Wewe ni taaluma gani kwani? Na una mafanikio kiasi gani?
 
Hivi unadhani IT ni programming tu... Sio kila mtu anatakiwa kujua kucode wengine wanajua command na ndio kazi zao.
 

Elimu, lakini je nchi yenyewe ina dhamini project zao?
 
kwa tanzania, kati ya masomo ya kusomea watoto wako, sio IT, atapata shida. huwa nawaangalia maIT waliomaliza UDSM, wanapata mshahara mdogo wakati mtu wa IT hata form six anakuwa amefaulu vizuri kuliko wengine, ni watu waliofaulu vizuru hesabu. ila wanakuja kuishi maisha magumu tu. IT ni ulaya, kwasababu wao hawahitaji kuajiriwa, wanajiajiri na kuwa na makampuni na wanafanikiwa sana. hapa bongo hata kumpata developer wa maana kuanzisha mavitu kama tiktok au youtube au chochote, hakuna, kidogo namwona benjamin fenandez kama amejitahidi, naye sio IT ni mwanauchumi. wanauchumi wanaingia kwenye IT wanapiga pesa wakati IT wanakodoa mimacho tu.
 
Pambana uvivuke hivyo vizingiti mkuu
 
Kuwa IT / developer haina maana ni lazima uwe na product kama tik tok app. Huko U.S unafahamu ni wangapi wana product zao?, na wangapi ni waajiriwa tu kwenye hizo platform.??

Wewe unaweza kuwa mmiliki wa tweeter, lakini ukaajili developers wafanye kazi.
 
INTERNSHIP ZA TECH. KWENYE KAMPUNI MBALIMBALI.. zingesaida sana Graduate
 
Waki onyesha uwezo wao mnawafukuza na kuwashtaki, na wakija peacefully mnawambia IT ajira amna mara cjui hawana project, mnashindwa kutofautisha IT na engineering
 
Mkuu umeongea ki professional sana. Watanzania wengi bado biazjara ya science ns teknolojia gawajui inayooendeshwa wanalinganisha na uchuuzivwa kariakoo.
Infua,baadhi ta nchi za ulaya America ya kusini nao wana strughle kama sisi. Ni nchi chache sana wameweza jama USA, China,Korea. Islael nk.
Nchi nyingi wanazalisha wataalamu wanaotimkia ulaya,cChina , Korea nk
 
Kusomea IT au kuijua IT sio kutajirika. Kuna mambo mengi ya kibiashara ukiyaunganisha na IT ndo unaweza ukatoboa.

Mfano unaweza kuta mtu anajua kutengeneza mobile apps, ila anakwama kwenye mawazo ya kibiashara, ubunifu, mtaji wa marketing, etc.
Hapo kwenye mtaji kweli mkuu, yaani kuna baadhi ya leseni zina gharama sana.
 
Umesema kweli mkuu, yaani watu wanaamini ukisoma IT tu basi ni rahisi sana kujiari na kutoboašŸ¤”.
Laiti wangejuašŸ˜‚
 
Kuna tofauti ya IT wa Udom,UD, na ma vyuo ya mbele huko! Ila wapo waliotusua, kuna mmoja ni CEO wa kampuni, ameajiri mpaka foreigners kuwa managers, kampuni ina matawi kadhaa Afrika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…