Itabidi nimwambie tu kakangu ukweli

Itabidi nimwambie tu kakangu ukweli

Acha kufuatilia Maisha ya watu ya ndoa. Kama hicho kitu kinakuuma tafuta mji wako mbali ukaishi huko. Na wewe subiri uoe watu wakumegee mkeo kama huyo kaka yako anavyofanyiwa maana naona unatukana mamba kabla hujavuka mto
 
Habari wakuu,

Kakangu yuko kwenye ndoa na mke wake yapata miaka 20 sasa,

Kakangu ni mtu wa kusafiri sana kutokana kazi zake,

Shemeji yangu hana shida kabisa,kila kitu ambacho mwanamke anahitaji kupewa na mume wake,shemeji yangu amepewa kila kitu na hata mimi shem ananiheshimu sana kama shem wake wa pekee hapa mjini ,kakazangu wengine wapo ila nao wanashughuli zao huko mkoani,

Tatizo la shem anaruka sana na wanaume mpaka mimi hii tabia yake nimeanza kuchukia sasa,

Sasa mimi namsubiri kaka yangu arudi kwake ili na mimi nikamwambie uchafu wa mke wake,

Najua hata nikimwambia kaka,hakuna ninayemtegemea kwa sasa,ila lazima niseme ukweli kwa kaka

Sent using Jamii Forums mobile app
cha kufanya tafuta namba nyingine ya siri umuandikie msg ya hali halic unayoiona kuhusu shemeji yeye mwenyewe atasuka au kunyoa
 
Una uhakika gani kama nitaoe?nina watoto c chini ya nane, kwanza tambua hilo,na niko bize kuwasomesha tu,kwa hiyo pigana na hali yako mkuu,Mimi niache kabisa
Utagongewa na sio risasi tu hata kibao utashindwa kupiga kudadadeki. Narudia usitukane mamba kabla hujavuka mto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usipomwambia ww akaja kugundua baadae atakulaumu sana
Ukimwambia kwa pupa mambo yakaharibika utalaumiwa wewe
Nakushauri tengeneza mazingira ya yeye mwenyewe kuja kugundua mchezo halafu achukue hatua!

Kuwa makini sana na mambo ya ndoa!
Unaweza kuitwa mchawi wewe
 
Tatizo la kukaa kwa kaka yako hadi umri huo. Ndo zina changamoto zake dogo funga bakuli. Anapewa kilakitu unamanisha pesa au? Ukikua utaelewa haya kaogeshe watoto, uangalie kama mifungo imeingia ufunge banda. Umsaidie dada kuosha vyombo mpike mkalale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ufala mkuu halafu wakiachana utafurahi watoto walelewe na baba tu au mama, mambo ya ndoa waachie wana ndoa.
Akiletewa ugonjwa utafurahi?? Mwambie tu kuna watu wamezoea kuchezea wenzao sababu hawajui uchafu wao!! Hakuna kitu kinaniudhi hapa duniani kama usaliti katika mapenzi.
 
Habari wakuu,

Kakangu yuko kwenye ndoa na mke wake yapata miaka 20 sasa,

Kakangu ni mtu wa kusafiri sana kutokana kazi zake,

Shemeji yangu hana shida kabisa,kila kitu ambacho mwanamke anahitaji kupewa na mume wake,shemeji yangu amepewa kila kitu na hata mimi shem ananiheshimu sana kama shem wake wa pekee hapa mjini ,kakazangu wengine wapo ila nao wanashughuli zao huko mkoani,

Tatizo la shem anaruka sana na wanaume mpaka mimi hii tabia yake nimeanza kuchukia sasa,

Sasa mimi namsubiri kaka yangu arudi kwake ili na mimi nikamwambie uchafu wa mke wake,

Najua hata nikimwambia kaka,hakuna ninayemtegemea kwa sasa,ila lazima niseme ukweli kwa kaka

Sent using Jamii Forums mobile app

Chunguza yakwako kwanza kijana hujui kuhusu mwenza wako unataka ya mke wa kaka ako
 
Back
Top Bottom